figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,483
- 54,851
Nadhani inabidi Watanzania tutoke hapa tulipo, na tujitambue, kwa maana kwamba, tuondokane na dhana ya kuitwa nchi masikini bila kutambua huu umasikini tunaotajwa ni upi. Tufike mahala tuwe SMART vichwani mwetu kama Watanzania wenye umasikini wa mali bali utajiri wa akili, japo nchi yetu ina rasilimali nyingi, ila tuangalie upande wa rasilimali watu kwanza.
Duniani, hasa kwa nchi zilizoendelea na zinazoendelea, hakuna mahali kunafanyika siasa za kipumbavu kama hizi zinazofanywa na hawa watu wanaojiita CHAMA CHA Mapinduzi. Kwa kuitazama picha hii hapo, ni wazi wananchi hao hawana wakijuacho kichwani, hawana malengo yoyote katika maisha yao, ni wananchi wanaoishi kwa sababu wapo, na wala hawana tumaini lolote in the near future.
Tunataka wananchi wanaomsikiliza mwanasiasa, wanamuuliza maswali, juu ya mipango ya nyuma ambayo haijakamilika, wanamuuliza juu ya mipango mipya, utekelezaji wa ahadi, wananchi wanaopima kama ahadi wanazopewa zinatekelezeka au hazitekelezeki, wananchi waliotayari hata kuandika ahadi zinazotolewa kwa kumbukumbu ya baadae, apate kuhoji na ajue ni wapi alidanganywa, ni wapi pameshindikana, ni nini cha kufanya.
Tanzania inataka Wananchi wanaoijua KATIBA ya nchi, ubora na mapungufu yake, haki zake, na sheria zinazomhusu, kama masuala ya uchaguzi, polisi, haki za raia, haki ya kuishi, uhuru wa mawazo nk. Wananchi wanaosikiliza kwa heshima na adabu kwa kujua kwamba huyu anayezungumza hapa mbele nikimpa ridhaa kwa kura yangu atakuwa mwakilishi na kiongozi wangu katika kutatua kero zote kwa kadiri ya makubaliano.
Niseme tu: Elimu na Akili ni vitu viwili tofauti, japo vikikutana hufanya kazi kubwa sana. Kuwa na akili kwatosha, kwani sio wote duniani wanakwenda kusoma shule mpaka elimu ya juu, tena kuwa na elimu pasipokuwa na akili ni kazi bure. Ila wote twahitaji kuwa na akili ya kutambua na kupambanua jambo, na kuona mbele.
Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wengi wao sifa hizi hawana, kama ionekanavyo katika picha hii, wengi wanaangalia kama amekula ugali mchana, inamtosha, kesho na mwaka kesho hajui, mtu kama huyu hawezi kutambua kuwa kodi zinamuelemea, hawezi kutambua umuhimu wa katiba kwa maisha yake, yeye atasubiri kuhongwa pesa na wagombea wake, akapige kura, apewe t-shirt ya kijani, apewe kofia, anunuliwe pombe, maisha yaendelee. Mia