PhD ya Musukuma yazua gumzo, Chuo kilichomtunuku hakitambuliki

Nilipokuwa sekondari Kuna mwandishi mmoja wa vitabu mwenye jina la kihaya nimemsahau alileta TAFRANI kwa baadhi ya VIONGOZI kwa kuwataja kuwa si madaktari wa kweli.......

Kuhusu hizi "HONORIS CAUSA" aliyopatiwa mh.Musukuma anaweza kupewa yeyote mwenye MCHANGO katika jamii ...hoja tu ni kutoka CHUO KIKUU GANI CHENYE ITHIBATI ZILIZOSIMAMA .....

Hata Nassib Abdul "alias" Diamond Platinumz naye ana SHAHADA ya heshima kutoka UDSM ........
Hii udsm sio jalalani au?
 
Wachunguzi wanadai kwamba eti Chuo hicho kiko India na kwamba kina matawi yake Uingereza na Marekani bali uchunguzi unaonyesha kwamba hakijawahi kusajiliwa Uingereza wala Marekani na wala hakipo huko.

Kingine ambacho wachunguzi wamekifuatilia ni vigezo ambavyo vimezingatiwa ili kumpa heshima hiyo Musukuma, yadaiwa ni mchongo mwanzo mwisho.

Baba Askofu Bagonza amenukuliwa kwamba aliombwa dola 500 na chuo hicho ili aingizwe kwenye mchakato wa watakaopewa PhD hiyo na hicho chuo cha Musukuma ila yeye akagoma na akawaambia wahusika kwamba anazo ofa kadhaa kutoka kwenye vyuo vikubwa duniani vinavyomuomba akubali kupewa PhD za heshima, tena kwa vyuo vyenyewe kumlipa hadi USD Elfu 10, siyo kwa yeye kuvilipa vyuo kama chuo cha Musukuma kinavyodai.

Swali ni hili, ni nani anafaidika na vyuo vya uongo kama hiki cha Musukuma na ili iweje?

Yani haya mashada katoka nayo kijijini kwake kuwahi mchongo,kofia utafikiria beseni,ccm kumejaa wajinga tupu
 
Aisee wanasiasa mnakatisha watu tamaa ya kusoma bhana, watu wanahangaika kusoma kwa taabu wanakesha usiku, Kuna wengine Familia zinauza Mali za ukoo ili kijana asome, wengine wa nashindwa kumaliza kwa kukosa Ada na wengine wanashindwa kwa kufeli mitihani(discontinuation).
Masikini ya Mungu na wengine watoto wa kike mpaka wanauza utu wao kwa waalimu wao kwa kutoa rushwa ya ngono, halafu huku nyie yaani mnapeanapeana tu, eti mara Degree ya heshima, mara PhD ya heshima, acheni mzaha na elimu jamani, Elimu ni IBADA.

Eti PHD, hivi wewe Kasheku unajua PHD au unaisikia tu!!!

Udaktari wa Heshima katika Siasa na uongozi, kwa hiyo Sasa hivi tumuite Dr. MSUKUMA? AFADHARI ya Dr. MAJI MAREFU Udaktari wake aliojitangaza nao ulikuwa unajulikana anafanya nini!

Wapi umewahi kusikia standard Seven anapata PHD?

Na mbona hizo shahada za heshima kila siku wanapewa wanasiasa tu???View attachment 2034376View attachment 2034377
Shule ya msingi kasoma kwa miaka 8
 
Mchango katika jamii kheri Zahir wa online TV anaitendea haki dunia ya wahitaji.
FB_IMG_16388487189086816.jpg
 
Udaktari wa Heshima katika Siasa na uongozi, kwa hiyo Sasa hivi tumuite Dr. MSUKUMA? AFADHARI ya Dr. MAJI MAREFU Udaktari wake aliojitangaza nao ulikuwa unajulikana anafanya nini!
Maji Marefu alikuwa akijiita Prof. Maji Marefu na siyo Dr.
 
Ukiona mwanasiasa kapata PhD au master jua ni ya mchongo.
Hahaha kweli kabisa. Nape, Angela kizigha walisoma pale mzumbe Dar aisee pale ukimpa dr. Barongo sijui prof. Kwa sasa? Ukimpa mpunga unaitwa kwenda kusaini vitabu vyeusi
 
Ninachokifahamu Juu ya American Universal Global Peace (AUGP).
_________
Francis Daudi

Mwaka 2013, Chuo kinachoitwa Academy (au Wakati Mwingine hujiita) American of Universal Global Peace (AUGP) kilizua mtafaruku huko Bangalore, India!

Aliyekuwa Waziri wa Kilimo na Kazi wa Jimbo la Chhattisgarh, Chandrashekhar Sahu alialikwa ili kutunikiwa Udaktari wa Heshima katika Kazi za Kijamii (Social Works). Hii ni kutokana na mchango wake katika maendeleo ya Kilimo na Wakulima! Na kwa Hakika, Sahu alikuwa amefanya kazi nzuri kwenye jimbo hilo lilizungukwa na Vilima.

Sahu akiwa ameshafika Bangalore toka Raiput, hakukuta kinachoitwa Academy of Universal Global Peace (AUGP). Na kibaya zaidi Chuo hiki hakikuwa kinatambuliwa na University Grants Commission(UGC) hii ni kama TCU ya Tanzania.

Mwakilishi wa AUGP alidai Chuo Chao kinatambulika na European Commission, World Peace Organisation na United Nations Global Compact. Hata hivyo iligundulika ni Utapeli Mtupu!

Jambo la kuchekesha ni kuwa, Mwenyekiti wa Academy of Universal Global Peace (AUGP), Dr. Madhu Krishan amekuwa akisafiri na Chuo; Hivyo kimewahi kuwepo Marekani, na Chennai, India!

Kwa bahati mbaya, Chuo hiki sio Christ University(Bangalore) wala International Christian University (Japan). Soma habari hii hapa: Chhattisgarh minister laps up fake honour

Baada ya kisa hiki cha 2013, Wanasiasa wengi wa India walianza kulalama kuwa Mawakala wa American of Universal Global Peace (AUGP) wamekuwa wakiwaomba kati ya Dola (za Marekani) 500 hadi 1,000 ili wapatiwe kinachoitwa "Doctor Honoris Causa"

Kelele zilipokuwa nyingi, hasa utapeli wa kuuza Stashahada: Wao waliandika majibu haya: Ambayo ukichunguza vema utagundua kitu, Rogue academy selling fake honorary doctorate responds to our initial report, accuses C. Hub of wanting to extract huge amount of money from them.

Wakati websites zote za vyuo vya Marekani zina .edu mfano: www.harvard.edu ,
twin-cities.umn.edu hiki Chuo cha Mchongo kinatumia .com yaani augpusa.com na kwa taarifa yako hako ni ka Blogu tu kwenye WordPress. Umeelewa? Ifungue kisha nenda hadi mwisho utaona!!

Mwisho: University Nations (UNU) University kilitangaza kwenye website yake kuwa hakina uhusiano wala ushirikiano na hiki kinachojiita American University of Global Peace!! Soma hapa: False claims of affiliation with UNU - United Nations University

Ni muhimu kabla haujatunukiwa Udaktari wa Heshima ukachunguza haya!

Francis Daudi.
 
Karibu yote uliyosema ni kweli....

Nilisema hivyo kwa sababu jamii yetu inathamini wenye pesa. Hata uwe profesa uliyeandika mavitabu 100 na unajulikana kimataifa kama huna pesa we ni takataka tu mbele ya jamii. Ndiyo maana akina Musukuma na Kishimba kila siku kutukana maprofesa kwa vile wana pesa japo hawajasoma!

