barafu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 6,726
- 32,818
Kauli za wazee wa kanisa,hasa kanisa katoliki kwa siku za karibuni zimetushitua wengi.Kauli za maaskofu mpaka mapadre walio chini yao.Hawa wote kama viongozi wa kiroho wanaoongoza wananchi wenye itikadi na mlengo tofauti,Kauli zao zinatustua,hasa sisi ambao ni waumini wao.
Hata katika mazingira ambayo haki inaokana kutokutendeka,hawa wazee wanapongeza tu.Tunapolalamika hali ya maisha imekuwa ngumu,wao hawapo na sisi.Sisi waumini tumebaki peke yetu.
Weekend hii nilihudhuria "Makusanyo ya Mwaka wa Mavuno Jimbo la Dar es Salaam".Makusanyo ya dekania zote,toka kwenye parokia kamili na parokia tarajiwa.Tumevuna kwelikweli...na pesa hizi zinakwenda kulitegemeza jimbo.Makusanyo haya hayana kodi,maana ni mali ya kanisa.Hili pia linaweza kuwa moja ya jambo linalofanya hawa watu wa kanisa wajisahau na kuona huku mtaani waumini wao maisha ni raha mustarehe
Pengine mavuno haya yanawasahaulisha hawa viongozi wetu,basi kupitia jukwaa hili nataka kuwaambia hawa mababa kuwa maisha ni magumu sana,milo mitatu ni huku kwa waumini wao ni kwa kubahatisha,wanapopata nafasi ya kukutana na mfalme au wasaidizi wa mfalme,basi wasimamie ukweli,wasimame na waumini wao.Wasione soni katika kukemea rushwa,uonevu,mauaji,ukiukwaji wa demokrasia na kudumazwa kwa siasa za ushindani.Hivi kweli muitikio wa leo katika uchaguzi wa serikali kanisa hili la Khalifa wa Mtume Petro linaona ni sawa tu!!?
Sisi waumini tunapokusanya mamilioni haya na wakati mwingine mpaka kuvuka kiwango,hawa mababa zetu wa kiroho waadhani tuna maisha mazuri sana,labda tuna pesa na tunaridhika na mfumo wa uchumi unavyokwenda kwa sasa.Wanajisahau na kuwa upande wanaopaswa kuukosoa kwa hekima,wanafungamana nao na kutusahau sisi tunaohitaji sauti zao na kauli zao katika mimbari zitusemee.
Angalisema Pengo peke yake tusingeshangaa sana,lakini sasa mpaka maparoko wameanza siasa kwenye mahubiri,wanaanza kampeni,wanaona kila jambo ni shwari na maisha ni sawa sababu waumini tunatoa mavuno yanayopita kiwango tulichojiwekea.
Mfano huu ni wa mavuno kwa Jimbo la Dar es Salam tu,tumevua mamilioni,labda ndioyanawsahaulisha hawa mababa nawanahisi tuna maisha mazuri tu.
MAVUNO JIMBO KUU LA DAR ES SALAAM.
DEKANI YA KIGAMBONI Tsh 263,226,750
1. KIGAMBONI 18,830,645
2. MBAGALA. 14,252,535
3. KIJICHI. 55,000,000
DEKANIA YA ST. JOSEPH Tsh 49397550/489,622,220
1. ST. JOSEPH. 216,250,210
2. UPANGA. 40,000,000/
3. MSIMBAZI. 61,300,00
DEKANIA YA GASPAR. Tsh 404,768,100/ 418,180,510
1. GASPAR. 53,164,300
2. TEGETA 12,673,700
3. BOKO. 31,000,500
4. SALASALA 20,126,550
5. T. MORE. 27,453,400
6. KUNGURU. 14, 968,000/
DEKANIA YA PETRO.
Tsh
532 670,575/ 489,823,712
1. PETRO. 153,51000
2. MIKOCHENI 32,000,000
3. MWEGE 70,272,500
4. SINZA. 48,260,000
5. MAGOMENI. 41,500,000
DEKANIA YA. UBUNGO. 278,816,650/ 300,301,000
1. UBUNGO 15,314,000
2. MANZESE. 43,000,000
3. MAKUBURI 27,338,000
4. C.KIKUU. 40,000,000
DEKANIA YA UKONGA 251,750,950 / 265,500 090
1. UKONGA 76,000,000
2. PUGU 35,275,000
3. KIWALANI 14,000,000
4. VITUKA 16,700 600
5. KITUNDA 36,523,770
DEKANIA YA SEGEREA. 270,176,700/ 254,827,050
1. SEGEREA. 43,631,700
2. TABATA. 102,213,850
3. KINYEREZI 16,800,000
4. KIPAWA. 30,452,300
5. KIMANGA. 15,000,000
DEKANIA YA KIBAHA. 145,532,050/ 161,976,300
1. KIBAHA 31,000,200
2. MLANDIZI 14,000,500
3. MKUZA. 14,000,000
4. KIBAMBA 23,390,500
5. KIBWEGERE. 28,000,000
DEKANIA YA KILIMAHEWA. 36,749, 100/ 37,309,850
1. KILIMAHEWA 5,573 700
2. MKURANGA 12,108 250
3. KIBITI 3,500,000
DEKANIA YA MBEZI LUIS. 257,613,300 /293,962,900
1. MB/LUIS 25,334,300
2. MAVURUNZA 68,100,250
3. TAGASTE. 27,000,000
4. TEGETA A 9,122,000
Makusanyo kama haya,ninadhani ndio yanawasahaulisha watu kama kina Pengo na Mapdre wengine,maana sasa wanafungamana na upande ambao bila shaka unawafanya waon udikteta ni bora kuliko utawala wa sheria.Kwenye kanisa ambalo ndani yake kuna watu weye fikra na itikadi mseto,viongozi wa kanisa mnapaswa kuchun sana ndimi zenu.
Juzi kati akiwa na RC Makonda,Muadhama P. Cardinal Pengo amewananga wanaoikosoa serikali ya awamu ya tano.Kwa tafsiri ya hotuba yake,ni kama Cardinal Pengo anasema kwake demokrasia si lolote kama tu watu wanaenda shule bure,wanajengewa barabara na hata kujengewa vituo vya afya.
Mwadhama ambaye kwa nafasi yake ni mmoja kati ya walio wachache wenye haki ya kikatiba pale Vatican kutuchagulia Papa ambaye ni khalifa wa mtume Petro na msimamizi wa kanisa katoliki lililo nyumba ya imani ya mabilioni ya watu duniani.
Pengo akavuka mipaka,akasema hata Hitler na Musolini walikuwa watu wema,maana udikteta wao ulileta maendeleo.Akasema kwa lugha ya kificho kuwa hata wale wayahudi dunia inayoambiwa waliuawawa na Hitler,si lolote ukilinganisha na maendeleo aliyoleta.Yaani kwa tafsiri ya juujuu,Pengo anasema hata Rais fulani akiuwa,akipoteza watu kwa njia ya watu wasiojulikana,akipiga watu risasi hadharani,akiminya demokrasia na kuharibu mifumo mizuri ya utawala wa kisheria,maadamu mtu huyo anatujengea shule na mabarabara,basi mtu huyo ni mwema,anafaa,na yote anayofanya katika kunywa damu za watu ni kama "kosa lenye heri".Pengo haamini katika utawala wa sheria,anaamini katika falsafa ya maguvu inayoleta "maendeleo".
Unaposika maneno haya toka kwa gwiji wa "Moral Theology" roho inakuuma sana,haya hayakupaswa kuwa maneno yanayotoka katika kinywa cha mtu aliyekaa darasani na kufungua kurasa za vitabu vya kina St.Thomas Acquinas ambao wameelezea kwa undani juu ya "Justice and Society".Pengo ni mwalimu na gwiji wa "Moral Theology",anapata wapi nguvu za kukana elimu yake kwa kuona "udikteta" ni bora kuliko utawala wa sheria??.Ninamkumbusha mwalimu wangu Cardinal Pengo kuwa "In civilized life,Law floats in a sea of ethics".Kwa gwiji wa moral Theology kama Pengo,huu si msemo mpya kwake.Leo Muadhama ni wa kuunga mkono udikteta dhidi ya utawala wa sheria?
Walatini wanasema "Legum servi sumus ut liberi esse possimus" i.e "We are slaves of law in order that we may be able to be free".Pengo awahimize marafiki zake wanaomtumia,na wawe watumwa wa sheria,maana utumwa wa sheria humuweka mtu kuwa huru.
Hatuwezi kusifia uvunjifu wa haki za binadamu,kudidimia kwa utawala wa sheria,kulegalega kwa haki ya kukusanyika na kupotea kwa misingi ya uchaguzi huru na wa haki eti kwa mbadala wa ujenzi wa majengo ya hospitali na baabara.
Mtakatifu Thomas Aquinas alisema "He who is not angry when there is just cause for anger is immoral. Why? Because anger looks to the good of justice. And if you can live amid injustice without anger, you are immoral as well as unjust"
Hata katika mazingira ambayo haki inaokana kutokutendeka,hawa wazee wanapongeza tu.Tunapolalamika hali ya maisha imekuwa ngumu,wao hawapo na sisi.Sisi waumini tumebaki peke yetu.
Weekend hii nilihudhuria "Makusanyo ya Mwaka wa Mavuno Jimbo la Dar es Salaam".Makusanyo ya dekania zote,toka kwenye parokia kamili na parokia tarajiwa.Tumevuna kwelikweli...na pesa hizi zinakwenda kulitegemeza jimbo.Makusanyo haya hayana kodi,maana ni mali ya kanisa.Hili pia linaweza kuwa moja ya jambo linalofanya hawa watu wa kanisa wajisahau na kuona huku mtaani waumini wao maisha ni raha mustarehe
Pengine mavuno haya yanawasahaulisha hawa viongozi wetu,basi kupitia jukwaa hili nataka kuwaambia hawa mababa kuwa maisha ni magumu sana,milo mitatu ni huku kwa waumini wao ni kwa kubahatisha,wanapopata nafasi ya kukutana na mfalme au wasaidizi wa mfalme,basi wasimamie ukweli,wasimame na waumini wao.Wasione soni katika kukemea rushwa,uonevu,mauaji,ukiukwaji wa demokrasia na kudumazwa kwa siasa za ushindani.Hivi kweli muitikio wa leo katika uchaguzi wa serikali kanisa hili la Khalifa wa Mtume Petro linaona ni sawa tu!!?
Sisi waumini tunapokusanya mamilioni haya na wakati mwingine mpaka kuvuka kiwango,hawa mababa zetu wa kiroho waadhani tuna maisha mazuri sana,labda tuna pesa na tunaridhika na mfumo wa uchumi unavyokwenda kwa sasa.Wanajisahau na kuwa upande wanaopaswa kuukosoa kwa hekima,wanafungamana nao na kutusahau sisi tunaohitaji sauti zao na kauli zao katika mimbari zitusemee.
Angalisema Pengo peke yake tusingeshangaa sana,lakini sasa mpaka maparoko wameanza siasa kwenye mahubiri,wanaanza kampeni,wanaona kila jambo ni shwari na maisha ni sawa sababu waumini tunatoa mavuno yanayopita kiwango tulichojiwekea.
Mfano huu ni wa mavuno kwa Jimbo la Dar es Salam tu,tumevua mamilioni,labda ndioyanawsahaulisha hawa mababa nawanahisi tuna maisha mazuri tu.
MAVUNO JIMBO KUU LA DAR ES SALAAM.
DEKANI YA KIGAMBONI Tsh 263,226,750
1. KIGAMBONI 18,830,645
2. MBAGALA. 14,252,535
3. KIJICHI. 55,000,000
DEKANIA YA ST. JOSEPH Tsh 49397550/489,622,220
1. ST. JOSEPH. 216,250,210
2. UPANGA. 40,000,000/
3. MSIMBAZI. 61,300,00
DEKANIA YA GASPAR. Tsh 404,768,100/ 418,180,510
1. GASPAR. 53,164,300
2. TEGETA 12,673,700
3. BOKO. 31,000,500
4. SALASALA 20,126,550
5. T. MORE. 27,453,400
6. KUNGURU. 14, 968,000/
DEKANIA YA PETRO.
Tsh
532 670,575/ 489,823,712
1. PETRO. 153,51000
2. MIKOCHENI 32,000,000
3. MWEGE 70,272,500
4. SINZA. 48,260,000
5. MAGOMENI. 41,500,000
DEKANIA YA. UBUNGO. 278,816,650/ 300,301,000
1. UBUNGO 15,314,000
2. MANZESE. 43,000,000
3. MAKUBURI 27,338,000
4. C.KIKUU. 40,000,000
DEKANIA YA UKONGA 251,750,950 / 265,500 090
1. UKONGA 76,000,000
2. PUGU 35,275,000
3. KIWALANI 14,000,000
4. VITUKA 16,700 600
5. KITUNDA 36,523,770
DEKANIA YA SEGEREA. 270,176,700/ 254,827,050
1. SEGEREA. 43,631,700
2. TABATA. 102,213,850
3. KINYEREZI 16,800,000
4. KIPAWA. 30,452,300
5. KIMANGA. 15,000,000
DEKANIA YA KIBAHA. 145,532,050/ 161,976,300
1. KIBAHA 31,000,200
2. MLANDIZI 14,000,500
3. MKUZA. 14,000,000
4. KIBAMBA 23,390,500
5. KIBWEGERE. 28,000,000
DEKANIA YA KILIMAHEWA. 36,749, 100/ 37,309,850
1. KILIMAHEWA 5,573 700
2. MKURANGA 12,108 250
3. KIBITI 3,500,000
DEKANIA YA MBEZI LUIS. 257,613,300 /293,962,900
1. MB/LUIS 25,334,300
2. MAVURUNZA 68,100,250
3. TAGASTE. 27,000,000
4. TEGETA A 9,122,000
Makusanyo kama haya,ninadhani ndio yanawasahaulisha watu kama kina Pengo na Mapdre wengine,maana sasa wanafungamana na upande ambao bila shaka unawafanya waon udikteta ni bora kuliko utawala wa sheria.Kwenye kanisa ambalo ndani yake kuna watu weye fikra na itikadi mseto,viongozi wa kanisa mnapaswa kuchun sana ndimi zenu.
Juzi kati akiwa na RC Makonda,Muadhama P. Cardinal Pengo amewananga wanaoikosoa serikali ya awamu ya tano.Kwa tafsiri ya hotuba yake,ni kama Cardinal Pengo anasema kwake demokrasia si lolote kama tu watu wanaenda shule bure,wanajengewa barabara na hata kujengewa vituo vya afya.
Mwadhama ambaye kwa nafasi yake ni mmoja kati ya walio wachache wenye haki ya kikatiba pale Vatican kutuchagulia Papa ambaye ni khalifa wa mtume Petro na msimamizi wa kanisa katoliki lililo nyumba ya imani ya mabilioni ya watu duniani.
Pengo akavuka mipaka,akasema hata Hitler na Musolini walikuwa watu wema,maana udikteta wao ulileta maendeleo.Akasema kwa lugha ya kificho kuwa hata wale wayahudi dunia inayoambiwa waliuawawa na Hitler,si lolote ukilinganisha na maendeleo aliyoleta.Yaani kwa tafsiri ya juujuu,Pengo anasema hata Rais fulani akiuwa,akipoteza watu kwa njia ya watu wasiojulikana,akipiga watu risasi hadharani,akiminya demokrasia na kuharibu mifumo mizuri ya utawala wa kisheria,maadamu mtu huyo anatujengea shule na mabarabara,basi mtu huyo ni mwema,anafaa,na yote anayofanya katika kunywa damu za watu ni kama "kosa lenye heri".Pengo haamini katika utawala wa sheria,anaamini katika falsafa ya maguvu inayoleta "maendeleo".
Unaposika maneno haya toka kwa gwiji wa "Moral Theology" roho inakuuma sana,haya hayakupaswa kuwa maneno yanayotoka katika kinywa cha mtu aliyekaa darasani na kufungua kurasa za vitabu vya kina St.Thomas Acquinas ambao wameelezea kwa undani juu ya "Justice and Society".Pengo ni mwalimu na gwiji wa "Moral Theology",anapata wapi nguvu za kukana elimu yake kwa kuona "udikteta" ni bora kuliko utawala wa sheria??.Ninamkumbusha mwalimu wangu Cardinal Pengo kuwa "In civilized life,Law floats in a sea of ethics".Kwa gwiji wa moral Theology kama Pengo,huu si msemo mpya kwake.Leo Muadhama ni wa kuunga mkono udikteta dhidi ya utawala wa sheria?
Walatini wanasema "Legum servi sumus ut liberi esse possimus" i.e "We are slaves of law in order that we may be able to be free".Pengo awahimize marafiki zake wanaomtumia,na wawe watumwa wa sheria,maana utumwa wa sheria humuweka mtu kuwa huru.
Hatuwezi kusifia uvunjifu wa haki za binadamu,kudidimia kwa utawala wa sheria,kulegalega kwa haki ya kukusanyika na kupotea kwa misingi ya uchaguzi huru na wa haki eti kwa mbadala wa ujenzi wa majengo ya hospitali na baabara.
Mtakatifu Thomas Aquinas alisema "He who is not angry when there is just cause for anger is immoral. Why? Because anger looks to the good of justice. And if you can live amid injustice without anger, you are immoral as well as unjust"