Picha: Hali Inavyotisha Hospitali ya Muhimbili

Kwa kweli tukio kama hili halijawahi kutokea tangu tunapata Uhuru. Ni tukio la kihistoria ambalo kamwe halitasahaulika. Jambo la kushangaza Watawala hawana hata wasiwasi. Hivi tunaelekea wapi Watanzania? Serikali Kuu chini ya Rais na mawaziri hawazungumzi lolote. Bunge hali kadhalika hawataki hata lijadiliwe. Tukumbuke hao wabunge ndio tumewchagua hili watuwakilishe. Je Wananchi watakuwa na Imani na Serikali, Wabunge na atendaji wengine wa Serikali? Je kama nchi itaingia kwenye machafuko Viongozi wa Serikali wana la kujitetea? Je taasisi muhimu kama iIDARA YA USALAMA WA TAIFA kuna mnachomshauri Rais? Au mpo kwa ajili ya kuwadhibiti wapinzani tu kwenye chaguzi mbalimbali? Maana nasindwa kuelewa Nini maan ya IDARA YA USALAMA WA TAIFA. Ipo kwa ajili ya kulinda Uslama wa nani? Je hili haliwezi kusababisha Usalama wa nchi ukapotea? Basi kama hakuna majibu mazuri kwenye hili ni bora Idara hiyo Isiwepo kabisa. Nina hakika ujumbe huu mtaupata na kuufanyia kazi. Siku zote yanapotokea masuala kama haya mnasingizia Wapinzani ndio wachochezi? Je hili nalo mnalizungumziaje wamehusika? Ninyi kama Serikali mmeshachukua hatua gani tangu mgomo uanze takribani wiki tatu sasa?
 
Naona sasa mna tafuta wa kulaumu sio?
Vijana wa UDSM unajua walipo saivi au una ropoka tu?
Unadhani wao hawaumwi?
Kuna mwanafunzi ana kansa,....kafariki jana kwa sababu ya matibabu kusimama
toka week ilo pita ingawa hakua mbali na kifo hicho anyway.

Una lalamikia wanafunzi wa UDSM?
Unajua what they are going through right now baada ya kuandamana kudai haki zao?
Watu zaidi ya 150 wame fukuzwa,...did you do anything about that?

Bro,Tanzania ya sasa is everyone for him/herself.
Ukilia njaa na kulaumu serikali wenzako jirani wana sherehekea huwezi walaumu kwa
kusherekea kwao.

Yeah,ndio Tanzania yetu,...NO BROTHER HOOD.

Tatizo lako ni lako,...la jirani yako ni lake,....aliye tupa roho mbaya hii naona kaweza kweli
maana hata ugumu wa maisha ukisema saivi utaambiwa "fanya kazi,acha uzembe"

Wabunge wana jifikiria peke yao,...kwamba wao tu ndo wanaona maisha magumu.
Watu wamesoma hadi std7,form4 wanakula mamilioni kwa kulala bungeni,....
mwingine kasoma PCB kwa taabu kweli,masomo magumu kweli,..ana jitahidi kuokoa maisha
ya watu,...leo anadai nyongeza ya mshahara na mazingira mazuri ya kazi hakuna
wa kumsikiliza zaidi ya siasa tu.

Usitafute wa kumlalamikia kwanini watu hawajaandamana leo,wengine bado tunauguza virungu
vya FFU,....wewe una fanya nini?
Mda wa kutangulizana mbele kama mazuzu umepita,.....nitaandamana
pale tu tutakapo kuwa tuna kataa Kiongozi yeyote kwenda kutibiwa nje ya nchi.

HUJUI TU JINSI NINAVYO OMBA WABUNGE WAPATE AJARI,ILA WASIFE WAONJE CHA MOTO KWANZA
KWA MDA HUU.

Poleni sana wagonjwa,....Ni mapito tu.

tumefika hapa tulipo kwa sababu "kila mtu na lwake" ubinafisi.
 
halafu leo Pinda atatembelea hosp ya muhimbili napia atakuwa na vikao kadhaa , hivi kweli inaingia akilini ??? nadhani kabla ya kwenda muhimbili anatakiwa kwanza awajibishe baadhi ya watu ili aweae kuwaeleza wananchi nini kinatakiwa kufanyika
 
Ona mzee kama huyu kajitolea kuandamana lakini vijana wamejipinda kwenye laptop tu....wanafunzi wa UDSM nao kimya lakini linapofika swala la bumu wako makini kweli kweli...

