Pemba: Viongozi wa ACT, Maalim Seif na Salim Bimani waitwa Polisi. Washutumiwa kufanya mkutano bila kibali, waachiwa kwa dhamana


Mshauri mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti wa Kamati ya Itikadi na Uenezi wa ACT Wazalendo Salim Bimani wameripoti katika Kituo cha Polisi Wete Pemba asubuhi ya leo.

Viongozi hao wa ACT Wazalendo wameitwa na Mkuu wa Upelelezi wa Jinai (RCO) Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Wananchi na Wanachama wa ACT - Wazalendo wamekuwa nje ya maeneo ya karibu ya jengo la Polisi la Mkoa wa Kaskazini Pemba kwa lengo la kujua hatma ya viongozi wao wanaohojiwa na inadaiwa wamejiandaa na kuwachukulia dhamana ikibidi.

UPDATE:
Mshauri Mkuu wa ACT Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Salim Bimani wameshutumiwa kufanya mkutano bila kibali mwezi Desemba 2019 huko Micheweni Zanzibar.

Hata hivyo, Viongozi hao wameachiwa kwa dhamana na kupitia Mtandao wa Twitter Chama chao kimedai kuwa walifanya mkutano wa ndani usiohitaji kibali.

Jeshi la Polisi limewachia kwa Dhamana Mshauri Mkuu wa Chama @ACTwazalendo Maalim Seif Sharif Hamad na M/kiti wa kamati ya Itikadi na uenezi wa Chama hicho Salim bimani Baada ya hii leo kuitwa kufanyiwa mahojiano na Jeshi hilo katika kituo cha Polisi mkoa wa kaskazini Pemba.
Whether tuhuma hizo ni za kweli au vinginevyo, nawapongeza Polisi kwa jambo moja - wamewaita wakaripoti kituo cha Polisi. Baada ya wao kutii agizo la Polisi, wamepewa dhamana. Hivyo ndivyo Jeshi la Polisi linavyotakiwa kufanya kazi zake.
Siyo mambo ya kuteka au kupoteza watu. Kuteka watu ni primitivity ya kuwango cha juu kinachotuondoa kwenye haki ya kuitwa binadamu wastaarabu. Hatuwezi kuishi kwenye nchi ya kuwindana kama simba na pundamilia. Sisi ni wanadamu, tunastahili kuonesha utofauti wetu na wanyama wa porini waliokosa akili na hekima.

Ni mapema sana kutamka kama vyombo vya ulinzi na usalama, vinaanza kurudi kwenye kanuni zake za utendaji kazi, au hii ni isolated case.
 
Kule Pemba JESHI LOTE LA POLISI NI WAFUASI WA MAALIM nyie maccm amri Zenu Kwa jeshi la polisi fanyeni huku bara wasikojitambua kule Wana itikadi tofauti ndiyo amepewa dhamana fasta na yupo nje anapiga zake siasa

Toka maktaba :

December 13, 2019

Waziri Masauni awa mbogo kutokana na jeshi la Polisi kutochukua hatua CCM inavyotaka. Waziri alishindwa kuelewa Polisi wameshindwa vipi kumdhibiti Maalim Seif na kutishia kuwashusha vyeo wakuu wa Polisi mkoa RPCs Pemba.

Waziri akaenda mbali na kutilia shaka vyombo vya ulinzi kusita kufanyia kazi na kutekeleza matamko ya serikali ya CCM awamu ya 5. Mh. Waziri akasema kwa kuburuza miguu huku wamejitia doa kama 2020 uchaguzi wataweza kuusimamia 'vyema' .
 

Mshauri mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti wa Kamati ya Itikadi na Uenezi wa ACT Wazalendo Salim Bimani wameripoti katika Kituo cha Polisi Wete Pemba asubuhi ya leo.

Viongozi hao wa ACT Wazalendo wameitwa na Mkuu wa Upelelezi wa Jinai (RCO) Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Wananchi na Wanachama wa ACT - Wazalendo wamekuwa nje ya maeneo ya karibu ya jengo la Polisi la Mkoa wa Kaskazini Pemba kwa lengo la kujua hatma ya viongozi wao wanaohojiwa na inadaiwa wamejiandaa na kuwachukulia dhamana ikibidi.

UPDATE:
Mshauri Mkuu wa ACT Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Salim Bimani wameshutumiwa kufanya mkutano bila kibali mwezi Desemba 2019 huko Micheweni Zanzibar.

Hata hivyo, Viongozi hao wameachiwa kwa dhamana na kupitia Mtandao wa Twitter Chama chao kimedai kuwa walifanya mkutano wa ndani usiohitaji kibali.

Jeshi la Polisi limewachia kwa Dhamana Mshauri Mkuu wa Chama @ACTwazalendo Maalim Seif Sharif Hamad na M/kiti wa kamati ya Itikadi na uenezi wa Chama hicho Salim bimani Baada ya hii leo kuitwa kufanyiwa mahojiano na Jeshi hilo katika kituo cha Polisi mkoa wa kaskazini Pemba.
Hii inaitwa tuguse tunuke
 
Hakuna awatiae hasira wananchi asivune alichopanda. Dharau, ukandamizaji, uuaji na uonevu waliowahi kufanyiwa na wanaofanyiwa Watu wanao ishi Pemba unajenga "mabomu" ambayo yatakua kulipuka siku moja
 
Hivi sheria za Bara ni tofauti na za Visiwani.... Tumeona watu wakisota lupango niezi na miezi kwa Makosa kama haya huku Bara.
 
January 15, 2020
Wete, Pemba
Tanzania

Naibu Kamishna wa Polisi akielezea nini maana ya mikutano ya nje, ambayo Maalim Seif aliitwa kituoni kuhojiwa na kisha kuachiwa kwa dhamana upelelezi ukiendelea.

Naye mshauri wa ACT Wazalendo Maalim Seif Sharrif azungumzia wito huo na kusisitiza amani lakini anazidi kuwasihi polisi kwamba amani huja kwenye usawa sio kukandamiza upande mmoja : Tazama aloyasema Maalim Seif ktk video hii:


Source: TV Wazalendo.
 
Sefu anamalizia uchaguzi wake wa mwisho na siasa zake za ukanda
Inawezekana chadema kushinda bara lakini sio kwa sefu kushinda Zanzibar
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom