Pendekezo: Kuwe na Daladala VIP kukabiliana na foleni

vunjo

JF-Expert Member
Jun 2, 2011
1,323
2,607
Nilikuwa na wazo katika mkoa wetu Dar es Salaam nafikiri likikifanyika litapunguza msongamano wa magari kwa asilimia kubwa.

Nilikuwa nafikiria zikisajiliwa daladala za VIP ambazo zitakuwa na Air conditioning usafi wa hali ya juu zikapiga ruti mfano Tegeta- Posta kwa Tsh 3,000 na abiria wote level seat hakuna kusimamisha abiria.

Kwa asilimia kubwa watu wataacha magari binafsi nyumbani na kutumia usafiri huu kwani kwa kiasi kikubwa wataokoa gharama za matumizi ya mafuta pia zitawaepusha misongamano ya kubanana kwenye daladala na pia mtu kufika ofisini kwake akiwa bado nadhifu na bila uchovu wowote.

Usumbufu abiria wanaopata kwenye daladala za kawaida unafanya watu wengi kukopa kupata usafiri binafsi ambao ndio huongeza msongamano kwenye barabara zetu hizi.

Kwenye Mabasi ya mikoa yapo VIP na Treni pia kuna madaraja tofauti hata ndege kwa nini kwenye daladala isifanyike.
 
Miaka kama mitano au Sita hivi kuna mtu aliishakuwa na Wazo kama lako pale Mbezi Mwisho Stendi.

Alikuwa na Coaster yake nzuri sana ya kutoka Mbezi Mwisho hadi pale nje ya Posta Mpya akishushia abiria wake nje ya Embassy Hotel kwa Buku tu wakati ule nauli ikiwa mia tano tu ka sikosei.

Hadi wale abiria wakafahamiana na akawa hata na muda maalumu wa kuondoka kituoni, saa 12.30 gari linang'oa nanga hadi Posta mpya bila kusimama vituoni.

Sijui hata aliishia wali lakini alikuwa amebuni mpango mzuri sana., na alikuwa anazipata!!
 
Ni wazo jema tu,vip lisipangiwe njia ya kupita ili kukwepa foleni nauli zake iwe 1000. bila kujali abiria atashuka wapi.tiketi zake zitolewe kwa machine.ili serekali ipate kodi yake stahili.
Hizi za 1000 zipo pale mbezi, Zinaenda kariakoo. ila hizi hazijasajiriwa rasmi.

Walipewa Kibari na Mh, Makonda kipindi chake, kupungiza msongomano kwenye mwendo kasi, kipindi kile cha korona ya mwanzo.
 
Back
Top Bottom