Mwenyekiti wa kamati ya bunge wa Ardhi, maliasili na Mazingira, James Lembeli, (kushoto) akiwa na mbunge wa Ngorongoro, Saning'o Ole Telele pamoja na wabunge wengine wa kamati hiyo, wakikagua ujenzi wa shule ya Sekondari Nainokanoka unaoendelea ndani ya Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro, ambapo
Wachezaji wa timu ya Kinesi Boys,wakiwa katika mazoezi ya kujiandaa na mashindano ya Ligi ya TFF,ngazi ya Wilaya kwenye Uwanja wa Kinesi jijini Dar es Salaam.Picha na Michael Matemanga
Abiria wa mamlaka ya Reli Tanzania na Zambia (Tazara) wakisubiri hatima ya safari yao baada ya wafanyakazi kuzuia usafiri huo kutokana na kutolipwa mishahara yao.
Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza na wanachama na wapenzi wa Chama hicho katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Magirisi Melinne, jimbo laMwanakwerekwe..
Abiria wakiwa kwenye foleni ya kupanda treni katika kituo cha Stesheni kwenda Ubungo jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Usafiri huo umesaidia kwa kiasi fulani kupunguza tatizo la usafiri jijini.
Wanafunzi wa Chuo Kikuu huria tawi la Kinondoni, wakiwa na mabango yanayopinga kupanda kwa bei za ada ya mitihani ambapo badala ya kulipa 30,000 kwa masomo yote wanatakiwa kulipa 5,000 kwa somo.
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam, Sheikh Ponda Issa Ponda akiwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliyopo jijini Dar es Salaam kusikiliza shauri linalomkabili jivi karibuni.
Mjasiliamali kutoka Arusha akipanga vizuri bidhaa zake wakati wa maonyesho yao yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Picha na Rafael Lubava
Wananchi wakiwa wamejificha mvua kwenye kituo cha kuuzia mafuta eneo la ubungo mataa jijini Dar es Salaam ambapo ni hatari kwa usalama wao. Picha na Michael Jamson
kijana akichoma moto chuma ikiwa ni hatua mojawapo ya kutengeneza zana za kilimo na ujenzi katika kijiji cha Itahwa kata Karabagaine Bukoba vijijini . Baadhi ya vifaa vinavyotengenezwa ni nyundo, majembe, kotama, visu, mikuki na mapanga.
Mgambo wakiwa katika gwaride wakipita mbele ya Afande mkuu wa wilaya ya Chemba, Francis Mtinga walipokuwa wakifunga mafunzo yao ya ukakamavu ili kuifanya kazi yao vizuri hivi karibuni.
Mkazi wa kijiji cha Kiraeni, Wilaya ya Rombo, Mkoa wa Kilimanjaro akikokota baiskeli kwenda kutafuta maji ambapo eneo hilo linatatizo la maji kwa muda mrefu na wananchi wake hutumia muda mwingi kutafuta huduma hiyo. Picha na Dionis Nyato
Mkazi wa Mwasanga jijini Mbeya Sosteli Mponzi (kulia) akimuonyesha Mshauri wa wanafunzi wa chuo kikuu cha Mzumbe tawi la MbeyaVictoria Zitta Mnyanyi moja ya nyumba za kale iliyokuwa inatumiwa na kabila la wasafwa mkoani humo. Mponzi ameamua kujitolea kujenga kituo cha utamaduni wa kabila hilo
Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Magesa Mulongo akimtwisha ndoo ya maji mkazi wa Tangeru juzi baada ya kuzindua kisima cha maji kilichochimbwa na Kanisa la International Evangelism (IEC) Sakila kwenye hospitali ya wilaya ya Meru,mkoa wa Arusha,kisima hicho kimegharimu Sh. 19ml. kulia ni Askofu Mkuu wa
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.