Peniela (Story ya kijasusi)

Kuna kitu kinamsukuma kufanya hivyo automatic Kwani wazazi wote wa Peniela waliuwawa na John

Mwisho wa story Mathew atamsaidia Peniela kuwajua ndugu zake kwa kupitia matukio yaliyofanywa na john
Anitha ataangukia mikononi Jason kwani keshaonyesha dalili za kumpenda
Jaji Elibariki yeye ataishi na Peniela kwani Flavian atadedi
Mathew atamuoa Anna baada ya Mathew kuyaanika mabaya yote ya baba yake

Dr Joshua yeye atapanda kizimbani baada ya ushahidi kupatikana wa kumuua Edson, mke wake na kutumia ofisi vibaya
Rais mstaafu mr Deus kwa kushirikiana na brigedia........
Niishie hapo kwanza
Wwe unaharibu utamu nyamaza bana Flaviana
 
SEASON 2
SEHEMU YA 36
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ hallow mheshimiwa “ akasema mzee Augustine baada ya waziri mkuu kupokea simu
“ samahani kwa kukusumbua mheshimiwa waziri mkuu mkuu”
“ Bila samahani Augustine”
“ Mheshimiwa waziri mkuu unakumbuka mchana nilikupigia simu na kukwambia kwamba pengine ningeweza kuja kukuona jioni ya leo?
“ Ndiyo nakumbuka Augustine”
“ Ok mheshimiwa basi nahitaji kuja kukuona usiku huu.Nina jambo kubwa sana ambalo haliwezi kusubiri hadi kesho.” Akasema mzee Augustine
‘ Ok Mr Augustine.Kama unaweza kuja hapa katika makazi yangu nitakusubiri”
“ Ahsante sana mheshimiwa .Ninakuja hapo muda si mrefu.Naomba nikufahamishe vile vile kwamba nitaongozana na vijana watatu.” Akasema mzee Augustine na kukata simu
“Waziri mkuu amekubali kuonana nasi kwa hiyo hatuna muda wa kupoteza hapa.Twendeni nyumbani kwake tukaonane naye.” Akasema mzee Augustine na kuyabeba mafaili yale na kwa haraka wakaingia garini na safari ya kuelekea kwa waziri mkuu ikaanza.

ENDELEA………………..
Saa tatu na nusu za asubuhi Peniela akawasili katika makazi ya John Mwaulaya akapokelewa na Josh.
“ Karbu sana peniela” akasema Josh na kumuongoza Peniela hadi sebuleni ambako kulikuwa na vijana wengine wawili waliovalia nadhifu.
“ Peniela kutana na Jacob na Francis ,hawa wako ofisi kuu na wamekuja kwa ajili ya lile suala nililokueleza.” Akasema Josh.Peniela akasalimiana na wale vijana na kuketi
“ Haya niambieni mlichokuwa mnataka kuniambia”akasema Peniela ambaye alionekana kuwa na haraka “
“ Peniela ni kama vile nilivyokueleza simuni.kwanza ni kuhusiana na mtu wa kutuongoza japo kwa muda mfupi.Alipoanza kuumwa John mwaulaya alimteua Osmund awe kiongozi wetu hadi alipofariki.Kwa sasa hatuna tena mtu wa kutuongoza hasa katika kipindi hiki ambacho John mwaulaya anaumwa na tukjokatika operesheni kubwa .Sisi watatu tumekaa na kuona kwamba tukuchague wewe utuongoze kwa wakati huu ambao hatuna mtu wa kutuongoza.Jambo la pili ni kuhusiana na ugeni unaokuja leo hii.Kuna wageni sita wanakuja leo wakitokea makao makuu nchini marekani.Bado hatufahmu nini kinawaleta watu hawa kwa hiyo tunahitaji mtu wa kuwapokea wageni hawa na kufahamu kilichowaleta.Tunaaminikwambawewe unaweza ukalibeba jukumu hilo Peniela” Akasema Josh.Peniela akafikiri kwa sekunde kadhaa na kusema
“Kwa nini ninyi peke yenu mfanye maamuzi kama haya ya kunitaka mimi niwaongoze? Mna hakika wenzenu watakubaliana nanyi? Akauliza Peniela
“ Watu wote wamekuwa wakijiuliza kuhusiana na nani ambaye atatuongoza .Kila mmoja wetu anafahamu majukumu yake lakini kuna mambo ambayo hatuwezi kuyafanya bila ya kupewa ruhusa na maelekezo toka kwa kiongozi kwa hiyo sisi kwa niaba ya wenzetu tunakupendekeza wewe ili uwe kiongozi wetu japo kwa muda na nina imani kwamba hata wenzetu wote watakubaliana na mapendekezo yetu.Wewe ni mtu unayeifahamu vyema team Sc41 na unaweza ukatuogoza vizuri.Tunaomba utukubalie ombi letu la kutaka utuongoze” akasema Jacob.
“ kwa kuongezea hapo alipoisha Jacob,hata mzee John mwenyewe ameonyesha kukukubali sana na anakuamini .Nina hakika hata akisikia kwamba tumefanya maaamuzi ya kukuomba utuongoze atakubaliana nasi” akasema Josh.Peniela kama kawaida yake akanyamaza kidogo akawaangalia wale vijana na kisha akasema
“ Ok nitafanya mnavyotaka lakini ni kwa wakati huu tuu wanaokuja hawa wageni.Baada ya wageni kuondoka basi John au makao makuu watawachagulia mtu mwingine wa kuwaongoza.Ok tuachane na hayo ,wageni hao wanaokuja tayari wametafutiwa mahala watakapofikia? Akauliza Peniela
“ Masuala yote alikuwa akiyashughulikia Osmund na hatufahamu kama tayari walikuwa wametafutiwa sehemu ya kufikia au bado”
“ Ok isiwe taabu,kuna hoteli nyingi nzuri hapa jijini. Nadhani Maryrose 72 hotel itawafaa sana. Josh shughulikia suala hilo ili wageni hawa watakapowasili tuwe tayari tumewatafutia sehemu nzuri ya kufikia.Jacob na Francis tunakwenda uwanja wa ndege kuwapokea wageni.” Akasema Peniela na kabla hawajaondoka akaomba Josh ampeleke chumbani kwa John Mwaulaya akamuangalie.
John mwaulaya alipomuona Peniela ameingia mle chumbani kwake alifurahi na kujitahidi kutabasamu.
“ P..Pe.Peniela..” akasema John kwa sauti dhaifu.Peniela akamtazama mzee yule pale kitandani ambaye alikuwa amelala hajiwezi akamuonea huruma sana.Akamsogelea karibu.
“ Pole sana John.” Akasema Peniela
“ Ahsante Penny…Ahsante kwa kuja kuniona” akasema John mwaulaya na kumfanyia ishara peniela asogee karibu zaidi.
“ Peniela najua sina muda mwingi wa kuendelea kuishi.I’m going to die soon.Kama nikifariki kabla operesheni 26B haijakamilika ,tafadhali hakikisha kwamba unafanikiwa kuikamilisha kwani ni operesheni muhimu sana.Ikisha kamilika nenda kaendelee na maisha yako.Kuna mambo mengi ambayo nilitaka nikufanyie kablaya kufa ili niweze kuyatengeneza upya maisha yako niliyoyaharibu lakini kutokana na afya yangu kuzorota sina hakika kama nitaweza tena kuyanfanya kwa hiyo nakusihi hakikisha ukikamilisha operesheni hii unaachana kabisa na team SC41.Go far away from here and live your life.Find yourself a man and start a family” akasema John.Peiela akalengwa na machozi
“ John you are not going to die.Iwill do anything in my power to make sure that you get well” akasema Peniela
“ usisumbuke Peniela.Sina maisha marefu .Tafadhali shughulikia kwanza suala la operesheni 26B na baada ya hapo shughulikia kuyajenga upya maisha yako.Nilikukabidhi kasha moja na kukupa maelekezo nini cha kufanya pindi ukiikamilisha operesheni 26B .Fuata maelekezo yangu niliyokupa’ akasema john mwaulaya.
“ Usiseme hivyo John.Nitafanya kila linalowezekana mpaka nihakikishe umekuwa salama.Utapona John.Nakuhakikishia utapona.Doctors are on the way coming.You’ll be ok John” akasema peniela
“ Peniela najua unanipenda na unaumia kuniona hivi lakini nakuhakikishia kwamba hata ufanye nini sintaweza kupona.Tafadhali usipoteze muda na mimi tena.Nimekwisha ishi vya kutosha hapa duniani na sehemu kubwa ya maisha yangu nimeishi nikiwa ndani ya team SC41 .Nimefanya mambo mengi makubwa,nimetoa uhai wa watu wengi na sasa na mimi ni wakati wangu umefika.I have to face death” akasema John.Peniela akashindwa kujizuia kutoa machozi
“ John..! akasema peniela lakini John akamfanyia ishara asiseme chochote.
“ Peniela ninakiona kifo changu.Sina ujanja wa kuweza kukikwepa.Ninakusi usiendelee tena kuwa ndani ya Team SC41.Mimi nimefanya mambo mengi mabaya ndaniya kikundi hiki.Nilikuwa nikitoa roho za watu bila huruma na sikujua kwamba sikumoja na mimi nitachungulia kifo.Sitaki uishi maisha kama niliyoishi mimi ndani ya Team SC41 na ndiyo maana nakuomba ukiikamilisha operesheni 26B achana kabisa na team SC41 na uende ukaishi mbali uendeshe maisha yako.”akasema John.Peniela akashindwa kuendelea kumuona John katika hali ile akatoka huku akilia.Josh akamfuata.
“ Its ok peniela.Tafadhali usilie.John will be fine” akasema Josh.
“ jana nilikuwa na hasira na John na sikutaka hata kumuona lakini baada ya kumuoa akiwa pale kitandani hajiwezi nimejikuta nikiumia tena” akasema Peniela.halafu akafuta machozi na kuufungua mkoba wake akatoa mkebe wa poda akajipaka usoni .
“ Josh muda unakwenda sana ,shughulikia suala lile la hoteli ya kufikia wale wageni.Suala hili la ugonjwa wa John niachie mimi nitalishughulikia” akasema peniela na kisha akaongozana na akina Jacob wakaingia katika magari yao na kuondoka kuelekea uwanja wa ndege
“ Nilimchukia sana John kwa kitendo chake cha kumteka Jason na kumtesa lakini baada ya kumuona tena leo hasira zangu zote zimepotea na nimejikuta nikumuhurumia tena.Pamoja na yote mabaya aliyoyafanyia lakini kuna mengimazuri ameyafanya katiamaisha yangu kwa hiyo natakiwa na mimi nionyeshe japo msaada wangu mdogo kwake kama shukurani zangu.Ni kweli ni yeye aliyeyaharibu masha yangu lakini ni yeye ambaye alihakikisha ninalelewa na kukua bila tatizo lolote licha ya kutokuwa na wazazi.Nadhani sintafanya jambo jema kama nikiweka hasira mbele na kumuacha mzee yule ateseke kitandani bila ya msaada.Team SC41 ni kama wamemtelekeza.Nitawasiliana na yule daktari rafiki yake afanye haraka kuja ili aweze kumfanyia upasuaji “ akawaza peniela akiwa garini kuelekea uwanja wa ndege

******

Saa nne za asubuhi,Mathew kwa kufuata maelekezo aliyopewa na peniela,aliwasili katika kituo cha kulelea watoto ambako ndiko Peniela alikolelewa toka akiwa mdogo..
“ Kituo kizuri sana.” Akawaza Mathew na kushuka garini akaeleka getini kulikokuwa na mlinzi aliyemuuliza shida yake.Mathew akaeleza shida yake kwamba ni kuonana na Bi Bernadetha mkuu wa kile kituo.Mlinzi yule akamfahamisha kwamba kwa wakati huo Bernadetha alikuwa mgonjwa na alikuwa amelala ndani na hatakiwi kusumbuliwa.Mathew akasisitiza kwamba ana jambo la muhimu sana lililompeleka pale.Mlinzi yule bado aligoma kabisa kumruhusu Mathew kuingia hadi alipokabidhiwa noyto mbili za elfu kumi kumi .Huku akitabasamu akamuomba Mathew amsubiri pele pale getini akaingia ndani na baada ya kama dakika tano akatoka na kumruhusu Mathew aingie ndani.
Nyumba ya bi Bernadetha ilikuwa pembeni ya bweni la ghorofa la watoto yatima anaowatunza.Alikaribishwa sebuleni na msichana mmoja , akapatiwa kinywaji na baada ya kama dakika kumi hivi Bi Bernadetha akatokea.kwa kumuangalia tu ungetambua kwamba alikuwa anaumwa kwa namna alivyokuwa amedhoofika.likuwa akitembea taratibu na kwa msaada wa fimbo
“ karibu sana kijana “ akasema Bi bernadetha kwa sauti ya chini
“ Ahsante sana bibi.Shikamoo” akasema Mathew
“ marahaba mwanangu”akajibu yule bibi
“ Pole sana bibi unaendeleaje? Akauliza Mathew
“ Hivyo hivyo mwanangu,Mungu ananisaidia.Magonjwa yananiandama.Ninasumbuliwa na kisukari,shinikizo la damu, mara miguu inavimba yaani ni mateso kila kukicha.Huu uzee nao unachangia sana kuumwa umwa.” Akasema bibi Bernadetha.
“ Pole sana bibi Mungu atakusaidia na utapona tu”
“ nashukuru kijana wangu.Nimeambiwa una shida na unahitaji kuniona”
“ ndiyo bibi nimekuja kwako nina shida kidogo na samahani sana kwa kukusumbua.Mimi ninaitwa Mathew na jambo kubwa lililonileta hapa ni kutaka kupata taarifa kuhusu msichana mmoja aliyewahi kulelewa hapa anaitwa Peniela.” Akasema Mathew na mara tu bi Bernadetha alipolisikia jina Peniela akastuka kidogo
“Peniela!..”
“Ndiyo bibi”
“ Ni mwanangu huyu na muda mrefu sijamuona wala hajafika kunijulia hali yule mtoto.Yuko wapi ? Yuko salama? Anaendeleaje na maisha yake? Akauliza bi Bernadetha
“ Peniela ni mzima ila sina hakika kama anafahamu kuhusiana na ugonjwa wako.Nina imani angekwishakuja kukutazama.Mara ya wisho umeonana naye lini? Akaliza Mathew.Bi Bernadetha akakaa kimya kidogo akazama katika kumbu kumu zake na kusema
“ Ni zaidi ya mwaka mmoja uliopita.” Akasema
“ Kuna tatizo lilimpata Peniela na ndiyo maana alishindwa hata kuja kukutazama.” Akasema Mathew
“ Alipatwa na tatizo gani? Akauliza Bi Bernadetha kwa wasi wasi
“ Kuna matatizo yalimpata akawekwa kizuizini lakini kwa sasa matatizo hayo yamekwisha na yuko huru.” Akasema Mathew
“ masikini Peniela ndiyo maana sijamuona akija kunisalimu.Nilishangaa sana kwani haikuwa kawaida yake kupitisha mwezi mmoja bila kuja kunitembelea.Wewe ni nani wake? mume wake? Akauliza Bi Bernadetha na Mathew akacheka kidogo
“Hapana bibi.Mimi si mume wake.Peniela bado hajaolewa”
“ anasubiri nini huyu binti? Nimekuwa nikimsisitiza kwamba aolewe bado mapema ili niweze kuwaona wajukuu zangu lakini sijui kwa nini mpaka leo hii hataki kabisa kuolewa”akasema Bi Bernadetha na kimya kifupi kikapita Mathew akasema
“ Bibi nimekuja hapa kutaka kufahamu kuhusiana na historia ya Peniela.Alifikaje hapa? Ana ndugu zake ? Wewe ni mtu pekee ambaye anamfahamu vizur Peniela na historia yake na ndiyo maana nimekuja kwako kutafuta taarifa hizo.” akasema Mathew.Bi Bernadetha akaonyesha wasi wasi kidogo na kuuliza
“ Kwa niniunataka kufahamu kuhusu historia ya peniela? Kuna tatizo gani limetokea?
Mathew akamtazama yule bibi kwa makini na kuamua kumdanganya
“ Bibi nadhani itakuwa vizuri kama niikuwekawazi ili uweze kunielewa .Mimi ni mchumba wa Peniela na kama ikimpendeza Mungu tunaweza tukafunga ndoa.Kabla hatujafunga ndoa nahitaji kumfahamu mwenzangu vizuri,asili yake ametoka wapi,ndugu zake ni nani n.k.Alinieleza kwamba yeye ni yatima na amekulia hapa na ndiyo maana nimekuja hapa bila ya yeye kufahamu ili noweze kulithibitisha hilo na kumfahamu vizuri mwenzangu ikiwemo na tabia zake kwani wewe ndiye uliyemkuza.” akadanganya Mathew.Bi bernadetha akatabasamu kidogo baada ya kusikia uongo ule wa Mathew
“ Ouh kumbe wewe ndiye mchumba wa Peniela.Ungejitambulisha toka mwanzo baba.Nimefurahi sana kukujua mwanangu.Karibu sana.Mimi ndiye niliyemlea peniela toka akiwa mdogo kabisa.Ninampenda sana peniela kama mtoto wangu wa kumzaa mwenyewe.” Akasema bi bernadetha na kukaa kimya kidogo.Mathew alikuwa makini akimsikiliza bibi yule aliyekuwa akiongea kwa sauti ndogo.Bi Bernadetha akaendelea
“ Peniela aliletwa hapa akiwa mdogo sana na mtu mmoja aitwaye John Mwaulaya.Huu ndiye baba yake mzazi Peniela” akasema Bi Bernadetha na kumstua sana Mathew ingawa hakutaka kuonyesha mstuko ule mbele ya yule bibi
“ John alisema kwamba alimchukua Peniela kutoka kwa mama yake ambaye alikuwa na tabia za kukesha baa na kufanya ukahaba huku akimuacha mtoto nyumbani akiteseka nahivyo alimua kumchukua na kumleta hapa ili nimlee.Alinitaka nimlee kwa siri bila ya mtu kufahamu.John aliniambia kwamba hataki peniela afahamu kama yeye ni baba yake.Ninamsifu John kwani alijitahidi sana kutoa ushirikiano na misaada mingi katika kumlea peniela.Misaada toka kwa John mwaulaya ilikuwa ikimiminika kila leo na ndiye aliyejenga hilo bweni la ghorofa unaloliona hapo nje.Nilimfahamisha Peniela kwamba vile vitu vyote alivyokuwa akivipata vilitoka kwa mfadhili aliyejitolea kumsaidia .Alitamani sana kumfahamu mfadhili huyo ni nani lakini hadi anamaliza darasa la saba hakuwa ameonana na mfadhili wake ambaye ni baba yake mzazi.” Bernadetha akanyamaza kidogo na baada ya muda akaendelea
“Peniela alipomaliza darasa la saba John alimzawadia jumba kubwa la kifahari na hapo ndipo peniela akahama nyumbani kwangu na kuanza rasmi maisha yake.Pamoja na kuwa na maisha yake lakini bado tuliendela kuwa karibu.Nilikuwa namtembela mara kwa mara kuhakikisha anaendelea vizuri.Alifanikiwa kumaliza kidato cha sita na akafaulu vizuri sana na baadae akanitaarifu kwamba anaelekea marekani kwa masomo ya chuo kikuu.Alipomaliza masomo yake alirejea nchini na tuliendelea kuwasiliana na kutembeleana kama kawaida lakini ghafla akapotea na sikumuona tena na nikadhani labda amekwenda kuendelea na masomo zaidi.Sikupata nafasi ya kutafuta taarifa zake kwani na mimi nilianza kusumbuliwa na magonjwa .Nimestuka sana uliponiambia kwamba alikuwa amefungwa gerezani” akasema Bi Bernadetha
“ Bibi,Peniela sasa yuko huru na mambo yake yamekwisha malizika.”
“ Ouh ahsante sana Mungu kwa kumjalia mtoto Yule amekuwa huru tena.Alifanya kosa gani hadi akawekwa kizuizini? Akauliza Bi Bernadetha
“ Alisingiziwa kesi “ akajibu Mathew kwa ufupi halafu kukawa kimya tena
“ Bibi huyo John aliwahi kukueleza aliko mama yake Peniela ?
“ John hHajawahi kunieleza mahala aliko mama yake Peniela.Alichowahi kunieleza ni kwamba mama yake Peniela alikuwa na tabia mbaya na alikuwa akifanya biashara ya ukahaba na ndiyo maana aliamua kumchukua mtoto na kumleta hapa na hakutaka kabisa Peniela amfahamu mama yake “
“ Kwa nini John alikataa usimweleze Peniela kama yeye ni baba yake?
“ Sifahamu ni kwa nini alifanya vile.Kila nilipomuuliza hakutaka kunipa jibu na alisisitiza nimwele peniela kwamba yeye ni mfadhili wake.Sina hakika kama mpaka sasa Peniela amefaikiwa kuonana na John kwani alikuwa akikwepa mno kuonana naye.” akasema Bi Bernadetha.Mathew akainama akafikiri halafu akasema
“ Bibi nakushukuru sana kwa kunikaribisha na kunipa maelezo mazuri.Nimefurahi sana kwa maelezo uliyonieleza.Nakuahidi nitarejea tena hapa kwako siku si nyingi kujua maendeleo yako na nitamfahamisha peniela kuhusu ugonjwa wako ” Akasema Mathew
“ Ahnte sana kijana wangu lakini kuna jambonataka nikuweke wazi.Nimekueleza jambo hili lakini tafadhali sana naomba usimweleze Peniela kwani ndiyo yalikuwa makubaliano yangu na John na sikuwahi hata mara moja kuyavunja kwa kumueleza Peniela kwa hiyo naomba na wewe usithubutu kumweleza chochote.Iko siku John mwenyewe atamueleza “ akasema Bi Bernadetha
“ Nimekuelewa bibi na sintafanya hivyo.Nitakachofanya nitamueleza tu kwamba nimekuja kukutembelea na kukuta unaumwa na nitamsisitiza kwamba aje akutembelee.” akasema Mathew kisha akamuaga Bi Bernadetha na kuondoka
“ John Mwaulaya ni baba yake Peniela??..akajiuliza Mathew akiwa garini
“ Hapana hainiingii kabisa akilini eti John Mwaulaya awe ni baba yake Peniela halafuakatae mwanae kumfahamu.Hili ni jambolisilowezekana.Kama kweli ni baba yakena hakutaka peniela afhamu na badala yake akatambulishwa kwake kama mfadhili basi kuna kitu alikuwa anakificha na ambacho lazima nikifahamu.Amakweli dunia imekuwa ndogo sana.Hatimaye mimi na John mwaulaya tunakwenda kukutana tena uso kwa uso.This time I’ll be the one making him talk.” Akawaza Mathew

TUKUTANE SEHEMU IJAYO
Umenipoteza hapa sielewi tena
 
Wakuu baada ya peniela nahangaika kutafuta stori kali nyingine, naomba list ya story 5 nyingine nzuri kama ama zaidi ya peniela na queen monica
 
SEHEMU YA 2
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Mathew na Anitha waliendelea kusubiri pale nje ya jengo lile na baada ya dakika kumi na mbili gari moja likawasha endiketa kuashiria kwamba linakata kona kuingia katika jengo lile la maegesho,na mara simu ya Mathew ikaita.Alikuwa ni Eva
“ Mathew ninaingia sasa katika jengo,gari yangu umeiona? Ninatumia hii BMW nyekundu”
“ Nimekuona Eva.Jamaa wao wanatumia gari gani?
“ Wanatumia Harrier yenye rangi nyeusi”
“ Ok Good ,Endelea kwenda mpaka juu kabisa.UKifika egesha gari na utoke garini ujifiche mahala ili tujue lengo lao ni nini” akasema Mathew na kukata simu.Gari la Eva likaingia ndani ya jengo lile na baada ya dakika mbili Toyota Harrier lenye rangi nyeusi nalo likakata kona kuingia ndani ya jengo lile.
“ Jamaa wenyewe ni hawa hapa.Its show time” akasema Mathew akaiwasha piki piki yake nao wakaingia ndani ya jengo lile wakiifuata ile gari iliyokuwa ikimfuatilia Eva.

ENDELEA……………………………..

