Peter Msigwa: Sisi hatuwashawishi Wananchi ili tupate ajira bali tunataka Demokrasia ifanye kazi

Mmawia

JF-Expert Member
Aug 20, 2013
121,900
95,159
Aliyekuwa mbunge wa Iringa mh Msigwa amewashukia na Seif. Peter Msigwa: "Sisi hatuwashawishi Wananchi ili tupate ajira bali tunataka Demokrasia ifanye kazi, sisi tukitaka ubunge tunapata tu hata kupitia CCM ila Sisi tunataka katiba mpya, tume huru na haki ipatikane.

"Maalim Seif na Zitto waliochofanya ni sawa na Mbwa kurudia matapishi yake na kilichowafanya wafanye hivyo ni mambo ma4 Uongo, Unafiki, Uoga na kujipendekeza, si wawe tu CCM. -:~ Peter Msigwa Mbunge wa zamani wa jimbo la Iringa kupitia Chadema.View attachment 1649744

 
Ms
Msigwa Ni katika like group la matapeli wa kisiasa tu,Ana bebwa Sana na MBOE kiasi hata Sossopi alifanyiwa udictator ilimradi yeye apewe ulaji wa uenyekiti wa Kanda.

Tumkumbushe tu hata yeye aliunga Juhudi serikali iliyopo madarakani,kwa unafikir akajidai kuomba msamaha
 
Ms
Msigwa Ni katika like group la matapeli wa kisiasa tu,Ana bebwa Sana na MBOE kiasi hata Sossopi alifanyiwa udictator ilimradi yeye apewe ulaji wa uenyekiti wa Kanda.


Tumkumbushe tu hata yeye aliunga Juhudi serikali iliyopo madarakani,kwa unafikir akajidai kuomba msamaha
CCM ndiyo saccoss ya mahene.
 
Kila mtu apambane na chama chake mbona CHADEMA waliporudia matapishi yao kwa kumleta Lowassa waliyekuwa wanamwita fisadi Zitto aliwakalia kimya?
Lowasa sasa hivi karudi kwenye kiota chake ccm cha kuibulia na kukuza mafisadi ya kimataifa.
 
Baada ya kupokelewa na CHADEMA wakamsafisha na kula matapishi yao
Wewe ndiyo ulikua unaongoza kumtukana matusi mazito wakati yupo cdm,leo hii mwenye ccm yake kamrudisha ccm wewe tena ndiyo unaye mramba miguu yake kwa unyenyekevu.
 
msigwa ndo nani
Mchungaji Msigwa humjui.
yahoo.gif
yahoo.gif
 
Sidhani kama kurushiana maneno huku kunasaidia upinzani, ilipaswa tuwe wamoja kuelekea 2025 ila kama tunagawanyika hivi hyo tume huru tutaidai vp bungeni.

Kama ambavyo ACT hawakuingilia suala la kina Mdee nadhani CHADEMA nao wangepotezea suala la Maalim maana ni chama chao wana uhuru wa kujiamulia.

Lissu kma presidential aspirant hakupaswa kuchukua upande mapema hivi. Angekua neutral tu coz bado ataihitaji Zanzibar uchaguzi wa 2025. Hii misuaguano haisaidii zaidi ya kudhoofisha upinzani tu na kuwapa credit CCM.

Just saying
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Wacha tudumishe amani upendo na ushirikiano


Maendeleo hayana vyama
 
Wewe ndiyo ulikua unaongoza kumtukana matusi mazito wakati yupo cdm,leo hii mwenye ccm yake kamrudisha ccm wewe tena ndiyo unaye mramba miguu yake kwa unyenyekevu.
Sikuwahi kumtukana Lowassa, ila niliamini ni Fisadi kuu kipindi cha the list of shame, nikaacha kuwaamini wanasiasa toka Chadema walivyompokea wakala matapishi yao. Mimi simuamini mwanasiasa wala chama cha siasa.

Ninachosema Msigwa aache unafiki, hata wao waliwahi mpokea mtu waliyemnanga kwa miaka mingi kwua ni fisadi kuu na msigwa mpaka kuna audio na videos zake akimsema vibaya. Hana moral authority ya kumjudge zitto maana zitto hata walipompokea hakuwasema vibaya.
 
Ushauri kwa jpm; Naomba mch Msigwa tumzawadie ki cheo kidogo apoze njaa..sio kwa wivu huo. Nothing more than wivu tu!!!
 
Sikuwahi kumtukana Lowassa, ila niliamini ni Fisadi kuu kipindi cha the list of shame, nikaacha kuwaamini wanasiasa toka Chadema walivyompokea wakala matapishi yao. Mimi simuamini mwanasiasa wala chama cha siasa. Ninachosema Msigwa aache unafiki, hata wao waliwahi mpokea mtu waliyemnanga kwa miaka mingi kwua ni fisadi kuu na msigwa mpaka kuna audio na videos zake akimsema vibaya. Hana moral authority ya kumjudge zitto maana zitto hata walipompokea hakuwasema vibaya.
Sasa endelea kumramba miguu.
 
Sasa endelea kumramba miguu
Aliyekula matapishi ya mbwa hawezi kumshauri anayekula matapishi ya mbwa. Msigwa hawezi kumshauri Zitto maana yeye na wenzake ndiyo walitangulia kula matapishi ya mbwa na hawajawahi kukiri kuwa walikosea.
 
Aliyekuwa mbunge wa Iringa mh Msigwa amewashukia na Seif.
Peter Msigwa: "Sisi hatuwashawishi Wananchi ili tupate ajira bali tunataka Demokrasia ifanye kazi, Sisi tukitaka ubunge tunapata tu hata kupitia CCM ila Sisi tunataka katiba mpya, tume huru na haki ipatikane.

"Maalim Seif na Zitto waliochofanya ni sawa na Mbwa kurudia matapjshi yake na kilichowafanya wafanye hivo ni mambo ma4 Uongo, Unafiki, Uoga na kujipendekeza, si wawe tu CCM. -:~ Peter Msigwa Mbunge wa zamani wa jimbo la iringa kupitia Chadema.View attachment 1649744
Maamuzi ya ACT yamefikiwa kwwnye chombo halali, yaheshimiwe hata kama hayapendezi wengine, ndio demokrasia yenyewe hiyo.
 
Aliyekuwa mbunge wa Iringa mh Msigwa amewashukia na Seif.
Peter Msigwa: "Sisi hatuwashawishi Wananchi ili tupate ajira bali tunataka Demokrasia ifanye kazi, Sisi tukitaka ubunge tunapata tu hata kupitia CCM ila Sisi tunataka katiba mpya, tume huru na haki ipatikane.

"Maalim Seif na Zitto waliochofanya ni sawa na Mbwa kurudia matapjshi yake na kilichowafanya wafanye hivo ni mambo ma4 Uongo, Unafiki, Uoga na kujipendekeza, si wawe tu CCM. -:~ Peter Msigwa Mbunge wa zamani wa jimbo la iringa kupitia Chadema.View attachment 1649744
Sasa Halima mdee vipi amekula mavi ya mbwa? Lissu anakula kuku ulaya Lema amewatelekeza Arusha, Mgombea urais wa Chadema kule Zanzibar aliipigia kampeni ccm na aliahidiwa kama angepata 5% vote angepata Uwaziri Zanzibar., Alimsaliti hata mbunge wake wa Chadema aliyesimamishwa kwenye jimbo lake anaitwa Lukman akampigia kampeni Mhe. Juma Hamad Omar ambaye alikuwa CUF zamani baadae akaja akaingia CCM huyu ni Ndugu na Makamo mwenyekiti wa Chadema Kule Pemba Zanzibar.

Na kwa bahati mbaya sana huyu Said Iissa Moh'd bado yupo kama senior leader wa Chadema baada ya Mbowe hukaa yeye kwenye meza za itifaki za chama cha Chadema. Mimi namshangaa sana Msigwa na Lissu hawana muda kuongelea migogoro ndani ya chama chao ya usaliti wanaongelea ACT chama ambacho kina mikakati yake hakiwahusu kabisa.

Na Maalim Seif amesema wazi Tundu Lissu anatumika kwa kiasi kikubwa kuhujumu upinzani Tanzania huko ulaya aliko., alisema hawezi kuja Tanzania kwa sababu waliompiga risasi hawajakamatwa lakini kwa sababu shida ilikuwa ni urais alijitosa akaja lakini jengine la ajabu bada uchaguzi amerudia kwenye hoja yake ya kuuliwa karudi zake belgium. maswali mengi tunajiuliza shida yake ni urais ilikuwa au kweli ana moyo na watanzania? lakini Lema sasa yuko canada wala hana mpang wa kurud tena.

Mimi nadhan Chadema kwanza waangalie boriti kwenye macho yao kuliko kibanz kwenye jicho la Maalim Seif.
 
Kwa hiyo yeye Msigwa ndiye mkweli? Nini kilimfanya amuombe radhi Kinana?

Kama nyinyi vipaumbele vyenu ni hivyo na ACT nao wanavyo vya kwao sasa mnawashwa nini na maamuzi na chama kingine?

Wao kuunda SUK kunawaathiri nini nyinyi kwenye vipaumbele vyenu?

Komaeni na CCM hayo ya ACT waachieni wenyewe huko Zanzibar kwenyewe hamjawahi kuwa hata na "sheha"
 
Back
Top Bottom