PICHA: Nyumba ya Mwalimu Shule ya Msingi Ipyana, Kyela

Raisi yupi aliyesoma shule ya Msingi Ipyana?
SAM_2238.JPG

Moja ya nyumba za walimu katika shule ya msingi Ipyana wilayani Kyela mkoani MbeyaHali ya nyumba za walimu katika shule hiyo ni mbaya kama inavyoonekana hapa

SAM_2239.JPG

Hili ni dirisha lenye kioo cha bati

Picha kwa hisani ya Gordon Kalulunga
 
kijijini utapata wapi nyumba za kupanga na shule zilivyo mbali kwanza kwa mshahara gani?

Tatizo kuna watu wamezaliwa upanga na wakakulia hapo maisha yao yote, kwa wao ni vigumu kujua hali zetu za vijijini zikoje ndiyo maana wanashauri walimu wapange nyumba
 
Acha tupate tabu watanzania mpaka ifike mahali mtu akipaza ''ppoooz!'' , badala ya kuitikha 'power' , tutakua tunakaa chini na kumwaga machozi kiukweli !
 
SAM_2238.JPG

Moja ya nyumba za walimu katika shule ya msingi Ipyana wilayani Kyela mkoani MbeyaHali ya nyumba za walimu katika shule hiyo ni mbaya kama inavyoonekana hapa

SAM_2239.JPG

Hili ni dirisha lenye kioo cha bati

Picha kwa hisani ya Gordon Kalulunga
K


ioo cha bati???? Hii kali!!!!! Sijawahi kusikia kioo cha bati toka nizaliwe!!!!!
 
SAM_2238.JPG

Moja ya nyumba za walimu katika shule ya msingi Ipyana wilayani Kyela mkoani MbeyaHali ya nyumba za walimu katika shule hiyo ni mbaya kama inavyoonekana hapa

SAM_2239.JPG

Hili ni dirisha lenye kioo cha bati

Picha kwa hisani ya Gordon Kalulunga

Inatia simanzi sana kama ukilifikiria kwa undani suala la walimu. hebu angalia nyumba hizo; natumai umefika wakati wa walimu wenyewe kutumia ushujaaa kama wa Mgaya kwa kuuungana na kukataa kuendelea kutaabika chini ya mwamvuli wa CCM: Dr Slaa alisema Elimu iwe bure kuna watu walimbeza sana. Leo Lowasa nae anasema hivyo hivyo kwamba yapo mapesa lukuki yaelekezwe kwa shule na walimu wake huenda suala hilo likapungua kama sio kumalizika. Kwa maneno mengine Uongozi mpya unaotarajiwa katika mageuzi usisahau suala la walimu na mazingira yao
 
ndio sababu kuna serikali za vijiji; viongozi wa vijiji kwa kushirikiana na wanavijiji husika wanaweza kabisa kutatua tatizo hili serikali kuu haiwezi kuwa kwenye kila kijiji hili ni tatizo ambalo wananchi wenyewe kwa kushirikiana na wabunge wao wanaweza kulifanyia kazi wanakijiji wanaweza kujitolea kufyatua matofali ya kuchoma mbunge akatoa mabati, hali kadhalika wananchi kutoka vijiji wenye vijinafasi hatukatazwi kuchangia maendeleo ya vijiji vyetu. Mkuu Nguruvi3 umeacha siasa na kuwa mwanaharakati turudi kwenye siasa tujenge nchi yetu

Chama



Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums

mdau; fikra zako ni za nadhari na haziakisi uhalisia, fikra hii ni uhalalrishaji wa uzembe , kutowajibika na matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi.nani anamiliki shule za sekondari na shule za msingi?jibu ni halmashauri zetu, je hazipati fedha kutoka serikali kuu?na je halmashuri hizi hazikusanyi mapato?na mapato haya yanakwenda wapi?na kama hayatoshi afisa elimu na amaafisa mipango wameandika maandiko mangapi kushirikisha wadau ili kuboresha nyumba hizo?wananchi sawa kushiriki, sababu kuna kamati zao za shule , je zina mamlaka halisia kisheria na kiutendaji?au ni nyoka wa kibisa kama mfumo tu?Kimsingi serikali kwenye suala hili haiwezi kukwepa wajibu wake wa kujenga mazingira bora ya walimu kama nyumba bora na nzuri; sababu rasilimali zinazotakiwa ni kubwa, na uhamasishaji unatakiwa uwe wa kina, toshelezi , na madhubuti.na si hizi blabla za kipropaganda ki ccm kuwaghiribu wananchi, pesa za walipa kodi kutoka pato la taifa zinatengwa , watendaji wanaishia kumeza na kutengeneza ufisadi.haikubaliki kuwasukumia mizigo wananchi kwa uzembe na utendaji mbovu, ufujaji wa rasilimali, na uwajibikaji duni.
 
ndio sababu kuna serikali za vijiji; viongozi wa vijiji kwa kushirikiana na wanavijiji husika wanaweza kabisa kutatua tatizo hili serikali kuu haiwezi kuwa kwenye kila kijiji hili ni tatizo ambalo wananchi wenyewe kwa kushirikiana na wabunge wao wanaweza kulifanyia kazi wanakijiji wanaweza kujitolea kufyatua matofali ya kuchoma mbunge akatoa mabati, hali kadhalika wananchi kutoka vijiji wenye vijinafasi hatukatazwi kuchangia maendeleo ya vijiji vyetu. Mkuu Nguruvi3 umeacha siasa na kuwa mwanaharakati turudi kwenye siasa tujenge nchi yetu

Chama



Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums

mdau; fikra zako ni za nadhari na haziakisi uhalisia, fikra hii ni uhalalrishaji wa uzembe , kutowajibika na matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi.nani anamiliki shule za sekondari na shule za msingi?jibu ni halmashauri zetu, je hazipati fedha kutoka serikali kuu?na je halmashuri hizi hazikusanyi mapato?na mapato haya yanakwenda wapi?na kama hayatoshi afisa elimu na amaafisa mipango wameandika maandiko mangapi kushirikisha wadau ili kuboresha nyumba hizo?wananchi sawa kushiriki, sababu kuna kamati zao za shule , je zina mamlaka halisia kisheria na kiutendaji?au ni nyoka wa kibisa kama mfumo tu?Kimsingi serikali kwenye suala hili haiwezi kukwepa wajibu wake wa kujenga mazingira bora ya walimu kama nyumba bora na nzuri; sababu rasilimali zinazotakiwa ni kubwa, na uhamasishaji unatakiwa uwe wa kina, toshelezi , na madhubuti.na si hizi blabla za kipropaganda ki ccm kuwaghiribu wananchi, pesa za walipa kodi kutoka pato la taifa zinatengwa , watendaji wanaishia kumeza na kutengeneza ufisadi.haikubaliki kuwasukumia mizigo wananchi kwa uzembe na utendaji mbovu, ufujaji wa rasilimali, na uwajibikaji duni.
 
Makala hii ni kutoka gazeti la Rai mwema. Mwandishi ni Joseph Mihangwa. Shukrani kwa hisani.

