Aristides Pastory
JF-Expert Member
- Feb 7, 2012
- 348
- 60
Nasikitikia watu kukaza bongo zao kwenye kitu cha kufikirika badala ya kifo kilichotokea. Tukiendekeza mambo ya vijiweni kuchukua nafasi tunapojadili mambo mazito tunaendekeza uswahili badala ya kupanda ngazi moja juu kuwa watu wa kupima mambo na mwenyendo wa matukio mbalimbali yatokeayo nchini.
Eneo la tukio ambako Kamanda ameuawa linaonyesha kila dalili ya kupangwa, kwa sababu ni makazi ya watu na walijua lini atatoka eneo aliko na wapi atafikia. Kuna kila dalili ya kufuatiliwa nyendo zake kwa siku nzima, na utaratibu huu si wa polisi wa kawaida kuna uwezekano wa Umoja wa wanawake kuhusika.
Siku mbili au tatu zilizotangulia Kamanda mwingine wa Uhamiaji amenusurika kwa njia, mwendo na mazingira haya haya. Inaelekea yule wa uhamiaji ni jasiri, lakini huyu walimpania eneo ambalo hawezi kupata nafasi.
Jiji la Mwanza kuna kila dalili ya kwamba uongozi wa polisi wanaruhusu vyama vya upinzani kufanya mambo yao bila bughudha, na watu kama hao hawatakiwa na serikali ya CCM. Wanawataka watu kama akina Kamanda Kamuhanda.
Kwa vyo vyote kuna kitu ambacho cha kujiuliza nini kinaendelea serikalini kikiogozwa na CCM yenye kushinda Uchaguzi Mkuu uliopita.
Kwa sasa ye yote anayeonekana kuwa hatari kushinda Urais anawindwa kama nyati msituni.
Nakupa saluti Mkuu! Umesema kitu ambacho kina mantiki mno. Hebu tujikumbushe MH.PINDA alivyozomewa, unganisha na tukio la leo.... Jibu tayari tunalo!