Jamani mnijuve kuusu hawa permanent secretaries ambao nasikiaga raisi akiwateua ktk wizara mbali mbali. Inamaana hawa watakaa ofisini maisha yao? Au hiyo 'permanent' hapa maana yake nini!
Mhhh....Umenifurahisha sana Triple9..
Lakini hata mimi hii kitu inanitesa kidogo, ingawa najua kwamba Permenent Secretary yeye hatokani na wabunge kama ilivyo kwa waziri, na yeye ataendelea na kazi tu mpaka hapo atakapoharibu mwenyewe..., wakati waziri akikosa ubunge ndo mwisho wa nafasi yake...ISTAND TO BE CORRECTED!
Permanent Secretary[senior civil servant] ni mtendaji mkuu wa wizara [Accounting Officer] ambaye wadhifa wake hautokani na siasa kama ilivyo kwa waheshimiwa mawaziri.Neno permanent secretary halina maana kwamba watatakiwa kukaa mawizani maisha yao yote hilo ni jina tu mwanzoni walikuwa wakiitwa Principal Secretary, kwa nchi nyingine za jumuiya ya madola wanaitwa Secretary General,Director General au Principal Secretary.
Ipi sahihi boss kwa nchi yetu kati ya General secretary na Permanent secretary?Permanent Secretary[senior civil servant] ni mtendaji mkuu wa wizara [Accounting Officer] ambaye wadhifa wake hautokani na siasa kama ilivyo kwa waheshimiwa mawaziri.Neno permanent secretary halina maana kwamba watatakiwa kukaa mawizani maisha yao yote hilo ni jina tu mwanzoni walikuwa wakiitwa Principal Secretary, kwa nchi nyingine za jumuiya ya madola wanaitwa Secretary General,Director General au Principal Secretary.