Pendekezo kwa TCU: Wao ndo washughulikie multiple selection.

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,663
18,037
Kwa utaratibu wa sasa, tutegemee karibu waombaji wote wenye divisheni 1 na II na baadhi ya wenye divisheni III kupata nafasi zaidi ya mbili kutegemea ameomba vyuo vingapi! Si rahisi MTU kuomba chuo kimoja tu, kwa hiyo kama ana sifa ya juu kuna uwezekano wa akapata nafasi katika vyuo vyote alivyoomba.
Hapo ndipo vyuo husika vinaweza kuchezeana faulo! Ili kuepuka msuguano kati ya vyuo na vyuo kugombania wanafunzi, napendekeza yafuatayo:
1. TCU ichukue jukumu LA kuwataka wanafunzi wenye multiple allocations kuconfirm TCU badala ya chuoni. Ninachokiona ni kuwa kuna vyuo viwili au zaidi vitakuja kudai kuwa mwanafunzi amekonfirm kwao, na kuleta usumbufu mkubwa kwa mwanafunzi.
2. Kama hilo LA juu halikubaliki, vyuo vizuiwe kuwataka wanafunzi kukonfirm mapema kabla ya muda uliowekwa na TCU. Maana tayari kuna vyuo vimeshaanza kuwahakikishia waombaji nafasi na vinawataka wathibitishe kama watajiunga navyo! Inabidi vyuo vyote vitoe matokeo kwanza na mhusika ajue amechaguliwa vyuo vipi ili afanye maamuzi.
Wadau MNA mchango gani katika hili?
 
Mbona Mkurugenzi wa TCU alishazungumzia hilo mkuu, wanafunzi watapewa siku 3 Ku confirm ni chuo gani watakwenda.

chase a check.. never chase a b!tch
 
Back
Top Bottom