KATIKA sehemu ya kwanza ya makala haya toleo lililopita la gazeti hili, tuliona jinsi Kampuni ya kifisadi iitwayo "Meremeta" ilivyoundwa bila kusajiliwa, mahsusi kwa ajili ya kukwapua mabilioni ya fedha kutoka nchini kupitia Benki Kuu (BoT) kwa ushirikiano wa watumishi wa ndani ya nchi na mafisadi wa nje, na kufanikiwa kukwapua zaidi ya shilingi bilioni 155. Tuendelee na sehemu hii ya leo.Kutokana na Kampuni ya Meremeta kujitangaza "mufilisi", lakini baada ya kukomba dhahabu zote za Buhemba, Buhemba Kusini, Nyamongo na Magunga, mbali na kukwapua bilioni 155/= kutoka Benki Kuu, iliundwa tume ya watu watano kuchunguza kampuni hiyo na kutoa mapendekezo serikalini.
Tume hiyo ilipendekeza kusitishwa shughuli za Meremeta, kununua dhahabu kutoka kwa wachimbaji wadogo, jukumu ambalo hata hivyo tayari ilikwishalitelekeza tangu mwaka 2003, na kujiingiza yenyewe katika uchimbaji na umiliki wa migodi niliyoitaja hapo juu.
Tume ilipendekeza pia kuanzishwa kampuni mpya ya kusimamia na kuendesha Mgodi wa Buhemba itakayomilikiwa na serikali tu.
Na kwa uzito wa mapendekezo ya tume hiyo ya Balali na wenzake tuliowataja hapo mwanzo, Meremeta ilifilisiwa, mali na madeni yake yalichukuliwa na Kampuni mpya ya "Tangold," inayodaiwa kumilikiwa na serikali, pia asilimia kwa 100. Na ingawa Meremeta (halisi) ilifungwa rasmi mwaka 2006 nchini Uingereza, shughuli zake hazikukoma nchini Tanzania wakati huo, kama tutakavyoona baadaye katika makala haya.
Hapa kuna utata mwingine, kwamba kumbukumbu zinaonesha kuwa, Kampuni ya Tangold ilianzishwa katika Visiwa vya Mauritius, Aprili 4, 2005; na kupewa Leseni ya Biashara Aprili 8, 2005 kama Kampuni binafsi. Lakini kumbukumbu nyingine zinaonesha kuwa, Tangold ilifungua Akaunti ya Benki Namba 011103024852, Tawi la Corporate Drive la NBC, Dar es Salaam, Januari mosi, 2003; kabla hata Tume ya Balali na wenzake haijaundwa kutatua tatizo la Meremeta.
Taarifa nyingine zimeonesha zaidi kuwa, Kampuni hiyo ni ya kigeni iliyosajiliwa nchini Mauritius na kupewa leseni nchini Tanzania, Februari 20, 2005 kama tawi la Kampuni ya kigeni; na ilianza kupatiwa fedha na BoT Agosti mosi, 2005 kwa kazi isiyojulikana.

Je, hii ina maana Tangold ilikuwapo Tanzania kabla ya kuanzishwa nchini Mauritius mwaka 2005, au ni aina fulani tu ya usanii? Hata kama ilikuwapo, iliwezaje kufungua Akaunti Benki, Januari mosi, 2003 ambayo ilikuwa Sikukuu ya Kitaifa ya Mwaka mpya? Kama ilikuwapo, kwa nini Tume ilipendekeza kuundwa kwa kampuni ambayo tayari ilikuwapo? Nini tofauti kati ya Tangold iliyofungua Akaunti Januari 2003, na Tangold iliyosajiliwa Mauritius April 4, 2005 kurithi Meremeta?
Ingawa mapendekezo ya Tume na tamko la Serikali yalikuwa kwamba, Tangold imilikiwe asilimia kwa mia na Serikali, utekelezaji wake ulikuwa kinyume chake, inaelekea wajumbe wa Tume iliyochunguza matatizo ya Meremeta, ndio hao hao waliogeuzwa au kujigeuza kuwa wakurugenzi wa kampuni hiyo mpya. Hao wanatajwa kuwa ni Daudi Balali, Gray S. Mgonja, Andrew Chenge, Patrick J. W. Rutabanzibwa na Vicent F. Mrisho.
Inawezekana, kwa mtazamo wa enzi hizo na kwa kusudio hilo, kwamba hao watano ndio walikuwa serikali yenyewe. Lakini kifungu cha saba cha Katiba ya ya Tangold kinatibua dhana yote hiyo, kinaposema, "Wenye hisa ya kampuni wanaweza kurithisha hisa zao kwa ndugu zao".

Je, ni kweli Tangold ilimilikiwa na Serikali asilimia mia kama ilivyopendekeza Tume ya Balali na kwa mujibu wa tamko la Serikali? Ni ndugu wapi hao wa serikali [kama kweli serikali ina ndugu binafsi!) waliostahili kurithishwa hisa za Serikali?.
Haya ni maswali magumu, na tunashawishika kuamini kwamba, huenda Tangold haikumilikiwa na Serikali asilimia mia; bali ilikuwa kampuni binafsi iliyorithishwa mali za Kampuni ya Meremeta.

