PCCB wafungua kesi dhidi ya Lugumi na Jeshi la Polisi, IGP na Katibu wa Wizara waitwa Bungeni Dodoma

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,499
9,279
Waziri wa Mambo ya ndani Charles Kitwanga amekana kuhusika kabisa na kampuni ya Lugumi ambayo kwa sasa inakabiliwa na kashfa nzito ya rushwa na uhujumu uchumi ambayo ilipewa tenda ya kufunga vifaa vya kuchukulia alama za vidole kwenye vituo vyote vya polisi kwenye Wilaya zote nchini na kushindwa kukamilisha tenda hiyo.

Juhudi mbalimbali zinazofanywa kuujua ukweli wa sakata hili umepelekea taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini(TAKUKURU) kutoa tamko la kuifungulia kesi mahakamani kampuni hii ya Lugumi pamoja na jeshi la polisi na kufanya uchunguzi wa kina wa sakata hili.

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali(PAC) imewaita bungeni IGP pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ambapo watakuwa na kikao leo bungeni Dodoma na baadae baada ya kikao hicho ndipo wataweza kuongea na waandishi wa habari kuhusu suala hili.
 
PCCB hawana jino la kwenda mahakamani, wao wakichunguza hupeleka faili kwa DPP ambaye huamua kufungua kesi mahakamani.
 
Wazo lako nafikiri litakuwa kweli, watu issue haikuwa kwao watafungua kesi ili iweje? (Isijadiliwe na mhimili Mwengine)
Nina shaka na hii hatua ya PCCB kabla ya kikao cha bunge kama dhumuni lake sio kuzuia ili hii kashfa kwenda bungeni!!
 
wanachunguza nini wakati Nipashe wameambiwa waombe msamaha na Bunge haina hata wiki kupita kuwa izo taharifa si za kweli...
 
Hivi jeshi la polisi limewasilisha mkataba wa lugumi na jeshi hilo bungeni ama bado wamegoma?maana walipewa muda wa kuwasilisha mkataba lakini danadana zikawa nyingi.
 
Nina shaka na hii hatua ya PCCB kabla ya kikao cha bunge kama dhumuni lake sio kuzuia ili hii kashfa kwenda bungeni!!

Halafu baadae weseme hatuwezi kujadili swala lililoko mahakamani.
 
PCCB hawana jino la kwenda mahakamani, wao wakichunguza hupeleka faili kwa DPP ambaye huamua kufungua kesi mahakamani.
Hivi DPP nao ni polisi au? Na boss wa PCCB ametokea wapi? Baadhi ya wabunge wanashutuma za nini?
Inabidi tuwe na imani tu
 
Waziri wa Mambo ya ndani Charles Kitwanga amekana kuhusika kabisa na kampuni ya Lugumi ambayo kwa sasa inakabiliwa na kashfa nzito ya rushwa na uhujumu uchumi ambayo ilipewa tenda ya kufunga vifaa vya kuchukulia alama za vidole kwenye vituo vyote vya polisi kwenye Wilaya zote nchini na kushindwa kukamilisha tenda hiyo.

Juhudi mbalimbali zinazofanywa kuujua ukweli wa sakata hili umepelekea taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini(TAKUKURU) kutoa tamko la kuifungulia kesi mahakamani kampuni hii ya Lugumi pamoja na jeshi la polisi na kufanya uchunguzi wa kina wa sakata hili.

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali(PAC) imewaita bungeni IGP pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ambapo watakuwa na kikao leo bungeni Dodoma na baadae baada ya kikao hicho ndipo wataweza kuongea na waandishi wa habari kuhusu suala hili.
Yaani Jeshi la Polisi kushitakiwa na TAKUKURU??
Na Jeshi la polisi likikaidi kwenda mahakamani, ni kina nani watatumwa waende wakalikamate hilo jeshi la Polisi? Polisi haohao??
 
"Kesi ikiwa mahakamani haipaswi kujadiliwa na mhimili au mtu yeyote".
Hata akili fupi inalitambua hilo.
 
Juhudi mbalimbali zinazofanywa kuujua ukweli wa sakata hili umepelekea taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini(TAKUKURU) kutoa tamko la kuifungulia kesi mahakamani kampuni hii ya Lugumi pamoja na jeshi la polisi na kufanya uchunguzi wa kina wa sakata hili.
Kwa nini TUKUKURU wanakimbilia kuwafungulia kesi kabla ya kufanya uchunguzi wa kina?!
Kama hawajamaliza uchunguzi wao kwa nini wasiache lijadiliwe bungeni na hata kwenda PAC?!
Nimevutiwa na jitihada za TUKUKURU ya sasa hivi lakini sina imani na mwenendo wao kwenye ili la LUGUMI!!
 
"Kesi ikiwa mahakamani haipaswi kujadiliwa na mhimili au mtu yeyote".
Hata akili fupi inalitambua hilo.
yaa mkuu kwa kuwa tuna sheria kandamizi na hazibadiliki kwa faida ya wenye akili ndefu..Tumeona Zuma kesi ipo mahakamani na bungeni anajadiliwa kaika ile kesi yake...bongo ni kosa kuonyesha kesi ikiendeshwa mahakani Live na sasa wamesema Bunge izo akili za wapi izo...
 
Back
Top Bottom