PICHA: Mchezaji wa Manchester United, Paul Pogba akiwa Macca

Hujaona clip ya mashehe wamevaa kanvu wanacheza kishoga na wanatunzana hela?
Acha kukariri maisha,

Kanzu ni vazi na haliwakilishi dini ya mtu,Misri kuna wakristo wanavaa kanzu coz kanzu ni vazi lao,Iraq ina wakristo wanavaa kanzu,Lebanon kuna wakristo wanavaa kanzu,Syria kuna wakristo wanavaa kanzu coz ni utamaduni wao,Nchi nyingi za middle east zinavaa kanzu coz ni vazi la utamaduni wao na moja ya sababu toka enzi na enzi ni kua kuna joto kali sana,

Acha kukariri kua kila anayevaa koti jeupe ni daktari,wengine ni wauza Bucha.
 
kwa hiyo sasa atakuwa alhaj paul au mmeshampa jina??
Kuna tofauti kati ya hija na umra, hija ni ibada ya siku maalum na sehemu maalum, na umra unaweza kuifanya muda wowote ila ni sehemu maalum, alichofanya Pogba ni umra kwa kuwa ni baada ya Ramadhani na hija hufanyika takriban siku sabini baada ya Ramadhani, huenda alishawahi kwenda hija huko nyuma hivyo akiitwa alhaj Paul haina neno kwa kuwa ameshafanya ibada hiyo huko nyuma.
 
Pogba ni muislamu mbona..ni wajibu wake kwa mujibu wa dini take...Ila I wonder how anakuwa na jina la kikristo kisha yeye ni muislamu??
Nadhani ni brand name tu ila akiwa huko kwenye dini yake analo jina lake,Mimi natokana na familia ya kikristo ila kwetu kuna Salim,Shaban Iddi na Halima so nadhani haya ni majina tu japokuwa huyatumia but imani siyo jina ni kuishi kile unachoamini kinakuelekeza kwa Mungu wako.
 
Yaani wewe ni tumbaf kabisa, hapo kuna ajabu? Samata alikuwa hapo juzi tu
Hata Samatta alifunguliwa thd hapa,sijaelewa point yako ni nini hasa? narudia tena,Pogba ni super star ni mtu maarufu,kila anachokifanya ni habari,hata akigombana na mkewe kama media zikijua zitaandika kama habari.
 
Sharia ya Kiislam ndiyo hukumu pekee inayompa fursa aliyeuwa kusamahewa na warithi.

Ukiona mtu kauliwa ujuwe warithi walikataa kumsamehe, walikataa fidia na wakaamua auliwe. Kumbuka ni warithi hao wenye maamuzi anapokutikana mtu na hatia.

Tena nchi zingine zinazofata sharia inatakiwa hao warithi ndiyo watimize hiyo hukumu na siyo kama kuna muuaji kaajiriwa alipe kisasi. Hii hupelekea 99% kutoweza kutimiza na kuishia au kusamehe au kuchukua fidia.

Kwa upande mwengine sasa, Tazama sheria yetu. Muuaji akikutwa na hatia anauliwa Kwa kunyongwa. Hakuna anaeweza kumsamehe isipokuwa Rais pekee na 99% hawajawahi kusàmehewa.

Pia huku kwetu kuna "mob justice" kibaka anaweza kupora simu tu, watu kama wewe mkampiga na kumuua hata kufikia kumchoma moto. Na hakuna anaechukuliwa hatua yoyote. Thubutu uuwe mwizi nchi za sharia.

Usome Uislam kijana, ni mwema sana usije na mihemko tu ya chuki za kujazwa ujinga.
Hahah grandma.............

You must be kidding,aliyeuwa anasamehewa na warithi?kivipi?hakika bora kuwa mpagani au kusoma gazeti la katuni kuliko kusoma kitu kama hiko.
 
Hahah grandma.............

You must be kidding,aliyeuwa anasamehewa na warithi?kivipi?hakika bora kuwa mpagani au kusoma gazeti la katuni kuliko kusoma kitu kama hiko.
Umeuliza maswali ili ufahamishwe kisha ukaleta dhihaka kabla hujafahamishwa ulichouliza!
huoni kua una tatizo kichwani mwako?

Iko hivi,mtu akiua anapohukumiwa kuuawa,wanaulizwa ndugu wa marehemu "warithi" wapo tayari kumsamehe muuaji ili akiepuke kifo au wamuache afe? na hizi hukumu huchukua muda mrefu kutekelezwa ili kutoa chance kwa warithi huenda wakaingiwa na imani na kusamahe.
 
Kwa hiyo cha ajabu ni nini hapo?
Mbona kama kila kitu akifanyacho ni habari mbona hujawahi kutuletea habari akienda haja?
Pogba ni mtu maarufu,kila akifanyacho ni habari,unataka Pogba awe kama wewe ambaye hata jirani yako tu hakujui? mnajitoa ufahamu kwa chuki mpaka mnaanza kuandika vitu vya kitoto!
 
Kwa hiyo cha ajabu ni nini hapo?
Wapi umeambiwa kua kuna kitu cha ajabu hapo?

Pogba hata leo tu akipakaa rangi nyeupe kwenye nywele zake itakua ni habari,wataandika Pogba abadili muonekano wake,japo hilo sio la ajabu na wengi wameshalifanya, Ronaldo alifuga vindevu kwenye World cup ikawa habari,leo hii Messi akikata ndevu itakua habari japo yeye hatokua wa kwanza kutokua na ndevu,Weka chuki zako pembeni ili uelewe,nimejitahidi sana kukufahamisha ila kama una chuki ya udini huwezi kuelewa.
 
Nilikuwa nataka urudi kwenye akili na ufahamu wako tu mkuu wala sina chuki yoyote ya kidini kuwa hakuna cha ajabu chochote kwa yeye kufanya takwa lake la kidini kiasi cha kufaa kuanzishiwa uzi hapa ili hali wapo mamilioni ya waislamu wafanyao hivyo

Wapi umeambiwa kua kuna kitu cha ajabu hapo?

Pogba hata leo tu akipakaa rangi nyeupe kwenye nywele zake itakua ni habari,wataandika Pogba abadili muonekano wake,japo hilo sio la ajabu na wengi wameshalifanya, Ronaldo alifuga vindevu kwenye World cup ikawa habari,leo hii Messi akikata ndevu itakua habari japo yeye hatokua wa kwanza kutokua na ndevu,Weka chuki zako pembeni ili uelewe,nimejitahidi sana kukufahamisha ila kama una chuki ya udini huwezi kuelewa.
 
Nilikuwa nataka urudi kwenye akili na ufahamu wako tu mkuu wala sina chuki yoyote ya kidini kuwa hakuna cha ajabu chochote kwa yeye kufanya takwa lake la kidini kiasi cha kufaa kuanzishiwa uzi hapa ili hali wapo mamilioni ya waislamu wafanyao hivyo
Mkuu kama umekukwaza huu uzi fumba macho pita kama hujauona vile kwani kila uzi lazima uchangie, we unadhani yote yanayoletwa humu hatuyajui. Ukiona sio newz piga chini
 
Umeuliza maswali ili ufahamishwe kisha ukaleta dhihaka kabla hujafahamishwa ulichouliza!
huoni kua una tatizo kichwani mwako?

Iko hivi,mtu akiua anapohukumiwa kuuawa,wanaulizwa ndugu wa marehemu "warithi" wapo tayari kumsamehe muuaji ili akiepuke kifo au wamuache afe? na hizi hukumu huchukua muda mrefu kutekelezwa ili kutoa chance kwa warithi huenda wakaingiwa na imani na kusamahe.

Sasa kama mrithi/warithi wakasamehe wauwaji Mungu nae atafanya kazi gani?huoni ulichoandika paragraph ya mwanzo kwenye post yako kikikurudi?
 
Nilikuwa nataka urudi kwenye akili na ufahamu wako tu mkuu wala sina chuki yoyote ya kidini kuwa hakuna cha ajabu chochote kwa yeye kufanya takwa lake la kidini kiasi cha kufaa kuanzishiwa uzi hapa ili hali wapo mamilioni ya waislamu wafanyao hivyo
Wewe ndiye unayetakiwa urudi kwenye ufahamu wako na akili zako,sasa ndio nimeelewa kua kumbe hii habari imekua ni mwiba kwako na imekuuma sana,
Hakuna jipya chini ya jua,so una maanisha JF ifungwe coz kila thd itakayoletwa hivyo vitu vimeshafanyika or happen somewhere? una umri gani kwanza? isije ikawa nahangaika na kitoto cha shule! the way unavyobuild arguments zako inanipa wasiwasi,ndio maana nimejaribu kukukadiria energy za kukujibu,naweza tumia so much energy unneccessary.
 
Uzi ukishawekwa hapa jukwaani kila mmoja ana haki ya kuchangia kama ulikuwa una lengo la wengine wafumbe macho ungeweka tahadhari hiyo pia
Mkuu kama umekukwaza huu uzi fumba macho pita kama hujauona vile kwani kila uzi lazima uchangie, we unadhani yote yanayoletwa humu hatuyajui. Ukiona sio newz piga chini
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom