Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
Na Peter Mwenda
ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Polycarp Kardinali Pengo amewataka wakristo kufuata dhamira ya Mungu ya kuchagua viongozi ambao hawawarubuni kwa khanga, bia na fulana.
Akihutubia waumini katika ibada ya kuombea amani na utulivu katika kipindi cha uchaguzi mkuu iliyofanyika katika Kijiji cha Hija, Parokia ya Pugu juzi, Kardinali Pengo alisema wakristo wakatoliki wajue kwamba kura zao zina thamani kubwa kwa jamii na mbele ya Mungu.
"Kama mngejua thamani ya kura yako kwa jamii na mbele ya Mungu huwezi kupokea zawadi za khanga na bia kwa ajili ya kumpigia mtu asiyefaa kupewa kazi ya kuongoza," alisema Kadinali Pengo.
Alisema Mwenyezi Mungu anafanya kazi kupitia dhamira ya kila mwanadamu, hategemei ushabiki wa vyama wala kumchagua kiongozi asiye na utashi ambaye anatoa rushwa ili apate uongozi.
"Si kuambiwa na mwenyekiti wa jumuiya, kasekista (Mwalimu wa dini), kadinali au padre kuwa mchague fulani, hakuna atakayesimama kwa dhamira yako, anayefaa ni yule anayejiepusha na matendo ya rushwa," alisema Kadinali.
Alisema kumetokea minong'ono hivi karibuni kuwa Kanisa Katoliki limeteua viongozi wa kupigiwa kura katika ngazi ya juu. "Huo si msimamo wa Kanisa Katoloki."
Alisema akiwa kiongozi wa kanisa hilo anaweka bayana msimamo wa Wakatoliki kuwa hawafungamani na itikadi za kichama, kisiasa au kabila.
"Kanisa Katoliki lingefanya hivyo likawa na watu wake au kusema fulani ni chaguo la Mungu ni balaa linaloweza kuleta machafuko na uvunjifu wa amani," alisema Kardinali Pengo.
Alisema uchaguzi wa kibinadamu ni chanzo cha mfarakano lakini wakristo ambao wana utashi wa Mungu wasimchague kiongozi wanayemjua kuwa ni mwizi na mla rushwa ambaye anatumia kushawishi ili achaguliwe.
"Tuchukue na kuamini hilo kuwa ni ukweli wa Kanisa Katoliki halina mtu kuwa huyu awe rais, mbunge au diwani. Haliwezi likasimama likasema fulani awe hivi," alisema Kadinali Pengo.
Alisema Wakristo nchini kote wapige kura kwa dhamira ya kumuogopa Mungu kuwa siku ya mwisho watasimama mbele yake na kusema madhambi yao.
Katika ibada hiyo ambayo Kadinali Pengo alisaidiwa na mapadri 15 kutoka parokia mbalimbali za Jimbo Kuu la Dar es Salaam alisema kutafuta madaraka kwa kutumia nguvu au ushawishi ili kuhalalisha madaraka si njia ya kuleta amani bali kuashiria machafuko ambayo kanisa inapinga vikali.
Mkurugenzi wa Haki na Amani wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Padri Alister Makubi aliwaasa waumini wa kanisa hilo nchini wasichoke kusali kuombea amani wakati wote wa uchaguzi.
ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Polycarp Kardinali Pengo amewataka wakristo kufuata dhamira ya Mungu ya kuchagua viongozi ambao hawawarubuni kwa khanga, bia na fulana.
Akihutubia waumini katika ibada ya kuombea amani na utulivu katika kipindi cha uchaguzi mkuu iliyofanyika katika Kijiji cha Hija, Parokia ya Pugu juzi, Kardinali Pengo alisema wakristo wakatoliki wajue kwamba kura zao zina thamani kubwa kwa jamii na mbele ya Mungu.
"Kama mngejua thamani ya kura yako kwa jamii na mbele ya Mungu huwezi kupokea zawadi za khanga na bia kwa ajili ya kumpigia mtu asiyefaa kupewa kazi ya kuongoza," alisema Kadinali Pengo.
Alisema Mwenyezi Mungu anafanya kazi kupitia dhamira ya kila mwanadamu, hategemei ushabiki wa vyama wala kumchagua kiongozi asiye na utashi ambaye anatoa rushwa ili apate uongozi.
"Si kuambiwa na mwenyekiti wa jumuiya, kasekista (Mwalimu wa dini), kadinali au padre kuwa mchague fulani, hakuna atakayesimama kwa dhamira yako, anayefaa ni yule anayejiepusha na matendo ya rushwa," alisema Kadinali.
Alisema kumetokea minong'ono hivi karibuni kuwa Kanisa Katoliki limeteua viongozi wa kupigiwa kura katika ngazi ya juu. "Huo si msimamo wa Kanisa Katoloki."
Alisema akiwa kiongozi wa kanisa hilo anaweka bayana msimamo wa Wakatoliki kuwa hawafungamani na itikadi za kichama, kisiasa au kabila.
"Kanisa Katoliki lingefanya hivyo likawa na watu wake au kusema fulani ni chaguo la Mungu ni balaa linaloweza kuleta machafuko na uvunjifu wa amani," alisema Kardinali Pengo.
Alisema uchaguzi wa kibinadamu ni chanzo cha mfarakano lakini wakristo ambao wana utashi wa Mungu wasimchague kiongozi wanayemjua kuwa ni mwizi na mla rushwa ambaye anatumia kushawishi ili achaguliwe.
"Tuchukue na kuamini hilo kuwa ni ukweli wa Kanisa Katoliki halina mtu kuwa huyu awe rais, mbunge au diwani. Haliwezi likasimama likasema fulani awe hivi," alisema Kadinali Pengo.
Alisema Wakristo nchini kote wapige kura kwa dhamira ya kumuogopa Mungu kuwa siku ya mwisho watasimama mbele yake na kusema madhambi yao.
Katika ibada hiyo ambayo Kadinali Pengo alisaidiwa na mapadri 15 kutoka parokia mbalimbali za Jimbo Kuu la Dar es Salaam alisema kutafuta madaraka kwa kutumia nguvu au ushawishi ili kuhalalisha madaraka si njia ya kuleta amani bali kuashiria machafuko ambayo kanisa inapinga vikali.
Mkurugenzi wa Haki na Amani wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Padri Alister Makubi aliwaasa waumini wa kanisa hilo nchini wasichoke kusali kuombea amani wakati wote wa uchaguzi.