Picha : Mashabiki Mbeya City wamfariji mchezaji wa Simba, Alex Christopher Massawe

Orketeemi

JF-Expert Member
Feb 12, 2013
4,310
10,010
Mashabiki wa mbeya city wamepitia nyumbani kwa mchezaji wa zamani Christopher Alex mjini dodoma wakati wakitoka mwanza na kumjulia hali pamoja na kumpatia kiasi cha shilingi 200,300
 

Attachments

  • 1.jpg
    1.jpg
    54.1 KB · Views: 1,378
  • 2.jpg
    2.jpg
    49.9 KB · Views: 1,312
  • 3.jpg
    3.jpg
    62.6 KB · Views: 1,281
Mchezaji wa Simba......
Mchezaji wa zamani wa timu kadhaa ikiwemo Simba
 
Daaah pole Alex,mungu akuponye haraka,kipi kimsumbuacho huyu fundi wa kitambo?,Simba wamefanya nini kumsaidia?,ina maana wamemsahau?,nakumbuka alipiga penati ya kuwatoa Zamarek kule Cairo miaka ile...Wachezaji wanaotamba sasa kuna kitu cha kujifunza hapa....Bongo soka hovyo sana.
 
mbarikiwe sana mbeya city fans. upendo mlio nao umetushangaza...... wanasimba na team nyingine tafadhar angalien jambo hili kwa mchezaji wetu wa zamani. kibinadamu tu si kwa kuwa mnadaiwa au whatever.
 
Daaah pole Alex,mungu akuponye haraka,kipi kimsumbuacho huyu fundi wa kitambo?,Simba wamefanya nini kumsaidia?,ina maana wamemsahau?,nakumbuka alipiga penati ya kuwatoa Zamarek kule Cairo miaka ile...Wachezaji wanaotamba sasa kuna kitu cha kujifunza hapa....Bongo soka hovyo sana.

Wana akili za kujifunza?
 
pole sana chriatopher kimsingi simba wajaribu kukumbuka mchango wake wamsaidie matibabu. mungu ni mwema utapona
 
Iwe funzo kwa wachezaji wa bongo yaaani hizi timu za kariaako hazina maana kabisa unakuwa na thamani wakikutumikksha ukiastafu Hawakujali
 
Dah! Aiseee! Hawa wachezaji wa sasa wajifunze kitu hapa. Inasikitisha mchezaji wa zamani kusahaulika kiasi hiki.
 
Christopher atakua anajiskia vibaya mno.....maana simba imemtupa kabisa na aliisaidia mengi...lakini kitakachomuumiza zaidi ni kutekelekezwa na baba yake mzazi....Tajiri na Mkongwe katika underworld east africa ...mkibosho Alex Massawe...a.ka carlos alieko jijini jo'burg akiponda raha...
 
Wachezaji na wanamuziki wasijisahau sana na kuponda raha! Kujisahau kuwekeza hasa kijumba cha kujisitiri!
 
Mashabiki wa mbeya city wamepitia nyumbani kwa mchezaji wa zamani Christopher Alex mjini dodoma wakati wakitoka mwanza na kumjulia hali pamoja na kumpatia kiasi cha shilingi 200,300

Pole sana mkuu christopher ALLEX nakukumbuka kipindi kile ulivyokuwa unapiga soka na kina pawasa , quresh Ufunguo, Kaseja, Matola, mpaka watangazji wa soka wanasema "mchaga wa kwanza kuchezea taifa staz" hakika hujafa hujaumbika , nakuombea kwa MOLA akiupe moyo wa faraja na matumaini katika kipindi hiki kigumu unacho pitia.
Pia mashabiki wa mbeya city hongereni sana kwa uzalendo wenu bila kujali upinzani wa kisoka.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom