Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
PENDEKEZO LA 1:TANGA, MAFIA, BAGAMOYO NA PANGANI ZIWE SEHEMU YA ZANZIBAR!
Na. M. M. Mwanakijiji
Hili ni pendekezo la kwanza kati ya mapendekezo kadhaa ambayo nitayatoa katika kusaidia kuleta fikra mpya katika mijadala mbalimbali ya kitaifa ambayo lengo lake ni kutupa uwanja mkubwa zaidi wa kuweza kufanyia maamuzi. Miaka 46 imepita tangu Muungano pekee wa nchi mbili za Kiafrika uasisiwe na hivyo kujenga katika bara la Afrika nchi pekee ambayo mipaka yake haikurithishwa na wakoloni! Tanzania tunayoishi leo hii ni tunda na zao la Watanzania wenyewe.
Pamoja na matatizo yote yaliyopo Muungano wetu unapaswa kutetewa, kulindwa na kudumishwa si kwa sababu ya woga, si kwa sababu hauwezi kuvunjika, na si kwa sababu hautakuwa na matatizo huko mbeleni. Tunapaswa kuulinda, kuudumisha na kuuboresha kwa sababu moja tunaupenda kwani ndio nchi pekee tuliyoijenga kwa ajili yetu sisi na watoto wetu.
Ninaamini kabisa kuwa siku watawala wetu watatoka kwenye ufinyu wa fikra wanaouonesha siku kwa siku wataweza hatimaye kuja na mapendekezo ya kuuboresha Muungano wetu na kuufanya uwe kwa faida ya kila Mtanzania na kuondoa manunguniko yasiyo ya lazima na ambayo utatuzi wake unahitaji dakika chache tu za fikara. Pendekezo hili, halijawahi kutolewa na mtawala yeyote, hawawezi kulitoa kwani hawana uwezo wa kifalsafa kulitetea! Hawawezi kulikumbatia kwa uharaka kwa sababu wamefungwa na siasa zao za utengano hadi wanatia aibu. Hili hata hivyo, haliwezi kuwazuia Watanzania wengine kutoa mawazo yao na kuyasogeza mbele kama pendekezo ili kila Mtanzania ajue kuwa hatuhitaji wazungu watuletee mapendekezo yao ili tuyakumbatie kama yameletwa na wajumbe wa Mungu! Hili ni pendekezo la kuthubutu, la nguvu, la mkakati, la kisiasa, la kiutu, na la kiumoja kuliko mapendekezo mengine yote yaliyowahi kutolewa kuhusu kudumisha Muungano au kuondoa kero za Muungano.
READ AT YOUR OWN INTELLECTUAL PERIL!
View attachment PENDEKEZO LA 1.doc
Na. M. M. Mwanakijiji
Hili ni pendekezo la kwanza kati ya mapendekezo kadhaa ambayo nitayatoa katika kusaidia kuleta fikra mpya katika mijadala mbalimbali ya kitaifa ambayo lengo lake ni kutupa uwanja mkubwa zaidi wa kuweza kufanyia maamuzi. Miaka 46 imepita tangu Muungano pekee wa nchi mbili za Kiafrika uasisiwe na hivyo kujenga katika bara la Afrika nchi pekee ambayo mipaka yake haikurithishwa na wakoloni! Tanzania tunayoishi leo hii ni tunda na zao la Watanzania wenyewe.
Pamoja na matatizo yote yaliyopo Muungano wetu unapaswa kutetewa, kulindwa na kudumishwa si kwa sababu ya woga, si kwa sababu hauwezi kuvunjika, na si kwa sababu hautakuwa na matatizo huko mbeleni. Tunapaswa kuulinda, kuudumisha na kuuboresha kwa sababu moja tunaupenda kwani ndio nchi pekee tuliyoijenga kwa ajili yetu sisi na watoto wetu.
Ninaamini kabisa kuwa siku watawala wetu watatoka kwenye ufinyu wa fikra wanaouonesha siku kwa siku wataweza hatimaye kuja na mapendekezo ya kuuboresha Muungano wetu na kuufanya uwe kwa faida ya kila Mtanzania na kuondoa manunguniko yasiyo ya lazima na ambayo utatuzi wake unahitaji dakika chache tu za fikara. Pendekezo hili, halijawahi kutolewa na mtawala yeyote, hawawezi kulitoa kwani hawana uwezo wa kifalsafa kulitetea! Hawawezi kulikumbatia kwa uharaka kwa sababu wamefungwa na siasa zao za utengano hadi wanatia aibu. Hili hata hivyo, haliwezi kuwazuia Watanzania wengine kutoa mawazo yao na kuyasogeza mbele kama pendekezo ili kila Mtanzania ajue kuwa hatuhitaji wazungu watuletee mapendekezo yao ili tuyakumbatie kama yameletwa na wajumbe wa Mungu! Hili ni pendekezo la kuthubutu, la nguvu, la mkakati, la kisiasa, la kiutu, na la kiumoja kuliko mapendekezo mengine yote yaliyowahi kutolewa kuhusu kudumisha Muungano au kuondoa kero za Muungano.
READ AT YOUR OWN INTELLECTUAL PERIL!
View attachment PENDEKEZO LA 1.doc