Wakati matatizo ya Meremeta yakiendelea, na wakati huo huo tayari mapendekezo ya Tume ya Balali ya watu watano yakiwa yameanza kufanyiwa kazi; Machi 18, 2004 iliundwa Kampuni nyingine iitwayo "Deep Green Finance" [DGF], ambayo madhumuni na shughuli zake hazijafahamika vizuri mpaka sasa. Wakurugenzi wa DGF walikuwa ni Mark Ross Weston wa New Zealand; Antón Taljaard wa Afrika Kusini na Rudolf Van Schalkwyk, pia wa Afrika Kusini.

Wanahisa wa DGF walitajwa kuwa ni Protase R. G. Ishengoma, Stella Ndikimi wa Kampuni ya uwakili ya IMMA, ya jijini Dar es Salaam; Benki ya Nedbank Africa Investment Ltd ya Afrika Kusini (ambayo Mshauri wake, Michael G. Garner, ndiye pia alikuwa Mshauri huru wa Tume ya Balali yenye watu watano, iliyochunguza matatizo ya Meremeta na kupendekeza kuundwa kwa Tangold), na Kampuni ya SBM Nedcor Holdings, ambayo haijafahamika bado, kama ina uhusiano wowote na Kampuni ya Nedcor Trade Service, iliyolipwa na BoT malipo tata ya zaidi ya Sh. 155 kwa niaba ya Meremeta.
Wakurugenzi hao watatu wa Deep Green Finance, ndio waliokuwa Ma-Afisa pia wa NedBank; na jina la Deep Green limetumiwa mara nyingi na NedBank katika miradi yake mingine ya kijamii. Haifahamiki pia ni kwa vipi na kwa njia ipi, Watanzania wawili pekee, Protase Ishengoma na Stella Ndikimi, walitembelewa na bahati ya kununua hisa za kampuni yenye kumilikiwa na wageni kama hii (DGF); na kama ni kweli inavyodaiwa, kwamba hatimaye walichukua hisa (kwa njia ya kuhamishia au kununua) katika Nedbank Ltd na Nedbank Africa Investments, hapo Aprili 15, 2004.
Kama ilivyokuwa kwa Kampuni ya Tangold, iliyofungua Akaunti siku ya Sikukuu ya mwaka mpya; ndivyo ilivyokuwa kwa Kampuni ya Deep Green Finance, iliyofungua Akaunti Benki ya NBC, Na. 011103024840, tawi hilo hilo la Corporate Drive; safari hii ilikuwa Sikukuu (ya mapunziko) ya Mei Mosi, 2004.

Kuna utata pia kuhusu utoaji wa namba za Akaunti za Benki hiyo kwamba, Akaunti ya Tangold, Namba 011103024852, iliyofunguliwa Januari mosi, 2003, ni kubwa (kwa Akaunti 12 zaidi,011103024852 – 011103024840), ikilinganishwa na Akaunti Namba 01110302840 ya Deep Green Finance, iliyofunguliwa zaidi ya mwaka mmoja baadaye, Mei mosi, 2004. Je, ni utaratibu wa NBC kutoa namba za Akaunti kuanzia na namba (kubwa) za juu, kushuka chini? Kama sivyo, basi kuna walakini mkubwa kutufanya tuamini kwamba kulikuwa na mchezo mchafu, ikizingatiwa pia kwamba akaunti zote mbili zilifunguliwa siku za mapumziko ya Sikukuu za kitaifa.

Tangu Mei mosi, 2004 akaunti ya Tangold ilipofunguliwa, hadi Julai 31, 2005 (zaidi ya mwaka mmoja), hapakuwa na shughuli za DGF zilizoingiza fedha katika akaunti hiyo; hadi Agosti mosi, 2005 ilipoanza kupokea mabilioni ya fedha kutoka ama BoT, Deep Green Finance au Tangold, kwenda ama Deep Green Finance, Tangold, Meremeta, IMMA Advocates ya Dar es Salaam, au kwingine kusikojulikana.

