Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,886
- 453,430
Mtunzi Juma Hiza
Sehemu ya 01
Niliamua kufunga pingu za maisha na Julieth kwasababu alikuwa ni mwanamke niliyempenda sana. Alikidhi kila aina ya vigezo ambavyo nilikuwa nikivihitaji kwa mwanamke hasa yule ambaye nilitarajia kufunga naye pingu za maisha.
Nakumbuka alivumilia mambo mengi mno, wakati wa mateso, huzuni na hata wakati mwingine wa furaha bado alikuwa na mimi. Sikutaka kumpoteza katika maisha yangu nilihakikisha naitimza ahadi yangu niliyomuahidi ya kumuoa.
Julieth alijaaliwa uzuri wa sura ya kitoto, macho makubwa legevu ya kurembuwa, umbo namba nane lililokuwa linawapagawisha wanaume wengi waliyokuwa wakimtazama kwa macho ya matamanio.
Nilikuwa nikipata kesi lukuki za wanaume ambao walikuwa wakimsumbua lakini wote hawakuweza kupata nafasi. Julieth alikuwa akinipenda sana, hakutaka kbisa kufanya kitu kibaya ambacho kingeweza kunigharimu maisha yangu. Alikuwa akizijali sana hisia zangu.
“Dominick mpenzi mimi siwezi kukusaliti nakupenda sana na ninakuahidi hutojutia kunipenda katika maisha yako yote,” yalikuwa ni maneno ya Julieth aliyokuwa akipenda kuniambia kila siku, wakati huo kichwa chake alikuwa amekilaza kifuani mwangu.
Nilizidi kumuamini sana Julieth na hii ndiyo sababu iliyonipelekea mpaka nikaamua kumkabidhi dhamana ya moyo wangu, moyo ambao sikumbuki kama uliwahi kupenda hapo kabla.
Ilikuwa ndiyo mara yangu ya kwanza kupenda na niliangukia mikononi mwa Julieth, mwanamke niliyekuwa nikimfananisha na kito cha thamani ambacho niliahidi kukitunza mpaka pale mwisho wa pumzi zangu utakapofika. Nilimpenda sana Julieth Mushi, nilimpenda mno.
Ingawa maneno ya Mama yangu, ndugu na marafiki hayakuwa mbali kipindi ambacho nilikuwa nataka kumuoa Julieth lakini hayakufanya niache kufanya kile ambacho nilidhamiria kwa wakati ule, kwa kuwa niliamini sisi ndiyo tulikuwa tumependana kwa dhati itokayo moyoni basi maneno ya watu hayakuweza kusitisha kile tulichokuwa tumepanga.
Kazi yangu ya ufundi wa simu niliyokuwa nikiifanya katika ofisi yangu ndogo iliyokuwepo mtaa wa Kariakoo ukijumlisha na Julieth ambaye hakuwa na kazi yoyote ilichangia kuzalisha maneno mengi kila kukicha, wengi wao hawakutaka kuamini kama kweli nilikuwa naoa tena nilikuwa naenda kumuoa mwanamke ambaye hakuwa amesoma wala hakuwa na kazi yoyote, katika maisha yake ya kielimu alibahatika kusoma mpaka darasa la saba tu!. Ugumu wa maisha ndiyo uliyochangia Julieth kutoendelea na elimu yake ya sekondari, wazazi wake hawakuwa na uwezo wa kuendelea kumsomesha. Huo ndiyo ulikuwa mwisho wa elimu yake.
Hakika nilichekwa sana, nilitukanwa kila aina ya tusi lakini katu sikutaka kuwasikiliza, nilisimamia katika kile nilichokuwa nakiamini.
“Nakupenda sana Julieth wangu,” nilimwambia Julieth huku nikimtazama kwa macho ya huba, alionekana kuwa mpole sana.
“Sawa unanipenda Dominick lakini Mama yako anaonekana kutonipenda, utawezaje kuishi na mimi?” aliniuliza Julieth swali lililokuwa na maana kubwa sana, ni kweli mama yangu alionekana kutompenda lakini sikutaka hilo liendelee kuwa tatizo litakalosababisha kuvunjika kwa uhusiano wetu.
“Julieth mimi ndiyo niliyokupenda Mama yangu asiwe kikwazo cha kukufanya utokwe na imani ya mapenzi yangu,” nilimwambia.
“Hata kama Dominick lakini nitawezaje kuishi na Mama yako na wakati hanipendi?”
“Julieth mpenzi wangu naomba uniamini kuwa nakupenda kwa dhati wala usiwe na wasiwasi wowote kuhusu Mama yangu usijali nitaongea naye na kila kitu kitakuwa sawa” nilimwambia maneno ambayo yalionekana kumuingia vyema, alikuwa ni muelewa sana.
****
Maneno ya Mama yangu bado yaliendelea kuwa tatizo katika mapenzi yangu kila siku nilikuwa nikigombana na Mama yangu kuhusu Julieth mwanamke ambaye alionekana kuwa takataka, hakuwa na kazi yoyote hivyo kila kitu kwake kilionekana kuwa kibaya. Mama yangu alikuwa akimsema sana Julieth, alinidharau kwa maamuzi ambayo nilikuwa nimeyachukua.
“Dominick mwanangu hivi una akili kweli wewe, utaendaje kumuoa mwanamke ambaye hana kazi wala nini” aliniambia Mama yangu huku akionekana kukasirishwa na kitendo nilichokuwa nimekifanya.
“Lakini mama nampenda sana,” nilimjibu huku nikimtazama usoni, alionekana kuwa na hasira mno.
“Utampendaje mwanamke ambaye hana mbele wala nyuma. Mwanangu wewe mwenyewe embu angalia kazi unayoifanya halafu bado unaenda kuoa mwanamke ambaye hana maisha hivi unafikiri maisha yako yatakuwaje?” aliniuliza Mama.
“Mama mapenzi hayaangalii kazi nzuri wala maisha mazuri bali moyo ndiyo unaopenda na moyo ukipenda kamwe huwezi kuukataza uache kupenda,” nilimjibu huku nikiwa nimeyaelekeza macho yangu chini, sikutaka kumtazama Mama yangu usoni.
Nilimuonea haya.
“Ati! nini! Unasamaje Dominick? Mimi na marehemu Baba yako hatukupendana kama unavyosema bali ni wazazi wetu waliamua kutuchagulia na kwa wakati ule Baba yako alikuwa na maisha mazuri tu! Sasa huo unaouita moyo hapa sijui ni moyo wa aina gani?”
“Mama ni moyo wa mapenzi na ukishapenda umependa kweli wala huwezi kuubadilisha. Nampenda sana Julieth na yeye ndiye mwanamke wa ndoto zangu,” nilimwambia.
Bado niliendelea kuushikilia msimamo wangu wa kumpenda Julieth mwanamke niliyekuwa nampenda kuliko kitu chochote kile wala siwezi kuficha kitu katika hilo.
Ingawa Mama yangu alionekana kutokukubaliana na mimi kumuoa Julieth lakini ilifikia kipindi akaamua kukubali hapa ni baada ya kuniona nimezidi kuwa kin’gang’anizi.
Hatimaye Dominick mimi niliyezaliwa miaka ishirini na Saba iliyopita nikaamua kufunga ndoa rasmi na Julieth na huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kuhama maisha ya nyumbani, nikayaanza maisha mapya ya ndoa yangu.
Maisha ambayo kiukweli mwanzo yalianza kama hadithi nzuri ya kimapenzi lakini kadri siku zilivyokuwa zikisonga mbele hadithi hiyo iliweza kubadilika na kuwa miongoni mwa hadithi za kutisha ambayo iliweza kuniacha na uadui mkubwa sana dhidi ya viumbe ambavyo vimefanya niishi maisha ya kutoitamani kesho yangu.
Je, nini kitaendelea?
Huu ni mwanzo tu wa simulizi hii ya kusisimua.
