Peter Kibatala: Tumeulizwa sana kuelezea kuhusu nini kinaendelea katika kesi ya Godbless Lema

Francis12

JF-Expert Member
Sep 30, 2016
7,533
22,276
Tumeulizwa sana kuelezea kuhusu nini kinaendelea katika case ya Godbless Jonathan Lema; na ninatoa full history hapa chini bila kuathiri Sub Judice Rule. Nitaelezea kilichotokea kama ambavyo kinavyoonekana katika records:

Tarehe 8 November 2016 Godbless Jonathan Lema alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha akishtakiwa kwa makosa mawili yanatokana na kile anachosema alikiota. Alishtakiwa katika case Nambari 441 na 442/2016. Case zikapangiwa kwa Hakimu mh. Kamigisha.

Upande wa Serikali ukapinga dhamana, na wakaleta kiapo cha Afisa wa Polisi kwamba, pamoja na sababu nyingine, ni kwa usalama wa Lema mwenyewe kubaki ndani bila dhamana.

Pakatokea mabishano ya kisheria; Mawakili wa Lemana Mahakama ikapanga kutoa uamuzi qa dhamana mnamo 11th November 2016. 11th November 2016 Mahakama ikaamuru Lema apate dhamana kwa masharti itakayotaweka. Mara tu baada ya Mahakama kutamka hivyo, lakini kabla masharti hayajatamkwa upande wa Serikali ukiongozwa na Wakili Paul Kadushi ukasimama na kutoa Notisi ya mdomo ya kusudio la kukata Rufaa kwa kuwa hawakuridhishwa na uamuzi wa kumpa dhamana Lema. Notisi ilitolewa chini ya sheria ya National Prosecution Services Act yenye kifungu kinachosema pale Serikali inapotoa Notisi ya kusudio la kukata Rufaa, basi ni kama Rufaa tayari imekatwa kisheria. Wakadai kwamba kwa kuwa tayari kuna Notisi ya kusudio la kukata Rufaa dhidi ya uamuzi wa kumpa Lema dhamana, basi Mahakama haina budi kusimamisha zoezi la dhamana mpaka Rufaa iamuliwe na Mahakama Kuu.

Yakaibuka mabishano mapya ya kisheria ya iwapo ni sahihi kwa Mahakama kusitisha zezi la dhamana wakati tayari imeshatamka kwamba dhamana iko wazi. Mahakama ikaamuru kwamba mikono yake imefungwa na Notisi ile.

Sisi hatukuridhika, na msimamo wetu ukawa kwamba mara tu baada ya Mahakama kutamka kwamba dhamana iko wazi, haina budi kuweka masharti ya dhamana na kumuachia Lema; na kama mtu anakata Rufaa, basi akate wakati Mahakama inasimamia na kukamilisha amri yake ya dhamana. Tukachukua hatua ya kuandika barua ya malalamiko kwa Judge Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ambayo ndiye msimamizi wa Mahakama zote za chini ili aitishe majalada ya cases husika na ili yakaguliwe na kujiridhisha kwamba Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ilisimamia vizuri mamlaka yake ya dhamana.
Njia hii imewahi kutumika mara kadhaa, na Mahakama za juu zimewahi hata zenyewe kuitisha majalada ya Mahakama zikipata taarifa kwa namna yoyote kwamba kuna tatizo la kisheria katika Mahakama ya chini. Kwa mfano pale ambapo Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ilipotoa Hati ya Kukamatwa Askofu Mokiwa, Mahakama ya Rufaa iliitisha jalada husika na kutengua amri ile. Ilifanya hivyo chini ya Mamlaka yake ya Usimamizi wa mahakama za chini yake bila mtu kukata Rufaa.

Baada ya kupokea barua yetu, Mahakama Kuu Arusha ikatuita ili itusikilize 18th November 2016. Siku ya kusikilizwa Serikali wakawasilisha pingamizi kwamba tulitakiwa kukata Rufaa. Sisi tukasisitiza kwamba 1.huwezi weka pingamizi kwa hoja iliyoibuliwa na Mahakama kwa maana ya kwamba tumeitwa na Mahakama yenyewe. 2. Kwamba kwa kuwa kuna kosa la wazi likilofanywa na Mahakama ya chini, Mahakama Kuu ina mamlaka na wajibu wa kulirekebisha bila kujali imepataje taarifa, na kwamba hiyo si mara ya kwanza wala ya mwisho Mahakama Kuu kufanya hivyo.

Mahakama Kuu (Moshi J) katika uamuzi wake wa 22nd November 2016 ikaamuru tulitakiwa kukata Rufaa.

Tukawa na tatizo kubwa la kisheria; wakati majalada yameitwa baada ya barua yetu, tusingeweza kutoa notisi ya kusudio la kukata rufaa kwani kwa kufanya hivyo tungekuwa tunajipiga ngwala wenyewe kwani huwezi omba marejeo ( kuiomba Mahakama Kuu ipitie majalada ya case husika) na kukata rufaa wakati huo huo.

Wakati Mahakama inatoa uamuzi kwamba ilitakiwa tukate rufaa, tayari siku 10 za kuta Notisi zishapita. Mahesabu tuliyofanya ilikuwa kwamba uamuzi wa dhamana ulitolewa Ijumaa 11th November saa 11 jioni. Siku inayofuata ilikuwa Jumamosi na kisha Jumapili. Kwa mujibu ya Interpration of Laws Act, Ijumaa 11th November 2016 haihesabiwi; hilo halikuwa na utata. Taabu ilikuwa kwamba sisi tulitoa notisi 22nd December mara tu baada ya uamuzi wa Moshi, J.

Mahakama Kuu (Masengi, J) ikaamuru kwamba zinajumuishwa, na kwamba Notisi yetu imechelewa kwa siku moja na kwamba siku ya mwisho ilikuwa 21st November 2016 (siku moja kabla Mahakama Kuu haijatoa uamuzi juu ya ombi la marejeo 22nd November 2016).

Tukawasilisha maombi ya nyongeza ya muda ili kutoa Notisi, na Mahakama Kuu ikatupa siku 10 za ziada mnamo 20th December 2016. Serikali hawakuridhishwa, na wakatoa Notisi ya kusudio la kukata Rufaa mnamo 21st December 2016.

Sisi tukawa tumewasilisha notisi pamoja na hati ya Rufaa. Lalamiko letu kuu ni kwamba Mahakama ya Hakimu Mkazi ilikosea kuacha kumpa dhamana Lema wakati kifungu cha 148 (6) cha Criminal Procedure Act kiko wazi kwamba ukisema 'dhamana iko wazi', lazima uweke masharti na kwamba dhamana na masharti yake havitenganishiki kisheria.

Rufaa yeti ikapangwa kusikilizwa 28th December 2016 mbele ya Maghimbi, J.

Wakati huo huo, Serikali wakawa wamewasilisha Rufaa iliyotokana na Notisi yao ya 11th November 2016 wakipinga Lema kupewa dhamana. Nayo ikapangiwa kusikilizwa 28th December 2016 mbele ya Maghimbi, J.
So kuna rufaa mbili mbele ya Maghimbi,J; ya Lema na ya Serikali. Zote kimsingi zinalalamikia uamuzi wa kumpa/kumnyima Lema dhamana lakini kwa mtazamo tofauti.

28th November 2016 Serikali ikadai kwamba Rufaa yetu haiwezi kuendelea kusikilizwa kwa kuwa kuna Notisi ya kusudio la kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa kutupa nyongeza ya muda kukata rufaa. Sisi tukasema, 'No problems'; tusimamishe rufaa yetu na kwa kuwa hakuna kizuizi cha kisheria dhidi ya rufaa ye serikali, basi isikilizwe hiyo. Jibu ni lile lile kwa swali la; Je, Mahakama ya Hakimu Mkazi ilipatia au ilikosea kuamuru Lema apate dhamana?.

Serikali wakaomba Rufaa yao isikilizwe kwa njia ya maandishi. Tukakubaliana hivyo by consent na records zinaonesha hivyo.

Mahakama ikaamuru rufaa ya Serikali isikilizwe kwa maandishi kama Serikali wenyewe walivyoomba. Ikapangwa; Serikali walete hoja zao mnamo 29th December 2016, Sisi tulete majibu 30th December 2016, na Serikali wajibu tena 2nd January 2017. Hukumu ikapangwa 4th January 2017.

29th December 2016 badala ya Serikali kuwasilisha hoja zao za Rufaa yao wao wenyewe; wakapeleka Notisi ya kusudio la kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu kuamuru Rufaa yao isikilizwe wakati tayari kuna Notisi dhidi ya Rufaa ya Lema.

Sisi tukatii amri ya Mahakama na tukawasilisha hoja zetu kama tulivyoamriwa. Tukaomba Mahakama itupe Rufaa ya Serikali kwa kuwa wamegoma/wameshindwa kwa makusudi kuendesha Rufaa yao wenyewe wakati amri ya Mahakama ilitokana na maombi yao wenyewe kwamba wako tayari Rufaa yao isikilizwe, na wao wenyewe wakaomba isikilizwe kwa maandishi; so, wanamkatia rufaa nani na kwa mantiki ipi ya kisheria? Tukasema pia kwamba hata Notisi yenyewe haihusiani na Rufaa yao, bali iliwekwa dhidi ya Rufaa ya Lema; ambayo tayari tuliomba kuisubirisha. Tukasema pia kwamba hata hivyo, Notisi husika ina mapungufu lukuki ya kisheria ikiwemo kukosea vifungu vya sheria. Tukasema kinachofanyika ni ujeuri wa kiTaasisi na kuikosea heshima Mahakama na mfumo wa haki kwa ujumla bila sababu za msingi.
Tukaiomba Mahakama itupe rufaa ya Serikali na kumpa yenyewe Lema dhamana.

Serikali wakagoma kupokea nakala ya hoja zetu za kimaandishi tuliyowapelekea ofisini kwao kwa mujibu wa amri ya Mahakama. Tukatafuta mpeleka wito wa Mahakama na akala kiapo kwamba Serikali wamegoma kupokea na tukawasilisha Mahakamani.

Tukasubiri Uamuzi 4th January 2017 kama ilivyopangwa. Tulitegemea kabisa Mahakama kutupilia mbali Rufaa ya Serikali.

Mahakama ikasema ime-note yote yaliyotokea; lakini mikono yake imefungwa na Notisi ya kusudio la kukata rufaa ya serikali iliyowasilishwa badala ya hoja za maandishi kama ilivyoamuru Mahakama yenyewe.

Baada tu ya kutoka Mahakamani hiyo 4th January 2017 tukaletewa taarifa ya kimandishi (Notice to withdraw Notice of Appeal) kwamba Serikali imeondoa ile Notisi ya 21st December 2016 (iliyokatia Rufaa sisi kupewa nyongeza ya muda kukata rufaa). Badala yake siku hiyo Serikali ikawasilisha Notisi mpya ili kufidia (replace) hiyo waliyoindoa.

Mahakama Kuu Arusha imefanya mambo mawili; 1.imepeleka Notisi ya Serikali ya 21st December 2016, Notisi ya kuondoa Notisi ya 21st December na Notisi mpya ya 4th January 2017 Mahakama ya Rufaa ili zishughulikiwe kwa mujibubwa kanuni za Mahakama ya Rufaa. Kanuni ya 77 inaeleleza kwamba ukiondoa notisi, Mahakama ya Rufaa inaifuta rasmi kwa mkono wa Msajili/Judge Mkuu. Kwa hiyo tunasubiri kupata taarifa ya kufutwa kwa notisi ya 21st December 2016 na kisha tubaki na kushughulikia Notisi ya 4th January 2017.

Mahakama Kuu Arusha pia imetoa nakala za mwenendo kwa pande zote na kusisitiza Serikali kuwasilisha Rufaa yake kwa haraka kwa mujibu wa sheria. Tunasubiri kushughulika na Rufaa hiyo kusudiwa (kama itakatwa) kwani ndiyo imesubirisha mambo yote ya dhamana (kwa mujibu wa uamuzi wa Mahakama Kuu wa 4th January 2017).

Tunaamini tutapata suluhisho la kudumu muda si mrefu. Mahakama ya Rufaa ndiyo ya mwisho.

Lema yuko imara sana, sana; na keshakuwa kama Mwanasheria na yeye huko aliko; anajua kila kitu cha kiSheria siku hizi.

Amesisitiza suala hili lipatiwe majibu ya kudumu kwani precedent inayoweza kuwekwa inaweza kuwa na madhara makubwa ya kisheria kwa watu wengine; hasa suala la dhamana vs Notisi ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa dhamana na iwapo inasimamisha uwekaji wa masharti ya dhamana.
 
Lema yuko imara sana, sana; na keshakuwa kama Mwanasheria na yeye huko aliko; anajua kila kitu cha kiSheria siku hizi.

Amesisitiza suala hili lipatiwe majibu ya kudumu kwani precedent inayoweza kuwekwa inaweza kuwa na madhara makubwa ya kisheria kwa watu wengine; hasa suala la dhamana vs Notisi ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa dhamana na iwapo inasimamisha uwekaji wa masharti ya dhamana.
 
Tumeulizwa sana kuelezea kuhusu nini kinaendelea katika case ya Godbless Jonathan Lema; na ninatoa full history hapa chini bila kuathiri Sub Judice Rule. Nitaelezea kilichotokea kama ambavyo kinavyoonekana katika records:

Tarehe 8 November 2016 Godbless Jonathan Lema alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha akishtakiwa kwa makosa mawili yanatokana na kile anachosema alikiota. Alishtakiwa katika case Nambari 441 na 442/2016. Case zikapangiwa kwa Hakimu mh. Kamigisha.

Upande wa Serikali ukapinga dhamana, na wakaleta kiapo cha Afisa wa Polisi kwamba, pamoja na sababu nyingine, ni kwa usalama wa Lema mwenyewe kubaki ndani bila dhamana.

Pakatokea mabishano ya kisheria; Mawakili wa Lemana Mahakama ikapanga kutoa uamuzi qa dhamana mnamo 11th November 2016. 11th November 2016 Mahakama ikaamuru Lema apate dhamana kwa masharti itakayotaweka. Mara tu baada ya Mahakama kutamka hivyo, lakini kabla masharti hayajatamkwa upande wa Serikali ukiongozwa na Wakili Paul Kadushi ukasimama na kutoa Notisi ya mdomo ya kusudio la kukata Rufaa kwa kuwa hawakuridhishwa na uamuzi wa kumpa dhamana Lema. Notisi ilitolewa chini ya sheria ya National Prosecution Services Act yenye kifungu kinachosema pale Serikali inapotoa Notisi ya kusudio la kukata Rufaa, basi ni kama Rufaa tayari imekatwa kisheria. Wakadai kwamba kwa kuwa tayari kuna Notisi ya kusudio la kukata Rufaa dhidi ya uamuzi wa kumpa Lema dhamana, basi Mahakama haina budi kusimamisha zoezi la dhamana mpaka Rufaa iamuliwe na Mahakama Kuu.

Yakaibuka mabishano mapya ya kisheria ya iwapo ni sahihi kwa Mahakama kusitisha zezi la dhamana wakati tayari imeshatamka kwamba dhamana iko wazi. Mahakama ikaamuru kwamba mikono yake imefungwa na Notisi ile.

Sisi hatukuridhika, na msimamo wetu ukawa kwamba mara tu baada ya Mahakama kutamka kwamba dhamana iko wazi, haina budi kuweka masharti ya dhamana na kumuachia Lema; na kama mtu anakata Rufaa, basi akate wakati Mahakama inasimamia na kukamilisha amri yake ya dhamana. Tukachukua hatua ya kuandika barua ya malalamiko kwa Judge Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ambayo ndiye msimamizi wa Mahakama zote za chini ili aitishe majalada ya cases husika na ili yakaguliwe na kujiridhisha kwamba Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ilisimamia vizuri mamlaka yake ya dhamana.
Njia hii imewahi kutumika mara kadhaa, na Mahakama za juu zimewahi hata zenyewe kuitisha majalada ya Mahakama zikipata taarifa kwa namna yoyote kwamba kuna tatizo la kisheria katika Mahakama ya chini. Kwa mfano pale ambapo Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ilipotoa Hati ya Kukamatwa Askofu Mokiwa, Mahakama ya Rufaa iliitisha jalada husika na kutengua amri ile. Ilifanya hivyo chini ya Mamlaka yake ya Usimamizi wa mahakama za chini yake bila mtu kukata Rufaa.

Baada ya kupokea barua yetu, Mahakama Kuu Arusha ikatuita ili itusikilize 18th November 2016. Siku ya kusikilizwa Serikali wakawasilisha pingamizi kwamba tulitakiwa kukata Rufaa. Sisi tukasisitiza kwamba 1.huwezi weka pingamizi kwa hoja iliyoibuliwa na Mahakama kwa maana ya kwamba tumeitwa na Mahakama yenyewe. 2. Kwamba kwa kuwa kuna kosa la wazi likilofanywa na Mahakama ya chini, Mahakama Kuu ina mamlaka na wajibu wa kulirekebisha bila kujali imepataje taarifa, na kwamba hiyo si mara ya kwanza wala ya mwisho Mahakama Kuu kufanya hivyo.

Mahakama Kuu (Moshi J) katika uamuzi wake wa 22nd November 2016 ikaamuru tulitakiwa kukata Rufaa.

Tukawa na tatizo kubwa la kisheria; wakati majalada yameitwa baada ya barua yetu, tusingeweza kutoa notisi ya kusudio la kukata rufaa kwani kwa kufanya hivyo tungekuwa tunajipiga ngwala wenyewe kwani huwezi omba marejeo ( kuiomba Mahakama Kuu ipitie majalada ya case husika) na kukata rufaa wakati huo huo.

Wakati Mahakama inatoa uamuzi kwamba ilitakiwa tukate rufaa, tayari siku 10 za kuta Notisi zishapita. Mahesabu tuliyofanya ilikuwa kwamba uamuzi wa dhamana ulitolewa Ijumaa 11th November saa 11 jioni. Siku inayofuata ilikuwa Jumamosi na kisha Jumapili. Kwa mujibu ya Interpration of Laws Act, Ijumaa 11th November 2016 haihesabiwi; hilo halikuwa na utata. Taabu ilikuwa kwamba sisi tulitoa notisi 22nd December mara tu baada ya uamuzi wa Moshi, J.

Mahakama Kuu (Masengi, J) ikaamuru kwamba zinajumuishwa, na kwamba Notisi yetu imechelewa kwa siku moja na kwamba siku ya mwisho ilikuwa 21st November 2016 (siku moja kabla Mahakama Kuu haijatoa uamuzi juu ya ombi la marejeo 22nd November 2016).

Tukawasilisha maombi ya nyongeza ya muda ili kutoa Notisi, na Mahakama Kuu ikatupa siku 10 za ziada mnamo 20th December 2016. Serikali hawakuridhishwa, na wakatoa Notisi ya kusudio la kukata Rufaa mnamo 21st December 2016.

Sisi tukawa tumewasilisha notisi pamoja na hati ya Rufaa. Lalamiko letu kuu ni kwamba Mahakama ya Hakimu Mkazi ilikosea kuacha kumpa dhamana Lema wakati kifungu cha 148 (6) cha Criminal Procedure Act kiko wazi kwamba ukisema 'dhamana iko wazi', lazima uweke masharti na kwamba dhamana na masharti yake havitenganishiki kisheria.

