Uchaguzi 2020 PICHA: Tofauti ya umati wa watu kati ya CHADEMA na CCM

Najua baada ya october 28 Jf itapooza sana

Itapooza kwa kipi? Mmenajisi uchaguzi wa SM, mbona jukwaa halikupooza? Ccm sio chama cha kizazi hiki, ndio maana unaona kimefanya siasa miaka mitano pekee yake, lakini bado wataka mabadiliko wako juu.
 
Tusubiriane sanduku la kura muda huu wa kufundishana .CCM ina wanachama matajiri walio tayari kutoa magari yao kusafirisha watu .Chadema matajiri wamewasusa hawako tayari kuwachangia kwa polite tofauti na kipindi cha Lowasa na Slaa.Chadema haiungwi mkono na matajiri ndio maana nawachangii usafiri wa wanachama

Pili mikutano ya chadema watu ni wachache sababu wanazindua kwa kanda hivyo ile mikutano watu wanatoka mikoa yote kwenye kanda husika kusema wanakuja kwa miguu uongo wengi wanasafiri kwa mabasi na malori toka majimbo ya mikoa mingine na kulala guest house kuhudhuria uzinduzi wa kanda kwa gharama za ofisi za kanda.Kihuhalisia wanaohudhuria mikutano ya chadema ni wachache sababu mikutano ya uzinduzi unayoiona ni ya watu kutoka kanda nzima za wilaya zote za mikoa iliyo kwenye kanda husika wakati CCM umati unaouona ni wa Jimbo husika tu.

Hapo ukitaka kujua mfano watu watu halisi wa mbeya mjini waluohudhuria mkutano wa Lisu wako wangapi? Chukulia hivi mkutano wa uzinduzi wa kanda mbeya mjini waluohudhuria mfano ni mia moja majimbo kwenye kanda yako kumi na yameleta watu kujua wa mbeya mjini tu wako wangapi chukua 120 hawa kwa majimbo 10 jimbo la Mbeya mjini wahudhuriaji halisi ni 12 wakati ukija CCM sisi hatuzindui kwa kanda ni kwa watu hapohapo ukiona waluiohudhuria ni 120 ni 120 jamii wakati wa happy.Kura zikipigwa Leo mahindi nani happy mbeya mjini? Ni CCM kwa kushinda kura 120 kwa 12
Endeleeni kudanganyana yaani mkutano wa kanda hata hamuelewi maana yake mfano kutoka Iringa au nyasa mtu aweza kuja hudhuria mkutano wa uzinduzi wa kanda mbeya mjini kwa miguu?
Vipi mko tayari kuruhusu picha za drone, ile tunaita aerial view, na oblique view,
 
Mkuu
Sema umati wa watu toka majimbo na wilaya kibao za kanda.Hao hawakuwa watu wa mbeya mjini tu usibinafsishe as if ni wa mbeya mjini tu.Huo uzinduzi haukuwa wa mbeya mjini ulikuwa wa kanda.Subiria CCM tuje hapo uone umati wa wana mbeya mjini tu.Wapiga kura wa TULIA pekee.Tofauti na hao waliotoka mikoa na wilaya zingine kuja kuhudhuria uzinduzi wa kanda ambao siku ya kupiga kura hawatakuwepo hapo kumpigia kura Sugu watakuwa kwao kwenye majimbo yao

Ndipo utaona Sugu anabwagwa mapema asubuhi sababu hana wapiga kura wengi hapo
Mkuu hiyo haina shida,hayo ni mapenzi makubwa sana kwa Rais mtarajiwa na kwa Mbunge wa Mbeya kama watu wamesafiri toka mbali kuja kusikiliza Sera kwa gharama zao
 
CCM Wanatafuta uhalali ili wakichakachua msilaumu kwan ati walikuwa na watu wengi mikutanoni mwao ila kiukweli hawakubaliki kabisa hawa nzi wa chooni
Uhalali lazima uwepo kwa sababu hao watu wamepanda wenyewe kwa hiari yao kwenye hayo mafuso na kwenda kwenye mkutano wa ccm kinyume na hivyo wangekataa,mfano wewe mkuu ukiona fuso la ccm utapanda kwenda kwenye mkutano wa ccm?
 
Mambo yanazidi kuwaendea kombo CCM, CHADEMA wanakuja kwa kasi ya ajabu na kuwafunika CCM kila uchao. Mikutano ya CHADEMA imejaa vijana ambao huenda peke yao kwa mapenzi yao kwa chama tofauti na mikutano ya CCM ambayo amri hutolewa kutoka juu kwa njia ya barua kuwataka wafanyakazi kuhudhuria. CCM hutumia malori na mabasi kusomba watu kutoka vijijini kama ilivyorekodiwa huko Bariadi hapa chini.

Hapa ni Mbeya 5th September 2020 ufunguzi wa kampeni kanda ya Nyasa na Mh. Tundu Lissu.
View attachment 1559996
Hapa ni Bariadi nyumbani kwa Magu cheki malori na mabasi ya kusomba watu.
View attachment 1559993
Hiyo picha ya hapo juu ni ya kampeni za Lowasa 2020, Lisu wapigakura wake wanamsubiri katika box la kura hawaji katika mikutano
 
Mnadanganyana kwamba wingi wa watu ndo wingi wa kura,subirini October mtalia na kusaga meno.
Hamtaamini kitakachowapata.
 
Mambo yanazidi kuwaendea kombo CCM, CHADEMA wanakuja kwa kasi ya ajabu na kuwafunika CCM kila uchao. Mikutano ya CHADEMA imejaa vijana ambao huenda peke yao kwa mapenzi yao kwa chama tofauti na mikutano ya CCM ambayo amri hutolewa kutoka juu kwa njia ya barua kuwataka wafanyakazi kuhudhuria. CCM hutumia malori na mabasi kusomba watu kutoka vijijini kama ilivyorekodiwa huko Bariadi hapa chini.

Hapa ni Mbeya 5th September 2020 ufunguzi wa kampeni kanda ya Nyasa na Mh. Tundu Lissu.
View attachment 1559996
Hapa ni Bariadi nyumbani kwa Magu cheki malori na mabasi ya kusomba watu.
View attachment 1559993
Hii picha ndo kitu nachosema siku zote.... wawekwe vijana wa upinzani kufichua huu upuuzi kwa vithibitisho.....

Na ikifika uchaguzi wawe wameandaliwa vijana katika kila kituo kuhakikisha wanafichua mbinu ovu hasa za kuleta mabox yankura fake nk...

Utandawazi unawaumbua kwa kweli...
 
Mambo mengine bwana
Sio kila anayeenda kweny kampen za cdm ni mfuasi Wengine hawajawah kumuona tundu

Kuhudhuria kampen ni hak ya kila raia kusikiliza hoja
Sio kura ni kampen
Mwisho wa siku subconcious inafunguka na kutuma taarifa kwenye cincious kwamba tundu lisu ndo mtu sahihi... hivyo lisu anapata wapiga kura wapya.....

Huoni hii ni faida hata kama wanaenda kumshangaa?
 
Ccm mmezoea sana kuiba kura,mwaka huu hamuwezi!
Mwaka huu CHEST TO CHEST, nose to nose
1599381216980.png
 
Back
Top Bottom