LH XiV
JF-Expert Member
- Nov 27, 2016
- 346
- 350
Hawa jamaa wanajiita ProEmploymentSolution ni hatari kwa afya yako. Ni kampuni inayojihusisha na udalali wa ajira, kwa maana ya wao kukutafuta then wanakutafutia ajira au makampuni kuajiri wafanyakazi kupitia wao.
Sasa naona wafanyakazi wao wanafanya kazi kama traffic. Wanauwezo kutoka nyumbani bila kitu na kurudi na rundo la pesa wanazojipatia kwa utapeli tu.
Wanatangaza ajira kadhaa uki apply unaitwa kwajili ya interview na hapo ndipo jamaa wanapopigia pesa, ukimaliza tu interview unaambiwa sasa kuna jamaa mwingine naye kaja leo anasifa kama zako ila hana hela....lazima mwanaume upinduke anakutajia kiasi anachohitaji ili akufanyie wepesi kutoka kwenye wimbi la kukosa ajira.
Basi kama kawa unaanza kushukuru Mungu na wengine wanaanza kuaga ndugu jamaa na marafiki kwamba muda wowote kuanzia sasa naitwa kazini basi utazeeka ukisubiri parachichi chini ya mgomba.
Kuweni makini na haya yanayojiita makampuni ya ajira.
Sasa naona wafanyakazi wao wanafanya kazi kama traffic. Wanauwezo kutoka nyumbani bila kitu na kurudi na rundo la pesa wanazojipatia kwa utapeli tu.
Wanatangaza ajira kadhaa uki apply unaitwa kwajili ya interview na hapo ndipo jamaa wanapopigia pesa, ukimaliza tu interview unaambiwa sasa kuna jamaa mwingine naye kaja leo anasifa kama zako ila hana hela....lazima mwanaume upinduke anakutajia kiasi anachohitaji ili akufanyie wepesi kutoka kwenye wimbi la kukosa ajira.
Basi kama kawa unaanza kushukuru Mungu na wengine wanaanza kuaga ndugu jamaa na marafiki kwamba muda wowote kuanzia sasa naitwa kazini basi utazeeka ukisubiri parachichi chini ya mgomba.
Kuweni makini na haya yanayojiita makampuni ya ajira.