...lakini kumbuka kuwa haya maandamano yameitishwa kwa muda mfupi sana tena hayakutangazwa sana isipokuwa kwenye mitandao ya jamii,sasa fikiria ni watu wangapi walikuwa na taarifa za uhakika juu ya hilo?
 
Aisee the hospital looks deserted, sitashangaa ikianza kazi utakuta vitu vingi hamna watu wamesha sabotage miundo mbinu.
 
More pictures from Muhimbili hospital

405827_318693284848499_129370793780750_963637_322825468_n.jpg



417282_318693308181830_129370793780750_963638_1902014866_n.jpg


418816_318693438181817_129370793780750_963640_68032707_n.jpg



424138_318693494848478_129370793780750_963641_1896594355_n.jpg


LHRC wakitafakari baada ya kuona hali halisi ilivyo

402631_318693548181806_129370793780750_963643_650928952_n.jpg


428256_318693571515137_129370793780750_963644_218317366_n.jpg


426753_318693628181798_129370793780750_963645_2011629004_n.jpg


432138_318693824848445_129370793780750_963651_2057943832_n.jpg



432098_318693854848442_129370793780750_963652_381356718_n.jpg



kuna watu wametulaumu kwa kugoma lakini tusingegoma mngeona maovu yanayofanyika mawodini?hivi yale mabilioni waliotumia kwenye sherehe za miaka 50 ya uhuru yasingeweza kuboresha sekta ya afya?hapo ndo mtakapojua priority ya serikali yetu ni matumbo yao na siyo maisha ya wananchi tuliowaweka kwenye hizo sehemu.
 
Tunashindwa nini kuwatimua hawa wapumbavu walio bungeni na Magogoni? Hii nchi ni yetu sio ya Mafisadi waliokuwa bungeni na Magogoni. Na mishahara wanaolipana ni kodi zetu. Hivi sisi watanzania tumerogwa na kina Kova au Mwema mpaka tuwaogope kutoka mitaani na kudai haki zetu? Haki haiombi Watanzania sasa, tufikie wakati tuweze kujitambua na kusema sasa basi imetrosha tumeyanyaswa sana na tumedhuliwa sana, tujikomboeni tusiwe wapumbavu na wajinga kila siku kupiga kelele na kusema sasa. Umefika wakati wa vitendo sio kupiga kelele tuamkeni kumeshakucha tuache ujinga na upumbavu wa woga

Akuroge nani?
Wewe hapo ulipo chukua hatua.Wenzako tumeshaonyesha njia.Hata kugoma huthubutu ndio itakuwa kuingia mtaani?
 
Kitu kimoja ambacho serikali hakikupigia mahesabu ni kuwa watu will turn against the government; wao walidhani watu waturn against the doctors "kwa kukosa uzalendo".. nilisema mwanzoni serikali "will lose" and in this case it is already losing![/QUOTE
"Kila system inapotaka kuanguka, hujitengenezea njia yake ya kuanguka"
Kitu ambacho serikali nailaumu ni kushindwa kukili tangu awali kuwa,ilikosea kutokuwalipa vijana wale kwa miezi mitatu,na hasa ukizingatia maisha ya Dar yalivyo magumu na mfumuko huu wa bei.Katika ajira hapa tayari mwajili anakua amebreach contract.lakini kwa sababu vijana wale Interns ,serikali liliwachukulia kama wanafunzi,haikujua umuhimu wao.Ukweli ni kwamba hawa vijana ndio huwa wanafanya sana kazi kuliko hao Doctors ambao muda mwingi wanautumia kwenye hospitali zao binafsi.Huwa wanakuja kusaidia pale tu ambapo vijana hawa uwezo wao unafikia kikomo.
Kama nimevuta kumbukumbu sawasawa,kuna mtu mwingine muhimu sana katika kuanzisha mgogoro huu, nae ni Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa,ya Muhimbili,ambaye baada ya vijana hawa kulipwa ile fedha yao,aliamua kuwatimua na kuwaambia waende wizarani.na hapa ndio pale alipokuwa ameshindwa "Kula na Kipofu"Suala hili lilikua ni dogo na wala tusingefika hapa tulipo,kama hawa vijana hela ndogo wanayohitaji kulipwa,ingekua inalipwa kwa wakati.Kuwacheleweshea malipo yao kwa miezi mitatu,halafu kuwanyanyasa kwa uzembe uliosababishwa na serikali yenyewe,kutowasikiliza wakati walipotaka kuongea na serikali,na pia hata mgomo ulipoanza, serikali kuleta propaganda kupitia vyombo vya habari kuwa hakuna mgomo na hali ni nzuri mahospitalini,kuanzisha propaganda za kuwadhihaki na kusema wengine hata hawajaidhinishwa kuwa madaktari,Kuwatishia kuwafukuza kazi na pia kauli tete za waheshimiwa wetu"ndio maana hata baba yangu alinikataza nisisomee udaktari" -Haya ndiyo mambo yaliyotufikisha hapa.
 
