Picha CHADEMA wilaya Mkalama; Ni kijiji kwa kijiji ya vuna mamia ya wanachama

yegella

JF-Expert Member
Nov 18, 2010
3,113
1,102
Chama cha Demokrasia na Maendeleo wilaya ya Mkalama jimbo la Iramba Mashariki chini ya kamanda George Gunda akishilikiana na viongozi mkoa wa Singida, kimezidi kujijenga baada ya kufanya mikutano kwenye vijiji vya Msiu, Mwangeza, Msisai, Nkungina na kujizolea wanachama wapya zaidi ya 330, mabalozi wa CCM 5 walioamua kuhamia chadema na kufanikiwa kumrudisha mwenyekiti wa chadema aliyenunuliwa miezi michache iliyopita na kutubu kuwa hato rudia kukisaliti chama hii kwani tangu akihame amekuwa hana amani moyoni mwake ingawa kifedha alivuna za kutosha kujengea nyumba ambayo sasa anaishi.. chadema pia ilitoa misaada kwenye kijiji cha Nkungi waliopata maafa ya kuezuliwa paa za nyumba zao na mvua kubwa.
SAM_0217.JPG
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Msiu waliojitokeza kumsikiliza Kamanda George Gunda..
SAM_0234.JPG
Wananchi wakijiandikisha ili wapatiwe kadi cha chadema
SAM_0220.JPG
Akinamama wakimsikiliza kijana wao Kamanda George Gunda..
SAM_0202.JPG
Hapa kijiji cha Msiu..

SAM_0078.JPG
SAM_0075.JPG
SAM_0077.JPG
Kamanda Gunda akiwa na OCD wa wilaya ya Nkalama
SAM_0253.JPG
Hapa ni kijiji cha msisai....
SAM_0110.JPG
Mwenyekiti wa chadema mkoa wa Singida ndg Shaban(Mwenye koti refu) akiongea na wahanga baada ya kuwapatia misaada.
 
Safi sana chadema... Wana mabadiliko tuko nyuma yenu.... Inafurahisha sana hii
 
Mh. Waziri wa Mambo ya ndani mtarajiwa Mwingulu amesikia hilo au anangojea kuapishwa kwanza ndo aje huko? Atajifunzia kwenu kulitumia hilo rungu la dola
 
Mh. Waziri wa Mambo ya ndani mtarajiwa Mwingulu amesikia hilo au anangojea kuapishwa kwanza ndo aje huko? Atajifunzia kwenu kulitumia hilo rungu la dola

Huyu akipewa wizara hiyo watu watabakwa watauliwa sana...
 
CHADEMA wamekuwa kama waganga wa kienyeji..

Wakikaa maofisi mnasema ruzuku haitumiki vizuri, wakitumia ruzuku kuzunguka majimbo kuwaeleza wananchi sera zao mnawaambia waganga njaa, Hebu acheni demokrasia ya vyama vingi imee, ninyi mnavyombo vya ulinzi na uslama vinawasaidia ingawa mwenyekiti alishawataadharisha kuwa msiwategemee polisi na JWTZ tena.
 
Kila hatua ya CDM ni tarajio jipya kwa umma, la kuchukua hatamu za utawala wa nchi.

God bless this 'prospective ruling party'...! It has been very clear that, with a new constitution, and a renewed NEC, renewed Voters Registration Register - NO ONE WILL EVER STOP CDM from taking the state office and ruling this blessed land, Tanganyika prosperously.

Mungu ibariki CDM leo na daima!
 
Back
Top Bottom