Lile gari lililokuwa likimfuatilia Eva ,lilipanda ghorofani na nyuma yake walikuwepo Mathew na Anitha wakiwa na piki piki
“Watu hawa ni akina nani? Kwa nini wanamfuatilia Eva? Akaendelea kujiuliza Mathew.Wakapanda hadi walipofika ghorofa ya pili ,watu wale wakasimamisha gari na mmoja wao akashuka na kuangaza angaza katika magari yaliyokuwa yameegeshwa ,alikuwa akilitafuta gari la Eva.Alipolikosa akarejea garini wakaendelea na kupanda juu zaidi.Mathew akachukua simu na kumpigia Eva
“ Eva jamaa wanapandisha huko juu.Egesha gari kisha shuka ujibanze mahala.Sisi tunaendela kuwafuatilia ili kufahamu nini lengo lao.” Akasema Mathew
“ Tayari nimekwisha shuka nimejibanza katika chumba cha mlinzi “ akasema Eva
Mathew na Eva waliendelea kulifuatilia lile gari hadi maegesho ya juu kabisa.Watu watatu wakashuka toka ile gari.Walianza kuangaza angaza huku na kule kana kwamba kuna gari walikuwa wanalitafuta.Mawazo ya Mathew yalikuwa sawa kwani watu wale walikuwa wakilitafuta gari la Eva.Jamaa mmoja akachungulia ndani ili kuona kama kuna mtu lakini hakukuwa na mtu ndani.Akatoa kidude Fulani kidogo na kukinasisha chini ya gari la Eva kwa haraka.Mathew ambaye macho yake alikuwa ameyaelekeza kwa Yule jamaa alikiona kile kitendo
“ Kuna kidede amekiweka katika gari la Eva.Ninahisi ni kifaa cha kumfuatilia na kuonyesha kila mahala alipo” akasema Mathew kwa sauti ndogo wakiwa wamejificha nyuma ya gari moja
Baada ya kuweka kifaa kile mtu Yule alirejea katika gari lao halafu wakaondoka.
“ Endesha piki piki tuendelee kuwafuata” akasema Mathew wakarukia piki piki yao na kuendelea kuwafuata wale jamaa.Mathew aliyekuwa nyuma akatoa simu na kumpigia Eva.
“ Eva tunaendelea kuwafuatilia wale jamaa ili tuwafahamu ni akina nani .Kuna kitu wamekitega katika gari lako nadhani ni kwa ajili ya kutaka kukufuatilia na kuzijua nyendo zako.Nataka tufahamu nini lengo la kutaka kukufuatilia na kujua kila mahala unakokwenda? “ akasema Mathew
“ Mathew nashukuru sana.Lakini watu hawa ni akina nani na kwa nini wanifuatilie? Akauliza Eva
“ Ni mapema sana kufahamu watu hawa ni akina nani na kwa nini wanakufuatilia .Kwa sasa endelea na kazi zako kama kawaida isipokuwa kitoe kifaa kile na ukibandike katika gari lolote la karibu Nitakupigia simu baadae kukufahamisha tumefikia wapi.Mpaka muda huo nitakapowasiliana nawe tena tafadhali chukua tahadhari” akasema Mathew na kukata simu
Waliwaendelea kuwafuatilia wale jamaa kwa ufundi sana bila ya wao kufahamu kama walikuwa wakifuatiliwa.Wale jamaa walizunguka sehemu kadhaa na hatimaye wakasimama katika mgahawa mmoja mkubwa ulioko kati kati ya jiji maarufu kama City centre.Wakashuka na kuelekea sehemu ya baa.Anitha na Mathew nao wakawafuata ndani ya ile baa,wakatafuta sehemu moja nzuri ambayo iliwawezesha kuwafuatilia wale jamaa vizuri.Waliagiza nyama choma na vinywaji baridi ,wakaendelea kula huku macho yao yakiwa makini kwa kila walichokifanya wale jamaa ambao walikuwa wakipata nyama choma na bia na waliendelea na maongezi yao bila wasi wasi
“ Mathew hawa jamaa hawaonekani kama wana mpango wa kuondoka hapa hivi karibuni.Wameagiza tena raundi nyingine ya vinywaji.Tutakaa sana hapa tukiwafuatilia na kupoteza muda mwingi ambao tungeutumia kwa kazi nyingine.Tunataka kujiingiza katika kazi nyingine wakati tayari tuna jukumu zito mbele yetu na bado hatujafika popote.Tumekwisha gundua lengo lao lilikuwa ni kumfuatilia Eva na anachotakiwa kukifanya kwa sasa ni kuongeza umakini na endapo atahitaji msaada wetu tena katika kuwafahamu zaidi watu hawa basi tutamsaidia baada ya kumaliza shughuli yetu ya msingi” akasema Anitha.Mathew bado aliendelea kuwakazia macho wale jamaa
“ Mathew are you listening to me? Akauliza Anitha
“ Anitha wait for a second” akajibu Mathew na kuendelea kuwakazia macho wale jamaa
Baada ya kama dakika tano hivi mmoja wa wale jamaa aliyekuwa amevaa suruali ya jeans ya bluu na shati jeupe akaitoa simu yake mfukoni ,alikuwa amepigiwa na mtu akabonyeza kituife cha kupokelea akaongea na alipomaliza akaufungua mkoba wake na kutoa simu ile kubwa aina ya Tablet akaelekezana jambo na wenzake wakagonganisha mikono ishara kwamba jambo lao limekwenda vizuri kisha Yule jamaa akatoka akiwa na ile tablet.
“ Nisubiri nakuja sasa hivi” akasema Mathew na kuinuka akatoka nje kumfuata Yule jamaa ambaye alielekea katika maegesho ya magari hadi katika gari moja aina ya Rav 4 rangi nyeusi.Kioo cha mlango wa dereva kikafunguliwa na ndani ya lile gari akaonekana mtu moja aliyevaa miwani myeusi.Jamaa aliyetoka ndani ya mgahawa akasalimiana na Yule jamaa ndani ya gari halafu wakaongea kidogo na akamkabidhi ile tablet.Yule jamaa wa ndani ya gari akaitazama tablet ile halafu wakaonekana kama wanaelekezana jambo Fulani na kisha akaiweka pembeni akafungua mkoba wake na kutoa bahasha ya khaki akamkabidhi Yule mwenzake ,kisha akafunga kioo cha gari lake na kuondoka.Mathew akampigia simu Anitha na kumtaka atoke mara moja.Bila kupoteza muda Anitha akatoka wakapanda piki piki na kuanza kumfuata yule jamaa aliyekuwa amepewa ile tablet
Toka katika mgahawa wa City Centre Yule jamaa alielekea hadi katika jengo Fulani zuri la ghorofa nne .Kabla ya kuingia ndani ya jengo lile kulikuwa na geti lililokuwa likilindwa na walinzi wa kampuni binafsi ya ulinzi.Yule jamaa mwenye Rav 4 alipita pale getini bila matatizo na walipofika akina Mathew wakasimamishwa na askari ambaye shida yake ilikuwa ni kujua mahala walikokuwa wakielekea.
“ Tunamfuata huyu jamaa aliyeingia na gari sasa hivi”
“ Arnold? Akauliza Yule mlinzi
“ Ndiyo tunamfuata Arnold.Tumeongozana naye” akasema Mathew na Yule mlinzi akawaruhusu wapite na kuwalekeza sehemu ya kuegesha piki piki.
“ Hizi ni ofisi za kampuni gani? akauliza akauliza Anitha wakati wakishuka katika piki piki yao.
“ hata mimi sifahamu .We’ll find out soon” akasema Mathew halafu wakaanza kupiga hatua kuelekea nsdani ya jengo lile
Walifika katika sehemu ya mapokezi na kumkuta mwanadada mmoja mrembo aliyewasalimu kwa heshima huku uso wake ukpambwa na tabasamu mwanana.Naye alitaka kufahamu ni ofisi gani ya lile jengo akina Mathew walikuwa wanaelekea.
“ Tunaelekea katika ofisi ya Arnold” akasema Mathew huku akitabasamu na mara Arnold akaonekana akishuka ngazi..Mathew akatabasamu na kusema
“ Ouh mtu mwenyewe tuliyekuwa tunamfuata ndiye huyo anashuka”
“ Hallow Atnmold” akasema Mathew huku akimpa mkono kana kwamba anamfahamu vizuri.
“ Hallow “ akasema Arnold huku akitoa tabasamu lenye mshangao kidogo kwani ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuonana na Mathew.
“ Arnold nina shida nawe ya kiofisi.Unatoka? akauliza Mathew
“ Yah ! ninatoka kidogo.Una shida gani? Akauliza Arnold
“Kama unatoka tunaweza tukaongelea hata nje” akasema Mathew kisha yeye na Anitha wakatangulia nje na kumuacha Arnold akitoa maelekezo Fulani kwa yule mwanadada wa mapokezi kisha akatoka na kuwafuata akina Mathew
“ Una shuda gani kaka? Halafu bado hatujafahamiana.Umetokea wapi?akauliza Arnold huku akionekana ni mwenye haraka sana ya kutaka kuwahi sehemu
“ Ninaitwa Mathew na yule dada anaitwa Anitha”
“ Ndiyo Mathew nikusaidie nini?akauliza Arnold
“ Arnold kwa kuwa una haraka can we talk in your car? Kuna kitu nataka kukuonyesha ” akasema Mathew huku akiingiza mkono mfukoni kana kwamba kuna kitu anataka kutoa.Arnold alisita kidogo lakini kwa kuwa alikuwa na haraka akaongozana na Mathew katika gari lake.Akafungua mlango na kungia garini
“Mathew nieleze shida yako.Nina haraka sana kuna mahala ninawahi” akasema Arnold huku akiwasha gari
“ Ghafla kwa kasi ya umeme ,Mathew akachomoa bastora toka katika mfuko wa koti na kumuwekea Arnold tumboni.Jicho likamtoka hakuamini alichokiona
“ Usithubutu kupiga kelele ndesha gari twende” akaamuru Mathew.Arnold alikuwa akitetemeka mikono akakanyaga mafuta na gari ikaanza kuondoka.Anitha akawasha pikipiki na kuwafuata.

******

Taarifa za Falviana kukimbizwa hospitali zilimfikia jaji Elibariki na kumstua sana.Bila kuaga mtu yeyote akaingia garini na kuondoka kuwahi hospitali
“ Flaviana alikuwa mzima kabisa na hakuonekana kuwa na tatizo lolote,nini kimemtokea na kusababisha akimbizwe hospitali? Akajiuliza Elibariki akiwa garini kuelekea hospitali
“ Inawezekana akawa alizidiwa baada ya kuona mwili wa mama yake? Lakini kama ni fahamu angepoteza kule hospitali tulipokwenda kuuchukua mwili na yeye na Anna wakapewa nafasi ya kutosha ya kuuaga mwili wa mama yao na aliweza kuhimili iweje aje apoteze fahamu huku uwanjani? Nitakwenda kufahamu huko huko hosspitali ,nini kimemtokea” akawaza Elibariki akiwa katika mwendo mkali akiwahi hospitali.Alipofika alipelekwa moja kwa moja katika chumba alichokuwa amelazwa Flaviana
“ Flaviana ..!! akasema Eli mara tu alipoingia mle chumbani na kumkuta mke wake akiwa amelala kitandani
“ Eli .!!! akasema Flaviana .Elibariki akamsogelea na kumbusu
“ Pole sana.Nini kimetokea?akauliza
“ Hata mimi sifahamu Eli.Sielewi nini kimetokea.Ninachokumbuka…..!!” akanyamaza kidogo na kusema
“Unakumbuka nini? Akauliza Elibariki
“Ninachokumbuka tukiwa pale uwanjani shughuli ikiendelea,alinifuata dada mmoja na kumiambia kwamba kuna mtu anahitaji kuniona katika gari la wagonjwa.Dada yule simfahamu lakini alikuwa amejitanda sare zilizovaliwa na akina mama pale msibani.Nikaongozana naye hadi tulipolikaribia gari la wagonjwa lililokuwa limeegeshwa pembeni ya uwanja mara nikahisi kizunguzungu na miguu ikaishiwa nguvu na macho yakashindwa kuona tena.Ninachokumbuka ni kwamba nilitaka kudondoka chini na watu Fulani wakanidaka na nilipozinduka nimejikuta hapa hospitali.Sielewi ni kitu gani kilinitokea na kunisababishia hali ile lakini nilikuwa mzima kabisa na sikuwa na tatizo lolote ”akasema Flaviana
“Pole sana mke wangu.Kwa sasa unajisikiaje?akauliza Elibariki
“Kwa sasa ninajisikia vizuri na madaktari wamesema hakuna tatizo hali yangu inaendelea vizuri na baadae nitaruhusiwa kurejea nyumbani nikapumzike” akasema Flaviana na mara daktari akaingia.Jaji Elibariki akamuuliza kuhusiana na kilichosababisha mke wake kupoteza fahamu ghafla
“ Tumempima lakini hatujaona tatizo lolote kila kitu kinafanya kazi vizuri.Inawezekana hali hii ikawa ilisababishwa na vitu vingine kama vile uchovu mwingi,msongo wa mawazo,n.k.Anatakiwa apate muda mwingi wa kupumzika .” akasema daktari na kuendelea kumpima Flaviana na alipohakikisha kila kitu kiko vizuri akatoka
“ Flaviana dada huyo aliyekwambia kwamba unahitajika katika gari la wagonjwa unaweza kumkumbuka ukimuona?
“ Ndiyo ! nikimuona lazima nitamkumbuka”
“ Alikueleza ni nani aliyekuwa anakuhitaji katika gari hilo la wagonjwa?
“ Hapana hakunieleza nilikuwa naitwa na nani lakini nilimuamini kutokana na na muonekano wake.”akasema Flaviana .Jaji Elibariki aliyekuwa amekaa kitandani pembeni ya mkewe akamtazama na kusema
“ Kuanzia sasa tafadhali usimuamini mtu yeyote yule ambaye humjui.Hata wale ambao unawafahamu kuwa nao makini sana.Dr Flora amefariki katika mazingira yenye utata mkubwa na mpaka hapo tutakapobaini ni akina nani waliosababisha kifo chake tunatakiwa tuwe makini sana”akasema Jaji Elibariki
“Unayoyasema ni ya kweli kabisa.Inanibidi kuwa makini sana “akasema Flaviana
“Ni nani lakini aliyekuwa anataka kuonana na Flaviana? Akajiuliza jaji Elibariki
“Suala hili linanipa mashaka sana.Nina wasiwasi sana na maisha ya mke wangu.Watu waliomuua Dr Flora wako ndani ya ikulu na hawatasita kufanya kila linalowezekana ili kujilinda wasijulikane.We’re in great danger.I have to talk to Mathew about this ”akawaza Elibariki akachukua simu yake na kumpigia Mathew lakini simu ikaita bila kupokelewa,akapiga tena bado haikupokelewa

********

John Mwaulaya alikuwa ameiweka mikono kifuani pake.Alionekana kuwa katika mawazo mengi
“Hali yangu inazidi kuwa dhaifu na ninafahamu kwamba sintopona ugonjwa huu lakini siko tayari kuja kuuliwa na mkono wa Dr Burke.Nina hakika Josh atafanikiwa kumuwahi kabla hajaniwahi. Nilifanya makosa makubwa kumpendekeza Osmund katika nafasi kubwa na kuwaacha vijana watiifu kama Josh.Endapo atafanikiwa kumuondoa Burke ,nitajitahidi kwa kila niwezavyo kabla pumzi zangu hazijakata kuhakikisha Josh anakuwa katika nafasi za juu kabisa ndani ya Team SC41”akawaza John na kumbukumbu zake zikamrejesha mbali
“ Bado naikumbuka siku ile nilipomuua seneta Joe Burke na yule rafiki yake mwanasiasa Elisante.Ni miaka mingi imepita lakini nahisi ni kama jana .” akawaza John Mwaulaya akafumba macho na kuikumbuka siku aliyofanya mauajiya seneta Joe Burke baba yake na Dr Burke
Kiza kimenza kutanda jijini Dar es salaam .Pilika pilika za jioni watu wakishughulika na usafiri wa kuwarejesha makwao ziliendelea kama kawaida.Katika hoteli ya Salama Spring hali ilikuwa ni ya utulivu mkubwa.Watu waliendelea kupata vinywaji chakula na kuburudika na muziki wa bendi
Saa mbili kasoro dakika nane ,gari moja aina ya Nissan Patrol ikapita katika geti la kuingilia hotelini hapo na kuelekea moja kwa moja katika maegesho.Haraka haraka mlango ukafunguliwa akashuka kijana mmoja na kuwahi kuufungua mlango wa mbele.Mtu mmoja mzee wa makamo akashuka na kuongozana na yule kijana kuelekea ndani ya hoteli.Huyu alikuwa ni Mr Elkisante kiongozi wa chama kikubwa cha siasa nchini ambaye amefika katika hoteli hii kukutana na seneta Joe Burke toka chama cha Republican cha nchini Marekani
Wakati Dr Elisante akiingia hotelini hapo hakuwa na habari kwamba kuna watu wanne waliokuwa wakimfuatilia.Akiwa ameongozana na mlinzi wake mmoja walielekea hadi katika chumba cha Seneta Burke
“ He’s in” John Mwaulaya akiwa amekaa katika sehemu ya baa akipata kinywaji akiwa amezungukwa na warembo wawili ,alitaarifiwa na kijana wake aliyekuwa amekaa ghorofa ya kwanza kuhusiana na kuwasili kwa Dr Elisante.Mara tu alipoipokea taarifa iIe John akainuka na kuwaomba wasichana wale waendelee kupata kinywaji na angerejea baada ya muda mfupi,kisha akatoka
Mara tu baada ya kuachana na wale warembo John akatoa simu na kumpigia mmoja wa vijana wake na bila kuchelewa kijana Yule akampa maelekezo
“ John ,nenda ghorofa ya pili ingia chumba namba 108,utakuta kila kitu tayari kimeandaliwa .Chumba cha Seneta Burke ni namba 123 ghorofa ya nne” akasema Scola muhudumu wa hoteli hii ambaye ni mmoja kati ya vijana wa John mwaulaya na ndiye alifanikisha mpango huu kwa kiasi kikubwa
Kwa mwendo wa kujiamini John akatembelea hadi chumba alichoelekezwa,akaangaza kama kuna mtu yeyote ambaye alikuwa anamfuatilia kisha akajitoma ndani ya ile chumba ambacho mlango wake ulikuwa wazi.Juu ya kitanda kuliwekwa suti nyeusi ,shati jeupe na tai nyekundu mavazi ambayo huvaliwa na wahudumu wa kiume wa hoteli hii.Haraka haraka akavua nguo zake na kuvaa zile sare za wahudumu akajitazama katika kioo alionekana kama kweli muhudumu wa hoteli .Ndani ya chumba kile kulikuwa na torori la kubebea vyakula na vinywaji lililokuwa na chupa kadhaa za vinywaji.Akaiweka bastora yake yenye kiwambo cha sauti chini ya kitambaa cheupe kilichofunika lile torori na kuanza kulisukuma akatoka na kupanda hadi ghorofa ya nne.Kila aliyekutana naye hakumtilia shaka hata kidogo kama si muhudumu wa hoteli ile.
John mwaulaya akafika hadi katika mlango wa chumba cha Seneta Burke akagonga na mlango ukafunguliwa na mlinzi wa Dr Elisante
“ Halow’ John akamsalimu yule muhudumu
“ Hallow ,nikuidie nini? Akauliza yule mlinzi
“ Nimeelekezwa nilete vinywaji katika chumba hiki” akasema John
“ Umeelekezwa na nani?
“ Kuna simu imepigwa na kuagiza vinywaji viletwe “ akasemaJohn. Mlinzi yule akamtazama John kwa makini na kumuomba asubiri palepale ili akamuulize bosi wake kama ni kweli vinywaji vimeagizwa.Kitendo cha kumpa mgongo John ni kosa kubwa alilolifanya yule mlinzi.Hazikupita hata sekunde tano kwa kasi ya ajabu John akaichukua bastora yake na kumiminia risasi mfululizo yule mlinzi ,ambaye alianguka chini .Haraka haraka John akaliingiza ndani lile torori la vinywaji na kufunga mlango.Chumba alichopanga seneta Burke kilikuwa na vyumba vitatu yaani sebule chumba cha chakula na chumba cha kulala.Sauti za watu wakijadiliana jambo zilisikika katika chumba cha kulia chakula.Hakutaka kupoteza muda akaufungua mlango ule kwa kasi na kujitoma ndani.Kitendo kile kiliwastua sana wazee wale waliokuwemo mle ndani.Kufumba na kufumbua bila hata kutamka neneo moja John akaanza kuifanya kazi iliyompeleka mle,aliwamiminia risasi wazee wale ,Seneta Joe Burke na DrElisante wakaanguka chini hawakuwa na uhai tena,Risasi nyingi zilizotoka katika bastora mbili za John zilizokuwa na viwambo vya sauti ziliwasambaratisha na kuwaharibu vibaya.Bila kupoteza hata sekunde moja John akakusanya makaratasi yote yaliyokuwapo pale mezani,akayapakia katika sanduku dogo akaenda chumbani na kuchukua kompyuta ndogo ya seneta Burke pamoja na kila kitu ambacho alikiona kinafaa kuchukuliwa halafu akaufunga mlango na kurejea katika chumba kile alichoacha mavazi yake akavua zile nguo za wahudumu wa hoteli akaziweka katika sanduku dogo na kuondoka.
“That’s how I killed seneta Burke.Baada ya miaka mingi kupita mwanae anakuja kulipiza kisasi,he’s coming to kill me”
Akawaza John Mwaulaya

TUKUTANE SEHEMU IJAYO……
 
SEASON 2
SEHEMU YA 4
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Watu hawa wanaomfuatilia Eva ni akina nani? Nafahamu Eva ana fanya kazi kwa siri katika idara ya usalama wa taifa.lazima kuna wau watakuwa wanataka kumchunguza.Hizi kazi niza hatari sana.Siku zote unaishi kama ndege.” Akawaza Mathew na mara Anitha na Noah wakaingia kujumuika naye pale mezani
“Anitha umefikia wapi kuhusu ile program ?
“ Ninaendelea na hiyo kazi .Lakini huyu jamaa Arnold anaonekana ni mtu anayeifahamu sana kompyuta .Nimeangalia namna alivyoitengeneza ile program dah ! yuko vizuri sana” akasema Anitha
“ Nimezungumza na Elibariki kwamba atajitahidi kufika jioni ya leo ili tuweze kuongea naye kuhusu lile suala la Peniela.Yeye ndiye tutakayemtumia katika kumchunguza Peniela.Peniela lazima kuna kitu anakifahamu kuhusiana na kifo cha Edson na Team SC41.Ili tuufahamu ukweli yatubidi tumfanyie uchunguzi mkubwa sana na nina hakika yeye ndiye atakayetuongoza kwenye ukweli ”akasema Mathew


