Picha: Inasikitisha sana! Jaji ashiriki kuhujumu uchumi wa nchi. DPP chukua hatua

nzagambadume

JF-Expert Member
Apr 9, 2018
2,430
5,769
Ona jinsi huyu Jaji namba 62 alivyokosa uzalendo kwa nchi yake,ni majuzi tu kijana mchapakazi,mnyenyekevu,muadilifu,higly intelligent RC Gambo alitoa amri kwa Jeshi la Polisi kuwakamata watanzania wanaotumiaka na mabeberu kuhujumu uchumi wa nchi kwa ku post kinachodaiwa eti ni barabara mbovu huko Ngorongoro

Kauli hiyo ya kijana huyo mpendwa wa mkuu wa nchi ilipokelewa haraka kwa utekelezaji na RPC mzalendo namba moja East Africa nzima,RPC mnyenyekevu, asiyejilimbikizia mali na anayefanya kazi kwa uadilifu bila kubagua wananchi kwa itikadi za vyama,RPC Shana ambaye ameahidi kuwashughulikia wote waliopost picha hizo hadi wachakae

Wakati wazalendo hao wa jiji la Arusha wakipambana kuhakikisha nchi inashinda vita hivi vya kiuchumi cha kushangaza Jaji namba 62 wa nchi hii anapost picha kama hii!

Natumai DPP atamfikisha Mahakamani haraka kwa uhujumu uchumi. Kishindo cha awamu ya tano kimesikika kote Duniani sema kuna watu wanatumika na mabeberu kuonesha kwamba tuna barabara mbovu kwa kupost vipicha vyao

Screen Shot 2020-02-18 at 4.42.10 PM.png
 
Ona jinsi huyu Jaji namba 62 alivyokosa uzalendo kwa nchi yake,ni majuzi tu kijana mchapakazi,mnyenyekevu,muadilifu,higly intelligent RC Gambo alitoa amri kwa Jeshi la Polisi kuwakamata watanzania wanaotumiaka na mabeberu kuhujumu uchumi wa nchi kwa ku post kinachodaiwa eti ni barabara mbovu huko Ngorongoro

Kauli hiyo ya kijana huyo mpendwa wa mkuu wa nchi ilipokelewa haraka kwa utekelezaji na RPC mzalendo namba moja East Africa nzima,RPC mnyenyekevu, asiyejilimbikizia mali na anayefanya kazi kwa uadilifu bila kubagua wananchi kwa itikadi za vyama,RPC Shana ambaye ameahidi kuwashughulikia wote waliopost picha hizo hadi wachakae

Wakati wazalendo hao wa jiji la Arusha wakipambana kuhakikisha nchi inashinda vita hivi vya kiuchumi cha kushangaza Jaji namba 62 wa nchi hii anapost picha kama hii!

Natumai DPP atamfikisha Mahakamani haraka kwa uhujumu uchumi. Kishindo cha awamu ya tano kimesikika kote Duniani sema kuna watu wanatumika na mabeberu kuonesha kwamba tuna barabara mbovu kwa kupost vipicha vyao

View attachment 1361979
Umeeleweka!
 
Back
Top Bottom