Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
PETE HAILAZIMISHWI!
Umeanza na mtu mahusiano! Wewe ni "mgeli" umejiachia weeee, ukagundua mwanaume yupo kimaslahi! Si ukaanza kumbania salamu huku unamlazimisha akuvishe pete! Mwanaume akakukata jicho akaona dawa yako akupe matumaini, kwamba "ataangalia"... Shoga yako akakupasukia, akakuzodoa, kwamba "wach iti" wanaume hawalazimishwi, wanabembeleeeezwa taaaratibu!
Pepo mchafu akakuchochea, ukabwabwaja, kwamba waonewa wivu! Mara, shogako hakutakii mema, ukamnanga na kumchafua! Haikutosha ukamvizia usiku akienda kwake, ukiwa umebeba mawe kama selasini hivi, ukamrushia! Lengo umkomeshe! Kwa bahati shogako akatenguka kiwiko na goti.....
Hapo umepewa kideti kabisa, kwamba ujiandae kupokea booooonge la sapraiz, ambalo ni "wini wini" kwenu wawili! Basi bichwa limekujaa! Umeshakusanya matarumbeta, kukuimbia! Paukwa, pakawa, siku ikafika....
Pati si pati, kisherehe cha kimagumashi kikaanza! Nawe kwe umbea ukaanza kukirusha laivu fesbuk.... Muda ukafika, mwanaume amekuja mikono nyuma! Kashika dubwasha humo...ukajua leoooooooo, watakukoma!
Mwanaume akakusogelea! Mapigo ya moyo "kuchu! Kuchu! Kuchu" unajua umemuweza!
Mwanaume akapiga goti! Kabla hajaanza kusema kitu ukajibu "YEEEEEEEEES! Akafungua boksi! Ndani kuna KALAMU aina ya BIC! na ujumbe unaosema "UTUMIAPO KALAMU HII MKUMBUKE MHENGA ALIYESEMA "MALI BILA DAFTARI HUISHIA BILA HABARI"
Hapo ushuzi wa huzuni na kuchanganyikiwa utakuhusu!
Ndo ivo
©Bibi Happy J.
Umeanza na mtu mahusiano! Wewe ni "mgeli" umejiachia weeee, ukagundua mwanaume yupo kimaslahi! Si ukaanza kumbania salamu huku unamlazimisha akuvishe pete! Mwanaume akakukata jicho akaona dawa yako akupe matumaini, kwamba "ataangalia"... Shoga yako akakupasukia, akakuzodoa, kwamba "wach iti" wanaume hawalazimishwi, wanabembeleeeezwa taaaratibu!
Pepo mchafu akakuchochea, ukabwabwaja, kwamba waonewa wivu! Mara, shogako hakutakii mema, ukamnanga na kumchafua! Haikutosha ukamvizia usiku akienda kwake, ukiwa umebeba mawe kama selasini hivi, ukamrushia! Lengo umkomeshe! Kwa bahati shogako akatenguka kiwiko na goti.....
Hapo umepewa kideti kabisa, kwamba ujiandae kupokea booooonge la sapraiz, ambalo ni "wini wini" kwenu wawili! Basi bichwa limekujaa! Umeshakusanya matarumbeta, kukuimbia! Paukwa, pakawa, siku ikafika....
Pati si pati, kisherehe cha kimagumashi kikaanza! Nawe kwe umbea ukaanza kukirusha laivu fesbuk.... Muda ukafika, mwanaume amekuja mikono nyuma! Kashika dubwasha humo...ukajua leoooooooo, watakukoma!
Mwanaume akakusogelea! Mapigo ya moyo "kuchu! Kuchu! Kuchu" unajua umemuweza!
Mwanaume akapiga goti! Kabla hajaanza kusema kitu ukajibu "YEEEEEEEEES! Akafungua boksi! Ndani kuna KALAMU aina ya BIC! na ujumbe unaosema "UTUMIAPO KALAMU HII MKUMBUKE MHENGA ALIYESEMA "MALI BILA DAFTARI HUISHIA BILA HABARI"
Hapo ushuzi wa huzuni na kuchanganyikiwa utakuhusu!
Ndo ivo
©Bibi Happy J.