Pendekezo la “Ukanda Mmoja, Njia Moja” lairudisha Marekani Afrika

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG31N1303728532.jpg

Hivi karibuni jarida ya Foreign Policy la Marekani lilikuwa na makala yenye kichwa “The United States Returns to Africa” kikiwa na maana Marekani inarudi tena Afrika. Yaliyoandikwa chini ya makala hiyo yametaja baadhi mambo ya kipaumbele kuhusu sera ya serikali ya Rais Joe Biden kwa Afrika, lakini pia yanakiri kuwa katika miaka minne ya serikali ya rais aliyepita Donald Trump uhusiano kati ya Marekani na bara la Afrika ulikuwa katika kiwango cha chini kabisa. Lakini kitu cha kushangaza ni kuwa makala hiyo inasema China imefanya Marekani irudi Afrika. Inaweza kuonekana kuwa ni jambo la ajabu, lakini imetajwa wazi kwenye makala hiyo kuwa ufanisi wa pendekezo la “ukanda mmoja, njia moja” ndio linaifanya Marekani irudi Afrika.

Tukijaribu kuangalia kauli hiyo kuwa “Marekani inarudi tena Afrika”, kwa upande mmoja tunaweza kuona ni jambo zuri kwa kuwa mshirika anarudi, kwa upande mwingine tunajiuliza kuna mshirika huyo atakuwepo kwa muda gani? Lakini pia kuna mambo ambayo tumeweza kujifunza kutokana na yaliyotokea hivi karibu kwenye uhusiano kati ya bara la Afrika na nchi kubwa duniani, na jinsi pendekezo la “Ukanda mmoja, Njia moja” linavyohimiza maendeleo barani Afrika.

Kwanza tumeona tofauti kubwa kati ya China na Marekani inapokuja kwenye kushughulikia uhusiano na nchi za Afrika. China ina sera madhubuti na endelevu, inayotekelezwa bila kujali ni Rais gani yuko madarakani. Mabadiliko yanayoweza kuonekana kwenye utekelezaji wa sera za China kwa Afrika kutokana na mabadiliko ya viongozi wa China, ni kuongezeka kwa yaliyomo, kasi au hata mtindo wa kutekeleza sera, lakini msingi wa sera ni ule ule. Mfano mzuri ni pendekezo la “Ukanda mmoja, Njia moja” lilitolewa na Rais Xi Jinping, ambalo limekuja kuchochea uhusiano uliopo kati ya China na Afrika.

Lakini inapokuja kwa Marekani tunaweza kuona ni kama Marekani haina sera ya taifa kuhusu Afrika, na kama ipo basi si sera ya kudumu. Tukiangalia wakati wa utawala wa George Bush tunaweza kuona ukaribu sana kati ya Afrika na Marekani, alipoingia Barack Obama ukaribu ulipungua kiasi, na alipoingia Donald Trump ulikuwa karibu kufutika kabisa kutokana na dharau, na lugha zake chafu, na sasa Rais Biden anasema Marekani inarudi Afrika. Hali hii inaonyesha kuwa uhusiano kati ya Marekani na nchi za Afrika unategemea nia binafsi ya Rais atakayekuwa madarakani, na sio sera ya taifa.

Pili, ni suala la vipaumbele kwenye sera hizo, na ufanisi wake katika kuimarisha ushirikiano na kuboresha maisha ya watu. Bila shaka vipaumbele kwenye serikali ya Joe Biden kuhusu sera ya Marekani kwa Afrika, vina mambo yanayofuatiliwa na nchi za Afrika. Ni kweli Afrika inaihitaji Marekani na jumuiya ya kimataifa kwa ujumla kwenye kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, afya, kuimarisha demokrasia na kupambana na changamoto za usalama kama vile ugaidi.

Hata hivyo tukiangalia undani wa hali halisi ya nchi nyingi za Afrika kwa sasa, tunaona kuna changamoto nyingi zaidi ya hizo na zinazogusa moja kwa moja maisha ya watu. Ushirikiano kati ya China na Afrika licha ya kugusa vipaumbele vilivyotajwa na Serikali ya Biden, unagusa moja kwa moja changamoto kama vile masoko ya bidhaa za kilimo, mitaji, miundombinu, ajira na bidhaa za matumizi ya kila siku wanazohitaji watu wa Afrika kuboresha maisha yao.

Pamoja na kuwa nchi yoyote inaamua kushirikiana na nchi nyingine kutokana na maslahi yake, kuna jambo moja ambalo China imekuwa ikisisitiza mara kwa mara kwenye uhusiano kati yake na nchi nyingine, yaani “ushirikiano wa kunufaishana” na ushirikiano uwe wa “kujenga jumuiya ya binadamu yenye hatma ya pamoja”. Bila shaka pendekezo la “Ukanda mmoja, njia moja” msingi wake ni kusaidia uwekezaji wa China katika nchi nyingine duniani, lakini pia halizingatii maslahi na faida ya China peke yake, kunufaishana ni kipengele muhimu kwenye pendekezo hilo.

Mbali na hilo, kuna lingine muhimu ambalo viongozi wa China na wa nchi za Afrika wamekuwa wakilitaja mara kwa mara kwenye uhusiano kati ya China na nchi za Afrika, “All-Weather Friendship” yaani urafiki bila kujali kuna hali gani. Wakati Marekani ilikuja, ikiondoka, na sasa Biden anasema imerudi Afrika, hatujui itakuwaje baada ya rais mwingine kuja madarakani. Lakini ni wazi kuwa China ilikuwepo wakati wa Mwenyekiti Mao, ipo wakati wa Xi Jinping, itakuwepo na itaendelea kuwepo Afrika katika siku za baadaye.
 
Mchina hana Nia nzuri na Afrika. Atafyeka kila Chaka ili kujinufaisha. Pesa Yake Ina masharti kibao inalenga faida SI kuwaendeleza wa-Afrika
 
Back
Top Bottom