Peter Kisumo Vs. Anne Killango - vita vya maneno

Indume Yene

Platinum Member
Mar 17, 2008
2,948
709
Ni jambo la kushangaza kuona Mtanzania Halisi ambaye amewahi kushika madaraka katika serikali ya SISEMU leo hii kumshambulia Mbunge Anne Kilango kwa vita dhidi ya VISADIZ.

Naamini anatumia haki yake kikatiba kutoa maoni yake ila siamini kama umri wake unapelekea fikra zake kuzeeka vilevile. Si ajabu hii itakuwa ni kujipendekeza kwa serikali na chama chake angalau wamuangalizie hata ubunge wa kuteuliwa if Makamba atakuwa sacked.

Soma hii habari hapa kutoka Tanzania Daima kisha utoe maoni yako.

Kisumo amlipua Mama Kilango

na Charles Ndagulla, Moshi

MOTO aliouwasha Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anne Kilango Malecela, kuhusu wizi wa fedha za akaunti ya malipo ya madeni ya nje (EPA), umeendelea kuzua makubwa, baada ya mwanasiasa mkongwe nchini, Peter Kisumo, kumshutumu mbunge huyo machachari kuwa ana idhalilisha CCM.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Moshi, Kisumo alisema Mama Kilango amejivisha jukumu la wapinzani kuishutumu serikali juu ya tuhuma za ufisadi, wakati yeye mwenyewe (Mama Kilango), anatokea CCM, inayoongoza serikali.

Alisema kutokana na kauli zake kali bungeni kuhusu suala la EPA, Kilango hastahili kabisa hata unaibu waziri, kwani alichokuwa akikisema ni sawa na kumtukana mkuu wa nchi, serikali na CCM.

Kisumo alisema matamshi yaliyotumiwa na Kilango kwenye kikao cha Bunge la bajeti kinachoendelea mjini Dodoma kwamba kama fedha za EPA hazitarejeshwa bungeni hapatatosha, ni maneno mazito na yasiyostahili kutolewa na mbunge wa chama kinachoshika madaraka.

Alibainisha kuwa matamshi ya Kilango yameonyesha jeuri ya hali ya juu kwa chama chake, kwa kuongea kwa ukali bungeni juu ya sakata la ufisadi katika akaunti hiyo ya EPA.

Alisema alichokifanya Kilango ni kutotii maelekezo ya chama chake yaliyotolewa kwa wabunge wote wa CCM na Katibu Mkuu, Yusuf Makamba, katika kikao cha wabunge wote wa chama hicho.

Kwa mujibu wa Kisumo, maagizo hayo ya CCM kwa wabunge wake kuhusu suala hilo, yalitaka mjadala huo usiendelee kuwa ajenda bungeni, kwani tayari lilikuwa linafanyiwa kazi na tume iliyoundwa na Rais Jakaya Kikwete.

Huyu Kilango jeuri hii ya kuzungumza mambo kama haya kaipata wapi wakati CCM walisema mjadala huo usiendelee bungeni kwa kuwa linatafutiwa ufumbuzi? Hafai hata kupewa unaibu waziri, alisema Kisumo.

Alisema wizi uliotokea Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kupitia akaunti ya malipo ya madeni ya nje (EPA), ulishaanza kufanyiwa kazi na Rais Jakaya Kikwete, kwa kumfukuza aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT), Daudi Balali, pamoja na kuunda tume iliyomaliza kazi hivi karibuni.

Alipotafutwa kwa simu kuzungumzia shutuma hizo, Mama Kilango alisema kwa ufupi kuwa, anatafakari kauli hiyo nzito iliyotolewa na mtu aliyedai anamheshimu sana.

Wakati Rais Kikwete alipochukua fomu kuwania nafasi hiyo, Kisumo alieleza msimamo wake wa kumuunga mkono, huku akipiga vijembe kuwataka wazee wamwachie Kikwete kushika nafasi hiyo.

Ingawa hakumtaja jina mzee aliyemlenga katika maelezo yake, lakini ni dhahiri kwamba alikuwa akimzungumzia mzee John Samwel Malecela, mume wa Mama Kilango, ambaye naye aliwania nafasi hiyo.

Katika hatua nyingine, Kisumo ameweka wazi tofauti zake dhidi ya mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM taifa, Aggrey Marealle, ambaye pia ni Naibu Kamanda wa Umoja wa Vijana wa CCM, Manispaa ya Moshi.

Kisumo amedai kuwa, kama CCM itampitisha Marealle kuwania ubunge katika Jimbo la Moshi Mjini, katika uchaguzi mkuu ujao mwaka 2010, jimbo hilo litaendelea kuwa kambi ya upinzani.

Alisema hata kama mbunge wa sasa wa jimbo hilo, Philemon Ndesamburo (CHADEMA), hatagombea katika uchaguzi mkuu ujao na Marealle akashindanishwa na mtu mwingine kutoka kambi hiyo ya upinzani, bado jimbo hilo litanyakuliwa na upinzani.

Ameongeza kuwa pamoja na jitihada za makusudi zinazofanywa na Marealle kutoa misaada ya kijamii katika maeneo mbalimbali ya mji wa Moshi kupitia Kampuni yake ya mahusiano ya Executive Solutions, jitihada hizo hazitamsaidia.

Hii ni mara ya pili kwa Kisumo kutoa maneno makali dhidi ya Marealle, ambapo mara ya kwanza ilikuwa kwenye mkutano mkuu wa CCM Manispaa ya Moshi mwaka jana.
 
Last edited by a moderator:
Kukemea serikali na chama tawala si lazima uwe mpinzani. Naamini hata kipindi yeye akiwa Waziri kulikuwa na baadhi ya viongozi ambao walikuwa na mtazamo na fikra tofauti na Marehemu Mwl. Nyerere. Ni kichekesho kuikosoa serikali, chama tawala au bunge tayari umeshakuwa Mpinzani. Ama kweli fikra nazo zinazeeka. Wakati wake ulishapita na kama anashindwa kuchangia mambo ya muhimu katika kuleta maendeleo ya nchi yetu ni bora atulie aendelee na shughuli zake binafsi.
 
Huyu Mzee ni vema akafunga mdomo wake tu................hizi sio enzi za ndio mzee........check list ya FMES (kwenye thread ya Mar Munanka) ndio utajua kuwa huyu Mzee hatakiwi kutupigia kelele kabisaa!!........maana ile list ingeingia dosari kama jina la huyu bwana lingekuwepo........
 
Kwa mujibu wa shutuma za Kisumo hivyo nini maana ya wabunge wa CCM kazi yao ni moja tu kuunga mkono serikali ya CCM. Lakini pia anasahau kuwa wao ni wawakilishi wa wanainchi pia. Na anasahau pia walikuwepo wabunge kipingi cha chama kimoja kulikuwa na wabunge walikokuwa wakishiriki vyema kuikosoa na kuakikisha serikali inafanya kulingana na inavyostahili kufanya.

Kwa kifupi anasema pumba.
 
...huyu Mzee Ni Mjinga...nimeshasema Mara Nyingi Hapa....nimebahatika Kukaa Naye Na Kumsikiliza Hasa Wakati Ule Wa Uteuzi...maneno Mabaya Aliyokuwa Akiongea Dhidi Ya Salim Na Malecela Hayaandikiki......

Lakini Si Kosa Lake....ni Mjinga Tangu Zamani Miaka Ya Mwisho Ya 50 Alipokuwa House Boy Na Kuli Wa Wahindi Pale Arusha....na Funza Miguuni...daima Mdomo Wake Mchafu Umemlisha..hassa Alipoweza Kuchaguliwa Kuwa Kiongozi Wa Wafanyakazi Wa Ndani..kwenye Chama Cha Wafanyakazi Enzi Zile Na Ikawa Njia Yake Kuingia Siasa....
 
wakubwa.
inaonesha nyie hamuitambui ccm, ni kwamba kisumo anatumiwa tu kumjenga mama yetu kilango kwani itaonekana ni mpinzani wa ndani na watatengeneza zengwe (kiinimacho) atimuliwe ktk chama ili ajiunge na upinzani ili apatikane tambwe hiza mwingine ambaye ataiharibu kambi ile na mwishowe atarejea kwa mbwembwe nyumbani.. am little bit nervous na bibie huyu (kilango) na harakati zake kwani ikimsoma between the lines kuna meseji tata mno anazoziwakilisha....

hivyo ccm tunavyowajua walivyo mabingwa wa propaganda wanasuka mpango muruwa wa kuwabakisha madarakani mpaka vizazi vyao viishe..
 
Nyoka akishauma utashtuka hata ukiona mtingiso wa nyasi. Hivyo siamini kama kuna chama chochote cha upinzani ambacho hakitakuwa macho na akina Tambwe wengine.
 
Huyu Mzee ni vema akafunga mdomo wake tu................hizi sio enzi za ndio mzee........check list ya FMES (kwenye thread ya Mar Munanka) ndio utajua kuwa huyu Mzee hatakiwi kutupigia kelele kabisaa!!........maana ile list ingeingia dosari kama jina la huyu bwana lingekuwepo........

Huyu mzee nilisema ni fisadi toka BCS kwa mara ya kwanza mtandao walipompa tu zile millioni 50, majuzi wamemuondoa mtu wake Mramba, sasa naona anataka ku-activate tena wamkumbuke,

Ahsante Mkuu Ogah kwa hiii kumbu kumbu! ya wale wale the protected! Wewe tafuta CV yake hlafu uniambie kwua aliwahi kuwa waziri, no wonder tuko hapa tulipo as a nation!
 
wakubwa.
inaonesha nyie hamuitambui ccm, ni kwamba kisumo anatumiwa tu kumjenga mama yetu kilango kwani itaonekana ni mpinzani wa ndani na watatengeneza zengwe (kiinimacho) atimuliwe ktk chama ili ajiunge na upinzani ili apatikane tambwe hiza mwingine ambaye ataiharibu kambi ile na mwishowe atarejea kwa mbwembwe nyumbani.. am little bit nervous na bibie huyu (kilango) na harakati zake kwani ikimsoma between the lines kuna meseji tata mno anazoziwakilisha....

hivyo ccm tunavyowajua walivyo mabingwa wa propaganda wanasuka mpango muruwa wa kuwabakisha madarakani mpaka vizazi vyao viishe..

Msanii with all respect, lakini kwa hili sina hakika kama uko sahihi. Jaribu kurudi nyuma kabla ya vikao vya uteuzi wa CCM Kisumo alikuwa upande upi na kwa sababu zipi, kabla hujaanza kufikiria unachofikiria. HUyu mzee ni fisadi wa kiimani na mblikimo wa mawazo.
 
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Moshi, Kisumo alisema Mama Kilango amejivisha jukumu la wapinzani kuishutumu serikali juu ya tuhuma za ufisadi, wakati yeye mwenyewe (Mama Kilango), anatokea CCM, inayoongoza serikali.

Alisema kutokana na kauli zake kali bungeni kuhusu suala la EPA, Kilango hastahili kabisa hata unaibu waziri, kwani alichokuwa akikisema ni sawa na kumtukana mkuu wa nchi, serikali na CCM.


Jamani huyu Mzee vipi? hajui kitu kabisa anapewaje jukwaa? hajui kwamba moja wapo ya kazi za bunge ni kuisimamia Serikali siyo chama. Eti kupinga ufisadi ni kumtukana Mkuu wa nchi. can't believe this!
 
Huyu mzee kaisha kabisa nadhani uwezo wake wa kufikiri haupishani na wa Kingunge! Kwani anavo sema inaonyesha wazi asivo elewa nini maana na kazi ya Mbunge!
 
...huyu Mzee Ni Mjinga...nimeshasema Mara Nyingi Hapa....nimebahatika Kukaa Naye Na Kumsikiliza Hasa Wakati Ule Wa Uteuzi...maneno Mabaya Aliyokuwa Akiongea Dhidi Ya Salim Na Malecela Hayaandikiki......

Lakini Si Kosa Lake....ni Mjinga Tangu Zamani Miaka Ya Mwisho Ya 50 Alipokuwa House Boy Na Kuli Wa Wahindi Pale Arusha....na Funza Miguuni...daima Mdomo Wake Mchafu Umemlisha..hassa Alipoweza Kuchaguliwa Kuwa Kiongozi Wa Wafanyakazi Wa Ndani..kwenye Chama Cha Wafanyakazi Enzi Zile Na Ikawa Njia Yake Kuingia Siasa....

Naona umetusaidia kuacha kukuna vichwa vyetu kumtafakari huyu hafidhina. Pia inatowa sura ya vipi tumefikishwa tulipo iwapo hawa ndio lilikuwa chaguo la Nyerere.
 
Unajua Mkuu FMES.......ulipozungumzia kuhusu ile habari yako ya meli na Fiasdi Munanka............yaani pale pale nikamkumbuka huyu Fisadi Kisumo......kwani hawatofautiani sana.............
 
Naona umetusaidia kuacha kukuna vichwa vyetu kumtafakari huyu hafidhina. Pia inatowa sura ya vipi tumefikishwa tulipo iwapo hawa ndio lilikuwa chaguo la Nyerere.
Hili zere nalo halina hata aibu, yaani hii extra time ya maisha yake baada ya kukaa na kuona anashiriki katika mkakati wa kuijenga nchi yake kwa maneno yanayojenga, yeye anazidi kupiga dongo. Hawa ndio kati ya watu wanaosaboteji Serikali ya Mh. Kikwete, na siku hizi watajitokeza wengi kwani mkakati wa mtandao wao ndio umepandisha bendera ili kuhakikisha watu wanaotetea maslahi ya Taifa hili kupitia utawala uliokuwepo hawapewi nafasi na wanapigwa vita kila kona. Kwa maana, hata hivi vikongwe basi navyo vimepewa mikakati. Huyuhuyu ni juzi tu alijipendekza kutetea na kusema Zanzibar si nchi, mimi niliona pale kuna kitu asingesema bure. Sasa, kwa taarifa yenu, watazameni wale watu wanaojiingiza katika migogoro inayojitokeza. Wengi wao hawaonekani katika kutafuta suluhisho bali wanakuwa na nia ya kulizidisha lile tatizo. Mmoja wao mwengine ni Mwinyi, Tambwe. Hawa wamekuwa kila sehemu wakichafua, wanapojiingiza tu basi utawaona hawapo katika kujenga bali maoni na maelezo yao ni kubomoa.

CCM kumpiga dongo CCM anaesimamia msimamo ambao wananchi wanaona ndivyo inavyostahiki. Kama si kubomoa, ni kitu gani? Kwa nia, wanaanzisha malumbano na wanaojaribu kumkingia Raisi Kifua, CCM Kikwete wanajaribu kuwakaba mafisadi. Wanazuka akina Kisumo wanawatetea mafisadi eti wanaowakaba mafisadi wanakidhalilisha Chama. Hapa unaipata ile picha ya mtandao wa mafisadi, na kama nilivyosema, angalieni sana watu wanaokandia kama akina Kisumo. Mkiwaona tu, basi wajumlisheni na wapinga mageuzi ya utawala bora. Kisumo, Mwinyi, na Tambwe nimeshawaweka katika kundi lisilo itakia mema nchi hii.
 
Chama Cha Mafisadi (CCM), ni kama genge la wezi vile, wakishapora wanagawana, ukiwa umesahaulika unatakiwa kupiga kelele usikike, huyu mzee naona mambo yanamuendea vibaya anapiga kelele ili wamtupie makombo sasa. Hakuna mantiki ya kumshutumu mtu kwa kusema ukweli, ukweli utabaki kuwa ukweli hata kama unadhalilisha chama. Ni wakati muafaka wa kujisafisha ili kelele ziishe. Kujisafisha sio kujiuzulu tu bali ni pamoja nakuwafikisha makamani watuhumiwa. Mbona wakati wa Nyerere wahujumu uchumi walishitakiwa?. Mafisadi ni sawa na wahujumu uchumi. Huyu mzee analia kwa kuwa wakati wake hakupata nafasi ya kukwapua kutokana kuwepo na Serikali inayojali watu zaidi kuliko kitu. Nina hakika huyu angekuwa leo serikalini nae angeingia kwenye ufisadi. Mafisadi hujitambulisha kwa kusingizia kukidhalilisha chama.
 
Peter Kisumo (nikiwa mdogo darasa la kwanza nilikuwa nikidhani kuwa jina lake halisi ni Kisumu) ameshindwa kabisa kulinda heshima yake kama mwanasiasa mstaafu. Wenye akili, wakishastaafu huwa wanajitahid kuwa neutral kadri ya uwezo wao ili waendelee kuheshimiwa. Yeye huyu anavurunda kabisa, sijui labda ni kwa sababu ya uzee au vippi. Asijeshangaa akiona watoto wanaaza kumwita fisadi hadharani kama alivyofanyiwa Mkapa; je ikimtokea hivyo naye ataomba msaada wa polisi tunaolipia?
 
Unajua Mkuu FMES.......ulipozungumzia kuhusu ile habari yako ya meli na Fiasdi Munanka............yaani pale pale nikamkumbuka huyu Fisadi Kisumo......kwani hawatofautiani sana.............

Guess what, hata na CV yake ya suspect sio tu kwamb aliwahi kuwa waziri, bali alishia kuwa mwenyekiti wa mamlaka ya bandari, hivi unaweza kweli kushangaa kwamba sasa bandari iko mkononi mwa Karamagi?

Yaani only in Tanzania!
 
Kisumo alikuwa upande wa Kikwete na mtandao. Hilo si jipya. Ila kama kuna watu walishapitwa na wakati mzee huyu anapaswa kuwa kwenye daladala ya watu waliopitwa na wakati.
 
Guess what, hata na CV yake ya suspect sio tu kwamb aliwahi kuwa waziri, bali alishia kuwa mwenyekiti wa mamlaka ya bandari, hivi unaweza kweli kushangaa kwamba sasa bandari iko mkononi mwa Karamagi?

Yaani only in Tanzania!

Pamoja na kwamba nilikuwa niko kwenye maombolezo ya kifo cha chacha wangwe!

Huyu FISADI kisomo amenisababisha nichangie. Baada ya kumusoma katika gazeti sikuweza kuamini alichosema. HIVI yeye ni nani hasa! unajua tembo akisifiwa!! huyu fisadi kisumo kasifiwa sana eti mdhamini wa CCM etc, lakini kama mdhamini wa CCM sioni ajabu yeye kutumiwa na mafisadi kwa kuwa mafisadi ndio wadhamini wa CCM. huyu mama Anna Kilango amemjibu vizuri sana katika gazeti la tanzania daima la leo. MAMA USIKATISHWE TAMAA JAPO KATIKA NCHI YETU LIMEKUWA JAMBO LA KAWAIDA KUWAPOTEZA WANAOWATETEA WANYONGE! LAKINI IKO SIKU TUTAFANUKIWA KUZIMA NGUVU ZA MAFISADI KWA NGUVU ZOTE VIFO SIYO SURUSHISO LA KUZIMA MOTO WA KUWASEMA MAFISADI!
BALI SOLUTION NI MAFISADI KUACHA NA KURUDISHA MALI ZA NCHI, JAMANI WANACHI WA TZ WAMEFANYWA KUWA MASIKINI KWA MAKUSUDI ILI WANUNULIKE KWA BEI YA CHEE WAKATI WA UCHAGUZI!

MAMA ANNA ALUTA CONTINUA! HUYO FISADI KISUMO ATALEGEA TU! NIJISIKIA KUMUITA MJINGA NA ANAZEEKA VIABAYA KAMA kiN...
 
Kisumo alitumika kuiua KNCU huyu jamaa alikuwa kibaraka mkubwa aliyekuwa akiitikia ndio mzee bila kuclick kwenye kichwa chake. Jamaa hafai pamoja na kuwa ni mwanasiasa mwandamizi wa CCM.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom