Gurudumu
JF-Expert Member
- Feb 5, 2008
- 2,349
- 261
Ndugu wana JF na wale ambao tumechangia kampeni kwa namna mbalimbali,
Uamuzi wa kuchangia kampeni za Dr. Slaa na CHADEMA kwa kupitia njia mbali mbali ulikuwa mzuri sana. Hivi karibuni kuna kundi linalojiita Friends of Slaa ambalo nalo linakusanya pesa kwa njia za electronic. Nawapongeza na kuwatakia ufanisi mzuri. Hata hivyo ningependa kuuliza taarifa ya mapato na matumizi na vile walivyojipanga katika lala salama.
1. Election materials kama bendera, kofia, T-shirts, stickers, beji za dr. slaa, n.k hazipatikani. Wakifika kwenye kampeni waliovaa ni wale tu ambao wamekuja na msafara vinginevyo kuna chache ambazo zinauzwa na tunatangaziwa ni kwa ajili ya kutunisha mfuko wa kampeni. Je, muda huu ambao watu wameshaamua si hizi materials zingegawiwa bure na kwa wingi kwa kutumia pesa ambazo zimeshakusanywa? Hatuwezi kuweka biashara pembeni ili kusaidia anguko la nguvu la CCM?
2. Kampeni za dr. slaa tunazichungulia kwenye taarifa za habari tu. Majuzi tulimuona kwenye mdahalo ITV na live kupitia TBC1 na Agape TV. Pia alialikwa kwenye mahojiano na Clouds FM. Lakini hata hizi hazikutangazwa kwa wingi ili wananchi wengi wawe na taarifa waweze kusikiliza/kutizama. Za kwenye TV wala hazikurudiwa na CHADEMA hawajalipia marudio. Swali ni kwamba, kwanini hizi pesa ambazo zinakusanywa zisitumike kulipia vipindi vya TV na redio? Kwa nini air time isinunuliwe kwenye radio za mikoa ile ambayo anatembelea ili warushe hotuba zake live? Siyo wananchi wote wanapata nafasi ya kufika eneo analohutubia lakini wangefaidika sana kama wangeweza kumsikiliza kwenye redio au TV. Hata kulipia matangazo ya ratiba yake pia imeshindikana? Kwa mfano, siku ya Jumamosi Dr. atakapohitimisha kampeni zake huku mbeya wananchi wanaweza kutizama na kusikiliza live? Hili ni muhimu ili aweze kujibu hoja za mkutano wa JK na waandishi wa habari wa tarehe 29 October.
Marafiki wa Dr. Slaa mnaweza kutolea haya mambo ufafanuzi. Kama maswali ya mapato na matumizi yanaweza kuwa magumu kwenu, basi tuarifuni tu mipango ya wananchi wote kupata fursa ya kusikiliza/kutazama hotuba yake ya mwisho hapo jumamosi. Mzee Mwanakijiji alikwisha tahadharisha kwamba hii hamasa iliyopo JF inahusisha watu wachache sana sana kwa hiyo tusidanganyike na ushabiki uliopo hapa tukadhani tayari tumeshashinda, ukiacha majimbo yale machache ambayo tayari tuna uhakika wa kushinda.
Uamuzi wa kuchangia kampeni za Dr. Slaa na CHADEMA kwa kupitia njia mbali mbali ulikuwa mzuri sana. Hivi karibuni kuna kundi linalojiita Friends of Slaa ambalo nalo linakusanya pesa kwa njia za electronic. Nawapongeza na kuwatakia ufanisi mzuri. Hata hivyo ningependa kuuliza taarifa ya mapato na matumizi na vile walivyojipanga katika lala salama.
1. Election materials kama bendera, kofia, T-shirts, stickers, beji za dr. slaa, n.k hazipatikani. Wakifika kwenye kampeni waliovaa ni wale tu ambao wamekuja na msafara vinginevyo kuna chache ambazo zinauzwa na tunatangaziwa ni kwa ajili ya kutunisha mfuko wa kampeni. Je, muda huu ambao watu wameshaamua si hizi materials zingegawiwa bure na kwa wingi kwa kutumia pesa ambazo zimeshakusanywa? Hatuwezi kuweka biashara pembeni ili kusaidia anguko la nguvu la CCM?
2. Kampeni za dr. slaa tunazichungulia kwenye taarifa za habari tu. Majuzi tulimuona kwenye mdahalo ITV na live kupitia TBC1 na Agape TV. Pia alialikwa kwenye mahojiano na Clouds FM. Lakini hata hizi hazikutangazwa kwa wingi ili wananchi wengi wawe na taarifa waweze kusikiliza/kutizama. Za kwenye TV wala hazikurudiwa na CHADEMA hawajalipia marudio. Swali ni kwamba, kwanini hizi pesa ambazo zinakusanywa zisitumike kulipia vipindi vya TV na redio? Kwa nini air time isinunuliwe kwenye radio za mikoa ile ambayo anatembelea ili warushe hotuba zake live? Siyo wananchi wote wanapata nafasi ya kufika eneo analohutubia lakini wangefaidika sana kama wangeweza kumsikiliza kwenye redio au TV. Hata kulipia matangazo ya ratiba yake pia imeshindikana? Kwa mfano, siku ya Jumamosi Dr. atakapohitimisha kampeni zake huku mbeya wananchi wanaweza kutizama na kusikiliza live? Hili ni muhimu ili aweze kujibu hoja za mkutano wa JK na waandishi wa habari wa tarehe 29 October.
Marafiki wa Dr. Slaa mnaweza kutolea haya mambo ufafanuzi. Kama maswali ya mapato na matumizi yanaweza kuwa magumu kwenu, basi tuarifuni tu mipango ya wananchi wote kupata fursa ya kusikiliza/kutazama hotuba yake ya mwisho hapo jumamosi. Mzee Mwanakijiji alikwisha tahadharisha kwamba hii hamasa iliyopo JF inahusisha watu wachache sana sana kwa hiyo tusidanganyike na ushabiki uliopo hapa tukadhani tayari tumeshashinda, ukiacha majimbo yale machache ambayo tayari tuna uhakika wa kushinda.