Rufaa yeti ikapangwa kusikilizwa 28th December 2016 mbele ya Maghimbi, J.

Wakati huo huo, Serikali wakawa wamewasilisha Rufaa iliyotokana na Notisi yao ya 11th November 2016 wakipinga Lema kupewa dhamana. Nayo ikapangiwa kusikilizwa 28th December 2016 mbele ya Maghimbi, J.
So kuna rufaa mbili mbele ya Maghimbi,J; ya Lema na ya Serikali. Zote kimsingi zinalalamikia uamuzi wa kumpa/kumnyima Lema dhamana lakini kwa mtazamo tofauti.

28th November 2016 Serikali ikadai kwamba Rufaa yetu haiwezi kuendelea kusikilizwa kwa kuwa kuna Notisi ya kusudio la kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa kutupa nyongeza ya muda kukata rufaa. Sisi tukasema, 'No problems'; tusimamishe rufaa yetu na kwa kuwa hakuna kizuizi cha kisheria dhidi ya rufaa ye serikali, basi isikilizwe hiyo. Jibu ni lile lile kwa swali la; Je, Mahakama ya Hakimu Mkazi ilipatia au ilikosea kuamuru Lema apate dhamana?.

Serikali wakaomba Rufaa yao isikilizwe kwa njia ya maandishi. Tukakubaliana hivyo by consent na records zinaonesha hivyo.

Mahakama ikaamuru rufaa ya Serikali isikilizwe kwa maandishi kama Serikali wenyewe walivyoomba. Ikapangwa; Serikali walete hoja zao mnamo 29th December 2016, Sisi tulete majibu 30th December 2016, na Serikali wajibu tena 2nd January 2017. Hukumu ikapangwa 4th January 2017.

29th December 2016 badala ya Serikali kuwasilisha hoja zao za Rufaa yao wao wenyewe; wakapeleka Notisi ya kusudio la kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu kuamuru Rufaa yao isikilizwe wakati tayari kuna Notisi dhidi ya Rufaa ya Lema.

Sisi tukatii amri ya Mahakama na tukawasilisha hoja zetu kama tulivyoamriwa. Tukaomba Mahakama itupe Rufaa ya Serikali kwa kuwa wamegoma/wameshindwa kwa makusudi kuendesha Rufaa yao wenyewe wakati amri ya Mahakama ilitokana na maombi yao wenyewe kwamba wako tayari Rufaa yao isikilizwe, na wao wenyewe wakaomba isikilizwe kwa maandishi; so, wanamkatia rufaa nani na kwa mantiki ipi ya kisheria? Tukasema pia kwamba hata Notisi yenyewe haihusiani na Rufaa yao, bali iliwekwa dhidi ya Rufaa ya Lema; ambayo tayari tuliomba kuisubirisha. Tukasema pia kwamba hata hivyo, Notisi husika ina mapungufu lukuki ya kisheria ikiwemo kukosea vifungu vya sheria. Tukasema kinachofanyika ni ujeuri wa kiTaasisi na kuikosea heshima Mahakama na mfumo wa haki kwa ujumla bila sababu za msingi.
Tukaiomba Mahakama itupe rufaa ya Serikali na kumpa yenyewe Lema dhamana.

Serikali wakagoma kupokea nakala ya hoja zetu za kimaandishi tuliyowapelekea ofisini kwao kwa mujibu wa amri ya Mahakama. Tukatafuta mpeleka wito wa Mahakama na akala kiapo kwamba Serikali wamegoma kupokea na tukawasilisha Mahakamani.

Tukasubiri Uamuzi 4th January 2017 kama ilivyopangwa. Tulitegemea kabisa Mahakama kutupilia mbali Rufaa ya Serikali.

Mahakama ikasema ime-note yote yaliyotokea; lakini mikono yake imefungwa na Notisi ya kusudio la kukata rufaa ya serikali iliyowasilishwa badala ya hoja za maandishi kama ilivyoamuru Mahakama yenyewe.

Baada tu ya kutoka Mahakamani hiyo 4th January 2017 tukaletewa taarifa ya kimandishi (Notice to withdraw Notice of Appeal) kwamba Serikali imeondoa ile Notisi ya 21st December 2016 (iliyokatia Rufaa sisi kupewa nyongeza ya muda kukata rufaa). Badala yake siku hiyo Serikali ikawasilisha Notisi mpya ili kufidia (replace) hiyo waliyoindoa.

Mahakama Kuu Arusha imefanya mambo mawili; 1.imepeleka Notisi ya Serikali ya 21st December 2016, Notisi ya kuondoa Notisi ya 21st December na Notisi mpya ya 4th January 2017 Mahakama ya Rufaa ili zishughulikiwe kwa mujibubwa kanuni za Mahakama ya Rufaa. Kanuni ya 77 inaeleleza kwamba ukiondoa notisi, Mahakama ya Rufaa inaifuta rasmi kwa mkono wa Msajili/Judge Mkuu. Kwa hiyo tunasubiri kupata taarifa ya kufutwa kwa notisi ya 21st December 2016 na kisha tubaki na kushughulikia Notisi ya 4th January 2017.

Mahakama Kuu Arusha pia imetoa nakala za mwenendo kwa pande zote na kusisitiza Serikali kuwasilisha Rufaa yake kwa haraka kwa mujibu wa sheria. Tunasubiri kushughulika na Rufaa hiyo kusudiwa (kama itakatwa) kwani ndiyo imesubirisha mambo yote ya dhamana (kwa mujibu wa uamuzi wa Mahakama Kuu wa 4th January 2017).

Tunaamini tutapata suluhisho la kudumu muda si mrefu. Mahakama ya Rufaa ndiyo ya mwisho.

Lema yuko imara sana, sana; na keshakuwa kama Mwanasheria na yeye huko aliko; anajua kila kitu cha kiSheria siku hizi.

Amesisitiza suala hili lipatiwe majibu ya kudumu kwani precedent inayoweza kuwekwa inaweza kuwa na madhara makubwa ya kisheria kwa watu wengine; hasa suala la dhamana vs Notisi ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa dhamana na iwapo inasimamisha uwekaji wa masharti ya dhamana.
Mwenendo wa kesi unaonyesha wanasheria wa Lema hawajaiva.Wanasheria wa serikali wanatumia mbinu za kisheria kumbakisha Lema

Wanasheria wa Lema wajipange hadi hapa walipofika wamefeli kwa sehemu kubwa
 
Tumeulizwa sana kuelezea kuhusu nini kinaendelea katika case ya Godbless Jonathan Lema; na ninatoa full history hapa chini bila kuathiri Sub Judice Rule. Nitaelezea kilichotokea kama ambavyo kinavyoonekana katika records:

Tarehe 8 November 2016 Godbless Jonathan Lema alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha akishtakiwa kwa makosa mawili yanatokana na kile anachosema alikiota. Alishtakiwa katika case Nambari 441 na 442/2016. Case zikapangiwa kwa Hakimu mh. Kamigisha.

Upande wa Serikali ukapinga dhamana, na wakaleta kiapo cha Afisa wa Polisi kwamba, pamoja na sababu nyingine, ni kwa usalama wa Lema mwenyewe kubaki ndani bila dhamana.

Pakatokea mabishano ya kisheria; Mawakili wa Lemana Mahakama ikapanga kutoa uamuzi qa dhamana mnamo 11th November 2016. 11th November 2016 Mahakama ikaamuru Lema apate dhamana kwa masharti itakayotaweka. Mara tu baada ya Mahakama kutamka hivyo, lakini kabla masharti hayajatamkwa upande wa Serikali ukiongozwa na Wakili Paul Kadushi ukasimama na kutoa Notisi ya mdomo ya kusudio la kukata Rufaa kwa kuwa hawakuridhishwa na uamuzi wa kumpa dhamana Lema. Notisi ilitolewa chini ya sheria ya National Prosecution Services Act yenye kifungu kinachosema pale Serikali inapotoa Notisi ya kusudio la kukata Rufaa, basi ni kama Rufaa tayari imekatwa kisheria. Wakadai kwamba kwa kuwa tayari kuna Notisi ya kusudio la kukata Rufaa dhidi ya uamuzi wa kumpa Lema dhamana, basi Mahakama haina budi kusimamisha zoezi la dhamana mpaka Rufaa iamuliwe na Mahakama Kuu.

Yakaibuka mabishano mapya ya kisheria ya iwapo ni sahihi kwa Mahakama kusitisha zezi la dhamana wakati tayari imeshatamka kwamba dhamana iko wazi. Mahakama ikaamuru kwamba mikono yake imefungwa na Notisi ile.

Sisi hatukuridhika, na msimamo wetu ukawa kwamba mara tu baada ya Mahakama kutamka kwamba dhamana iko wazi, haina budi kuweka masharti ya dhamana na kumuachia Lema; na kama mtu anakata Rufaa, basi akate wakati Mahakama inasimamia na kukamilisha amri yake ya dhamana. Tukachukua hatua ya kuandika barua ya malalamiko kwa Judge Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ambayo ndiye msimamizi wa Mahakama zote za chini ili aitishe majalada ya cases husika na ili yakaguliwe na kujiridhisha kwamba Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ilisimamia vizuri mamlaka yake ya dhamana.
Njia hii imewahi kutumika mara kadhaa, na Mahakama za juu zimewahi hata zenyewe kuitisha majalada ya Mahakama zikipata taarifa kwa namna yoyote kwamba kuna tatizo la kisheria katika Mahakama ya chini. Kwa mfano pale ambapo Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ilipotoa Hati ya Kukamatwa Askofu Mokiwa, Mahakama ya Rufaa iliitisha jalada husika na kutengua amri ile. Ilifanya hivyo chini ya Mamlaka yake ya Usimamizi wa mahakama za chini yake bila mtu kukata Rufaa.

