PendoLyimo
JF-Expert Member
- Sep 30, 2014
- 866
- 939
SIRI YA SAKATA LA VITI MAALUMU CHADEMA HII HAPA. MDEE 19 NA SPIKA WANAONEWA BURE.
Na Philipo Mwakibinga
0758910403
Tatizo siyo Mdee 19 bali ni nani anapelekwa baada ya akina mdee kuondolewa. Viongozi waandamizi wa CDM wamepanga kuwa wanataka kupeleka sura mpya kabisa Bungeni na siyo hawa akina Mdee 19. Sababu kubwa ambazo zinafanya ni ileile tabia ya Maslahi Binafsi mbele, chama baadaye.
Baada ya Wabunge Nguli na Viongozi wa CDM kushindwa uchaguzi ndipo, uliibuka mkakati wa kupanga safu ya kupeleka Viti maalumu watakavyo nufaika navyo wao binafsi kwa miaka 5. Hali hii ilipelekea kuanza kwa mkakati wa kutaka kupora haki ya BAWACHA ya kupendekeza majina kwenye CHAMA kwakuzingatia vigezo vya nani awe mbunge na, kwasababu zipi.
Mfano Aliyekua Mbunge wa Iringa kwa upande wake tayari ameapa kumpeleka Mwanaye ili akawe Mbunge kiti Maalumu. Tayari keshaanza kumpigia chapuo hata kwenye media ili aonekane anauwezo. Mwamba kama kawaida yake yeye anao wake na ndugu zake ambao kukosa Ubunge, kwake anaona kama hajatendewa haki kwani kwake imekua kama sheria kwamba lazima bibie mdogo awe mbunge kila baada ya uchaguzi.
Aliyekuwa Mbunge wa Tarime, yeye anao Wabunge wake mabinti ambao alishakubaliana nao kuwa, kila mmoja akiingia bungeni atalazimika kukopa milioni 300 kisha jamaa anachukua milioni 200 na bidada anabaki na milioni 100 na ubunge wake unakua chini ya uangalizi. Hii ndiyo sababu ya kwamba wanapeleka sura mpyaa kabisa. Unaweza kujiuliza sura mpya kabisa kwa chama kama CDM kule bungeni kutakua na tija!?
Ndipo ukweli unabaki kuwa, kumbe tatizo siyo kwamba CDM haitaki nafasi za viti Maalumu pamoja na kwamba walisema hawatambui ule uchaguzi na kusema kuwa ulikuwa ni uchafuzi hapana, Wanachotaka ni kupeleka majina ya watu wao wengine watakao nufaisha viongozi na siyo Chama.
Katika hili nilazima kwa mpenda Demokrasia yeyote kutetea akina Mdee 19 kwasababu, viongozi wa CDM wanatumia nguvu kubwa kuendelea kuwashambulia ili ionekane hawafai. Hii siyo tabia nzuri na Wanachama wa CDM wanapaswa kujua kiundani hili jambo.
Wanajaribu kumchafua Spika wa Bunge Ili aonekane kawabeba akina Mdee 19 wakati, WAO CHADEMA wanajua kuwa barua yao rasmi ya kupeleka majina ipoTUME YA UCHAGUZI na siku wakienda mahakamani upo uwezekano wa Mahela kuwaumbua ndiyo maana wanahofu kubwa ya kupeleka jambo hilo mahakamani kama alivyokuwa ameahidi MNYIKA.
Kuna madudu mengi sana kwa hawa jamaa. Mfano Wanaitumia vibaya sana BAWACHA ilikujaribu kushinda hiyo vita yao...
Hadi sasa Bado Mdee 19 wananguvu kubwa na kila kukicha jamii inazidi kuelewa ukweli hili nalo ni pigo jingine kwa Team Mnyika mzee wa kulilia viti 19 vya WANAWAKE.
Nitaendelea kuwajuza
Sent from my EVA-L09 using JamiiForums mobile app
Na Philipo Mwakibinga
0758910403
Tatizo siyo Mdee 19 bali ni nani anapelekwa baada ya akina mdee kuondolewa. Viongozi waandamizi wa CDM wamepanga kuwa wanataka kupeleka sura mpya kabisa Bungeni na siyo hawa akina Mdee 19. Sababu kubwa ambazo zinafanya ni ileile tabia ya Maslahi Binafsi mbele, chama baadaye.
Baada ya Wabunge Nguli na Viongozi wa CDM kushindwa uchaguzi ndipo, uliibuka mkakati wa kupanga safu ya kupeleka Viti maalumu watakavyo nufaika navyo wao binafsi kwa miaka 5. Hali hii ilipelekea kuanza kwa mkakati wa kutaka kupora haki ya BAWACHA ya kupendekeza majina kwenye CHAMA kwakuzingatia vigezo vya nani awe mbunge na, kwasababu zipi.
Mfano Aliyekua Mbunge wa Iringa kwa upande wake tayari ameapa kumpeleka Mwanaye ili akawe Mbunge kiti Maalumu. Tayari keshaanza kumpigia chapuo hata kwenye media ili aonekane anauwezo. Mwamba kama kawaida yake yeye anao wake na ndugu zake ambao kukosa Ubunge, kwake anaona kama hajatendewa haki kwani kwake imekua kama sheria kwamba lazima bibie mdogo awe mbunge kila baada ya uchaguzi.
Aliyekuwa Mbunge wa Tarime, yeye anao Wabunge wake mabinti ambao alishakubaliana nao kuwa, kila mmoja akiingia bungeni atalazimika kukopa milioni 300 kisha jamaa anachukua milioni 200 na bidada anabaki na milioni 100 na ubunge wake unakua chini ya uangalizi. Hii ndiyo sababu ya kwamba wanapeleka sura mpyaa kabisa. Unaweza kujiuliza sura mpya kabisa kwa chama kama CDM kule bungeni kutakua na tija!?
Ndipo ukweli unabaki kuwa, kumbe tatizo siyo kwamba CDM haitaki nafasi za viti Maalumu pamoja na kwamba walisema hawatambui ule uchaguzi na kusema kuwa ulikuwa ni uchafuzi hapana, Wanachotaka ni kupeleka majina ya watu wao wengine watakao nufaisha viongozi na siyo Chama.
Katika hili nilazima kwa mpenda Demokrasia yeyote kutetea akina Mdee 19 kwasababu, viongozi wa CDM wanatumia nguvu kubwa kuendelea kuwashambulia ili ionekane hawafai. Hii siyo tabia nzuri na Wanachama wa CDM wanapaswa kujua kiundani hili jambo.
Wanajaribu kumchafua Spika wa Bunge Ili aonekane kawabeba akina Mdee 19 wakati, WAO CHADEMA wanajua kuwa barua yao rasmi ya kupeleka majina ipoTUME YA UCHAGUZI na siku wakienda mahakamani upo uwezekano wa Mahela kuwaumbua ndiyo maana wanahofu kubwa ya kupeleka jambo hilo mahakamani kama alivyokuwa ameahidi MNYIKA.
Kuna madudu mengi sana kwa hawa jamaa. Mfano Wanaitumia vibaya sana BAWACHA ilikujaribu kushinda hiyo vita yao...
Hadi sasa Bado Mdee 19 wananguvu kubwa na kila kukicha jamii inazidi kuelewa ukweli hili nalo ni pigo jingine kwa Team Mnyika mzee wa kulilia viti 19 vya WANAWAKE.
Nitaendelea kuwajuza
Sent from my EVA-L09 using JamiiForums mobile app