PICHA: Majengo marefu zaidi Duniani, Jengo la kwanza lipo Dubai(UAE), China yaongoza kuwa na majengo mengi marefu Duniani

Katika pitapita zangu mitandaoni, nikapita forum kubwa zaidi Dunia(Skyscraper City forum) nikakutana na uzi katika miongoni mwa sub forum huko ukizungumzia majengo marefu katika miji husika.

Nikavutiwa, nikaamua kutafuta orodha ya majengo marefu zaidi Duniani. Nikabahatika kupata Top 100 Tallest Buildings.

Jengo refu kuliko yote Duniani linaitwa Burj Khalifa lipo Dubai lina urefu wa Mita 828, floors 163.

La pili linaitwa Shanghai Tower lipo Shanghai (China) lina urefu wa mita 632, floors 128.

La tatu linaitwa Makkah Royal Clock Tower lipo Mecca (Saudi Arabia) lina urefu wa mita 601, floors 120.

La nne linaitwa Ping An Finance Center lipo Shenzhen(China) lina urefu wa mita 599.1, floors 115.

La tano linaitwa Lotte World Tower lipo Seoul(Korea Kusini) lina urefu wa mita 554.5, floors 123.

China ina majengo mengi zaidi marefu Duniani, ina jumla ya majengo 49 ambayo yapo top 100 Duniani, Jiji la Shenzhen linaongoza kwa kuwa na majengo mengi(majengo 8) zaidi kati ya majiji 19 nchini China yanayojumuisha majengo 49 marefu zaidi Duniani.

Nchi ya pili kuwa na majengo mengi marefu Duniani ni Arab Emirates(Falme za Kiarabu) , ina jumla ya majengo 21 marefu Duniani .

Nchi ya tatu kuwa na majengo mengi marefu Duniani ni Marekani, ina jumla ya majengo 15 marefu zaidi Duniani.

Nchi zingine zenye majengo marefu zaidi Dunia ni Taiwan(2), Vietnam(1), Malaysia(3), Kuwait(1), Urusi(3), Thailand(1) na Australia(1).

Matumizi makubwa ya haya majengo ni kwa ajili ya Ofisi, Hotel na Makazi ya watu.

Afrika hamna jengo hata moja ambalo lipo top 100, sijui tunakwama wapi?

NB: Wahandisi mtatusaidia kufafanua, kuna majengo mengine ni marefu zaidi lakini yana Floors chache na kinyume chake, mfano: Ping An Finance Center ni refu kuliko Lotte World Tower lakini lina floors chake kuliko Lotte World Tower.

View attachment 1093932View attachment 1093933View attachment 1093934View attachment 1093935View attachment 1093936View attachment 1093950
Kwann waingereza huwa hawana majengo marefu?
 
Ujenzi wa majengo marefu huwa unatokea wakati wa "economic boom" na uchumi ukipoa na ujenzi wa sky scrapper nao unasimama. Hapa Tanzania second term ya Mkapa uchumi uliimarika ndipo majenga kama Mafuta house lililoanza enzi za 2nd term ya Mh. Mwinyi lilimaliziwa na PPF tower na Twin tower za BoT zilijengwa. Enzi za Kikwete mambo yaliendelea kuwa mazuri na majengo yakajengwa mengi tena nchi nzima.

Magufuli term yake ya kwanza inaisha hakuna hata jengo moja refu limejengwa. Yaliyopo marefu na yanayoendelea kumaliziwa yote yalianza enzi ya JK.

Kumbuka Mkapa kwenye utawala wake ndipo lilijengwa jengo refu kuliko yaliyokuwepo na JK akajengwa marefu kuliko ya enzi za Mkapa. Kwa Magufuli hamna ujenzi wowote wa majengo marefu.
Awamu ya 5 eti inaisha na hakuna hata jengo moja refu! Hivi kuwa na jengo refu kunatusaidia nini sisi wananchi wa kawaida?
 
Back
Top Bottom