Pengo: Sikutarajia polisi kuua raia

Unajua sikutegemea Polisi wetu wawe vihiyo namna hii. Maelezo yao jana hayana mantiki hata chembe. Kama viongozi wa Chadema walikuwa tayari mikononi mwa Polisi pale kituoni waliweza kuwasiliana vipi na vijana mitaani na kuwachochea wavamie kituo cha polisi ili kuwaokoa vongozi wao? Vile vile ilikuwaje basi Polisi wakavunja vioo vya magari barabarani kama tulivyoona kwenye luninga? Je na magari nao yalikuwa yakielekea kituo cha polisi kuwaokoa kina Mbowe? Yale yale ya 2005 wakati Mahita alisema CUF wameingiza contena na majambia!! Complete hogwash!!
 
Wote mlio-comment kuanzia mwanzo mnaugonjwa wa akili ndio maana siku zote mnaingiza udini. Haya jana Mbeya napo polisi wameua naomba tusubiri viongozi wa dini, viongozi wa serikali na wa kisiasa watasemaje.
 
Kweli Zawadi. Huyu askofu anaongea utadhani hajawahi kuishi Tanzania.

Polisi wameshaua watu wengi katika mazingira ya kutatanisha lakini hawa viongozi wa dini wapo kimya tu. Leo anajidai kushtuka kinafiki.

Tunahitaji maaskofu kama DESMOND TUTU ambao watakemea uovu popote bila kujali nani anahusika na wakati gani umetokea.

Sema nyie ni viziwi na hamtaki kuchimba mambo mengi ambayo ameeongele Mh.Pengo ni yeye mara nyingi ambaye amekataza wananchi kuchukua sheria mkononi kwa kuwapiga mpaka kufa amekema mara nyingi tabia hii lakini kwa sababu mnaa lenu jambo endeleeni tuu tutaona udini utakapokomaa hapa nchini mutakachofanya nawaonea huruma
 
Mkuu alisemaje, hebu tujuze kidogo tafadhali..!
Alisema analipongeza jeshi la polisi kwa kazi waliyoifanya MWEMBECHAI kwa madai kuwa polisi walijihami kwa mawe na ata akanukuu frm Daud kuwa aliuwa kwa jiwe so ina maana vifo vya waislamu pale mwembechai ni Halali. Apo ndo huwa anakosea pengo,mauaji yeyote yanatakiwa kukemewa awe muislamu,mkristo hata mpagani. Hakuna dini inayoruhusu mauaji. Sasa anapokuwa anaelemea upande mmoja je si unafki huu?? Je alikemea pemba kama anavyokemea sasa? Au sababu mtawala wa nchi mwaka 2001 alikuwa mdini mwenzake? Ushauri wa bure kwa Pengo,kemea kila baya sio leo unanyamaza au kupongeza polisi kwa mauaji ya upande mwingine na kesho ikikugusa unakuwa mbogo. Ni hayo tu... Nawakilisha!
 
Yarushe aliyosema kama una kanda tuyasikie ili naye tumhukumu mi nilikuwa mdogo sikuhifadhi kumbukumbu napenda nisikie tamko lake lilivyokuwa.
Mnafiki mkubwa huyu, sitaki hata kumsikia wala kumuona. HIVI AMESAHAU ALISEMA NINI KATIKA REDIO TUMAINI WAKATI WA MAUAJI YA MWEMBE CHAI. Na yale ya PEMBA?

Hivi pale Polisi waliuwa WANYAMA? Huyu ndio tatizo la Tanzania. Hana hata aibu anazungumza kama vile matukio ya Mwembechai na PEMBA yalitokea miaka 70 iliyopita.

Mwenye kumbukumbu ndogo juu ya maneno yake wakati huo anieleze niweke sauti yake hapa JF. KANDA NINAZO LAKINI SITAKI KUPOTEZA WAKATI KWANI NYIE WOTE MLIMSIKIA NA KUMUUNGA MKONO.

Maendeleo ya Tanzania yanategemea KIFO CHA HUYU MNAFIKI.
 
Huko mbeya jana polisi waliwatungua raia wawili kwa risasi. Cha kujiuliza ni wapi hawa polisi wamepata ujasiri wa kuwapiga risasi raia wasio na silaha? Jibu linabaki kwamba polisi nchini wamepewa maelekezo na mkuu wa nchi kutumia nguvu kubwa sana dhidi ya raia baada ya yeye kuwa ameingia madarakani kwa kuchakachua. Mkuu hajiamini kabisa na anajihisi kufuatiliwa nyuma baada ya kukwapua. Inaonekana kuwatandika raia risasi ndio njia pekee ya kuwaacha salama katika dhuluma zao.
Nawashauri watawala wajitathmini kwa kuchunguza na kujiuliza hivi marais dikteta wa kiafrika walimaliza je maisha yao.
.
 
Nafikiri swala la ukristu na uislam halina nafasi katika mauaji ndio maana kuna muislam na mkristu wameua katika tukio hilo hivyo basi swala la imani lisiingizwe sana na kutoa maneno makali au matusi kwamba fulani mnafiki tungoje afe kwa maendeleo ya taifa hatutafika, ni maoni yangu binafsi'
 
hii mada kuandikwa Polisi kuua raia wa tanzania bara, mbona imekaa kama kimajungu?


lengo kutaka kutupambanisha baina ya wazanzibari na watanzania bara, tuamini kuwa maaskofu huwa na uchungu zaidi na wakristo wenzao kulikoni waislam na hasa wazanzibar

Kule upande wapili kuna dini pinzani hata wakifa hakuna neno!
 
Kule upande wapili kuna dini pinzani hata wakifa hakuna neno!

77413530.jpg
 
Unajua sikutegemea Polisi wetu wawe vihiyo namna hii. Maelezo yao jana hayana mantiki hata chembe. Kama viongozi wa Chadema walikuwa tayari mikononi mwa Polisi pale kituoni waliweza kuwasiliana vipi na vijana mitaani na kuwachochea wavamie kituo cha polisi ili kuwaokoa vongozi wao? Vile vile ilikuwaje basi Polisi wakavunja vioo vya magari barabarani kama tulivyoona kwenye luninga? Je na magari nao yalikuwa yakielekea kituo cha polisi kuwaokoa kina Mbowe? Yale yale ya 2005 wakati Mahita alisema CUF wameingiza contena na majambia!! Complete hogwash!!

Ndugu inaonyesha haukufatilia kwa makini yaliyotea Arusha, polisi wako sahihi ya kwamba Slaa na Ndesamburo ndio waliowachoichea wafuasi wao na kusababisha mauji Arusha na hili watu wengi pamoja na wanachadema wanajitahidi kulificha soma hapa:

Mbowe na wabunge hao ndio walikuwa wa kwanza kukamatwa jana mchana wakati wakiongoza maandamano hayo huku Dk Slaa akiwa amekamatwa jioni ya saa mbili kasorobo usiku pamoja na mbunge wa Moshi mjini, Philemon Ndesamburo.

Kabla ya Dk Slaa na Ndesamburo kukamatwa walihutubia maelfu ya wananchi waliokuwa wamefurika katika viwanja vya NMC eneo la Unga Limited lakini baadae walitangaza kuuvunja mkutano huo na kuamuru umati wote uelekee kwenye kituo kikuu cha polisi walikokuwa wameshikiliwa Mbowe na viongozi wengine ili wakafuatilie kwa pamoja hatima ya viongozi wao.

Source: Tanzania Daima, ukurasa wa 2, alhamisi tarehe 6 Januari. 2011
 
Wewe mtu wa ajabu kweli unatuuliza sisi tena wakati wewe ndiye unayetujuza, binafsi sijawahi sikia maneno kama hayo umeyatunga kama hujayatunga tuwekee guote zake hapa.

Quinine acha jazba, twende kwa hatua.


  1. Haya ni maneno ya POLYCARP PENGO katika mahojiano DTV "Hamza Kasongo Hour" Kipindi cha tarehe 12 April, 1998. Alipoulizwa kama polisi kufyatua risasi za moto kwa raia wasio na silaha, kuwa hafikirii kuwa polisi walitumia nguvu za ziada (excessive force). Pengo alijibu: Matumizi ya risasi za moto ilikuwa ni sahihi kabisa kwa sababu waislam nao walikuwa na silaha za mawe. Na mawe yanaweza kuua. Alieleza kisa cha DAVID na GOLIATH kuhalalisha nguvu iliyotumika na serikali.
  2. Haya ndio majibu yake, kama nyie mnaona sahihi toeni hukumu wenyewe na ulinganishe na haya ya yeye kushangazwa.

 
Mnafiki mkubwa huyu, sitaki hata kumsikia wala kumuona. HIVI AMESAHAU ALISEMA NINI KATIKA REDIO TUMAINI WAKATI WA MAUAJI YA MWEMBE CHAI. Na yale ya PEMBA?

Hivi pale Polisi waliuwa WANYAMA? Huyu ndio tatizo la Tanzania. Hana hata aibu anazungumza kama vile matukio ya Mwembechai na PEMBA yalitokea miaka 70 iliyopita.

Mwenye kumbukumbu ndogo juu ya maneno yake wakati huo anieleze niweke sauti yake hapa JF. KANDA NINAZO LAKINI SITAKI KUPOTEZA WAKATI KWANI NYIE WOTE MLIMSIKIA NA KUMUUNGA MKONO.

Maendeleo ya Tanzania yanategemea KIFO CHA HUYU MNAFIKI.


Hapo kwenye RED sijaelewa kwani pengo ndio ameshikilia uchumi wa tanzania??? It seems una chuki binafsi na pengo maana ulivyo mshambulia!!!!!!!!!1 Anyway dua la kuku.............................
 
Pengo: Sikutarajia polisi kuua raia


"Sikutegemea hata mara moja kwamba walinda usalama wanaweza kutumia silaha wakaua watu. Sikutegemea kwamba wanaweza kuua hata mtu mmoja. Wale wanapaswa kutetea uhai wa Watanzania. Wachukue silaha dhidi ya Watanzania, waue watu haidhuru wamekosaje, ni jambo ambalo sikutegemea kamwe kwamba lingeweza kutokea," alisema kardinali Pengo.

Na Peter Mwenda
ASKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo amesema
kitendo cha polisi waliopewa dhamana ya kulinda wananchi kuua watu wasio na hatia kinaashiria maafa makubwa kutokea nchini.

Akihutubia waumini wa Kanisa Katoliki wa Jimbo la Dar es Salaam katika misa ya kuwaombea wafiadini wa Pugu iliyofanyika Kituo cha Hija, Pugu juzi, Kardinali Pengo alisema hakutarajia jambo hilo linaweza kutokea Tanzania bara, ambako kuna historia ya kuitwa kisiwa cha amani duniani.

"Sikutegemea hata mara moja kwamba walinda usalama wanaweza kutumia silaha wakaua watu. Sikutegemea kwamba wanaweza kuua hata mtu mmoja. Wale wanapaswa kutetea uhai wa Watanzania. Wachukue silaha dhidi ya Watanzania, waue watu haidhuru wamekosaje, ni jambo ambalo sikutegemea kamwe kwamba lingeweza kutokea," alisema kardinali Pengo.

Kutokana na tukio hilo kiongozi huyo aliwataka Watanzania bila kujali madhehebu yao wasimpuuze Mungu, bali warejee kumuomba ili arejeshe amani Tanzania iliyoachwa na waasisi wa nchi hii, Mwalumu Julius Nyerere na Abeid Amani Karume.

Kardinali Pengo alisema tukio la polisi kuua raia lililotokea Arusha kwa wananchi wasio na hatia kupigwa risasi liimetia doa Tanzania, limeipaka matope Tanzania.

Watanzania lazima tufaham ya kuwa polisi sio kwamba wameanza kuua kule A town,kama kuna mwana JF toka pemba atawakumbusha watanzania,
polisi walishamwaga damu ya watu wasio na hatia pemba,nani hajui yaliyotokea mwembechai?,
Kila jambo linapotokea lina maslah yake iwe la kisiasa,kiuchumi na kijamii lakini madhara yake ni makubwa!,
Utu ndio msingi
 
Chagonja katangaza rasimi kwamba wataendelea kuua na wala hajutii kutoa uhai wa watanzania ili kulinda serikali iliyoko madarakani hata kama imekosea hata kama imepora haki amesema polisi iko teyari kuendelea kuua kwa miaka mitano mpka 2015 tutakapopata chama kingine ambacho hakitakuwa teyari kuua. Hii ni hatari maneno haya kutoka kwa kiongozi wa pili wa jeshi la polisi.
 
mdini ni Mdini tu.dini ya warabu mnaifagilia tafuta historia huone walivyotesa babu zako laiti ungejua leo hii usingekuwa na hasira ya uislamu au ukristo.kuwa na amani tu uelewe Mungu yupo Umtegemee lakini usione mwenzio kwa vile si wa dini yako ni adui.acha acha acha kabisa utaishi kwa furaha hapa duniani kabla hujafa.

kuku ni kuku tu jogoo jina!,
huyo mwarabu alikamata babu zetu na kwenda kuwauza kwa wafaransa na maingereza kutumika kwenye mashamba ya sukari!,
hizi dini zote zilikuja kutushika akili ili tutawalike,
utake usitake huo ndio ukweli,nawe ukaamua kumwita babu yako anaabudu dini za kishenzi kwenye miembe,ambako sasa hakuna tofauti na sanam!
 
Alisema analipongeza jeshi la polisi kwa kazi waliyoifanya MWEMBECHAI kwa madai kuwa polisi walijihami kwa mawe na ata akanukuu frm Daud kuwa aliuwa kwa jiwe so ina maana vifo vya waislamu pale mwembechai ni Halali. Apo ndo huwa anakosea pengo,mauaji yeyote yanatakiwa kukemewa awe muislamu,mkristo hata mpagani. Hakuna dini inayoruhusu mauaji. Sasa anapokuwa anaelemea upande mmoja je si unafki huu?? Je alikemea pemba kama anavyokemea sasa? Au sababu mtawala wa nchi mwaka 2001 alikuwa mdini mwenzake? Ushauri wa bure kwa Pengo,kemea kila baya sio leo unanyamaza au kupongeza polisi kwa mauaji ya upande mwingine na kesho ikikugusa unakuwa mbogo. Ni hayo tu... Nawakilisha!

UNA UFINYU WA AKILI SANA. Sikutegemea kwa upeo wako mdogo hivyo ungeweza kuwa member wa blog ya great thinkers kama hii. Kama thinking capacity iogekuwa kipimo cha mtu cha kukua (mwili) we ungeanza kudumaa mara tu baada ya kuzaliwa.
 
Mnafiki mkubwa huyu, sitaki hata kumsikia wala kumuona. HIVI AMESAHAU ALISEMA NINI KATIKA REDIO TUMAINI WAKATI WA MAUAJI YA MWEMBE CHAI. Na yale ya PEMBA?

Hivi pale Polisi waliuwa WANYAMA? Huyu ndio tatizo la Tanzania. Hana hata aibu anazungumza kama vile matukio ya Mwembechai na PEMBA yalitokea miaka 70 iliyopita.

Mwenye kumbukumbu ndogo juu ya maneno yake wakati huo anieleze niweke sauti yake hapa JF. KANDA NINAZO LAKINI SITAKI KUPOTEZA WAKATI KWANI NYIE WOTE MLIMSIKIA NA KUMUUNGA MKONO.

Maendeleo ya Tanzania yanategemea KIFO CHA HUYU MNAFIKI.

Tatizo hawa maaskofu wamezoea kupigiwa goti na kila kiongozi wa nchi yetu, na ikitokea tofauti na matakwa yao ndio utawasikia wanatoa kilio cha mbwa. I weje leo wang'ake kwa kuuwawa watu wawili Arusha na kutoa matamko makali na kutolivalia njuga lile la mauaji ya watu 23 lililotokea tarehe 28/1/2001 kule visiwani?
Angalizo:
waislamu hawaungi mkono mauaji ya aina yoyote ya raia wasio na hatia lakini unakemea tabia ya maaskofu kuchagua ni wakina nani wakifa ndio polisi ilaumiwe.
Cha ajabu juzi kuna mauaji ya watu wawili yaliyofanywa na polisi Mbeya lakini sijawasikia wakilisemea hili, hapo ndio tunapo hoji kulikoni?
Msije mkatusababishi kama yale yaliyo tokea Rwanda na Burundi, maana walio hukumiwa wengi wao ni maaskofu.
 
SIUNGANI NA NDUGU PENGO KATIKA HILI.....polisi wapigwe mawe wakae kimya tu....vituo vivamiwe wakae kimya tu.....watoe amri ya kutawanyika na ikaidiwe wakae kimya tu......NINI MAANA YA POLISI SASA.......NA HUWEZI KUAMRISHA MTU ASITUMIE SILAHA ALIYONAYO ATI KWA KUWA WEWE UNA SILAHA DHAIFU ZAIDI YAKE.......BASI NA MAJAMBAZI YAKITUVAMIA NA MAPANGA NA MARUNGU TUSITUMIE BUNDUKI KWANI TUNAKIUKA SHERIA ZA CHADEMA........
 
Back
Top Bottom