Pendekezo la timu ya kampeni ya CHADEMA kwenye uchaguzi wa marudio Sumbawanga

TUMBIRI

JF-Expert Member
May 7, 2011
1,933
1,199
Wakuu wote heshima mbele,
Kama tunavyojua miezi michache ijayo CHADEMA itaingia kwenye kinyang'anyiro cha kuwania Ubunge wa Jimbo la Sumbawanga. Ni muda muafaka tutafakari kwa pamoja na kumshauri Katibu Mkuu wetu Dr. Willbrod Slaa namna atakavyounda timu ya kampeni hususani timu kuu ya kuratibu Kampeni za Chama. Hapa chini nimejaribu kuweka altenative nane (Plan A to Plan H). Tujaribu kuchagua Plan moja au kufanyia maboresho ili tuikabidhi majukumu ya Kikampeni huko ya huko Sumbawanga.

Chini ya hizi Plan kuna Kamati yetu ya Ufundi (Evaluation & Monitoring Team) ambayo kimsingi hii inabaki kama ilivyo kama tulivyokuwa tunaitumia katika chaguzi zilizopita. Pia timu ya Washauri (Consultants). Hii nayo itabaki kama ilivyo kama tulivyokuwa tunaitumia kwenye chaguzi zetu za nyuma. Tujikite kupembua ni "Plan" ipi inafaa au kama haipo basi tutoe mapendekezo kwa Chama, ni timu gani unayoona itafaa kuituma Sumbawanga kufanya Kampeni na tuibuke na ushindi mnono.


PLAN A
1. Kampeni Meneja - Peter Msingwa
2. Naibu Kampeni Meneja - Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu
3. Kamanda wa Operesheni - Godbless Lema
4. Naibu Kamanda wa Operesheni - Ally Banaga

PLAN B:
1. Kampeni Meneja - Vincent Nyerere
2. Naibu Kampeni Meneja - Meshak Opulukwa
3. Kamanda wa Opereshini - Mwita Waitara
4. Naibu Kamanda wa Operesheni - Joshua Nassari

PLAN C:
1. Kampeni Meneja - Godbless Lema
2. Naibu Kampeni Meneja - Peter Msingwa
3. Kamanda wa Operesheni - John Heche
4. Naibu Kamanda wa Operesheni - David Silinde

PLAN D:
1. Kampeni Meneja - Tundu Lissu
2. Naibu Kampeni Meneja - Vincent Nyerere
3. Kamanda wa Operesheni - John Mrema
4. Naibu Kamanda wa Opereshini - Msafiri Mtemelwa

PLAN E:
1. Kampeni Meneja - Ezekiel Wenje
2. Naibu Kampeni Meneja - Godbless Lema
3. Kamanda wa Opereshini - Benson Kigaila
4. Naibu Kamanda wa Opereshini - Tumaini Makene

PLAN F:
1. Kampeni Meneja - Mabere Marando
2. Naibu Kampeni Meneja - John Mnyika
3. Kamanda wa Opereshini - Halima Mdee
4. Naibu Kamanda wa Opereshini - Joshua Nassari.

PLAN G:
1. Kampeni Meneja - Israel Natse
2. Naibu Kampeni Meneja - Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu
3. Kamanda wa Operesheni - David Silinde
4. Naibu Kamanda wa Opereshini - Tumaini Makene

PLAN H:
1. Kampeni Meneja - Vincent Nyerere
2. Naibu Kampeni Meneja - Godbless Lema
3. Kamanda wa Operesheni - Mwita Waitara
4. Naibu Kamanda wa Operesheni - James Ole Millya

MONITORING AND EVALUATION (M&E) TEAM
1. Freeman A. Mbowe
2. Dr. Willbrod Slaa

STRATEGISTS / CONSULTANTS:

1. Said Arfi - Mzee Arfi atatushauri kwenye masuala ya mila na destruri za Wenyeji wa Sumbawanga. Pia atatusadia kupanga mbinu za ushindi kwa kuwa ni mzoevu wa siasa za Nyanda za Juu kusini especially Mkoa wa Rukwa.

2. Prof Abdallah Safari - Huyu ni Mtaalamu wetu wa Sheria. Tumtumie ku-monitor mwenendo wa kampeni za CCM, mchakato wa kupiga kura na kutangaza matokeo. Hili swala ni muhimu kwa sababu litatusaidia kukusanya ushahidi wa kupeleka Mahakamani baada ya Matokeo ya Uchaguzi kutangazwa kama ikibidi kufanya hivyo.

3. Dr Kitila Mkumbo - Mtaalamu wetu wa Saikolojia. Tumtumie kupanga mbinu za kisiasa kuwaandaa wapiga kura kisaikojia kujitokeza kupiga kura na kulinda kura zao kama walivyofanya Wana Arumeru Mashariki. Ni mtaalamu pia wa mbinu za kikampeni kwenye chaguzi.

4. Prof Mwesiga Baregu - Mtalaamu wetu wa Sayansi ya Siasa. Ushauri wake wa kisomi utumiwe kuendesha kampeni za kisomi zisizohitaji raslimali nyingi na zenye matokeo chanya.

5. Edwin Mtei - Uzee ni dawa. Wazee wameona mengi hadi hapo walipofika. Kuna mambo tunaweza kuona ni mageni kwetu lakini kwa wazee si mageni. Tunapopata changamoto za kikampeni si vibaya kuwasiliana nae kupata mchango ushauri wake.

Nawasilisha.

