Picha - Dodoma Capital City ever green, mawe pambo maridhawa.

Wewe, unajua maana ya ever green?
Nimeishi mkoa huo kwa miaka ishirini(20).....Idodomya, phew!
Nimewinda sana pimbi kwenye hicho kilima.
Acha tu nijibanze huku niliko.

dodoma29.jpg


Naijua Dodoma (Idodomya) kutosha, mlima huo ni karibu na Iringa Road kama sijashau. Hapa unaona Dodoma Airport ya miaka mingi sana tu upande wa kulia ni njia iendayo kule Msalato na ukitaka kuendelea hadi Kondoa-Babati-Arusha kazi kwako.

Nimeikumbuka Dodoma kuna wakati nimeendesha kwenye vumbi na mchanga gari toka Shinyanga - Nzega - Singida - Dodoma kwenya mashimo, mchanga, vumbi usiombe, ukiona tu Dodoma unajisikia uhueni kwani lami ndo ukombozi unajua Dar ni karibu. Safari nyingi bora kuzungukia Kwamtoro kwenda Singida utokapo Dodoma kuliko kupitia Manyoni balaa tupu.

Dodoma pazuri kama pangeendelezwa, na waliochagua hapo waliona mbali, ingekuwa Washington DC ya Afrika kama ilivyo Arusha mfano wa Jiniva ya Africa.

Ukiteremka kwa gari moshi pale station utachoka mwenyewe na zabibu nzuri hadi usahau kama uko safarini na kutamani safari ingeishia hapo.

Maji ndio tatizo, labda kama siku hizi wamelitatua, la sivyo ndoto za Mkapa kuyaleta ya kule Ziwa Nyanza ingekuwa ukombozi.
 
dodoma29.jpg


Naijua Dodoma (Idodomya) kutosha, mlima huo ni karibu na Iringa Road kama sijashau. Hapa kwa njia unaona Dodoma Airport ya miaka mingi sana tu upande wa kulia ni njia iendayo kule Msalato na ukitaka kuendelea hadi Kondoa-Babati-Asrusha kazi kwako.

Nimeikumbuka Dodoma kuna wakati nimeendha kwenye vumbi na mchanga gari toka Shinyanga - Nzega - Singida - Dodoma kwenya mashimo, mchanga, vumbi usiombe, ukiona tu Dodoma unajisikia umeahueni kwani lami ndo ukombozi unajua Dar ni kaziru. Safari nyingi bora kuzungukia Kwamtoro kwenda Singida utokapo Dodoma kuliko kupitia Manyoni balaa tupu.

Dodoma pazuri kama pangeendelezwa, na waliochagua hapo waliona mbali, ingekuwa Washington DC ya Afrika kama ilivyo Arusha mfano wa Jiniva ya Africa.

Ukiteremka kwa gari moshi pale station utachoka mwenyewe na zabibu nzuri hadi usahau kama uko safarini na kutamani safari ingeishia hapo.

Maji ndio tatizo, labda kama siku hizi wamelitatua, la sivyo ndoto za Mkapa kuyaleta ya kule Ziwa Nyanza ingekuwa ukombozi.
Mkuu mimi nina business interests hapo Dodoma na nilikuwa hapo jumamosi hii-2 days ago.

Dodoma ya sasa ni evergreen, tofauti na ilivyokuwa 30-40 years ago.
Mji una maji ya uhakika na kwa hivi sasa mitaa mingi inawekwa barabara za lami.

Dodo is slowly rising like a phoenix.
 
Mkuu mimi nina business interests hapo Dodoma na nilikuwa hapo jumamosi hii-2 days ago.

Dodoma ya sasa ni evergreen, tofauti na ilivyokuwa 30-40 years ago.
Mji una maji ya uhakika na kwa hivi sasa mitaa mingi inawekwa barabara za lami.

Dodo is slowly rising like a phoenix.

Afadhali we umeona hili, wengine wanakatisha tamaa tu kuwa ni nusu jangwa, je watu wanaishije?
 
mkuu candid scope dodoma ya sasa ni nzuri tofauti na zamani lami mpaka mwanza kupitia kondoa kazi imeshaanza kwa ujumla serikali imejitahidi ila kilio kitakuja wakati wa kulipa deni la taifa,lami wanaweka kweli ila wakikopa bil 200 wanatumia 100 kuleta maendeleo na 100 wanaweka tumboni ila deni tutalipa sisi.
karibu dom ununue kiwanja ni kama 10m siku hizi maeneo ya kisasa,ipagala na swaswa.
 
nenda wakati huu wa kiangazi na hiyo picha kisha ulinganishe uone.
 
dodoma29.jpg


Naijua Dodoma (Idodomya) kutosha, mlima huo ni karibu na Iringa Road kama sijashau. Hapa kwa njia unaona Dodoma Airport ya miaka mingi sana tu upande wa kulia ni njia iendayo kule Msalato na ukitaka kuendelea hadi Kondoa-Babati-Asrusha kazi kwako.

Nimeikumbuka Dodoma kuna wakati nimeendha kwenye vumbi na mchanga gari toka Shinyanga - Nzega - Singida - Dodoma kwenya mashimo, mchanga, vumbi usiombe, ukiona tu Dodoma unajisikia umeahueni kwani lami ndo ukombozi unajua Dar ni kaziru. Safari nyingi bora kuzungukia Kwamtoro kwenda Singida utokapo Dodoma kuliko kupitia Manyoni balaa tupu.

Dodoma pazuri kama pangeendelezwa, na waliochagua hapo waliona mbali, ingekuwa Washington DC ya Afrika kama ilivyo Arusha mfano wa Jiniva ya Africa.

Ukiteremka kwa gari moshi pale station utachoka mwenyewe na zabibu nzuri hadi usahau kama uko safarini na kutamani safari ingeishia hapo.

Maji ndio tatizo, labda kama siku hizi wamelitatua, la sivyo ndoto za Mkapa kuyaleta ya kule Ziwa Nyanza ingekuwa ukombozi.

Umesahau,pole.

BTW: Dodoma sio evergreen. Huonekana hivyo kipindi fulani tu cha mwaka.
Suala la fursa za kibiashara halina mjadala...things are now opening up at an amazing speed!
 
hahaha! unatufanya hutuijui dodoma sio! hako ni kamsimu tu ndo kukuwa na hiyo green! but dodoma ni kame na imekauka vya kutosha!
 
Back
Top Bottom