Wako wapi madaktari wa China, Cuba, India, na kule kwetu katavi? Sometimes we have to be serious in our thinking. Siasa haina majawabu ya kila matatizo yanayotuzunguka. Tanzania kazi pekee ya maana ni kuajiriwa kwenye wizara fulani fulani hivi, ingawa wabunge nao wameamua kijitwalia nafasi kwa kulazimisha...wengine wanaonekana sio wafanyakazi.
Yaani acha tu ndugu yangu, kibaraka mmoja anayejidai anatumia sana busara katika kujibu hoja, lakini wapii, anajiaibisha tu kwa kauli zake za kizandiki, kutoka katika kichwa chenye upeo finyu!
 
Duh hali inasikitisha wakuu
Ni jambo la kusikitisha kuacha hali kama hii ikiendelea kw amuda mrefu as if hatuna viongozi wanaojali afya za wananchi wake
hali kama hii huwezi kujizuia kulia machozi maana wanaoumia sana sana ni wale wasio na uwezo wa kwenda kwenye hospitali za binafsi au wasio na uwezo wa kwenda kutibiwa India
 
Tunaposema ccm na uozo wao waondoke mnabaki kusema hakuna chama mbadala wajinga kweli watanzania serikali ya ccm muendelee hivyo hivyo kutochukua hatua ili watu wafe tu wengi wengi tu ndiyo watanzania wataamka toka usingizini.kiburi cha wabunge ni ujinga wa watanzania hawaelewi shida yao ni pilau na tshirt na kofia,ccmk hoyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!

Nadhani tuna hitaji kukusanywa kwa pilau, kanga na fulana ili pia tuelimishwe kuhusu uozo wa uongozi wetu.
 
Its time to remove trash (CCM)........I hate you ccm na serikali yako ya kipuuzi pamoja na wabunge wako wanofikiria kwa kutumia masaburi :embarassed2:

jamani inatia uchungu sana lakini wao hawajui hii shida wanakula,kutibiwa nje ya nchi kwa kodi zetu.
 
nashangaa, mbona vyama vya upinzani vimepoa namna hiyo? kimyaaa

CCK tumekutana na Madaktari na kujua ukweli wa mambo, mgomo huu ulikuwa unakwisha, shida iko serikalini, Tarehe moja Februari baada ya kukutana na Madaktari tukaibeba hoja na mapendekezo ya kumaliza mgomo kwa Waziri wa Afya Haji Mponda, tukiamini kesho yake mambo yakekwisha lakini wapi. Madaktari wanataka kuwepo na Good-will hata kama serikali haina pesa, wanatambua serikali imefirisika kwa sababu ya wizi na ufisadi lakini, serikali ionyeshe tu usikivu, hilo nalo limeshindikana. NDG ZANGU CCM NA SERIKALI YAKE HAWAWEZI KUENDELEA AKUUA NDUGU ZETUTHE GOVERNMENT HAS TO STEP DOWN
 
naamini inatupasa kuchukua hatua zaidi kwani njia tumeiona , ngoja tusikie bla bla za Pinga anavyopindisha muhimbili
 
Hata tukisema sana haisaidii, tunawasihi watanzania kuandamana kupinga kiburi cha serikali vinginevyo tunakufa jamani. Hakuna haja ya kuogopa risasi
 
I have always told friends and my co-workers that, this is the beginning of the end! And now all eyes can clearly see that, CCM is already heading into a deep pit which I believe it shall die a natural death. However for all these to happen, we shall lose many of our beloved ones, through police brutality, army intervention, diseases (like the current situation at Muhimbili and elsewhere in the country). So ndugu zangu we should brace ourselves for the very very heavy loss of important relatives, husbands, wives, kids and friends. That’s how regime changes shall set in, lazima kuwe na agano!
 
Back
Top Bottom