Wadau salaam. Nimekuwa nikisikiliza na kutazama nyimbo za maombolezo kufuatia kifo cha JPM, hakika sijasikia ToT wakitamba kama ilivyokuwa enzi za marehemu John Komba (hata Kama wametunga).
Mtakumbuka alipofariki dunia Baba wa Taifa, hayati Julius K. Nyerere, Komba ndiye alikuwa 'habari ya mjini'. Nyimbo zake za simanzi zilileta taifa katika maombolezo sahihi. Nyimbo za Komba zilianza kusikika saa 12 tu tangu kutangazwa kifo cha Baba wa Taifa.
Safari hii sivyo. Naona Bongo Fleva ndiyo wanatamba. Kidogo na za dini ambazo hata hivyo, siyo lengwa kwa maombolezo husika. Je, ToT hajatokea wa kuziba pengo la Komba au ni mabadiliko ya wakati?
Mtakumbuka alipofariki dunia Baba wa Taifa, hayati Julius K. Nyerere, Komba ndiye alikuwa 'habari ya mjini'. Nyimbo zake za simanzi zilileta taifa katika maombolezo sahihi. Nyimbo za Komba zilianza kusikika saa 12 tu tangu kutangazwa kifo cha Baba wa Taifa.
Safari hii sivyo. Naona Bongo Fleva ndiyo wanatamba. Kidogo na za dini ambazo hata hivyo, siyo lengwa kwa maombolezo husika. Je, ToT hajatokea wa kuziba pengo la Komba au ni mabadiliko ya wakati?