Sijui kama Musukuma anatumia pesa zake kuwakanyaga wengine ila nijuavyo mimi ni mtu mwema na anayejitolea sana jimboni mwake...
Mimi namthamini kila mtu kwa jinsi Mungu alivyomjalia na si kwa sababu ya pesa maana ni pesa zake na si zangu na sina mgao kwa pesa zake. Katika jamii tunaishi kwa kutegemeana - mwenye pesa anamtegemea mtu mwingine asiye na pesa kwa kitu au jambo alilo na shida nalo. Mfano, mwenye pesa akiumwa jino ataenda kwa dentist, ambaye hata hajajenga nyumba, hana gari, lakini anaweza kumtibu. Watoto wa mwenye pesa atawapeleka shule au kwa baadhi ya wenye pesa atawanyima elimu ya shule na kuwapa mali. Lakini kuwa na mali hakuondoi umuhimu wa elimu kwa mwanadamu. Heri uwe na pesa na uwe umesoma kuliko kuwa na pesa na uwe hujasoma au huna elimu ya darasani.
 
Kwani ina tofauti gani na ya Jaffo?
Haya, kuna ile PhD ya Magufuli nayo ilizua mjadala, ambao ulizimwa baada ya mpingaji mkuu wa PhD hiyo kupotezwa jadi leo. Ben Saanane. Ya Jaffo sijaifuatilia binafsi, lakini tunaweza kuorodhesha hapa PhD zenye utata:
1) Dr. Magufuli
2) Dr. Msukuma Kasheku
3) Dr. Jaffo
Hivi ile ya Lyatonga Mrema ilikiwa ni Bachelors au Masters au PhD? maana watanzania kwa digirii za kuchonga tu hatujambo
 
Taarifa yako haiko sawa. Msukuma hakupewa PhD bali Doctorate pamoja na kwamba ni ya kuchonga.
Wachunguzi wanadai kwamba eti Chuo hicho kiko India na kwamba kina matawi yake Uingereza na Marekani bali uchunguzi unaonyesha kwamba hakijawahi kusajiliwa Uingereza wala Marekani na wala hakipo huko.

Kingine ambacho wachunguzi wamekifuatilia ni vigezo ambavyo vimezingatiwa ili kumpa heshima hiyo Musukuma, yadaiwa ni mchongo mwanzo mwisho.

Baba Askofu Bagonza amenukuliwa kwamba aliombwa dola 500 na chuo hicho ili aingizwe kwenye mchakato wa watakaopewa PhD hiyo na hicho chuo cha Musukuma ila yeye akagoma na akawaambia wahusika kwamba anazo ofa kadhaa kutoka kwenye vyuo vikubwa duniani vinavyomuomba akubali kupewa PhD za heshima, tena kwa vyuo vyenyewe kumlipa hadi USD Elfu 10, siyo kwa yeye kuvilipa vyuo kama chuo cha Musukuma kinavyodai.

Swali ni hili, ni nani anafaidika na vyuo vya uongo kama hiki cha Musukuma na ili iweje?

 
Wachunguzi wanadai kwamba eti Chuo hicho kiko India na kwamba kina matawi yake Uingereza na Marekani bali uchunguzi unaonyesha kwamba hakijawahi kusajiliwa Uingereza wala Marekani na wala hakipo huko.

Kingine ambacho wachunguzi wamekifuatilia ni vigezo ambavyo vimezingatiwa ili kumpa heshima hiyo Musukuma, yadaiwa ni mchongo mwanzo mwisho.

Baba Askofu Bagonza amenukuliwa kwamba aliombwa dola 500 na chuo hicho ili aingizwe kwenye mchakato wa watakaopewa PhD hiyo na hicho chuo cha Musukuma ila yeye akagoma na akawaambia wahusika kwamba anazo ofa kadhaa kutoka kwenye vyuo vikubwa duniani vinavyomuomba akubali kupewa PhD za heshima, tena kwa vyuo vyenyewe kumlipa hadi USD Elfu 10, siyo kwa yeye kuvilipa vyuo kama chuo cha Musukuma kinavyodai.

Swali ni hili, ni nani anafaidika na vyuo vya uongo kama hiki cha Musukuma na ili iweje?

Eti anaitwa dr Msukuma KWa Sasa, ila sawa mbona tulishakua na prof maji marefu,
 
Back
Top Bottom