Picha.Mtihani wa Moko mkoa Mwanza ulitolewa kwenye gazeti la Elimu haina Mwisho kabla ya kufanyika

Lugogo

JF-Expert Member
Sep 16, 2013
304
67
Tukisema Elimu ya Tanzania CCM wameipeleka ICU wanafiki wanakataa na kuleta siasa kwenye Elimu.Mtihani wa utimilifu (mock) Darasa la saba mkoa wa Mwanza uliofanyika mei 21 na 22,2014 ulitolewa kwanza kwenye gazeti la Elimu haina Mwisho linalotolewa na kituo cha kisomo cha Taifa Mwanza.Magazeti hayo yalisambazwa mashuleni wiki moja kabla ya mtihani huo kufanyika.Tunaposema Kawambwa ni mzigo analindwa kwa undugu wa mzee wakaya wanaccm wanabisha.Mtihani huo pia swali la 32,25,na 27 hayakuwa na majibu.Mungu tunakuomba CCM washindwe uchaguzi wa 2015 chadema washinde aminaaaaaaaaaaaaa.
 

Attachments

  • DSC07459.JPG
    DSC07459.JPG
    649.8 KB · Views: 403
  • DSC07461.JPG
    DSC07461.JPG
    406 KB · Views: 336
  • DSC07463.JPG
    DSC07463.JPG
    403 KB · Views: 307
  • DSC07467.JPG
    DSC07467.JPG
    323.9 KB · Views: 318
  • DSC07472.JPG
    DSC07472.JPG
    454.2 KB · Views: 237
BRN at work. Subiri Waziri atakavyosimama kifua mbele akijigamba kuwa BRN inaleta mapinduzi katika elimu, ufaulu umeongezeka!!!!!!
 
Naomba kufahamu kwani gazeti inaonesha lilitoka desemba 2013 na kutoa chapisho hilo.

Yote ni yote nasikitika sana kwa kufanyiwa maigizo katika elimu yetu. hii ni makusudi ili kutaka watoto wetu washindwe kushindana katika soko la ajira. ni majanga matupu.
 
Jamani hali ya Tanzania yetu ni mbaya katika nyanja zote, sie elimu, si uchumi, si afya, etc, kwa kweli hali inasikitisha. Taifa linaangamia, CCM wanasifiana. Viongozi wetu hususani Rais na wabunge tuliowachagua wametusaliti, na wameamua kuungana kulihujumu taifa. Wananchi tumekosa nguvu na sauti ya "kudemand mabadiliko sasa" badala yake tunatumaini kuwa wanasiasa tutakaowachagua 2015 ndiyo watakaoleta mabadiliko tunayoyataka. Sasa sijui itakuwaje ikiwa nao watakuwa sawa na waliopo madarakani sasa.
 
Back
Top Bottom