Wakati imeelezwa Tangold ilianzishwa Aprili 5, 2005 na kupewa leseni ya biashara Aprili 8, 2005 kuchukua nafasi ya Meremeta, na mali na madeni ya Meremeta kuhamishiwa au kuchukuliwa na kampuni mpya kwa maana kwamba Meremeta ilikuwa imefilisiwa na kufungwa; lakini kumbukumbu zinaonesha kwamba, Oktoba 12, 2005, jumla ya Shs. 1,690,500,000 zilihamishwa kutoka Tangold kwenda Kampuni (mfu?) ya Meremeta; na vivyo hivyo Novemba 23 (Tshs. 555,300,048), na Desemba 12 (Shs. 551,060,000). Iliwezekanaje Meremeta kulipwa fedha hizo wakati ilikwishafilisiwa? Nani aliifufua na kwa utaratibu gani?.

Kwa kifupi, kati ya Agosti mosi, 2005 na Desemba 21, 2006, jumla ya Sh. bilioni 32 zilihamishwa kutoka Benki Kuu kwenda Deep Green Finance na Tangold; mbali na zile zilizopelekwa kusikojulikana. Tunashawishika kuamini, Deep Green Finance iliundwa kurahisisha na kuhakikisha utoroshaji wa fedha za Meremeta na Tangold kwenda nje ya nchi, na si kwa sababu nyingine yoyote ile.

Baada ya purukushani hizo, na kuonekana kwamba Mradi wa Tangold hauwezi kuendelea; Serikali iliuza haki za Mgodi huo kwa Kampuni ya "Rand Gold" ya Afrika Kusini, kwa bei ya chini ya soko, na kusababisha kwa Serikali hasara ya dola za Marekani milioni 100; na pia Serikali kutakiwa kulipa dola miliono 132 (adhabu na riba), kutokana na Serikali kudhamini wakopaji/wawekezaji waliofilisika, na hivyo kuachiwa mzigo wa kulipa madeni hayo ya kitapeli.

Huku ikielewa fika juu ya uporaji wa madini na ukwapuaji wa zaidi ya Shs. 55 uliofanywa na kampuni hizo za kitapeli; Serikali ya awamu ya tatu ilikubali na kuridhia "hasara" ya dola milioni 232 (Sh. bilioni 232) kwa Kampuni hizo. Na kwa kasi ya kushangaza na ya kutisha, Serikali hiyo ililipa madai hayo Oktoba 2005, mwezi mmoja tu kabla ya kumaliza muda wake wa kuwa madarakani.

Kwa hiyo, wanaodai kwamba kashfa ya Meremeta haizungumziki, eti kwa sababu inagusa mambo ya Usalama wa Taifa, ni waongo. Tunawataka wajichunguze kwanza kabla ya kusema, kisha watueleze hayo wanayatoa wapi; vinginevyo tutawahesabu wasaliti wa Taifa letu.

Wakati huo huo, ni maoni sahihi kwamba hoja ya Zitto Kabwe, juu ya kukwapuliwa kwa Sh bilioni 155 (pia Sh. bilioni 232) na kutoroshewa kwenye benki za nje ya nchi, ina uzito na mantiki ya kutosha. Kujaribu kuzuia au kuteka nyara hoja hiyo, ni kujipambanua au kujitangaza "adui wa umma" wa Kitanzania
My take: Bado tunashawishika kuwa serikali haina pesa za kujenga nyumba za walimu.
Bado tunashawishiwa kuwa Mwalimu ajenge nyumba yake siku moja baada kupata ajira.
 
Hakuna kipengele kinachomkataza mtumishi wa umma kupanga nyumba; au kujijengea kama haridhiki na nyumba aliyopewa na mwajiri wake.

Chama
Gongo la mboto DSM

Mkuu Mwalimu kupanga nyumba na mshahara upi?.........
 
Tutazungumza watasema ni upepo tu na utapita.

1. Wanakaa kwenye ma estate na ma mansion, wanafikia five stars hotels watafamu lini kuwa kuna maisha ya watu wa chini wanaolala kwenye nyumba za tope?

2. Barabara za rami zipo hadi chooni, 24/7 wapo angani lini watafahamu kuna barabara ya vumbi?

3. watoto wao wanasoma UK,Canada, USA lini watafahamu kuna St. Kayumba schools hazina madawati wala waalimu?

4. wana umeme majumbani kwao muda wote eti wanakaa kwenye special lines ambazo ni marachache umeme kukatika pia wanastandby generators lini watajua kuwa kuna mgao wa umeme?

5. Wana maccounts uswizi ya kuwalisha wao na watoto wwao na vijukuu vyao miaka nenda rudi lini watafahamu kuna watanzania wanakosa hata 200 ya unga?

6.watoto wao wanatembelea gari za Anasa wengine za serikali lini watafahamu kuwa Kuna wasiojiweza wanaohitaji hata baiskeli za gurudumu tatu?

7. Wanatibiwa India na UK lini watafahamu kuwa kuna hospital hazina wauguzi?

8. Magari yanassimamishwa wakiwa wanapita kwa raha zao lini watajua kwamba kuna foleni za gari waongeze barabara au watafute njia mbadala?

TUSIDANGANYANE: Hao viongozi wataishia kupiga kelele tutawajengea barabara,mara mgao wa umeme utaisha, ohh tutainua mfumo wa elimu mara hii mara lile lakini kutokana na sababu ya kwamba hawa experience tunayo experience sisi watu wa hali ya chini hata siku moja hawawezi leta maendeleo zaidi wataishia kuendelea kutunyonya na kuimagine kuwa tunaishi kama wao yani kwa kifupi wanaconclude kwamba wote tunaishi kama wao wanavoishi na hakuna haja ya maendeleo.

We ushawahi ona wapi mtu anakua kiongozi miaka 40, lini ataonja shida ndio maana wakiingia huko hawataki kutoka kwa sababu wanajua nini kiko juu huko. tubadilishane nao hata kwa muda wa saa 3 waje huku twende huko uone kama wakirudi hawatabadilisha maisha ya watu.

sio siri kuna vitu vinakera sana ila hata tukisema tuliowapa dhamana ya kututetea nao washajisahau wakifika huko wanakuwa na kale ka usemi "For God and for my Stomach" Badala ya "For God and for my people"

Vizazi vijavyo mtatusamehe kwa haya yafuatayo;


  • kushindwa kuwaandalia Tanzania ambayo mtaishi kwa raha.
  • Kushindwa kuzuia vitendo vya rushwa
  • Kushindwa kukemea maovu yanayofanyanywa na viongozi.
  • Kushindwa kuzuia unyonyaji wanaofanya wawekezaji
​
Mtusamehe tu walisema maisha bora kwa kila Mtanzania, tukawapa kura lakini matokeo yake yakawa maisha duni kwa kila Mtanzania.

As long as hayo hapo juu yapo tutaendelea kuwa masikini daima
Vizazi vijavyo mtatusamehe kwa kushindwa kuwa
 
Zakumi, sidhani kama kuna tatizo lolote kuifanya elimu yetu iwe ya ubora unaohitajika.
Na wala sidhani kuwa kuna umuhimu wa mwananchi anayelipa kodi sasa hivi kuchangia kwa kiasi hicho.

Tatizo letu kubwa ni kukosa nidhamu, kutowajibika, kutowawajibisha na kuogopa mabadiliko.
Miaka 50 baada ya uhuru bado tunahemea nje kwenye misaada hatujaweza ku-balance bajeti hata siku moja.
Miaka 50 baada ya uhuru bado serikali iliyopo inakusanya kodi kutoka katika vocha za simu, bia na sigara.

Haihitaji akili ya ziada kubaini kuwa ubunifu umefika mwisho na tunahitaji ubunifu mwingine.
Real? vocha ya simu ndiyo source of income kwa taifa lililojaa utajiri kama letu.

Mkuu Zakumi, pitia hesabu za CAG uone kiasi kilichopotea ndani ya miaka 10 kama si sawa na bajeti ya mwaka mzima ya nchi. Pitia matumizi ya serikali katika miaka 10 uone pesa za kufanya dhifa za kitaifa, makongamano ngurudoto na upuuzi mwingine halfu upate mahesabu.

Pitia wizi unaotokana na madini katika migodi kwa miaka 5 iliyopita.
Nenda bandarini kaangalie ukwepaji kodi kwa miaka 5 iliyopita.

Na mwisho pitia hazina uone pesa zinazopotea bila kujulikana, nenda BoT na kwingine ujionee miujiza.

Wakati hayo yakitokea bila majibu wala kuonyesha kushtuka tunaye Rais, Makamu na Waziri mkuu achilia majuha wengine. Wao afya zao zinachekiwa Uingereza na wana mafaili yao Appolo.
Si unajua ni kiasi gani kinatumika kutibu waheshimiwa kule India, South na UK.

Linapokuja suala la Walimu hilo tunaambiwa si tatizo la kitaifa. Piga mahesabu ya vitu nilivyokutajia hapo juu halafu uniambie ingechukua muda gani kujenga nyumba za Walimu.
Hatuhitaji kitu cha ziada, tunahitaji Viongozi wenye akili timamu ya kupanga na kusimamia nidhamu

Kuwaahidi walimu katika ilani ya uchaguzi halafu kuwaacha njia panda ndio theory ya kuwatumia kama toilet paper! nitty gritty.

Hatuwezi kuondoka hapa tulipo tukiendekeza hili genge la wahalifu lililopo.
Kama yupo mwendawazimu anayetaka kuongoza nchi hii mwenye mtizamo na fikra, hata kama nitaambiwa tatizo lake limetulizwa na dawa nitampa kura.

Hatuwezi kuwa na wahuni kwa miaka 50 halafu tusubiri matokeo tofauti.
Tumeambiwa kuwa kuna wizi umetokea, eti leo serikali inafanya kazi kwa kutumia tafiti za Zitto.Ni uhuni tu.
Sasa huyu anaweza kusimamia elimu kweli!

I know inauma sana lakini tuweni wakweli wa nafsi zetu. Tusidhulumu nafasi zetu kwa kujifanya hatusikii wala kuona. Tunajidanganya na kujifanya wapumbavu na wajinga bila sababu.

Huwezi kukamua kodi ya mkulima anyeishi kwa dola moja kwa siku ili iende kutibu watu Appolo, kusomesha watoto Cambridge na upuuzi mwingine, halafu tumshauri mkulima huyo huyo alipe kodi nyingine.

Tusijifanye wajinga huku tukielewa kuwa huwezi kumfunza mbwa mzee mbinu mpya.
Kufanya jambo lile lile kwa namna ile ile na watu wale wale kwa miaka 50 ni ujinga uliokithiri.

Ninarudia, hata kama mkoloni ataonyesha interest za kurudi, ili mradi kufanya hivyo kutaiondoa CCM madarakani nitakwenda uwanja wa ndege kumpokea nikiwa na matawi ya majani.

Endapo sitafanya hivyo, basi itabidi niwaombe walimu radhi kwasababu nami pia nitakuwa nimetumika kama toilet paper. Sipo tayari! Nimejifunza kutoka kwa walimu na ni kosa kurudia kosa.

Sitaidhukumu nafsi yangu wala kuidhalilisha akili yangu kwa kuamini kuwa baada ya miaka 50 kuna kipya kitatokea.
Mkuu Nguruvi3, usishangae kuona hii post yako wakina chama wanaikwepa kama vile hawaioni...ndivyo walivyo! CCM inapofusha macho, inadumaza akili na kulemaza viungo. Hebu fikiria mtu na akili zake timamu leo hii anathubutu kuisifia CCM kwa kuzaliwa upya kwa kupata viongozi wapya! Akina nani hao? Mang'ula, Kinana, Meghji na wengineo, duh!
 
Tatizo kuna watu wamezaliwa upanga na wakakulia hapo maisha yao yote, kwa wao ni vigumu kujua hali zetu za vijijini zikoje ndiyo maana wanashauri walimu wapange nyumba

Acha uwongo mwalimu vijijini upo kwenye net saa hizi! wote na mnaodandia kwenye hii mada mpo town mnapiga deal kama kawaida hamsemi ukweli walimu vijijini wapo poa na maisha yao; semeni advantages ukiwalinganisha na wajini; sikuchagua kuzaliwa upanga matokeo tu yamaisha
 
Back
Top Bottom