TUMBIRI (PhD, HULL University - United Kingdom),
tumbiri@jamiiforums.com

Nakala: POMPO, Mungi, Crashwise, Kimbunga, Matola, Ben Saanane, Mikael P Aweda, Mzee Mwanakijiji, Candid Scope, Yericko Nyerere, Pasco, Mwita Maranya, Molemo, Mkandara, Excy, Isango, Invisible, Josephine, zomba, Rejao, TUNTEMEKE, Losambo, BAK, Eliah G Kamwela, Katavi, only83, Arushaone, Ngongo, Polisi, Mohamedi Mtoi, Saint Ivuga, Mzito Kabwela, Raia Fulani, nk
 
Last edited by a moderator:
Hakuna haja wa kuwaumiza wazee, Dr. Slaa atakwenda na panel yake kuongeza nguvu. Mi nadhani plan C ina apply Sumbawanga
 
TUMBIRI
Mpango mzima ndio umeukamilisha. Nitapenda kuweka masahihisho machache kama ifuatavyo:
Kwa hali halisi ilivyosasa hivi si vema kuwaingiza kwenye ratiba za mara kwa mara viongozi wakuu wenye majina kitaifa CHADEMA kwa sababu za kiusalama, wawepo pale tu inapohitajika na kuhakikisha usalama wao kwa kila njia.

:A S 465:Ukiona CCM na serikali yake wenyewe kwa wenyewe:A S 465:
:A S 465:wanaanza kukimbizana na majambia ujue kumekucha.:A S 465:
 
plan A applies better ila uwepo wa Lema sidhani kama waweza kuwa guaranteed CCM watapenda zaidi kuitisha chaguzi nyingi wakati mmoja ili iwe rahisi kuwagawanya wana CHADEMA. Ila nathani ni vizuri na James Ole Millya akawepo pia maana defectors esp. wa CCM huchagiza mambo!

Tundu Lissu na Mabele Marando wana majukumu mengi ila uwepo wao as observers kuhakikisha haki inatendeka au wanarekodi matukio ni wa muhimu sana haswa kwenye zile purukushani na Polisi CCM! Maana mwisho wa siku kuna mambo ya kimahakama haswa pale watakaposhindwa isivyo halali.

Heche pia asikose kama representative wa vijana! Otherwise nimependa timu yako ya strategists/consultants! Na tusisahau jina "Nyerere as a brand" siri iliyofichika iliyomfanya mzee Mkapa kuropoka na kubwabwaja mitusi isiyo na hekima na kupelekea kushindwa uchaguzi siku ya kwanza alipopanda jukwaani!

:poa
 
TUMBIRI
Mpango mzima ndio umeukamilisha. Nitapenda kuweka masahihisho machache kama ifuatavyo:
Kwa hali halisi ilivyosasa hivi si vema kuwaingiza kwenye ratiba za mara kwa mara viongozi wakuu wenye majina kitaifa CHADEMA kwa sababu za kiusalama, wawepo pale tu inapohitajika na kuhakikisha usalama wao kwa kila njia.

:A S 465:Ukiona CCM na serikali yake wenyewe kwa wenyewe:A S 465:
:A S 465:wanaanza kukimbizana na majambia ujue kumekucha.:A S 465:

Mkuu umeandika vema.
Nadhani chama kinapaswa kuongeza ulinzi maradufu kwa Dr Slaa na Freeman Mbowe.Kuwe na mpango maalum wa ulinzi popote viongozi hawa watakapotembelea hasa katika operesheni za kichama.
 
UBARIKIWE TUMBIRI, na aliyekuzaa abarikiwe pia. Unaiwazia mema Tanzania na watanzania wote! Plan zonte ni njema na nzuri mno, any of them, ninaikubali sana, tena sana tu.
 
TUMBIRI
Mpango mzima ndio umeukamilisha. Nitapenda kuweka masahihisho machache kama ifuatavyo:
Kwa hali halisi ilivyosasa hivi si vema kuwaingiza kwenye ratiba za mara kwa mara viongozi wakuu wenye majina kitaifa CHADEMA kwa sababu za kiusalama, wawepo pale tu inapohitajika na kuhakikisha usalama wao kwa kila njia.

:A S 465:Ukiona CCM na serikali yake wenyewe kwa wenyewe:A S 465:
:A S 465:wanaanza kukimbizana na majambia ujue kumekucha.:A S 465:

Mkuu plan C imetulia sana hao makamanda wametulia sana Hivi tunavyoongea kamanda heche yupo field anakamua......hapo kwenye plan C ukimuongeza Vicent Nyerere........lazima wakae
 
Jamani msimsahau mzee wa NOCK OUT -VICENT NYERERE huyu jamaa alitupa ushindi round ya kwanza pale arumeru ,sitamsahau hakika !
 
Plan ' A' nimeipenda sana, itatupa ushindi, but hata plan zingine ni nzuri sana kwasababu CDM 2po wamoja.
 
Mimi naona kama kutakuwa na uchaguzi mdogo mmoja tu wa ubunge kipindi hicho basi plan zote zitumike kila plan ipewe eneo na wabadilishane maeneo kila baada ya siku kadhaa ili kuwapa utamu wakazi wa sumbawanga mjini maana najua kila mwanasumbawanga anahamu ya kuwaona na kusikia kutoka kwa makamanda.

Nadhani kuna mtu amesahaulika wa muhimu sana maana yale pia ni maeneo yake ya kujidai bwana ZZ kabwe. Anaweza asiwepo muda wote lakini ni muhimu achukue jukumu hili kama kiongozi wa chama na ukweli kwamba maeneo haya anayafahamu pia.
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom