Jua linachelewa kuzama.Why?
Je majengo mafupi zaidi Duniani yanapatikana wapi?
Majengo mafupi zaidi duniani yako ktk mji wa kibera nchini kenya
Mm nikisimama tu kwenye 2nd floor napata kizunguzungu huko kwenye hayo magorofa yataka moyo.
Tumezoea matembe yetu.
Wanasemaga mambo hujulikana mbele kwa mbele
Kwann waingereza huwa hawana majengo marefu?Katika pitapita zangu mitandaoni, nikapita forum kubwa zaidi Dunia(Skyscraper City forum) nikakutana na uzi katika miongoni mwa sub forum huko ukizungumzia majengo marefu katika miji husika.
Nikavutiwa, nikaamua kutafuta orodha ya majengo marefu zaidi Duniani. Nikabahatika kupata Top 100 Tallest Buildings.
Jengo refu kuliko yote Duniani linaitwa Burj Khalifa lipo Dubai lina urefu wa Mita 828, floors 163.
La pili linaitwa Shanghai Tower lipo Shanghai (China) lina urefu wa mita 632, floors 128.
La tatu linaitwa Makkah Royal Clock Tower lipo Mecca (Saudi Arabia) lina urefu wa mita 601, floors 120.
La nne linaitwa Ping An Finance Center lipo Shenzhen(China) lina urefu wa mita 599.1, floors 115.
La tano linaitwa Lotte World Tower lipo Seoul(Korea Kusini) lina urefu wa mita 554.5, floors 123.
China ina majengo mengi zaidi marefu Duniani, ina jumla ya majengo 49 ambayo yapo top 100 Duniani, Jiji la Shenzhen linaongoza kwa kuwa na majengo mengi(majengo 8) zaidi kati ya majiji 19 nchini China yanayojumuisha majengo 49 marefu zaidi Duniani.
Nchi ya pili kuwa na majengo mengi marefu Duniani ni Arab Emirates(Falme za Kiarabu) , ina jumla ya majengo 21 marefu Duniani .
Nchi ya tatu kuwa na majengo mengi marefu Duniani ni Marekani, ina jumla ya majengo 15 marefu zaidi Duniani.
Nchi zingine zenye majengo marefu zaidi Dunia ni Taiwan(2), Vietnam(1), Malaysia(3), Kuwait(1), Urusi(3), Thailand(1) na Australia(1).
Matumizi makubwa ya haya majengo ni kwa ajili ya Ofisi, Hotel na Makazi ya watu.
Afrika hamna jengo hata moja ambalo lipo top 100, sijui tunakwama wapi?
NB: Wahandisi mtatusaidia kufafanua, kuna majengo mengine ni marefu zaidi lakini yana Floors chache na kinyume chake, mfano: Ping An Finance Center ni refu kuliko Lotte World Tower lakini lina floors chake kuliko Lotte World Tower.
View attachment 1093932View attachment 1093933View attachment 1093934View attachment 1093935View attachment 1093936View attachment 1093950
Linaweza kuwa Dodoma kwenye nyumba za tembe au Greenland kwenye Igloos za Waeskimo. Sina uhakika kati ya Watu Dodoma na Waeskimo nani anashika jaki poti kwa kujenga nyumba fupi.Je majengo mafupi zaidi Duniani yanapatikana wapi?
Ndiyo inawezekana kwa sababu usawa wa ardhi (ground floor) jua likizama kule juu linakuwa bado linaonekana. Waislam wa Dar wanafuturu kwanza kabla ya wa Kigoma.
Kule ni self contained, jambo kama hilo sidhani kama linaweza kutokea
Pyongyang, Seoul ulikua huyajui? Hapo ndo mzazi wangu alisoma Msc. In Electronics engineeringNilikuwa sijui kama kuna jiji linaitwa Seoul, kwa sasa nishalijua.
Mengine changanya na zako.
ShinyangaJe majengo mafupi zaidi Duniani yanapatikana wapi?
Awamu ya 5 eti inaisha na hakuna hata jengo moja refu! Hivi kuwa na jengo refu kunatusaidia nini sisi wananchi wa kawaida?Ujenzi wa majengo marefu huwa unatokea wakati wa "economic boom" na uchumi ukipoa na ujenzi wa sky scrapper nao unasimama. Hapa Tanzania second term ya Mkapa uchumi uliimarika ndipo majenga kama Mafuta house lililoanza enzi za 2nd term ya Mh. Mwinyi lilimaliziwa na PPF tower na Twin tower za BoT zilijengwa. Enzi za Kikwete mambo yaliendelea kuwa mazuri na majengo yakajengwa mengi tena nchi nzima.
Magufuli term yake ya kwanza inaisha hakuna hata jengo moja refu limejengwa. Yaliyopo marefu na yanayoendelea kumaliziwa yote yalianza enzi ya JK.
Kumbuka Mkapa kwenye utawala wake ndipo lilijengwa jengo refu kuliko yaliyokuwepo na JK akajengwa marefu kuliko ya enzi za Mkapa. Kwa Magufuli hamna ujenzi wowote wa majengo marefu.