Baada ya kupokea barua yetu, Mahakama Kuu Arusha ikatuita ili itusikilize 18th November 2016. Siku ya kusikilizwa Serikali wakawasilisha pingamizi kwamba tulitakiwa kukata Rufaa. Sisi tukasisitiza kwamba 1.huwezi weka pingamizi kwa hoja iliyoibuliwa na Mahakama kwa maana ya kwamba tumeitwa na Mahakama yenyewe. 2. Kwamba kwa kuwa kuna kosa la wazi likilofanywa na Mahakama ya chini, Mahakama Kuu ina mamlaka na wajibu wa kulirekebisha bila kujali imepataje taarifa, na kwamba hiyo si mara ya kwanza wala ya mwisho Mahakama Kuu kufanya hivyo.

Mahakama Kuu (Moshi J) katika uamuzi wake wa 22nd November 2016 ikaamuru tulitakiwa kukata Rufaa.

Tukawa na tatizo kubwa la kisheria; wakati majalada yameitwa baada ya barua yetu, tusingeweza kutoa notisi ya kusudio la kukata rufaa kwani kwa kufanya hivyo tungekuwa tunajipiga ngwala wenyewe kwani huwezi omba marejeo ( kuiomba Mahakama Kuu ipitie majalada ya case husika) na kukata rufaa wakati huo huo.

Wakati Mahakama inatoa uamuzi kwamba ilitakiwa tukate rufaa, tayari siku 10 za kuta Notisi zishapita. Mahesabu tuliyofanya ilikuwa kwamba uamuzi wa dhamana ulitolewa Ijumaa 11th November saa 11 jioni. Siku inayofuata ilikuwa Jumamosi na kisha Jumapili. Kwa mujibu ya Interpration of Laws Act, Ijumaa 11th November 2016 haihesabiwi; hilo halikuwa na utata. Taabu ilikuwa kwamba sisi tulitoa notisi 22nd December mara tu baada ya uamuzi wa Moshi, J.

Mahakama Kuu (Masengi, J) ikaamuru kwamba zinajumuishwa, na kwamba Notisi yetu imechelewa kwa siku moja na kwamba siku ya mwisho ilikuwa 21st November 2016 (siku moja kabla Mahakama Kuu haijatoa uamuzi juu ya ombi la marejeo 22nd November 2016).

Tukawasilisha maombi ya nyongeza ya muda ili kutoa Notisi, na Mahakama Kuu ikatupa siku 10 za ziada mnamo 20th December 2016. Serikali hawakuridhishwa, na wakatoa Notisi ya kusudio la kukata Rufaa mnamo 21st December 2016.

Sisi tukawa tumewasilisha notisi pamoja na hati ya Rufaa. Lalamiko letu kuu ni kwamba Mahakama ya Hakimu Mkazi ilikosea kuacha kumpa dhamana Lema wakati kifungu cha 148 (6) cha Criminal Procedure Act kiko wazi kwamba ukisema 'dhamana iko wazi', lazima uweke masharti na kwamba dhamana na masharti yake havitenganishiki kisheria.

Rufaa yeti ikapangwa kusikilizwa 28th December 2016 mbele ya Maghimbi, J.

Wakati huo huo, Serikali wakawa wamewasilisha Rufaa iliyotokana na Notisi yao ya 11th November 2016 wakipinga Lema kupewa dhamana. Nayo ikapangiwa kusikilizwa 28th December 2016 mbele ya Maghimbi, J.
So kuna rufaa mbili mbele ya Maghimbi,J; ya Lema na ya Serikali. Zote kimsingi zinalalamikia uamuzi wa kumpa/kumnyima Lema dhamana lakini kwa mtazamo tofauti.

28th November 2016 Serikali ikadai kwamba Rufaa yetu haiwezi kuendelea kusikilizwa kwa kuwa kuna Notisi ya kusudio la kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa kutupa nyongeza ya muda kukata rufaa. Sisi tukasema, 'No problems'; tusimamishe rufaa yetu na kwa kuwa hakuna kizuizi cha kisheria dhidi ya rufaa ye serikali, basi isikilizwe hiyo. Jibu ni lile lile kwa swali la; Je, Mahakama ya Hakimu Mkazi ilipatia au ilikosea kuamuru Lema apate dhamana?.

Serikali wakaomba Rufaa yao isikilizwe kwa njia ya maandishi. Tukakubaliana hivyo by consent na records zinaonesha hivyo.

Mahakama ikaamuru rufaa ya Serikali isikilizwe kwa maandishi kama Serikali wenyewe walivyoomba. Ikapangwa; Serikali walete hoja zao mnamo 29th December 2016, Sisi tulete majibu 30th December 2016, na Serikali wajibu tena 2nd January 2017. Hukumu ikapangwa 4th January 2017.

29th December 2016 badala ya Serikali kuwasilisha hoja zao za Rufaa yao wao wenyewe; wakapeleka Notisi ya kusudio la kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu kuamuru Rufaa yao isikilizwe wakati tayari kuna Notisi dhidi ya Rufaa ya Lema.

Sisi tukatii amri ya Mahakama na tukawasilisha hoja zetu kama tulivyoamriwa. Tukaomba Mahakama itupe Rufaa ya Serikali kwa kuwa wamegoma/wameshindwa kwa makusudi kuendesha Rufaa yao wenyewe wakati amri ya Mahakama ilitokana na maombi yao wenyewe kwamba wako tayari Rufaa yao isikilizwe, na wao wenyewe wakaomba isikilizwe kwa maandishi; so, wanamkatia rufaa nani na kwa mantiki ipi ya kisheria? Tukasema pia kwamba hata Notisi yenyewe haihusiani na Rufaa yao, bali iliwekwa dhidi ya Rufaa ya Lema; ambayo tayari tuliomba kuisubirisha. Tukasema pia kwamba hata hivyo, Notisi husika ina mapungufu lukuki ya kisheria ikiwemo kukosea vifungu vya sheria. Tukasema kinachofanyika ni ujeuri wa kiTaasisi na kuikosea heshima Mahakama na mfumo wa haki kwa ujumla bila sababu za msingi.
Tukaiomba Mahakama itupe rufaa ya Serikali na kumpa yenyewe Lema dhamana.

Serikali wakagoma kupokea nakala ya hoja zetu za kimaandishi tuliyowapelekea ofisini kwao kwa mujibu wa amri ya Mahakama. Tukatafuta mpeleka wito wa Mahakama na akala kiapo kwamba Serikali wamegoma kupokea na tukawasilisha Mahakamani.

Tukasubiri Uamuzi 4th January 2017 kama ilivyopangwa. Tulitegemea kabisa Mahakama kutupilia mbali Rufaa ya Serikali.

Mahakama ikasema ime-note yote yaliyotokea; lakini mikono yake imefungwa na Notisi ya kusudio la kukata rufaa ya serikali iliyowasilishwa badala ya hoja za maandishi kama ilivyoamuru Mahakama yenyewe.

Baada tu ya kutoka Mahakamani hiyo 4th January 2017 tukaletewa taarifa ya kimandishi (Notice to withdraw Notice of Appeal) kwamba Serikali imeondoa ile Notisi ya 21st December 2016 (iliyokatia Rufaa sisi kupewa nyongeza ya muda kukata rufaa). Badala yake siku hiyo Serikali ikawasilisha Notisi mpya ili kufidia (replace) hiyo waliyoindoa.

Mahakama Kuu Arusha imefanya mambo mawili; 1.imepeleka Notisi ya Serikali ya 21st December 2016, Notisi ya kuondoa Notisi ya 21st December na Notisi mpya ya 4th January 2017 Mahakama ya Rufaa ili zishughulikiwe kwa mujibubwa kanuni za Mahakama ya Rufaa. Kanuni ya 77 inaeleleza kwamba ukiondoa notisi, Mahakama ya Rufaa inaifuta rasmi kwa mkono wa Msajili/Judge Mkuu. Kwa hiyo tunasubiri kupata taarifa ya kufutwa kwa notisi ya 21st December 2016 na kisha tubaki na kushughulikia Notisi ya 4th January 2017.

Mahakama Kuu Arusha pia imetoa nakala za mwenendo kwa pande zote na kusisitiza Serikali kuwasilisha Rufaa yake kwa haraka kwa mujibu wa sheria. Tunasubiri kushughulika na Rufaa hiyo kusudiwa (kama itakatwa) kwani ndiyo imesubirisha mambo yote ya dhamana (kwa mujibu wa uamuzi wa Mahakama Kuu wa 4th January 2017).

Tunaamini tutapata suluhisho la kudumu muda si mrefu. Mahakama ya Rufaa ndiyo ya mwisho.

Lema yuko imara sana, sana; na keshakuwa kama Mwanasheria na yeye huko aliko; anajua kila kitu cha kiSheria siku hizi.

Amesisitiza suala hili lipatiwe majibu ya kudumu kwani precedent inayoweza kuwekwa inaweza kuwa na madhara makubwa ya kisheria kwa watu wengine; hasa suala la dhamana vs Notisi ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa dhamana na iwapo inasimamisha uwekaji wa masharti ya dhamana.
Narudia tena nina wasi wasi na uwezo wa kisheria wa hawa mawakili wa Lema
 
Mwenendo wa kesi unaonyesha wanasheria wa Lema hawajaiva.Wanasheria wa serikali wanatumia mbinu za kisheria kumbakisha Lema

Wanasheria wa Lema wajipange hadi hapa walipofika wamefeli kwa sehemu kubwa
Tatizo lipo kwa mawakili wa serikali pamoja na Majaji wanasikiliza kesi ya Lema .
 
Mkuu Francis siku unatuanguangusha kwenye kutupa update siku za kes ya lema .tunaanza kukutilia shaka
 
Back
Top Bottom