Pendekezo: Wale wote waliodhulumiwa chochote na Serikali ya Tanzania ya awamu ya 5 Wajitokeze hadharani Tufunge mjadala

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
116,490
215,332
Sasa ni dhahiri kwamba Wimbi la watu kudhulumiwa mali zao wakati wa Utawala wa John Magufuli liko bayana na ni kubwa kuliko tulivyodhani.

Watu wameporwa karibu kila kitu, wako walioporwa hela zao , humu wamo walioguswa kwenye akaunti zao (bila kujali kama wanadaiwa au hawadaiwi yaani ukiwa na hela nyingi tu hata kama uliuza mahindi yako unaporwa ), wako pia wale wa Plea bargain akiwemo Habhinder Seth na wamo pia wenye maduka ya kubadilishia fedha za kigeni (Bureau De Change), wako walioporwa Mashamba yao akiwemo Sumaye , Wamo wengi walioporwa mifugo yao kwa kisingizio cha kuchunga kwenye hifadhi , yaani ngedere walionekana bora kuliko ng'ombe , Wavuvi waliporwa kila kitu , zikiwemo samaki walizovua , nyavu , mitumbwi , boti na vifaa vyao vyote , wako walioporwa Viwanja na nyumba , akiwemo GSM , Wako walioporwa magari na kesi zingali Mahakamani , Bila shaka wako walioporwa Wake ama Waume zao kwa utaratibu ule ule wa kishamba wa " Unanijua mimi nani " , Wako wengine walioporwa Uhai wao akiwemo Lwajabe , mnyororo wa walioporwa ni mrefu sana , hatutaweza kuumaliza .

Kwa vile serikali ya awamu ya 6 imetambua uporaji huu na imeanza kuwarejeshea pesa zao baadhi ya wahanga , basi Natoa Wito kwa watu wote waliodhulumiwa chochote kile na serikali ya kikatili ya awamu ya 5 , wajitokeze hadharani tuwafahamu na kufahamu njia zilizotumika kuwapora mali zao ili tuangalie namna ya kuwasaidia , hakuna haja ya kuficha ficha mambo, hakuna haja ya kuogopa kufichua maovu ili kuanika kila uchafu uliofanywa kwenye awamu ile .

Jambo hili ni muhimu kufanyika kwa sababu si wote walioporwa ni maarufu , si wote walioporwa wana ujasiri wa kuyatoa mambo yao hadharani wao wenyewe bila kulindwa , watu waliowatisha na kuwapora wengine bado wako hai na wengine bado wamekalia vitengo.

FB_IMG_1652379712226.jpg
 
Wapo waliobomolewa nyumba zao,kwa baadhi ya maeneo zaidi ya kaya 800,na hata leo zoezi la urasimishaji ardhi haliendi sawa huenda vimelea vya mgogoro bado vingalipo.Japo ulionekana kupoa baada ya baadhi ya waliosimamia zoezi kuwekwa pembeni,kutoka nyadhifa walizozitumia kufanikisha dhulma hizo za kijambazi🤔
 
Wapo waliobomolewa nyumba zao,kwa baadhi ya maeneo zaidi ya kaya 800,na hata leo zoezi la urasimishaji ardhi haliendi sawa huenda vimelea vya mgogoro bado vingalipo.Japo ulionekana kupoa baada ya baadhi ya waliosimamia zoezi kuwekwa pembeni,kutoka nyadhifa walizozitumia kufanikisha dhulma hizo za kijambazi
Tunaomba hili nalo lishughulikiwe
 
Mlifika wewe na nani? huyo anaekupumlia kisogoni?
Wale wa maduka ya kubadili fedha,wafanya biashara,kama hata akina Dangote,Mo,na wengine wengi orodha ni ndefu kiasi haiwezekani kuwataja wote,hata dhuluma ile ya kuwa dhuluma watumishi zaidi ya miaka 5🤔.Hapo hatuja taja dhuluma ndani ya mfumo wa siasa,na maamuzi ya kisiasa yaliyowaathiri wengi.
 
Wale wa maduka ya kubadili fedha,wafanya biashara,kama hata akina Dangote,Mo,na wengine wengi orodha ni ndefu kiasi haiwezekani kuwataja wote,hata dhuluma ile ya kuwa dhuluma watumishi zaidi ya miaka 5
Kila ubaya utalipwa
 
kuna tofauti kubwa kati ya kupora na kutaifisha, vyeti feki na waliosota juu ya madawati, kupambania mali za watanzania ama kuogopa kushtakiwa MIGA, kucheka na nyani shambani ama kuweka misingi nchi isiwe shamba la bibi hayo na mengine mengi alituonesha mwamba mmoja tu, na kizuri wote tulio timamu tunajua na tutamuenzi daima. Mungu amlaze mahali pema, Amen.
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom