Penye mnara wa Vodacom weka mbali na spidi zaidi ya 50 km/hr

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Juzi nikiwa mkoani Tanga nilijikuta nikisimamishwa na askari polisi akaniambia kuwa kilomita 9 kabla ya kituo chao nilipigwa tochi tena mwanzo wa kibao kinachomalizia limit ya spidi ya 50 km/hr. Nilipoiangalia picha ilipigwa kwa nyuma ya gari ikionyesha nina 53 km/hr. Kwa maana nyingine nilianza kuongeza spidi nilipokaribia kibao hicho.

Hoja hapa ni nini?
Nilimdadisi yule askari wa usalama barabarani na nikaichukua simu yake ili kujiridhisha. Lakini nilipokuwa naiangalia simu yake zikawa zinatumwa picha nyingi sana za magari yaliyozidisha spidi kwenye eneo lile ambalo kimsingi hapakuwa na askari yeyote aliyekuwa akichukua picha. Wapo wanaosema kuwa zile picha huwa zinatumwa na askari aliyejificha kichakani. Nikabaini ni uongo. Asingeweza kuchukua picha zile kwa kiwango kile.

Kufuatilia magari lukuki ambayo mengine yanaanza kupunguza spidi mwanzo wa kibao cha speed limit wengine wwnaanza kuongeza mwishoni na kutuma picha mfululizo vile isingewezekana.

Nilichogundua.
Askari alijichanganya kwa kusema kuwa maeneo haya huwa kuna minara ina "scan" magari kwa kuangalia "speed limit" kwenye vile vibao vyao. Kwakweli nikagundua kuwa vibao vingi vya "Speed limit" barabara ya Tanga na Bagamoyo vipo maeneo ambayo kuna minara ya Vodacom! Hili nimejidhihirisha wakati nikiendelea na safari na kila kwenye kibao cha "speed limit" vingi ya hivyo nimekutana na minara hiyo! Upo uwezekano kuwa wafanyakazi wa Vodacom ndiyo hasa wanaohusika na picha zile na huenda ndiyo hata sababu ya wao kuwa sehemu ya kukusanya tozo za barabarani.

Jihadhari sana usiendeshe zaidi ya spidi 50 kwenye vibao ambavyo ukivikagua utakutana na hii minara ya mawasiliano.

Vilevile ushahidi mwingine ni kuwa zile kamera za askari wetu huwa zinaanza kusoma kuanzia 60 km/hr! Yupo askari mmoja wa kike aliwahi kunikamata maeneo ya Pwani na akaniambia kuwa nimezidisha mwendo ila bahati ni kuwa tochi lake lilikuwa linaanza kusoma kuanzia 60. Na kweli nilikuwa na spidi ya 56. Siku hizi hata 51 tu unaonyeshwa! Jiongeze uchukue tahadhari!
 
Mi nikinunua gari kuna siku nitasusa gari nitamuachia trafiki.

Spidi limit 50 nipo 53 unanisimamisha? hiyo si kibinadamu zaidi?
 
Mi nikinunua gari kuna siku nitasusa gari nitamuachia trafiki.

Spidi limit 50 nipo 53 unanisimamisha? hiyo si kibinadamu zaidi?
Acha kabisa mkuu. Unalalamika huku jamaa anatoa risiti kumbe zile picha wanaopiga wanatuma hadi kwa maboss zao kuweka ushahidi!
 
Mi nikinunua gari kuna siku nitasusa gari nitamuachia trafiki.

Spidi limit 50 nipo 53 unanisimamisha? hiyo si kibinadamu zaidi?
Kuna jamaa mmoja jimbo la New Jersey Marekani aliwashitaki polisi kwamba wamemdaka akiwa ameipita speed limit kidogo tu, kwa namna ambayo si ya uhalisi kuweza kuwa chini ya speed limit muda wote, kwa sababu gari ni mashine na kuna wakati mtu anaweza kuwa kajisahau kidogo tu kaenda kidogo tu juu ya speed limit, anapunguza mwendo, wewe unamlimatochi hapo hapo.

Jamaa likashinda kesi, mpaka leotrafiki akiona ukojuu kidogo tu ya speed limit hakusumbui, anajua hamna kesihapo, kuna precedent tayari.

Tatizo, Tanzania kuna wabishi wa namna hiyokuwashitaki polisi?
 
Mi nikinunua gari kuna siku nitasusa gari nitamuachia trafiki.

Spidi limit 50 nipo 53 unanisimamisha? hiyo si kibinadamu zaidi?
Hahahaaaa kuna jamaa hakuwa na leseni Trafiki akamkamata jamaa akamwambia Trafiki nimesahau wallet ina leseni akafunga gari akaondoka akamwachia Traffic alinde,kuanzia saa mbili asubuhi akarudi jioni akalikuta gari Trafiki kaondoka.
 
Kuna jamaa mmoja jimbo la New Jersey Marekani aliwashitaki polisi kwamba wamemdaka akiwa ameipits speed limit kidogo tu, kwa namna ambayo si ya uhalisi kuweza kuwa chini ya speed limit muda wote, kwa sababu gari ni mashine na kuna wakati mtu anaweza kuwa kajisahau kidogo tu kaenda kidogo tu juu ya speed limit, anapunguza mwendo, wewe unamlimatochi hapo hapo.

Jamaa likashinda kesi, mpaka leotrafiki akiona ukojuu kidogo tu ya speed limit hakusumbui, anajua hamna kesihapo, kuna precedent tayari.

Tatizo, Tanzania kuna wabishi wa namna hiyokuwashitaki polisi?

Tanzania is full of megalomaniacs.
 
Hahahaaaa kuna jamaa hakuwa na leseni Trafiki akamkamata jamaa akamwambia Trafiki nimesahau wallet ina leseni akafunga gari akaondoka akamwachia Traffic alinde,kuanzia saa mbili asubuhi akarudi jioni akalikuta gari Trafiki kaondoka.
Huyo ndiyo role model wangu nikinunua gari
 
Back
Top Bottom