Sehemu ya 01
Niliamua kufunga pingu za maisha na Julieth kwasababu alikuwa ni mwanamke niliyempenda sana. Alikidhi kila aina ya vigezo ambavyo nilikuwa nikivihitaji kwa mwanamke hasa yule ambaye nilitarajia kufunga naye pingu za maisha.
Nakumbuka alivumilia mambo mengi mno, wakati wa mateso, huzuni na hata wakati mwingine wa furaha bado alikuwa na mimi. Sikutaka kumpoteza katika maisha yangu nilihakikisha naitimza ahadi yangu niliyomuahidi ya kumuoa.
Julieth alijaaliwa uzuri wa sura ya kitoto, macho makubwa legevu ya kurembuwa, umbo namba nane lililokuwa linawapagawisha wanaume wengi waliyokuwa wakimtazama kwa macho ya matamanio.
Nilikuwa nikipata kesi lukuki za wanaume ambao walikuwa wakimsumbua lakini wote hawakuweza kupata nafasi. Julieth alikuwa akinipenda sana, hakutaka kbisa kufanya kitu kibaya ambacho kingeweza kunigharimu maisha yangu. Alikuwa akizijali sana hisia zangu.
“Dominick mpenzi mimi siwezi kukusaliti nakupenda sana na ninakuahidi hutojutia kunipenda katika maisha yako yote,” yalikuwa ni maneno ya Julieth aliyokuwa akipenda kuniambia kila siku, wakati huo kichwa chake alikuwa amekilaza kifuani mwangu.
Nilizidi kumuamini sana Julieth na hii ndiyo sababu iliyonipelekea mpaka nikaamua kumkabidhi dhamana ya moyo wangu, moyo ambao sikumbuki kama uliwahi kupenda hapo kabla.
Ilikuwa ndiyo mara yangu ya kwanza kupenda na niliangukia mikononi mwa Julieth, mwanamke niliyekuwa nikimfananisha na kito cha thamani ambacho niliahidi kukitunza mpaka pale mwisho wa pumzi zangu utakapofika. Nilimpenda sana Julieth Mushi, nilimpenda mno.
Ingawa maneno ya Mama yangu, ndugu na marafiki hayakuwa mbali kipindi ambacho nilikuwa nataka kumuoa Julieth lakini hayakufanya niache kufanya kile ambacho nilidhamiria kwa wakati ule, kwa kuwa niliamini sisi ndiyo tulikuwa tumependana kwa dhati itokayo moyoni basi maneno ya watu hayakuweza kusitisha kile tulichokuwa tumepanga.
Kazi yangu ya ufundi wa simu niliyokuwa nikiifanya katika ofisi yangu ndogo iliyokuwepo mtaa wa Kariakoo ukijumlisha na Julieth ambaye hakuwa na kazi yoyote ilichangia kuzalisha maneno mengi kila kukicha, wengi wao hawakutaka kuamini kama kweli nilikuwa naoa tena nilikuwa naenda kumuoa mwanamke ambaye hakuwa amesoma wala hakuwa na kazi yoyote, katika maisha yake ya kielimu alibahatika kusoma mpaka darasa la saba tu!. Ugumu wa maisha ndiyo uliyochangia Julieth kutoendelea na elimu yake ya sekondari, wazazi wake hawakuwa na uwezo wa kuendelea kumsomesha. Huo ndiyo ulikuwa mwisho wa elimu yake.
Hakika nilichekwa sana, nilitukanwa kila aina ya tusi lakini katu sikutaka kuwasikiliza, nilisimamia katika kile nilichokuwa nakiamini.
“Nakupenda sana Julieth wangu,” nilimwambia Julieth huku nikimtazama kwa macho ya huba, alionekana kuwa mpole sana.
“Sawa unanipenda Dominick lakini Mama yako anaonekana kutonipenda, utawezaje kuishi na mimi?” aliniuliza Julieth swali lililokuwa na maana kubwa sana, ni kweli mama yangu alionekana kutompenda lakini sikutaka hilo liendelee kuwa tatizo litakalosababisha kuvunjika kwa uhusiano wetu.
