Picha husema bila maneno. Tunakoelekea ndiko huko picha hii inakotuelekeza. Yaliyopita pia yanaonekana kwenye picha hii.
Tanzania tunayoelekea ni Tanzania ya mazungumzo na maelewano. Ni Tanzania ya demokrasia na sio Tanzania ya kiburi na maamuzi binafsi.
Mwanga utajadiliana na giza, na demokrasia itang’ara zaidi kuliko uhafidhina. Wasiopenda demokrasia wataachwa nyuma na hawatakuwa na marafiki, watafifia na kusahaulika.
Angalia, atakayetuongoza miguu yake imetangulia wengine, kavaa kama askari wa demokrasia, anajua siasa si uadui.
Alivyosimama, anaonekana ni mwamba anayewategemeza wengine. Anasikiliza hekima za watangulizi wake kwa unyenyekevu, ataongeza na hekima zake mwenyewe na atatuvusha! Mungu ibariki Tanzania na watu wake.
Tanzania tunayoelekea ni Tanzania ya mazungumzo na maelewano. Ni Tanzania ya demokrasia na sio Tanzania ya kiburi na maamuzi binafsi.
Mwanga utajadiliana na giza, na demokrasia itang’ara zaidi kuliko uhafidhina. Wasiopenda demokrasia wataachwa nyuma na hawatakuwa na marafiki, watafifia na kusahaulika.
Angalia, atakayetuongoza miguu yake imetangulia wengine, kavaa kama askari wa demokrasia, anajua siasa si uadui.
Alivyosimama, anaonekana ni mwamba anayewategemeza wengine. Anasikiliza hekima za watangulizi wake kwa unyenyekevu, ataongeza na hekima zake mwenyewe na atatuvusha! Mungu ibariki Tanzania na watu wake.