Pesa na maisha ya furaha.

kunyala

Member
Apr 11, 2013
76
18
Wadau nawasalimu wote,Ndio tunakaribia mwisho wa mwaka 2013.kuna waliotimiza ndoto zao na wengine bado wanapambana cha msingi ni kuto kukata tamaa.

Langu leo ni swala la maisha ya furaha na pesa.wengi wetu tunajua kuwa kuwa na pesa za kutosha ndio chanzo cha furaha ktk familia lakini nimejaribu kuangalia ktk familia zetu nimeona hivyo ni vitu viwili tofauti.Kwani wapo matajiri wa kutupa bt hawana furaha kabisa ktk familia zao na wapo maskini ambao hata hawajui wata kula.kulala hata kuvaa nn lakini wana raha sana ktk familia zao.
Nimejaribu pia kuangalia tofauti ya watumishi ktk ofisi moja mfano mzuri ni kati ya mlinzi/dereva na mtumishi mwingine hapo kuna tafauti kubwa sana ya kipato lakini ukiangalia furaha ktk familia utagundua kuwa mlinzi/dereva anaishi maisha ya furaha sana.

Huu ni mtazamo wangu na hapa nakubaliana na mistari ktk biblia "MBONA NDEGE WA ANGANI WANAISHI KWA FURAHA NA HAWAPANDI WALA HAWALIMI NA HAWAJUI KESHO" huo mstari naomba anayeujua vizuri autupie hapa.
 
Back
Top Bottom