GAMBLER
JF-Expert Member
- Nov 22, 2009
- 303
- 11
MKAZI wa Ukonga Mombasa, Charles David Shauritanga (31) leo amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Mwanzo ya Samora pamoja na Mahakama ya Wilaya ya Ilala na kusomewa mashtaka tofauti likiwemo kosa la kujifanya daktari katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kutaka kumfanyia upasuaji mtoto wa Bi. Fatuma Mathayo kwa gharama ya 80, 000/=.
Mtuhumiwa huyo awali alipelekwa Mahakama ya Mwanzo ya Samora na kusomewa mashtaka mawili na Mwendesha Mashtaka wa mahakama hiyo, Musa Gumbo, mbele ya Hakimu Janeth Kinyage.
Akiwa mahakamani hapo alisomewa kosa la kwanza la kujifanya daktari na kosa la pili kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Baadaye mtuhumiwa alipandishwa Mahakama ya Wilaya ya Ilala na kusomewa kosa moja la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na mwendesha mashtaka wa mahakama hiyo Musa Gumbo mbele ya Hakimu Benjamini Mwakasonda.
Mtuhumiwa alikana makosa yote na kutakiwa kuwekewa dhamana ya 40,000/= na mtu mmoja kwa kosa la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kuwekewa dhamana na watu wawili kila mmoja mil. 3/= kwa kosa la kujifanya daktari.
Kesi hiyo itatajwa tena mahakamani hapo Januari 28 mwaka huu.
Mtuhumiwa huyo awali alipelekwa Mahakama ya Mwanzo ya Samora na kusomewa mashtaka mawili na Mwendesha Mashtaka wa mahakama hiyo, Musa Gumbo, mbele ya Hakimu Janeth Kinyage.
Akiwa mahakamani hapo alisomewa kosa la kwanza la kujifanya daktari na kosa la pili kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Baadaye mtuhumiwa alipandishwa Mahakama ya Wilaya ya Ilala na kusomewa kosa moja la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na mwendesha mashtaka wa mahakama hiyo Musa Gumbo mbele ya Hakimu Benjamini Mwakasonda.
Mtuhumiwa alikana makosa yote na kutakiwa kuwekewa dhamana ya 40,000/= na mtu mmoja kwa kosa la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kuwekewa dhamana na watu wawili kila mmoja mil. 3/= kwa kosa la kujifanya daktari.
Kesi hiyo itatajwa tena mahakamani hapo Januari 28 mwaka huu.