“Julieth mimi ndiyo niliyokupenda Mama yangu asiwe kikwazo cha kukufanya utokwe na imani ya mapenzi yangu,” nilimwambia.
“Hata kama Dominick lakini nitawezaje kuishi na Mama yako na wakati hanipendi?”
“Julieth mpenzi wangu naomba uniamini kuwa nakupenda kwa dhati wala usiwe na wasiwasi wowote kuhusu Mama yangu usijali nitaongea naye na kila kitu kitakuwa sawa” nilimwambia maneno ambayo yalionekana kumuingia vyema, alikuwa ni muelewa sana.
****
Maneno ya Mama yangu bado yaliendelea kuwa tatizo katika mapenzi yangu kila siku nilikuwa nikigombana na Mama yangu kuhusu Julieth mwanamke ambaye alionekana kuwa takataka, hakuwa na kazi yoyote hivyo kila kitu kwake kilionekana kuwa kibaya. Mama yangu alikuwa akimsema sana Julieth, alinidharau kwa maamuzi ambayo nilikuwa nimeyachukua.
“Dominick mwanangu hivi una akili kweli wewe, utaendaje kumuoa mwanamke ambaye hana kazi wala nini” aliniambia Mama yangu huku akionekana kukasirishwa na kitendo nilichokuwa nimekifanya.
“Lakini mama nampenda sana,” nilimjibu huku nikimtazama usoni, alionekana kuwa na hasira mno.
“Utampendaje mwanamke ambaye hana mbele wala nyuma. Mwanangu wewe mwenyewe embu angalia kazi unayoifanya halafu bado unaenda kuoa mwanamke ambaye hana maisha hivi unafikiri maisha yako yatakuwaje?” aliniuliza Mama.
“Mama mapenzi hayaangalii kazi nzuri wala maisha mazuri bali moyo ndiyo unaopenda na moyo ukipenda kamwe huwezi kuukataza uache kupenda,” nilimjibu huku nikiwa nimeyaelekeza macho yangu chini, sikutaka kumtazama Mama yangu usoni.
Nilimuonea haya.
“Ati! nini! Unasamaje Dominick? Mimi na marehemu Baba yako hatukupendana kama unavyosema bali ni wazazi wetu waliamua kutuchagulia na kwa wakati ule Baba yako alikuwa na maisha mazuri tu! Sasa huo unaouita moyo hapa sijui ni moyo wa aina gani?”
“Mama ni moyo wa mapenzi na ukishapenda umependa kweli wala huwezi kuubadilisha. Nampenda sana Julieth na yeye ndiye mwanamke wa ndoto zangu,” nilimwambia.
Bado niliendelea kuushikilia msimamo wangu wa kumpenda Julieth mwanamke niliyekuwa nampenda kuliko kitu chochote kile wala siwezi kuficha kitu katika hilo.
Ingawa Mama yangu alionekana kutokukubaliana na mimi kumuoa Julieth lakini ilifikia kipindi akaamua kukubali hapa ni baada ya kuniona nimezidi kuwa kin’gang’anizi.
Hatimaye Dominick mimi niliyezaliwa miaka ishirini na Saba iliyopita nikaamua kufunga ndoa rasmi na Julieth na huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kuhama maisha ya nyumbani, nikayaanza maisha mapya ya ndoa yangu.
Maisha ambayo kiukweli mwanzo yalianza kama hadithi nzuri ya kimapenzi lakini kadri siku zilivyokuwa zikisonga mbele hadithi hiyo iliweza kubadilika na kuwa miongoni mwa hadithi za kutisha ambayo iliweza kuniacha na uadui mkubwa sana dhidi ya viumbe ambavyo vimefanya niishi maisha ya kutoitamani kesho yangu.
Je, nini kitaendelea?
Huu ni mwanzo tu wa simulizi hii ya kusisimua.