Elections 2010 Pesa wanazokusanya friends of slaa ziko wapi?

Gurudumu

JF-Expert Member
Feb 5, 2008
2,349
261
Ndugu wana JF na wale ambao tumechangia kampeni kwa namna mbalimbali,

Uamuzi wa kuchangia kampeni za Dr. Slaa na CHADEMA kwa kupitia njia mbali mbali ulikuwa mzuri sana. Hivi karibuni kuna kundi linalojiita Friends of Slaa ambalo nalo linakusanya pesa kwa njia za electronic. Nawapongeza na kuwatakia ufanisi mzuri. Hata hivyo ningependa kuuliza taarifa ya mapato na matumizi na vile walivyojipanga katika lala salama.

1. Election materials kama bendera, kofia, T-shirts, stickers, beji za dr. slaa, n.k hazipatikani. Wakifika kwenye kampeni waliovaa ni wale tu ambao wamekuja na msafara vinginevyo kuna chache ambazo zinauzwa na tunatangaziwa ni kwa ajili ya kutunisha mfuko wa kampeni. Je, muda huu ambao watu wameshaamua si hizi materials zingegawiwa bure na kwa wingi kwa kutumia pesa ambazo zimeshakusanywa? Hatuwezi kuweka biashara pembeni ili kusaidia anguko la nguvu la CCM?

2. Kampeni za dr. slaa tunazichungulia kwenye taarifa za habari tu. Majuzi tulimuona kwenye mdahalo ITV na live kupitia TBC1 na Agape TV. Pia alialikwa kwenye mahojiano na Clouds FM. Lakini hata hizi hazikutangazwa kwa wingi ili wananchi wengi wawe na taarifa waweze kusikiliza/kutizama. Za kwenye TV wala hazikurudiwa na CHADEMA hawajalipia marudio. Swali ni kwamba, kwanini hizi pesa ambazo zinakusanywa zisitumike kulipia vipindi vya TV na redio? Kwa nini air time isinunuliwe kwenye radio za mikoa ile ambayo anatembelea ili warushe hotuba zake live? Siyo wananchi wote wanapata nafasi ya kufika eneo analohutubia lakini wangefaidika sana kama wangeweza kumsikiliza kwenye redio au TV. Hata kulipia matangazo ya ratiba yake pia imeshindikana? Kwa mfano, siku ya Jumamosi Dr. atakapohitimisha kampeni zake huku mbeya wananchi wanaweza kutizama na kusikiliza live? Hili ni muhimu ili aweze kujibu hoja za mkutano wa JK na waandishi wa habari wa tarehe 29 October.

Marafiki wa Dr. Slaa mnaweza kutolea haya mambo ufafanuzi. Kama maswali ya mapato na matumizi yanaweza kuwa magumu kwenu, basi tuarifuni tu mipango ya wananchi wote kupata fursa ya kusikiliza/kutazama hotuba yake ya mwisho hapo jumamosi. Mzee Mwanakijiji alikwisha tahadharisha kwamba hii hamasa iliyopo JF inahusisha watu wachache sana sana kwa hiyo tusidanganyike na ushabiki uliopo hapa tukadhani tayari tumeshashinda, ukiacha majimbo yale machache ambayo tayari tuna uhakika wa kushinda.
 
Ndugu wana JF na wale ambao tumechangia kampeni kwa namna mbalimbali,

Uamuzi wa kuchangia kampeni za Dr. Slaa na CHADEMA kwa kupitia njia mbali mbali ulikuwa mzuri sana. Hivi karibuni kuna kundi linalojiita Friends of Slaa ambalo nalo linakusanya pesa kwa njia za electronic. Nawapongeza na kuwatakia ufanisi mzuri. Hata hivyo ningependa kuuliza taarifa ya mapato na matumizi na vile walivyojipanga katika lala salama.

1. Election materials kama bendera, kofia, T-shirts, stickers, beji za dr. slaa, n.k hazipatikani. Wakifika kwenye kampeni waliovaa ni wale tu ambao wamekuja na msafara vinginevyo kuna chache ambazo zinauzwa na tunatangaziwa ni kwa ajili ya kutunisha mfuko wa kampeni. Je, muda huu ambao watu wameshaamua si hizi materials zingegawiwa bure na kwa wingi kwa kutumia pesa ambazo zimeshakusanywa? Hatuwezi kuweka biashara pembeni ili kusaidia anguko la nguvu la CCM?

2. Kampeni za dr. slaa tunazichungulia kwenye taarifa za habari tu. Majuzi tulimuona kwenye mdahalo ITV na live kupitia TBC1 na Agape TV. Pia alialikwa kwenye mahojiano na Clouds FM. Lakini hata hizi hazikutangazwa kwa wingi ili wananchi wengi wawe na taarifa waweze kusikiliza/kutizama. Za kwenye TV wala hazikurudiwa na CHADEMA hawajalipia marudio. Swali ni kwamba, kwanini hizi pesa ambazo zinakusanywa zisitumike kulipia vipindi vya TV na redio? Kwa nini air time isinunuliwe kwenye radio za mikoa ile ambayo anatembelea ili warushe hotuba zake live? Siyo wananchi wote wanapata nafasi ya kufika eneo analohutubia lakini wangefaidika sana kama wangeweza kumsikiliza kwenye redio au TV. Hata kulipia matangazo ya ratiba yake pia imeshindikana? Kwa mfano, siku ya Jumamosi Dr. atakapohitimisha kampeni zake huku mbeya wananchi wanaweza kutizama na kusikiliza live? Hili ni muhimu ili aweze kujibu hoja za mkutano wa JK na waandishi wa habari wa tarehe 29 October.

Marafiki wa Dr. Slaa mnaweza kutolea haya mambo ufafanuzi. Kama maswali ya mapato na matumizi yanaweza kuwa magumu kwenu, basi tuarifuni tu mipango ya wananchi wote kupata fursa ya kusikiliza/kutazama hotuba yake ya mwisho hapo jumamosi. Mzee Mwanakijiji alikwisha tahadharisha kwamba hii hamasa iliyopo JF inahusisha watu wachache sana sana kwa hiyo tusidanganyike na ushabiki uliopo hapa tukadhani tayari tumeshashinda, ukiacha majimbo yale machache ambayo tayari tuna uhakika wa kushinda.

Ndugu Gurudumu,

Friends of Slaa (FOS) au Supporters of Slaa (SOS = Save Our Souls) walishauriwa mwanzoni kwamba waweke michango yao katika akaunti za benki. Akaunti mojawapo ipo CRDB Bank na ni nambari 01J1080100600 kwa jina: "CHADEMA M4C". Mimi nime-deposit fedha jana ktk akaunti hii na nimethibitisha kwamba Dk. Slaa na Mwenyekiti Mbowe ndio wana-operate hiyo akaunti. Of course wengine wanaendelea kuchangia electronically.

Kuhusu bendera na mavazi yanayotambulisha CHADEMA haya yaliagizwa mapema hata kabla ya kampeni kuanza. Vifaa vingine vya matangazo vinatengenezwa kadri fedha zinavyopatikana, I assume. Lakini fedha nyingi sana zinahitajika kwa helikopta na magari (fuel, tairi na matengenezo ya mara kwa mara), pamoja na vipindi ktk redio na TV etc. na michango ya FOS au SOS ndiyo inawezesha hayo.

Tuendelee na ukarimu huu hadi tumwingize SLAA Ikulu na Chadema idhibiti Bunge.
 
Ungekuwa unatumia jina halali na sio bandia ningeweza kukujibu kwa undani na kukupa mawasiliano ya watu wa kuuliza kuhusu suala hilo lakini FOS Kazi yao kubwa ni kuhamasisha michango na kutoa habari zingine kuhusu mgombea uraisi lakini sio wanaomiliki hizo account za pesa ambapo hutumwa either kwa njia ya simu au kwa njia ya benki hilo ni chadema na chadema wana uongozi wao kwahiyo ufike kwa uongozi uulize swala hilo - unapouliza usisahau masuala mengine ya sheria za uchaguzi na mengine mengi
 
Kilasara na shy,

Nawashukuru sana kwa ufafanuzi. Nawashukuru pia kwa jitihada hizo za kuhamasisha michango kwa niaba ya uongozi wa chadema. Nafurahi kujua kwamba mnatumia akaunti za benki za chadema zinazosimamiwa na uongozi wa chama. Ni matumaini yangu kwamba uongozi wa chadema utanijibu maswali yangu yaliyobakia kwa mujibu wa thread yangu hapo juu.
 
jamani chadema tupeni majibu, angalau mkakati wa live coverage jumamosi
 
ndugu come out open kwa jina lako na mawasiliano yako utapewa taarifa zote kwa mtindo huu sijui utapata nini - tume ya uchaguzi ndio anayetakiwa kupatiwa taarifa hizo wewe huna mamlaka kisheria
 
nazitakazo baki tutapleka kule Bagamoyo kusaidia maendeleo ya Shule hii.

69044_1304865922155_1845735565_590428_7980395_n.jpg
 
sijui kama sasa tuko pamoja, siulizi tena mapato na matumizi nimeshawaelewa. naulizia kama mmepanga kutoa kampeni za mwisho za dr. live tuweze kumsikiliza nchi nzima kwenye redio na TV? kuchanga nimechanga

au hilo nalo ni siri? mmezoea kutushutukiza dakika chache kutuambia kuna live coverage ama TBC au Agape, au Clouds. kutokana na kutokujua mapema kama kutakuwepo na live coverage watu wanashindwa kujipanga kusikiliza/kutazama.
 
Back
Top Bottom