demolisher
Member
- Apr 11, 2011
- 37
- 100
Ninapendekeza kwa Mwenyekiti wa tume ya katiba na jamii pana ya waTanzania ukusanyaji maoni upate live coverage ya TV na Radio. Hii itasaidia watanzania kuona na kusikia kila kitakachokuwa kinaendelea. Hili litasaidia kuondoa shaka na kutimiliza msemo maarufu wa kisheria: "Haitoshi tu haki kutendeka bali na idhihirike bayana imetendeka". Kama pendekezo hili likikataliwa ni kiashiria tosha kuwapo dhamira ya kuchakachua maoni ya wa-TZ. Mwishoni waibuke eti waTZ wanapenda raisi ateue tume, wabunge wawe mawaziri n.k