ENDELEA…………………………
Jua limeanza kupungua nguvu yake kuashiria kwamba siku inaelekea ukingoni.Shughuli ya kuuaga mwili wa Dr Flora ilimalizika katika viwanja vya ukombozi halafu ukapelekwa katika makazi binafsi ya rais ambako ungelala kule kabla ya kusafirishwa kesho yake asubuhi kuelekea kijijini alikozaliwa kwa mazishi.Zoezi lilichukua muda mrefu zaidi ya ilivyokuwa imetazamiwa kutokana na idadi kubwa ya watu waliojitokeza kumuaga mwanamama huyu ambaye katika kipindi cha uhai wake alijitoa sana katika kuwakomboa kiuchumi wanawake na vijana.
Nyumbani kwa rais mwili wa Dr Flora uliwekwa katika chumba maalum ambako watu mbali mbali ambao hawakupata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho katika viwanja vya ukombozi walikuwa wanaendelea na zoezi hilo.Watu walikuwa wengi sana na ulinzi ulikuwa mkali
Saa kumi na mbili na dakika nane za jioni Dr Joshua akaingia katika chumba alichokuwamo Flaviana akiwa na mdogo wake Anna pamoja na binamu zao watatu
“ Flaviana pole sana.Nilipata taarifa kwamba ulipoteza fahamu ghafla ukakimbizwa hospitali.Nilimuagiza Amos aje akutazaame.Unaendeleaje hivi sasa?akauliza Dr Joshua
“ Ninaendelea vizuri sana baba.Madaktari walinipima wakasema kwamba uchovu wa mwili na mawazo mengi ndivyo vilisababisha hali ile kunitokea.Dr Amos naye ametoka hapa kunipima muda si mrefu na kila kitu kinakwenda vizuri hakuna shida yoyote” akasema Flaviana
“ Pole sana Flaviana hali kama hiyo ni ya kawaida sana kwa nyakati kama hizi.Unachotakiwa ni kujipa mapumziko ya kutosha.Tomorrow we’ll have a big day.I need you all to be strong” akasema Dr Joshua
“ Usihofu baba,tutajitahidi “ akajibu Anna
“ Ok ! Kuna watu ninaohitaji kuonana nao mida hii .Tutaonana baadae “ akasema Dr Joshua na kutaka kutoka Flaviana akamuita
“ baba vipi kuhusu lile suala ? Umekwishaanza kulifanyia kazi?
“ Ndiyo .Tayari limekwisha fanyiwa kazi na tayari nimepokea taarifa ya madaktari walioufanyia uchunguzi mwili wa mama yenu ili kujua chanzo cha kifo chake”
“ really? Akauliza Flaviana
“ Inasemaje? Wamegundua nini?akauliza Anna
“ Bado sijaifungua na kujua kilichomo ndani yake .Nilitaka tuifungue tukiwa wote kesho baada ya kurejea toka katika mazishi.Ile ni taarifa ya familia kwa hiyo inabidi ifunguliwe na sisi sote.Nadhani tulifanye zoezi hilo kesho baada ya kurejea toka katika mazishi”akasema Dr Joshua
“ Dady can we open it today? Akauliza Flaviana
“ It’s ok .Tunaweza kuifungua ripoti hiyo hata leo.Tukutane katika chumba cha maongezi baada ya dakika ishirini .Kuna watu ambao nahitaji kuonana nao sasa hivi”akasema Dr Joshua na kutoka akiwa ameongozana na walinzi wake.Baada tu ya Dr Joshua kutoka,Flaviana akachukua simu na kumpigia mumewe
“ Hallow Flaviana unaendeleaje? Akauliza jaji Elibariki
“Ninaendelea vizuri.Dr Amos ametoka hapa kunipima muda si mrefu na kila kitu kinaendelea vizur.Uko wapi ?
“ Niko na wafanyakazi wenzangu wamekuja kutupa pole kwa msiba” akasema Elibariki
“ Ok vizuri.Eli unaweza ukaja mara moja huku ndani ? Baba anatuhitaji kuna kitu anataka kutuambia” akasema Flaviana
“ Ok ninakuja” akasema jaji Elibariki
Baada ya dakika ishirini Dr Joshua akafika katika chumba cha maongezi kama alivyokuwa amewaahidi wanae.Alionyesha mshangao Fulani baada ya kumkuta Jaji Elibariki ndani ya kile chumba.Ilionekana wazi hakuwa amependezwa kumkuta jaji Elibariki mle ndani.Wakasalimiana halafu akaketi
“ Elibariki nimeshukuru na wewe umefika katika kikao hiki.Nimewaambia wenzako tukutane hapa kuna jambo nataka tulizungumze” akasema Dr Joshua .Flaviana ,Anna,jaji Elibariki walikuwa kimya kabisa wakimsikiliza
“ Kufuatia kifo cha ghafla cha mama yenu ,ilinilazimu kufanya uchunguzi kuhusiana na nini kilisababisha kifo chake” akanyamza kidogo halafu akaendelea
“Niliunda timu ya madaktari bingwa toka katika hospitali kuu ya taifa kwa ajili ya kufanya uchunguzi huo na kubaini sababu ya kifo cha ghafla cha mma yenu.Leo mchana wametoa ripoti yao.Anna hebu fungua mlango na mwambie Captain Amos ailete ile ripoti hapa atusomee ” akasema Dr Joshua.Jaji Elibariki ambaye alionekana kuwa katika mshangao kidogo akauliza
“ Mzee ni uchunguzi gani tena uliofanyika? Ulifanya uchunguzi mwingine kuhusiana na kifo cha Dr Flora ukiacha mbali ule ambao tuliufanya sisi?
“Najua utashangaa Elibariki kwamba kuna uchunguzi mwingine ulifanyika lakini ilinilazimu kufanya uchunguzi kwa kuwatumia madaktari bingwa ili kubaini nini chanzo cha kifo cha Dr Flora” akasema Dr Joshua katika sauti ambayo ilionyesha wazi kwamba hakuwa akihitaji tena maswali yoyote toka Elibariki
“ Lakini mzee uchunguzi si tulishaufanya na nikawaletea ripoti kuhusiana na kilichosababisha kifo cha mama na wewe mwenyewe ukaahidi kulifanyia kazi sasa uchunguzi juu ya uchunguzi inakuwaje hapa? Akauliza Jaji Elibariki
“ Elibariki suala hili ni suala zito linahusu uchunguzi wa kifo cha mtu ,tena mke wa rais,hivyo lazima ufanyike uchunguzi mkubwa na kina.Ninashukuru kwa kujitahidi kufanya uchunguzi wako lakini sisi katika serikali huwa hatufanyi kazi kwa kutegemea taarifa ya kutengenezwa,taarifa isiyokuwa na kichwa wala mkia,taarifa isiyo na uthibitisho wowote wa daktari anayetambuliwa na serikali.Nakupongeza kwa juhudi zako na kwa kujali lakini wataalamu wangu hawakuwa tayari kuifanyia kazi taarifa uliyoitoa.Taarifa itakayofanyiwa kazi ni taarifa ambayo imefanyiwa kazi na madaktari bingwa na kuthibitshwa na daktari mkuu wa serikali na si taarifa ya kuokoteza okoteza.” Akasema Dr Joshua katika hali iliyoonyesha wazi alikuwa akimkebehi Jaji Elibariki kwa ripoti aliyoileta.Jaji Elibariki akasimama na kutaka kusema jambo lakini kabla hajasema chochote Captain Amos daktari wa familia ya rais akaingia akiwa na bahasha mkononi
“Karibu sana Captain Amos.Familia yote imekutana tayari kuipokea ripoti ya madaktari.Tafadhali tusipoteze wakati ifungue na utuambie ni kitu gani kimeandikwa na madaktari” akasema Dr Joshua
“ Ripoti hii ni ya uchunguzi wa kubaini sababu ya kifo cha ghafla cha Dr Flora.” Akasema Captain Amos.Akaipitia ripoti ile yenye karatasi tano ,kisha akasema
“ Kwa mujibu wa madaktari bingwa waliofanya uchunguzi huu wamebaini kwamba kifo cha ghafla cha Dr Flora kilisababishwa na shinikizo la damu.Hawajaona kitu kingine chochote kilichosababisha kifo chake” akasema Captain Amos daktari wa familia ya rais
“ Ahsante Amos.Unaweza kwenda”akasema Dr Joshua.Captain Amos akatoka
“ Nyote mmeisikia taarifa ya madaktari bingwa .Mama yenu alikufa kutokana na shinikizo la damu na si sababu nyingine yoyote. Taarifa hii ya madaktari bingwa inapingana na taarifa aliyotuletea mheshimiwa jaji ambayo inasema kwamba kifo cha mama yenu kilisababishwa na sumu.Ukiachana na taarifa hiyo nimepokea pia taarifa toka kwa vijana wangu niliowatuma wafanye uchunguzi kuhusiana na mambo yale mliyoniambia kwamba inawezekana kuna watu walihusika katika kusababisha kifo cha mama yenu.Taarifa ya vijana wangu inasema kwamba hakuna mtu yeyote ambaye alihusika katika kusababisha kifo cha Dr Flora na wala hakuna uzembe wowote uliofanyika.Mlimzungumzia Dr Kigomba kwamba alisikika akipiga simu kuzuia uchunguzi usifanyike lakini ukweli ni kwamba Dr Kigomba alipata taarifa ya kwamba kuna watu waliokuwa wakifanya uchunguzi wa siri na ndiyo maana akatoa amri kwamba watu hao wazuiliwe haraka sana kwa sababu tayari kulikuwa na mpango wa kuufanyia uchunguzi wa kina mwili wa mama yenu kwa kuwatumia madaktari bingwa .Dr Flora ni mtu mkubwa kwa hiyo uchunguzi wa kifo chake unatakiwa uwe maalum pia na si kwa kuwatumia madaktari wa kuokoteza mitaani.Sijaongea chochote kuhusiana na kitendo cha kihuni kilichofanywa na Elibariki na wenzake .Naomba leo niweke wazi kwenu kwamba nimechukizwa sana na kitendo kile na ninaomba kisijirudie tena.Sijataka kuchukua hatua zozote kwa sababu Elibariki wewe ni mwanangu na ninakuheshmu sana lakini wewe na wenzako mlipaswa kupewa adhabu kali sana kwa kitendo cha kihuni mlichokifanya.Mmefanya uhuni na kutuletea taarifa ya uongo ambayo imetusababishia matatizo makubwa ndani ya familia yetu na kwa watu wetu wa karibu tunaowaamini.Dr Kigomba ambaye mmemtuhumu kwamba anahusika katika kusababisha kifo cha Dr Flora ni mtu wangu wa karibu na nimefanya naye kazi kwa muda mrefu ni mtu ninayemuamini sana lakini mmetaka kunifanya niamini kwamba ni mtu mbaya.Sintafanya lolote kuhusiana na jambo lile lakini naomba mfahamu kwamba nimechukizwa sana .Kwa maana hiyo basi mjadala mzima wa kuhusina na sababu ya kifo cha mama yenu nimeufunga rasmi leo na sitaki kabisa kuendelezwa kwa mambo yasiyokuwa na ukweli wowote.Tayari madaktari bingwa wamekwisha thibitisha kwamba mama alikufa kifo cha kawaida kilichosababishwa na shinikizo la damu.” Akasema Dr Joshua halafu akamuomba Flaviana watoke wakaongee nje.Jaji Elibariki alibaki amepigwa na butwaa hakujua aseme nini.Alikuwa na hasira zisizomithilika.Dr Joshua na Flaviana wakatoka nje ya kile chumba
“ Flaviana I’m so disappointed with you” akasema Dr Joshua ambaye uso wake ulionyesha wazi kwamba alikuwa amechukia sana
“ Why father?akauliza Flaviana
‘ kwa nini umemjumuisha Elibariki katika kikao cha familia?
“ Baba,Eli ni mume wangu na ni sehemu ya familia yetu pia.Mbona katika mambo yetu mengine mengi ya kifamilia anashirikishwa? Niliona nimuite kwa sababu hata yeye kikao kile kilimuhusu kama mmoja wa wanafamilia
“ Ulifanya kosa kubwa Flaviana.Elibariki hakutakiwa kuwepo katika kikao kile.Kikao kile kilituhusu sisi pekee na si watu wengine wa hovyo hovyo”
“ dady ! Elibariki ni mume wangu na si mtu baki wala wa hovyo hovyo”
“ Vyovyote unavyomchukulia I don’t care lakini ninachokwambia na kwamba sitaki kumuona katika vikao vyetu vyovyote vya kifamilia.Ni kijana mshenzi sana yule.Ametaka kunisababishia matatizo makubwa na watu wangu wa karibu ninaowaamini na kufanya nao kazi kwa karibu.Ameleta ripoti ya kihuni na kutusababishia matatizo makubwa ndani ya familia yetu.Ninakuweka wazi kwamba ninamchukia sana huyo unayemuita mumeo.Ninasikitika sana kwa kukubali kuolewa na mtu kama yule.Ninashangazwa pia na jinsi unavyosimama na kumtetea leo wakati ni hivi majuzi tu ulikuja hapa ukilia na kusema humtaki tena yule mwanaume.”akasema Dr Joshua kwa ukali
“ dady ,Elibariki hapaswi kulaumiwa katika hili.Mimi ndiye ninayepaswa kubeba lawama kwa sababu ni mimi ndiye niliyemtuma baada ya kuhisi kwamba kuna sintofahamu kuhusiana na sababu ya kifo cha mama na hasa baada ya daktari mmoja pale katika hospitali kuu ya jeshi kuniambia kwamba kuna taarifa iliwafikia kwamba wasifanye uchunguzi wa kuhusiana na kifo cha mama.Yawezekana taarifa aliyopewa Elibariki na madaktari waliomsaidia kufanya uchunguzi ndiyo yenye matatizo na haikuwa na ukweli.Mimi ndiye ninayepaswa kuzibeba lawama hizi kwa sababu Elibariki alifanya kazi ile kwa shinikizo langu” akasema Flaviana
“ Flaviana naomba unisikilze mwanangu,hata wewe ulifanya kosa kubwa sana,ulipaswa kabla ya kushirikiana na mumeo kufanya jambo la hatari kama lile uje kwanza kwangu kunieleza na kwa pamoja tungeona nini cha kufanya.Lakini pamoja na hayo endapo angeleta taarifa yenye ukweli ndani yake basi kusingekuwa na tatizo lakini yeye ameleta taarifa ya uongo mkubwa ambayo imetusababishia sisi matatizo makubwa ndani ya familia,hata mimi taarifa ile imenipa wakati mgumu sana.Sielewi lengo lake ni nini hasa kwa kutuletea taarifa ile ya uongo.Nimejizuia kuchukua hatua zozote kwa sababu yako lakini kama angekuwa si mumeo angepata adhabu kali sana.Siku nyingine kama kuna jamo unataka kulifanya tafadhali usimuamini mumeo,njoo kwangu moja kwa moja.” Akasema Dr Joshua halafu akaondoka na kuelekea katika chumba chake akachukua simu na kumpigia Dr KIgomba
“ Hallow mzee” akasema Dr Kigomba
“ Dr Kigomba naomba tuonane ndani ya dakika tano”
“ Ok mzee ninakuja sasa hivi” akasema Dr Kigomba
Dr Joshua akavuta pumzi ndefu akakaa juu ya kitanda
“ Tayari nimekwisha limaliza lile suala ambalo lilitaka kutuletea matatizo makubwa.Nimewaondoa hofu kuhusiana na kifo cha mama yao kwa kuwasomea ripoti ile.Kwa sasa wote wanaamini kwamba kilichomuua mama yao ni shinikizo la damu.Tatizo linabaki kwa mtu mmoja tu ambaye ni Elibariki.Huyu ndiye anayeufahamu ukweli japokuwa tayari nimemjengea mazingira ya kutokuaminiwa tena lakini bado ni hatari kwetu.Kumuacha hivi hivi ni sawa na kulishikilia bomu mkononi na muda wowote linaweza kutulipukia.Siko tayari Elibariki awe ni mtu wa hatari kwetu eti kwa kuwa tu nimume wa mwanangu.Sintojali hilo na lazima ashughulikiwe haraka sana.Vile vile wanatakiwa wafahamike watu ambao alishirikiana nao kuifanya kazi ile ili nao washughulikiwe haraka sana .Jambo hili si la kufanyia mzaha hata kidogo.Na yotehaya yamesababishwa na Flaviana .Bila yeye tusingefika hapa tulipo hivi sasa.” Akawaza Dr Joshua
Flaviana alihisi kuchanganyikiwa na hakujua afanye nini.Alishindwa amuamini nani kati ya baba yake au mumewe Elibariki
“ Who is telling the truth? Nimuamini nani? Akajiuliza
“Lakini inawezekana baba akawa sahihi kwamba taarifa aliyoileta Elibariki haikuwa imejitosheleza.Haikuwa na usahihi ndani yake .Sina uhakika na uwezo wa madaktari waliomsadia kuufanya uchunguzi huo.Taarifa ile ya baba nadhani ndiyo sahihi kwani imefanyiwa kazi na madakari bingwa.Kinachofuata hapa sasa ni kulifunga rasmi jambo hili ililisiendelee kutuchanganya.” akawaza Flaviana na kurejea katika chumba cha maongezi alikomuacha mumewe.Jaji Elibariki alikuwa ameinama akiwaza.Flaviana akamsogelea karibu
“ Eli naombausiwaze sana mume wangu kuhusu mambo aliyoyasema baba” akasema Flaviana
“ Flaviana please believe me,taarifa hiyo anayoisema baba yako haina ukweli wowote.Rais amedanganywa,amepewa taarifa isiyo ya kweli.Tafadhali naomba usiiamini taarifa hiyo hata kidogo.Kuna kitu kinafichwa hapa ,believe me something is going on” akasema Elibariki
“ Elibariki hata mimi nimechanganyikiwa na sijui niamini lipi lakini nimeamua ni vyema endapo tutaachana na suala hili kwani litatuchanganya sana.” akasema Flaviana
“ Flaviana my love, kama kuna wakati unaopaswa kuniamini basi ni sasa.Please believe me,we did everything to get that report.Uhai wa mtu umepotea katika kuutafuta ukweli lakini matokeo yake taarifa yangu inakataliwa na kuonekana ni ya kuunga unga .Fumbua macho Flaviana something is going on here”
“ Eli I’m confused right now.Sielewi niende upande upi.Ninyi nyote ni watu ninaowaamni lakini …” Flaviana akasita kidogo
“ lakini nini? Akauliza Elibariki
“ Nashindwa nifanye nini.Please Eli I need to be alone for now” akasema Flaviana.Elibariki akamtazama kwa makini na kuuliza.
“ So you don’t trust me?
“Si kwamba sikumaini Eli but ……” akajibu
“ Its ok ..ninajua unachotaka kukisema” akasema Elibariki na kutoka kwa hasira akaubamiza mlango

*******

Dr Kigomba alifika haraka kuitika wito wa mheshimiwa rais
“ Kigomba tayari nimelimaliza lile suala”akasema Dr Joshua
‘ “That’s good news Mr President”akasema Dr Kigomba huku akitabasamu
“ Nimetoka kuongea na familia na wote wameridhika na ripoti ile uliyoileta.Umefanya kazi nzuri sana .Kwa sasa wote wanaamini kwamba mama yao alifariki kwa shinikizo la damu na si kwa kuchomwa dawa yenye sumu kama alivyodai yule muhuni.Pamoja na hayo bado tuna tatizo “
“ Tatizo gani mheshimiwa rais?
“ Ni Jaji Elibariki.Lile ni bomu tumelishika na siku moja linaweza kutulipukia na kutujeruhi.Sitaki nitakapokuwa nimemaliza muda wangu wa uongozi nianze tena kupata usumbufu wa aina yoyote ile.Ninataka baada ya kumaliza uongozi wangu niishi maisha ya raha mustarehe kwa hiyo kitu chochote kinachoonekana kuwa ni kikwazo katika mpango wetu basi nitakiondoa mara moja kama nilivyofanya kwa Flora.Elibariki anaufahamu ukweli wa kifo cha Flora na nina hakika siku moja anaweza akatulipua.Ninahitaji ashughulikiwe haraka iwezekanavyo.” Akasema Dr Joshua
“Unataka tumshughulikie vipi mzee? Ukumbuke huyu ni mkweo”
“ Take him away,but in a proffesional way.No mistake “ akasema Dr Joshua
“ Are you sure about this Mr President? Akauliza Dr Kigomba
“ Yes I’m sure.Hili ni bomu na tunatakiwa kulitegua haraka sana.Lakini kazi hii inatakiwa ifanyike kwa uangalifu mkubwa sana.Wakabidhi kazi hii vijana ambao wana ujuzi wa hali ya juu.Ninarudia tena no Mistake this time.Elibariki ni hatari sana kwetu kuliko hata Flora.Baada ya Elibariki tutaangalia namna ya kumuondoa pia na Captain Amos” Akasema Dr Joshua
“ Ok Mr president nimekwisha kuelewa.Nitalifanyia kazi hilo suala” akasema Dr Kigomba na kuondoka
“ Siko tayari kuona kizingiti chochote katika mpango wangu huu mkubwa ambao uo mbioni kukamilika.Yeyote atakayeonekana kuwa ni kikwazo kwangu nitamuondoa hata kama ni mwanangu “akawaza Dr Joshua

*******

“ Kuna jambo linaendelea hapa ikulu si bure.Ukweli wa kifo cha Dr Flora unazidi kufichwa na sasa hata rais amekubali kudanganywa na taarifa ya uongo na akaiamini.Hata familia yake wote wameonekana kuiamini taarifa ile.Nimeumizwa sana na maneno aliyoyasema Dr Joshua dhidi yangu.Amediriki kuniita mimi muhuni .Mimi na heshima zangu leo hii ninaitwa muhuni .Ninajuta kwa kukubali kuifanya kazi ile ya Flaviana.Juhudi zote za kutaka kuupata ukweli zimekuwa ni kazi bure na badala yake nimeambulia matusi.Kinachoniumiza kichwa ni kwa nini ukweli unafichwa? Kwa nini Dr Flora aliuawa? Akajiuliza jaji Elibariki
“ Ninamuamini sana Mathew na katu hawezi kunipa taarifa isiyo ya kweli.Yeyena timu yake wamehangaika sana na kuhatarisha maisha yao kwa sasabau tu ya kuipata taarifa ile .Hapana siwezi kukubali juhudi zao zipotee bure.Lazima tufahamu ni kwa nini ukweli wa kifo cha Dr Flora unafichwa? Lazima kuna kitu kinaendelea pale ikulu.Lazima nionane na Mathew na nimueleze kuhusu jambo hili ili tuone namna ya kuweza kulifanyia uchunguzi na kuubaini ukweli.NImeanza kuwa na wasi wasi sana hata kuhusiana na kifo cha Edson kwani hata naye alikuwa ni mfanyakazi wa ikulu” akawaza Elibariki halafu akachukua simu na kumpigia Mathew
“ Hallow Mathew” akasema jaji Elibariki
“hallow Elibariki”
“ Mathew kuna tatizo limetokea tena ndugu yangu”
“ Tatiza gani Eli?
“ Siwezi kukuelaza simuni.Uko nyumbani”
“ Ndiyo niko yumbani lakini nitatoka muda si mrefu kuna mahala nitaelekea”
“ Ok nakuja sasa hivi” akasema Elibariki na kukata simu akaelekea katika gari lake na kuondoka”

TUKUTANE SEHEMU IJAYO………
 
SEASON 2

SEHEMU YA 14


ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Kifo cha Noah kimeniumiza sana Elibariki.Lakini hatuna namna ya kufanya imeshatokea imetokea.Kwa sasa uko wapi? Akauliza Mathew
“ Kuna sehemu nimejificha”

“ Is it a safe place? Are you sure you are safe? Akauliza Mathew
“ Yes I’m sure.I’m safe”
“ Ok good.Endelea kujificha hapo hapo .Kwa sasa tunashughulikia msiba wa Noah.Nimewasiliana na wazazi wake tayari nchini Zimbabwe na wamesema kwamba tutawasiliana tena asubuhi ili wanitaarifu kuhusiana na walichokipanga.Noah alikuwa ni kama mdogo wangu kwa hiyo nitaweka kila kitu pembeni kwa sasa na baada tu ya kumzika ndipo nitaanza tena kazi.Ninakuahidi kwamba yeyote aliyehusika katika tukio hili hatabaki salama.Nitakaporejea utashuhudia nitakachokifanya.Kila risasi iliyoingia mwilini mwa Noah italipwa.Kwa sasa endelea kukaa hapo hapo hadi nitakaporejea.Endapokukiwa na tatizo lolote unitaarifu mara moja.Lakini mpaka hapo tutakapoonana tena please stay safe” akasema Mathew na kukata simu



ENDELEA………………………..


“ Mathew ameumizwa sana na kifo cha Noah .Nimeisikia sauti yake na anaonekana wazi kwamba ana nia ya dhati ya kulipiza kisasi.Hata mimi ninamuunga mkono kwa hilo.Lazima watu wote waliofanya kitendo kile wapatikane .Watu wale walikuwa na lengo la kuniua lazima niwafahamu ni akina nani kwa nini wanataka kuniua? Akawaza jaji Elibariki.Mawazo mengi yakamjia kichwani kutafakari kuhusiana na tukio lile .

“ Ama kweli maisha ya mwanadamu ni mafupi sana.Dakika chache zilizopita nilikuwa naongea na kucheka na Noah lakini ghafla tu watu wameukatili uhai wake.Tukio lile litaendelea kukaa katika kumbukumbu zangu kwa miaka mingi sana .Ni tukio baya sana kuwahi kunitokea lakini kwa msaada wa Mathew nina hakika nitawafahamu waliofanya tukio lile.” Akawaza na kukumbuka toka alipopigiwa simu na Yule mwanamke na kumzuia asiingie katika gari

“ Mawazo yananijia kwamba yawezekana kabisa sababu ya kutaka kuniua chanzo chake kikawa ni kifo cha Dr Flora ambaye akifo chake kimetawaliwa na utata mwingi. Nilifanikiwa kuufahamu ukweli wa kilichomuua Dr Flora lakini nilishangaa baadaya taarifa yangu kutupwa mbali kwamba ni taarifa ya uongo na ya kuunga unga.Ninamuamini Mathew na hawezi kunipa taarifa ya uongo.Ninahisi kitendo changu cha kuufahamu ukweli wa kifo cha Dr Flora kimewapa mashaka sana watu waliomuua na hivyo ili kuendelea kuificha siri hii wakaona njia bora ni kuniua na mimi pia.Ni akina nani watu hawa? Kwa nni walimuua Dr Flora? Kuna mambo mengi hapa ya kujiuliza na kuyatafutia majibu “ akawaza na taratibu kijiusingizi kikaanza kumpitia kutokana na dawa alizokuwa amepewa .Peniela akamfunika vizuri na kulala pembeni yake.
“ Lini na mimi nitampata mwanaume wa kulala naye kitandani kama hivi ambaye nitakuwa na uhakika kwamba ni mwanaume wangu? Nitakuwa nikilala na wanaume wa wenzangu hadi lini? Nimekwisha anza kuchoshwa na maisha haya.Sitaki tena kuwa sehemu ya Team SC41.Nataka niishi maisha ya kawaida kama wanawake wenzangu.Lakini yote haya mwisho wake umekaribia sana.Nikishaikamilisha operesheni 26B lazima nirejee katika maisha ya kawaida.” akawaza Peniela akiwa ameuweka mkono wake kifuani kwa jaji Elibariki


********

Kumepambazuka na nchi ikia imeamshwa na taarifa kubwa ya kushambuliwa kwa jai wa mahakama kuu.Vyombo vyote vya habari hii ndiyo ilikuwa habari yao kubwa siku hii.Hakuna aliyeweza kufahamu mahal aliko jaji Elibariki japokua kulikuwa na juhudi kubwa za jeshi la polisi katikakumtafuta mahala aliko.Flaviana Hakuweza kabisa kupata usingizi kutokana na hofu aliyokuwa nayo.Mpaka kunapambazuka hakuwa amepata taarifa zzote kuhusiana na wapi alipo mume wake.Akampigia smu baba yake na kumuuliza kama kuna taarifa zzote za kuhsu mahala aliko mume wake lakini mheshimiwa rais akamuhakikishia kwamba vypmbo vya uslama vinaendelea kmtafuta kila mahala .
“Nakuomba baba tafadhali fanya kila linalowezekana ili mume wangu aweze kupatikana.” Kasema Flaviana
“ Flaviana nimekwisha kuahidfi kwamba nitafanay akila linalowezekana ilikuhakkisha kwamba Elibariki anapatikana tena akiwa hai” akasema DrJoshua na kuwaomba wajiandae kwa ajiliya safari ya kueleka mazishini kijijini alikozaliwa mama yao


*******


Mlio wa simu ukamstua Mathew aliyekuwa amejilaza sofani.Akainuka na kuichukua simu yake.Alikuwa ni baba yake Noah ambaye alimfahamisha kwamba wamekaa kikao cha familia na wameafikiana kwamba Noah azikwe jijini Dar es salaam kwa hiyo familia nzima itakuja jijini Dar kwa mazishi.Baada ya kuongea na baba yake Noah Mathew akampigia simu Jason na kumfahamisha mambo aliyoongea na baba yake Noah.Hakumueleza chochote kuhusiana na Ebariki.Kisha ongea na Jason akaenda kumgongea Anitha ambaye macho yake yalikuwa yamevimba kwa kulia akamfahamisha kilichokuwa kinaendelea

“ Anitha there is one more thing” akasema Mathew
“ Kitu gani Mathew?

“ Nimeongea na Elibariki jana usiku”
“ Elibariki?! Anitha akastuka

“ Ndiyo nimeongea naye jana usiku “

“ Kwa nini hukuniambia usiku ule kama uliongea na Elibariki ili nisiwe na mawazo kama amekufa?

“ Usingeweza kunisikia kwa namna ulivyokuwa na uchungu ” akasema Mathew
“ Yuko wapi ? Is he ok? Is he safe? Akauliza Anitha

“ Hakuniambia kama yuko wapi lakini alinihakikishia kwamba yuko salama.”

“ Are you sure he’s safe? Akauliza Anitha

“ Sina hakika sana kama yuko salama lakini yeye mweyewe alinihakikishia kwamba yuko salama”

“ Nina wasi wasi asije kuwa ametekwa na watu na wakamlazimisha apige simu ili kuwaondoa watu wasi wasi” akasema Anitha

“ Hilo linawezekana kabisa .Unajua kwa wakati ule hata mimi kichwa changu hakikuwa sawa.Nilikuwa na mambo mengi sana” akasema Mathew
“ Namba alizokupigia unazo? Akauliza
“ Ndiyo ninazo “ akasema Mathew

“ Tunatakiwa tuzifuatilie namba hizo tuzifahamu ni za nani ili tujue ni wapi tunaweza kuanza kumtafutia jaji Elibariki.We need to find him Mathew.We need to bring him here.This is the only place we can be sure he’s safe” akasema Anitha. Mathew akamtajia namba alizotumia jaji Elibarki kumpigia simu usiku ,Anitha akainuka na kuchukua kompyuta yake ndogo akafungua program Fulani na kuziandika zile namba alizotumia Elibariki kumpigia Mathew.Baada ya kama sekunde ishirini hivi akamgeukia Mathew

“ What ! Umegundua nini? Akauliza Mathew

“ Peniela !..

“ Peniela? Akauliza Mathew

“ Ndiyo.Namba aliyoitumia Elibariki jana kukupigia ni namba ya simu ya Peniela”

“ Are you sure? Akauliza Mathew

“ Yes I’m sure.Ni namba ya Peniela.Are you sure he’s safe there?
“ I think he’s safe.” Akasema Mathew

“ Amefikaje kwa Peniela? Akauliza Anitha

“ Hata mimi sifahamu bado amefikaje lakini nina hakika ni sehemu ambayo amechagua kuwepo kwa sasa.Ukumbuke niliwaambia mapema kwamba Elibariki na Peniela wana mahusiano kwa hiyo atakuwa ameamua kwenda kujificha kule”
“ What about Team SC41? Akauliza Anitha

“ Anitha kwa sasa kilichopo mbele yetu ni kwanza kushughulika na msiba wa Noah na baada ya hapo tutarejea tena kazini na safari hii tutakuwa na kazi kubwa ya kuweza kuwatafuta wale wote waliomuua Noah ,vile vile tuna kazi kubwa ya kufahamu kuhusiana na zile karatasi,na mwisho tuna kazi kubwa ya …” Mathew akasita
“ Kazi kubwa ya nini? Akauliza Anitha

“ Ouh sorry forget about that.Inuka ujiandae leo tuna siku ndefu sana” akasema Mathew na kutoka.
“ Kazi yangu ya mwisho ni kupambana na Team SC41.Sikutaka Anitha afahamu hili kwa sababu hiki ni kisasi changu peke yangu na sitaki yeyote ahatarishe maisha yake kwa sababu ya kazi hii.Nitapambana peke yangu” akawaza Mathew na kuingia chumbani kwake.


********


Miale ya jua ilipenya ndani ya chumba cha Peniela.Sauti za mbwa wa jirani waliokuwa wakibweka ndizo zilizomstua jaji libariki akafumbua macho.
“ Kumekucha” akasema na macho yake yakatua katika saa kubwa ya ukutani ambayo ilionyesha ni saa mbili kasoro za asubuhi.Kitandani alikuwa mwenyewe Peniela hakuwepo

“ Pamoja na matatizo niliyonayo lakini nimelala usingizi mzuri sana japokuwa ulitawaliwa na ndoto mbaya za tukio la jana.Nilisikia raha ya ajabu kulala nikiwa nimekumbatiwa na Peniela.” Akawaza jaji Elibariki na kujitazama majeraha yake akajaribu kusimama hakuwa akisikia maumivu makali kama aliyokuwa akiyasikia usiku
“Ninaendelea vizuri sana.Sisikii maumivu kama yale ya jana usiku” akawaza jaji Elibariki akijaribu kuunyoosha mguu wake ambao ulikuwa na maumivu makali jana na mara mlango ukafunguliwa akaingia Peniela akiwa na sinia lililokuwa na mlo wa asubuhi

“ Elibariki umekwisha amka? Unajisikiaje? Akauliza penny
“ Ninajisikia vizuri sana na sisikii maumivu kama yale niliyokuwa nikiyasikia jana .Nashukuru sana usiku wangu ulikuwa mzuri mno zaidi ya nilivyotegemea japokuwa picha ya tukio lile la jana bado inaendelea kunijia kila mara” akasema Elibariki
“ Ok ni muda wa kupata kifungua kinywa.Leo utapata kifungua kinywa kitandani kwa sababu sitaki utoke kabisa chumbani.Unatakiwa upate mapumziko ya kutosha.Daktari atakuja baadae kuja kukuangalia unaendeleaje pamoja na kukuchoma sindano” akasema Peniela na jaji Elibariki hakusema kitu alibaki anatabasamu akapanda kitandani .
“ Peniela nashukuru sana.” Akasema jaji Elibariki
“ Unashukuru kwa lipi? Akauliza Peniela

“ Kwa kila kitu kwa namna ulivyonipokea na kwa namna unavyonijali.Nashukuru sana na ndiyo maana nilisema kwamba niko sehemu sahihi ninakotakiwa kuwepo” akasema jaji Elibariki .Peniela akatoa tabasamu pana sana na kusema

“ Wewe ni mtu wangu wa muhimu sana na lazima nikuhudumie.Bila wewe hivi sasa ningekuwa nimekwisha anza kuyazoea maisha ya jela.Mimi ndiye ninayepaswa kukushukuru sana kwa kila kitu ulichonifanyia” akasema Peniela na kumnywesha Elibariki uji halafu akauliza
“Nina hakika mkeo atakuwa katika wakati mgumu sana hivi sasa baada ya kupata taarifa za kilichotokea jana na hajui uko wapi.Kwa nini usimtaarifu kwamba uko sehemu salama ili asiwe na wasi wasi?
“ Usihofu kuhusu hilo Peniela na wala sihitaji ajue niko wapi.”

“ Kwa nini Elibariki? Yeye ni mke wako na anapaswa kufahamu kila kinachokutokea”
“ Sitaki tu afahamu chochote kuhusiana na mahala nilipo.Kubwa ni kwa sababu za kiusalama.Unajua sifahamu ni nani aliyefanya shambulio lile kwa hiyo nahitaji kukaa mafichoni kwa muda .Katika jambo hili ninakuamini wewe tu” akasema jaji Elibariki na mara simu ya Peniela ikaita.Akainuka na kwenda kuipokea

“ Hallow Osmund habari yako? Akasema Penny
“ Habari yangu nzuri.Peniela niliongea na John nikamtaarifu kuhusiana na ombi lako la kutaka kumuona akakubali na akasema kwamba uonane naye jioni ya leo lakini kwa jioni ya leo sina hakika kama itawezekana kwa sababu hivi sasa naelekea uwanja wa ndege kumpokea Dr Burke anatoka Marekani kuja kuangalia afya ya John kwa hiyo basi nitamtuma kijana aje akuchukue asubuhi hii ukaonane na John ili jioni ya leo awe na daktari akifanyiwa uchunguzi.Uko tayari kwenda kuonana naye asubuhi hii? Akauliza Osmund.Peniela akafikiri kidogo na kusema
“ Ndiyo niko tayari Osmund.Nitakwenda kuonana naye” akajibu Penny

“ Ok vizuri basi kuna kijana nimemuelekeza atakuja kukuchukua hapo nyumbani na atakupeleka kwa John “

“ Ahsante sana Osmund kwa msaada wako huo” akasema Peniela
“Peniela kabla sijakata simu nataka kesho tukutane kwa ajili ya kuongelea kuhusu operesheni 26B “

“ Nitaangalia kama nikipata nafasi nitakueleza Osmund” akasema Peniela na kukata simu akamgeukia jaji Elibariki

“ Are you going somewhere? Akauliza jaji Elibariki

“ Utanisamehe Elibariki kuna mtu ninahitaji kuonana naye asubuhi ya leo lakini sintakawia sana.Sipendi kuondoka na kukuacha peke yako lakini ni mtu wa muhimu sana kuonana naye leo hii” akasema peniela

“ Usijali Peniela.Hata hivyo ninajisikia vizuri na hupaswi kuacha shughuli zako nyingine na kunihudumia mimi” akasema jaji Elibariki
“ Usiseme hivyo Elibarki.Wewe ni mtu muhimu sana kwangu na niko tayari kuahirisha kila kitu isipokuwa mtu huyu ni muhimu sana kuonana naye “ akasema Penny

“ Ni mchumba wako? Akauliza Elibariki.Penny akatabasamu na kusema

“ Sina mchumba ..”
“ Usinidanganye Penny.Usione aibu kuniambia kama una mchumba kwa sababu hata mimi ni mume wa mtu na kisheria sitakiwi kuwepo hapa lakini niko hapa kwa sababu mbili kubwa .kwanza kwa usalama na pili ni kwa furaha ya moyo wangu . I feel so happy around you kwa hiyo basi kama una mchumba ni vizuri ukaniambia ili yasije yakatokea kama yaliyotokea siku ile” akasema jaji Elibariki

“ Elibariki naomba naomba unisamehe sana kwa kilichotokea siku ile lakini nitakaueleza kwa undani baade kuhusiana na suala lile “ akasema Peniela

“ Foregt about what happened Penny.Huna haja ya kutoa maelezo yoyote yale.Hata kama ulikuwa na mahusiano yoyote na Jason mimi hayanihusu kwa sababu mwenye uamuzi na maisha yako na nani uwe naye maishani ni wewe mwenyewe lakini ni vizuri kuwa wazi kama uko katika mahusiano na mtu Fulani ili niweze kufahamu na hasa katika kipindi hiki ambacho niko mafichoni” akasema jaji Elibariki.Peniela akasogelea akambusu na kusema

“ Elibariki naomba uniamini sina mahusiano na mtu yeyote Yule.Jason sina mahusiano naye alikuwa akinitaka siku nyingi lakini sikuwa tayari kumkubalia.Unajua nimepitia kipindi kigumu sana baada ya Edson kuuawa kwa hiyo moyo wangu ulikuwa mzito kufunguka kwa mtu mwingine yeyote lakini nashangaa kwa namna ulivyofunguka kwako kiurahisi.Elibariki you are safe here na utakaa hapa kwa muda wowote utakaotaka hata maisha yako yote kama utahitaji” akasema Peniela na wote wakacheka

“ Ninatamani sana kama ningepata nafasi ya kukaa hapa kwa maisha yangu yote lakini tayari niko katika kiapo cha ndoa kwa hiyo siwezi kuishi hapa maisha yangu yote japokuwa ninatamani sana kama ingekuwa hivyo” akasema jaji Elibariki.Penny akanyoosha mkono wake na kuigusa midomo ya jaji Elibariki halafu akasema

“ Marriage is in hearts and not papers.” Akasema Peniela na kumuacha jaji Elibariki na mawazo mengi


*******


Saa nne za asubuhi tayari Peniela alikwisha jiandaa kwa ajili ya kwenda kuonana na John mwaulaya.Dr Jonesia tayari alikwisha fika na kumuona Elibariki na kuridhika kwamba alikuwa anaendelea vizuri akamchoma sindano na kuondoka.
Gari iliyotumwa kuja kumchukua Peniela na kumpeleka kwa John Mwaulaya iliwasili na akamuaga jaji Elibarki.
“ Elibariki nasikitika kukuacha mwenyewe kwa muda lakini sintachukua muda mrefu sana nitarejea baada ya muda mfupi.Usihofu chochote uko salama.Ili kuongeza usalama zaidi nitafunga mitambo ya usalama na kuweka kamera za ulinzi kila kona ili kuweza kuimarisha ulinzi “ akasema Peniela
“ Nashukuru sana Peniela.Usihofu chochote kuhusu mimi niko salama sana.Hakuna yeyote anayweza kufikiri kwamba ninaweza kuwa hapa” akasema Jaji Elibariki na Peniela akambusu akatoka.
“Sielewi ni kwa nini sehemu ya kwanza kufikiria kujificha nilichagua kwa Peniela ? Ningeweza kwenda kwa Mathew ambako ni salama zaidi lakini sielewi ni kwa nini niliacha sehemu hizo zote na kuchagua kuja kwa Peniela.Nilikuwa sahihi kabisa kuchagua kuja hapa kwa sababu pamoja na matatizo niliyonayo lakini ninapata furaha ya ajabu nikiwa na Peniela na kuna wakati ninasahau kabisa kwamba nina matatizo.Moyo wangu haujawahi kujisikia furaha ya namna hii nikiwa na Flaviana.Ninahisi Flaviana hakuwa mtu sahihi kwangu na ndiyo maana ndoa yetu haina furaha hata kidogo.Kila siku mikwaruzano haiishi.Penny ananijali sana na ananifanya nijsikie furaha ya ajabu” akawaza Elibariki akainuka na kwenda dirishani akachungulia nje
“ Ama kweli maisha ni kitu cha ajabu sana.Leo hii nimekuwa mtu wa kujificha ndani na sitakiwi kuonekana nje.Ni akina nani hawa wanaoitafuta roho yangu? Nimewafanya kitu gani hadi watake kunitoa roho yangu? Lakini bado nina uhakika mkubwa sana kwamba kilichotaka kunipotezea uhai ni taarifa ile ya kifo cha Dr Flora.Ninaufahamu ukweli kwa hiyo wanahofu kwamba siri yao haiko salama.Ni nani walimuua Dr Flora na kwa nini? Hiki ni kitendawili ambacho lazima kiteguliwe na ndipo tutakapoweza kupata majibu ni nani anayetaka kuniua,kwani jambio hili limetokea baada tu ya kuufahamu ukweli ” akawaza jaji Elibariki na kurejea kitandani akakaa

“ Yule mwanamke aliyeniokoa ni nani? Sijawahi kumuona hata mara moja na hakutaka hata kujitambulisha kwangu yeye ni nani na kwa nini aliniokoa.Ninahisi ndiye Yule aliyenipigia simu na kunionya kwamba nisipande gari langu.Laiti kama ningemsikiliza ningeweza hata kuokoa maishaya Noah .Endapo nikifanikiwa kumpata mwanamke Yule yeye ndiye anayefahamu kila kitu kuhusiana na mpango wa kuniua na nina hakika lazima atakuwa akiwafahamu watu waliopanga njama ile. Kazi hii nitakabidhi Mathew yeye ndiye mwenye uwezo wa kulichunguza jambo hili.” Akawaza Elibariki halafu akajilaza kitandani
Peniela aliwasili katika makazi ya John.Lilikuwa ni jumba kubwa sana na la kupendeza.Hii ilikuwa ni mara ya pili kwa Penny kufika mahala hapa.Geti likafunguka wakaingia ndani na gari likaenda kusimama mbele ya jumba kubwa lenye rangi nyeupe.Dereva akashuka haraka haraka na kumfungulia Peniela mlango na kumuongoza kuelekea ndani

“ Nilipokuja siku ya kwanza ilikuwa usiku na sikuushuhudia uzuri wa jumba hili.Dah ni nyumba nzuri sana.” Akawaza Penny huku wakiingia ndani na kupanda ngazi kuelekea ghorofani kilipo chumba cha John Mwaulaya.Yule kijana akagonga mlango wa chumba cha John halafu ukafunguliwa na mtu mwingine aliyekuwa amevaa koti jeupe la kitabibu.Huyu ni kijana mwenye taaluma ya ukadktari naye akiwa ndani ya Team SC41.Alipomuona Peniela akamsalimu kwa heshima kisha akamruhusu aingie ndani na kumuogoza moja kwa moja hadi chumbani kwa John.Uso wa John siku hii ulionekana kuwa na nuru tofauti na siku zilizotangulia

“ Ouh my queen is here” akasema John kwa sauti ndogo na kumfanya Peniela atabasamu

“ Come here.Hug me my queen” akasema John Mwaulaya.Peniela akamsogelea na kumkumbatia pale kitandani
“ Nilikuwa nikihitaji siku nyingi sana kuipata nafasi hii ya kukuona siku moja na kukukumbatia kwani umenifanyia mambo mengi mazuri” akawaza Peniela na kisha akainuka na kuchukua kitambaa.Macho yake yalikuwa yamejaa machozi

“ Unalia nini Peniela? Akauliza John ambaye naye macho yake yalionekana kuwa na machozi

“ Ni miaka mingi nimekuwa nikikuomba nionane nawe nikufahamu lakini umeniruhusu nikuone katika kipindi hiki unachoumwa.Umenihudumia toka nikiwa mtoto mdogo hadi leo hii .Japokuwa sikuwahi kukuona lakini wewe ni zaidi ya baba yangu.” Akasema Penny

“ Peniela usilie tafadhali.Huu ni wakati wa kufurahi na si kutoa machozi” akasema John

“ Ninashindwa kujizuia kutoa machozi kupata nafasi ya kukuona wakati ukiwa katika hali hii.Ninaumia sana kukuona hivi” akasema Penny na mara mlango wa chumba cha John ukafunguliwa akaingia Josh

“ Josh ! naomba unipishe kwanza nina maongezi muhimu na binti yangu Peniela” akasema

“ John ni jambo la muhimu” akasema Josh.John akamfanyia ishara Peniela atoke nje kidogo ili aongee na Josh

“ Mzee ile kazi yako nimeimaliza” akasema Josh

“ Dr Burke is dead? Akauliza John
“ Ndiyo tayari amekwisha fariki.Lakini ilinilazimu kumuua vile vile na Osmund”
“ Good Job.How it happened? Akauliza John

“ Asubuhi ya leo nilimfuatilia Osmund hadi uwanja wa ndege bila ya yeye kufahamu.Alimpokea Dr Burke na kumpeleka katika hoteli aliyompangishia na baada tu ya kuingia katika hoteli hiyo niliwatokea ghafla na bila kupoteza hata sekunde moja niliwamiminia risasi kupitia bastora yenye kiwambo cha sauti kwa hiyo hakuna mtu yeyote aliyeweza kusikia kitu chochote kilichotokea.Dr Burke na Osmund wote wamekufa.Kwa hiyo mzee uko salama.You are safe now” akasema Josh
“ Josh nakushukuru sana kijana wangu.Umeyaokoa maisha yangu.Nina deni kubwa kwako” akasema John Mwaulaya

“ sijali mzee.Siku zote nitakuwa mtiifu kwako “ akasema Josh na kutoka.Peniela akaingia na kumkuta John akiwa na uso wenye furaha sana

“ Nina furaha sana Peniela kwanza kwa kutembelewa na wewe na vile vile kwa kuletewa habari njema na Josh” akasema John
“ Hata mmi ninafuraha sana ya kukutana nawe japokuwa ni kwa muda mfupi kwani Osmund aliniambia kwamba leo kuna daktari anakuja kukufanyia uchunguzi wa afya yako kwa hiyo sitakiwi kuchukua muda mrefu sana.Ninatamani sana kupata muda mrefu wa kukaa nawe ninatamani kukuhudumia hasa katika kipindi hiki unachoumwa na nina mambo mengi ambayo ninahitaji kuongea nawe” akasema Penny

“ Penny usijali kuhusu alichokwambia Osmund.Hakutakuwa na huo uchunguzi wa daktari kama alivyodai.Tafadhali naomba ushinde nami leo hii.Hata mimi nina hamu sana ya kukaa na wewe kuna mambo mengi ambayo nahitaji kukueleza” akasema John

“ Hakutakuwa na uchunguzi wa daktari? Aliniambia kwamba anaelekea uwanja wa ndege kwenda kumpokea Dr Burke.” Akauliza Penny
“ Ugonjwa wangu si wa kutibiwa na Dr Burke.Nahitaji daktari mtaalamu sana wa mishipa ya fahamu.”

“ Kwani unasumbuliwa na nini baba ? akauliza
“ Nina tatizo katika mishipa ya fahamu ya kichwa na ndiyo maana kuna baadhi ya viungo Fulani vya mwili havifanyi kazi sawasawa,”

“ Umepata matibabu gani mpaka sasa hivi? Akauliza Penny

“ Bado sijapata matibabu ya maana mpaka sasa.” Akajibu John

“ Wewe ni kiongozi wa Team SC41 ambayo inafanya kazi ya kulinda maslahi ya marekani kwa nini basi wasikutibu? Marekani kuna hospitali kubwa na nzuri na zenye wataalamu wakubwa sana wanaoweza kuutibu ugonjwa huu.Kwa nini wanakuacha uteseke? Hivi ndivyo team SC41 ilivyo kwamba ukiumwa wanakuacha bila huduma? Akauliza Penny
“Si hivyo Peniela.Jambo hili ni gumu tofauti na unavyofikiri.” Akasema John na kumpa namba Peniela afungue kasiki lililokuwa ukutani na achukue albamu la picha amletee.Peniela akachukua albamu lile kubwa la picha akamletea.Ukurasa wa tatu kulikuwa na picha ya kijana mmoja mtanashati aliyevaa suti nzuri yenye kupendeza akiwa amekaa juu ya jiwe ukingoni mwa bahari

“ Unaiona picha hii? Akauliza John

“ Ndiyo ninaiona” akajibu Penny

“ Huyu kijana unayemuona hapa katika hii picha ni mimi” akasema John.Penny akapatwa na mshangao mkubwa.Kijana Yule aliyeko katika picha ile na John Mwaulaya ni watu wawili tofauti kabisa.

“ This is you? Akauliza Paniela
“ Ndiyo “
“ Mbona hamfanani kabisa “ akauliza Penny

“ Hapa ilikuwa ni kabla ya kujiunga na Team SC41.Wakati huu nilikuwa katika chuo cha kijeshi nchini Marekani nikijifunza masuala ya urubani wa ndege vita.”

“ Wewe ni mwanajeshi? Akauliza Penny
“ Yah nilikuwa mwanajeshi.Wakati nilipopiga picha hii sikuwa na wazo kama siku moja nitakuwa kiongozi wa Team SC41.” Akasema John
“Nilikuwa kijana mtanashati sana nyie vijana mnasema Handsome boy “ akasema John na kumfanya Penny atabasamu

“ IIinilazimu kuibadili sura yangu mara mbili na ndiyo maana unaniona nikiwa katika sura hii ya tofauti kabisa na ile iliyoko katika hiyo picha.” Akasema John
“ Kitu gani kilisabababisha ukabadilisha sura yako? Akauliza Penny

“ Penny ni mambo mengi sana makubwa yametokea ndani ya Team SC41 na ndiyo maana nkalazimika kuibadili sura yangu mara mbili .Nilianza kusumbuliwa na ugonjwa huu baada ya kufanyiwa upasuaji wa pili wa kuibadili sura.”

“ Kitu gani kilipeleka ukabadili sura yako ? akauliza Peniela

“ Penny kuna mambo mengi sana ambayo huyafahamu na ninatamani sana kukueleza lakini ninashindwa kwa sababu Team SC41 si sehemu sahihi unayostahili kuwepo.”
Peniela akamtazama John na kusema

“ Bado hujanieleza ni kwa nini team Sc41 wameshindwa kukupatia matibabu?akauliza tena Penny
“ Its because I’m dead “
“ You are dead? Akauliza Penny kwa mshangao
“ Yes I’m dead” akasema
“ Ninashindwa kuelewa baba John umekufa vipi?
“ Ngoja niliweke hivi ili unielewe.Ni kwamba kwa miaka kadhaa sasa hivi ninajulikana kwamba nimekwisha fariki.Mimi ni mtu niliyekuwa nikitafutwa sana na serikali mbalimbali duniani kwa hiyo nililazimika kutumia njia hii ya kutengeneza kifo changu ili nisiendelee kutafutwa na ndiyo maana kuna ugumu mkubwa kwa mimi kutibiwa hapa nchini na nje ya nchi”akasema John
“ Kitu gani kilisababisha utafutwe? Akauliza Peniela
“ Nilifanya jambo kubwa sana ambalo sintaweza kukueleza” akasema John


JOHN MWAULAYA ALIFANYA JAMBO GANI KIASI CHA KUTAFUTWA NA SERIKALI MBALI MBALI DUNIANI? ENDELEA KUIFUATILIA SIMULIZI HII…
story inaniliaa muda san hii ila ntafika tu tamati
 
Back
Top Bottom