Pay As You Earn (PAYE): Wafanyakazi mna maoni gani?

Hizi double taxation ni balaa, maraisi watakaofuata watarithi mambo ya ajabu sana.
Naona Kenya wanatoza 16% kwenye VAT. Hapa kwetu tunatozwa 21% kwenye nishati. I can't wait to leave the "employee" arena.
Sijakuelewa unasemaje? Kwenye nishati unatozwa VAT 21% au ni kodi gani? Nadhani inabidi uangalie haiwezi kuwa VAT.

Ukweli kodi ni kubwa lakini kwa kulinganisha na nini? Ni nini vyanzo mbadala.

Pia Ukiangalia vizuri utaona bajeti ya Tz ni kama imedouble kwa kipindi cha miaka 2-3. Ingawa impact yake yake haionekani kwenye macho ya Watanzania. Ingawa kupungua kwa thamani ya shs kunaweza kuwa chanzo lakini kasi ya depreciation sio hii inayooonekana kwenye budget.

Changamoto nadhani iwe kwenye budget inayozingatia matumizi, vipaumbele na inayopimika. Haiwezekani budget ikawa inaongezeka lakini athari za ongezeko hazionekani kwa Watz.

Lakini pia wafanyabiashara, NGO's na taasisi za dini nazo zinakwepa mno kodi. Ipo haja ya kuitazama mianya hii.
 
Sidhani kama tunahitaji kujadili chanzo mbadala cha kuipatia seriakli mapato. na wala sidhani kama serikali haipati fedha ya kutosha inamaanisha iwakamue sana wafanyakazi. Na pia wale wanaodhani kwamba wenye makampuni wao wanapeta si kweli kwani na wao wameajiri na wameajiriwa. Na kodi kidogo kwenye makampuni inaweza ikawa ni kivutio cha watu wengine kujianzisha makampuni.

Ukweli ni kwamba kodi ipo juu sana, na mbaya zaidi hatuoni cha msingi ambacho fedha zetu wavuja jasho zinachokifanyia. tunatakiwa tuungane walipa kodi wote kama walivyofanya madereva na tuelezwe mustakabli wa matumizi ya jasho letu. kama kweli inatukera raia ni rahisi kuhoji juu ya ili na kupata majibu manyoofu.
vinginevyo tutapigwa sound daily.
 
Sidhani kama tunahitaji kujadili chanzo mbadala cha kuipatia seriakli mapato. na wala sidhani kama serikali haipati fedha ya kutosha inamaanisha iwakamue sana wafanyakazi. Na pia wale wanaodhani kwamba wenye makampuni wao wanapeta si kweli kwani na wao wameajiri na wameajiriwa. Na kodi kidogo kwenye makampuni inaweza ikawa ni kivutio cha watu wengine kujianzisha makampuni.

Ukweli ni kwamba kodi ipo juu sana, na mbaya zaidi hatuoni cha msingi ambacho fedha zetu wavuja jasho zinachokifanyia. tunatakiwa tuungane walipa kodi wote kama walivyofanya madereva na tuelezwe mustakabli wa matumizi ya jasho letu. kama kweli inatukera raia ni rahisi kuhoji juu ya ili na kupata majibu manyoofu.
vinginevyo tutapigwa sound daily.
Tuungane km madereva wa mabasi??? Hiyo sikubaliani na wewe. Haikuwa njia sahihi ile kuaddress grievances zao. Mtu kapatikana na hatia mahakamani nyie mnagoma kuendesha mabasi. Kwanini msikate rufaa? Kubwa na la msingi ni kwamba licha ya uwepo wa kodi nyingi mfumuko wa bei umekuwa mkubwa mno kiasi kwamba pesa inayopatikana haifai kitu. Kwahiyo kwanza wadhibiti mfumuko na kuporomoka kwa thamani ya shs. Wahimize uwekezaji kwenye kilimo lakini wadhibiti vyanzo mbadala na kuangalia kiasi cha mshahara kinachoqualify kwa PAYE exemption. Kwa sasa ilikuwa laki moja, kuna haja kubadilisha ile bracket mpaka 150,000.
 
Tuungane km madereva wa mabasi??? Hiyo sikubaliani na wewe. Haikuwa njia sahihi ile kuaddress grievances zao. Mtu kapatikana na hatia mahakamani nyie mnagoma kuendesha mabasi. Kwanini msikate rufaa? Kubwa na la msingi ni kwamba licha ya uwepo wa kodi nyingi mfumuko wa bei umekuwa mkubwa mno kiasi kwamba pesa inayopatikana haifai kitu. Kwahiyo kwanza wadhibiti mfumuko na kuporomoka kwa thamani ya shs. Wahimize uwekezaji kwenye kilimo lakini wadhibiti vyanzo mbadala na kuangalia kiasi cha mshahara kinachoqualify kwa PAYE exemption. Kwa sasa ilikuwa laki moja, kuna haja kubadilisha ile bracket mpaka 150,000.

Asante mpenzi wa Tanzania kwa kuonyesha mapenzi yako kwa serikali na kusahau considerations zozote kwa hao wanaobeba mzigo wa serikali yetu yenye huge overheads za governance with inverse proportinate outcome

BNHAI, you may be right... to the people you report to, but just for second be in the victims shoes, so that for once you can think with others discussing this thread outside the box

Usilewe STK na bahasha za Khaki!!!
 
Tujenge hoja yenye kueleweka.
Ni kweli nakubaliana na nyie PAYE ni kubwa nini chanzo mbadala km kodi ikipunguzwa? Nchi nyingine wanakata asilimia ngapi? Hiyo PAYE ni asilimia ngapi ya kodi yoote ya serikali?

Mkuu wakiamua hata wakate 100% paye lakini huyu punda asife apate huduma muhimu maji, umeme, barabara nzuri, afya n.k. Tatizo wanakata fweza nyingi halafu punda hata maji hawezi kunywa. Mwisho wa siku unakuwa na mapunda punda tu

Chanzo mbadala mkuu ni mfano wa ndoo na maji. Ukienda kuchota maji na ndoo yenye tundu, usitegemee utafika na maji yote. Ziba kwanza tundu, nenda kisimani, utagundua hata safari zitapungua na utasave nguvu kibao. Tz izibe mianya ya kuibiwa kodi kwanza na sio kuongeza kodi
 
Ukweli ni kwamba kodi ipo juu sana, na mbaya zaidi hatuoni cha msingi ambacho fedha zetu wavuja jasho zinachokifanyia. tunatakiwa tuungane walipa kodi wote kama walivyofanya madereva na tuelezwe mustakabli wa matumizi ya jasho letu. kama kweli inatukera raia ni rahisi kuhoji juu ya ili na kupata majibu manyoofu.
vinginevyo tutapigwa sound daily.

sasa hivi ni ngumu kuungana kwani hatuna platform moja. kuna vyama vya wafanyakazi lukuki (walimu, manesi, higher learning institutions, nk) na sasa tumeanza kupingana wenyewe kwa wenyewe!!! ni aibu sana
 
Asante mpenzi wa Tanzania kwa kuonyesha mapenzi yako kwa serikali na kusahau considerations zozote kwa hao wanaobeba mzigo wa serikali yetu yenye huge overheads za governance with inverse proportinate outcome

BNHAI, you may be right... to the people you report to, but just for second be in the victims shoes, so that for once you can think with others discussing this thread outside the box

Usilewe STK na bahasha za Khaki!!!
Sipo kwenye STK wala kinachofanana na hicho. Ni Mkulima kabisa. Ila kuna maeneo tuwe wakweli inahitajika proffessionalism. Kama serikali haiwatendei haki wananchi ni kuiweka kando. Lakini katika kila nchi kodi ni muhim saana na ndio maana tunaweza kupata misaada. Tulipe kodi, tuweke madarakani serikali itakayokuwa ya wananchi. Nimejaribu hapo juu kuonyesha nini cha kufanya.

Ukweli vipato ni vidogo. Je kuondoa kodi au kuipunguza na kuendelea na budget tegemezi ni sawia. Km tunavyojulikana JF, kuwa tunaweza kufikiria, then tutoe na suluhisho.

Mie ninasisitiza usimamizi mmbora wa rasilimali. Ila kodi hazikwepeki
 
Nadhani kodi ya PAYE haijaongezeka kama umekuwa unaifuatilia kwa karibu kuanzia act ya mwaka 1974 (ukiachalia mbali ammendment chache) na ya sasa. Tatizo la haya maumivu ni kutetereka kwa uchumi. Mfumuko wa bei ndio umetufikisha hapa. Tunahitaji policy za kueleweka. Wadhibiti mfumuko wa bei, wasogeze huduma na kuziboresha, wapimwe kutokana na utendaji na wawajibike kwa wananchi. Tunalipa kodi tuwaulize barabara zikowapi? Tuwaulize utajiri wao wanautoa wapi?
 
Sipo kwenye STK wala kinachofanana na hicho. Ni Mkulima kabisa. Ila kuna maeneo tuwe wakweli inahitajika proffessionalism. Kama serikali haiwatendei haki wananchi ni kuiweka kando. Lakini katika kila nchi kodi ni muhim saana na ndio maana tunaweza kupata misaada. Tulipe kodi, tuweke madarakani serikali itakayokuwa ya wananchi. Nimejaribu hapo juu kuonyesha nini cha kufanya.

Ukweli vipato ni vidogo. Je kuondoa kodi au kuipunguza na kuendelea na budget tegemezi ni sawia. Km tunavyojulikana JF, kuwa tunaweza kufikiria, then tutoe na suluhisho.

Mie ninasisitiza usimamizi mmbora wa rasilimali. Ila kodi hazikwepeki

Sasa wewe uko wapi? Naona haya maoni kama yanatolewa na Mkullo. Hivi ni kazi ya mwananchi wa kawaida (in this case mfanyakazi) kuishauri serikali kutafuta vyanzo mbadala vya kodi? Naona kama huu ni utani. Vinginevyo tuwe tunasoma maoni ya msemaji wa Ikulu au Hazina!!
 
"Mishahara ya public sector (Basic) iko chini sana na ukizingatia threshhold kwa sasa ni 100,000, unakuta mtu basic yake ni 150,000 which means anatakiwa akatwe kodi kwenye 50,000! But in reality unakuta kwa mwezi mtu huyu anatoka na like 1, 2,3mil kama gross income from sitting allowance, acting allowance, extra duty allowance, honorarioum, perdiem etc ambazo they don't tax kabisa! So wanaendup kuienjoy income kubwa but pay less tax, kumbe private mishahara ni mikubwa but hakuna eti malipo ya sitting allowance, acting sijui nini......! so mara nyingi utakuta gross income = basic income......maanake hakuna income inayokwepa machine ya PAYE."

Hizo allowance zote ulizozitaja hapo ni TAXABLE


Ni ukweli usiopingika kwamba wafanyakazi kwenye public sector wana malipo mengi ambayo hayakatwi kodi ingawa yangestahili yakatwe kodi. Mfano, payroll za wafanyakazi wa serikali ziko 'centralised' hazina/wizarani na malipo ya extra duty allowance, sitting allowances hayapitii kwenye payroll kwani haya hufanywa moja kwa moja katika level ya department husika kupitia vifungu vingine.
Lakini hii si hoja ya msingi hapa, ma-zakayo wanatakiwa kuweka mfumo ambao utawezesha watu wote wanalipa kodi. TRA inahitaji kutumia sheria ambayo inayowalazimu registered entities kuwakilisha makision yao ya kodi kila quarter pamoja na vitabu vya hesabu na kuchukua hatua madhubuti za kuwawajibisha defauters. Haitii akilini kuwa PAYE ndiyo inaongoza katika makusanyo ya TRA na hii inaonyesha udhaifu mkubwa ktk taasisi hii ya kodi.
 
Nadhani kodi ya PAYE haijaongezeka kama umekuwa unaifuatilia kwa karibu kuanzia act ya mwaka 1974 (ukiachalia mbali ammendment chache) na ya sasa.

Hapa sina uhakika kama mwenyewe unazungumza kitu unachokifahamu au laa! Ulitaka usemaje labda...ili binafsi nikosime vizuri?
 
"Mishahara ya public sector (Basic) iko chini sana na ukizingatia threshhold kwa sasa ni 100,000, unakuta mtu basic yake ni 150,000 which means anatakiwa akatwe kodi kwenye 50,000! But in reality unakuta kwa mwezi mtu huyu anatoka na like 1, 2,3mil kama gross income from sitting allowance, acting allowance, extra duty allowance, honorarioum, perdiem etc ambazo they don't tax kabisa! So wanaendup kuienjoy income kubwa but pay less tax, kumbe private mishahara ni mikubwa but hakuna eti malipo ya sitting allowance, acting sijui nini......! so mara nyingi utakuta gross income = basic income......maanake hakuna income inayokwepa machine ya PAYE."

Hizo allowance zote ulizozitaja hapo ni TAXABLE


Ni ukweli usiopingika kwamba wafanyakazi kwenye public sector wana malipo mengi ambayo hayakatwi kodi ingawa yangestahili yakatwe kodi. Mfano, payroll za wafanyakazi wa serikali ziko 'centralised' hazina/wizarani na malipo ya extra duty allowance, sitting allowances hayapitii kwenye payroll kwani haya hufanywa moja kwa moja katika level ya department husika kupitia vifungu vingine.
Lakini hii si hoja ya msingi hapa, ma-zakayo wanatakiwa kuweka mfumo ambao utawezesha watu wote wanalipa kodi. TRA inahitaji kutumia sheria ambayo inayowalazimu registered entities kuwakilisha makision yao ya kodi kila quarter pamoja na vitabu vya hesabu na kuchukua hatua madhubuti za kuwawajibisha defauters. Haitii akilini kuwa PAYE ndiyo inaongoza katika makusanyo ya TRA na hii inaonyesha udhaifu mkubwa ktk taasisi hii ya kodi.

Mkuu, hilo ndo bonde. Siku zote maji hayapandishi kilima au vipi?
 
Sasa wewe uko wapi? Naona haya maoni kama yanatolewa na Mkullo. Hivi ni kazi ya mwananchi wa kawaida (in this case mfanyakazi) kuishauri serikali kutafuta vyanzo mbadala vya kodi? Naona kama huu ni utani. Vinginevyo tuwe tunasoma maoni ya msemaji wa Ikulu au Hazina!!
Ninaamini katika constructive criticism. Tuseme ukweli na kuweka ubinafsi pembeni. Tuangalie mistari yote. Well kodi ipunguzwe, then??? Tuweke mawazo yetu kiutalaam. Wapi hawalipi kodi? au sie tunalipa kodi kubwa kulinganisha na wapi? Mie naliona tatizo lipo kwenye mfumuko wa bei na depreciation ya currency yetu ndio maana mishahara inakuwa midogo. Tudhibiti hayo na tuhakikishe pesa inakusanywa na kutumika ipasavyo, kama hawezekani tuwaweke watakaoweza kusimamia pesa ya wananchi inavyotakiwa
 
Hapa sina uhakika kama mwenyewe unazungumza kitu unachokifahamu au laa! Ulitaka usemaje labda...ili binafsi nikosime vizuri?
Ninachoeleza kodi ya PAYE haijaongezeka. Isipokuwa brackets zimewekwa nyingi na taxable amount imekuwa kubwa. Kama unakumbukumbu kabla 100,000 haijawa exempted, ilikuwa 80,000 then 60,000. Kwahiyo relief imekuwa ikitolewa. Mie nadhani tuchachamae kwenye mfumuko wa bei
 
Ninachoeleza kodi ya PAYE haijaongezeka.

Hapa ndio mimi sikubaliani kabisa na wewe. Yes, inawezekana kabisa rates za kodi kny bands hazijaongezeka i.e. 18.5% mim na 30% max......! but provisions na regulations za kny sheria ya kodi zimebadilika sana!

Kwanza unakosea kusema sheria ya kodi haijabadilika tangia ile ya mwaka 1974....! moja hatuna sheria ya mwaka 1974 ipo ile ya ITA 1973! Pili, sheria ya kodi nyingine ambayo tunaitumia sasa ni ile ya Mwaka 2004....ITA 2004....So unaweza kuona hapo hizo ni sheria mbili tofauti kabisa...sawa bro?

Tatu sheria ile ya 2004 ukilinganisha na ile ya 1973 ina mbana sana employee.....kwa maana kwamba hana income ambayo it goes untaxed mkuu! every thing kipo taxed! Kumbe ile ya mwaka 1973 ilikuwa imeacha mwanya wa kutopigwa kodi mapato fulani ya mwajiliwa e.g Interest free loans, free given vehicles, cateria services, medical services, gratuities etc.....!

Kwa maana hiyo ukolinganisha sheria ile ya mwaka 1973 na ile 2004 kodi imeongezeka sana kwa upande wa mwajiliwa!

Need we say more!
 
Hapa ndio mimi sikubaliani kabisa na wewe. Yes, inawezekana kabisa rates za kodi kny bands hazijaongezeka i.e. 18.5% mim na 30% max......! but provisions na regulations za kny sheria ya kodi zimebadilika sana!

Kwanza unakosea kusema sheria ya kodi haijabadilika tangia ile ya mwaka 1974....! moja hatuna sheria ya mwaka 1974 ipo ile ya ITA 1973! Pili, sheria ya kodi nyingine ambayo tunaitumia sasa ni ile ya Mwaka 2004....ITA 2004....So unaweza kuona hapo hizo ni sheria mbili tofauti kabisa...sawa bro?

Tatu sheria ile ya 2004 ukilinganisha na ile ya 1973 ina mbana sana employee.....kwa maana kwamba hana income ambayo it goes untaxed mkuu! every thing kipo taxed! Kumbe ile ya mwaka 1973 ilikuwa imeacha mwanya wa kutopigwa kodi mapato fulani ya mwajiliwa e.g Interest free loans, free given vehicles, cateria services, medical services, gratuities etc.....!

Kwa maana hiyo ukolinganisha sheria ile ya mwaka 1973 na ile 2004 kodi imeongezeka sana kwa upande wa mwajiliwa!

Need we say more!
Yah its true nimechanganya madude kuna ITA ya 1973 na ya 2004 ambayo ilibecome operational July 2004.
Sasa ukija kwenye hoja kuu kabla haijaanza kutumika hiyo ya 2004 kama unakumbukumbu za kutosha vitu kama gratuities vilikuwa vinapigwa kodi tayari na walikuwa wameshafika kwenye loan kabisa. Lakini pia ukiangalia hizo brackets unazozizungumza utaona zimebaki kama zilivyo ispokuwa minimum exemption imeongezeka. na ukiongeza hiyo inamaana umepunguza kodi maana kuna pesa iko exempted.
Hoja ya msingi PAYE ni kubwa? Kulinganisha na wapi? If we account for time series utaona imepungua, kama tutaongeza other benefits bado kuna loops ambazo zipo wazi na legal unaweza kukubaliana na mwajiri wako ingawa uwe tayari kufeel pain yake kwenye contributions
 
Ninaamini katika constructive criticism.
I agree with you 100%

Tuseme ukweli na kuweka ubinafsi pembeni. Tuangalie mistari yote. Well kodi ipunguzwe, then???
Heading inasema employees wanalipa kodi kubwa (kulinganisha na makundi mengine)....so kama na hao wengine walipa kodi vizuri, then automatically employees wanaweza kuwa releived mkuu!

Tuweke mawazo yetu kiutalaam.


Naam mkuu!

Wapi hawalipi kodi? au sie tunalipa kodi kubwa kulinganisha na wapi?
Are you serious mkuu?

Umeshajiuliza hata siku moja landloards wa nchi hii wanalipa kodi kiasi gani? ulishajiuliza hawa wafanyabiashara kny informal sector (small &medium size) wanapata mapato kiasi gani na wanalipa kodi kivipi? umeshajiuliza hayo mahekalu ya hapo dar wealth billions of shilings ile capital imelipiwa kodi wapi? umeshajiuliza hawa watu kama MCs, tarumbetas, Bongoflavas,tax cabs, hotelians etc wanaoendesha mambo yao informally wanatengeneza pesa ngapi na wanalipa kodi kiasi gani?

Ukijiuliza hayo maswali na kupata majibu then will get to know kwamba employees wanalipa pesa mingi sana. Ukishindwa takuletea mifano na maelezo zaidi mkuu!

Mie naliona tatizo lipo kwenye mfumuko wa bei na depreciation ya currency yetu ndio maana mishahara inakuwa midogo.
Si kweli, depreciation of currency and inflation inawakumba wote kwa pamoja si employees tu kaka!
 
Yah its true nimechanganya madude kuna ITA ya 1973 na ya 2004 ambayo ilibecome operational July 2004.
Tupo pamoja hapo mkuu!

Sasa ukija kwenye hoja kuu kabla haijaanza kutumika hiyo ya 2004 kama unakumbukumbu za kutosha vitu kama gratuities vilikuwa vinapigwa kodi tayari na walikuwa wameshafika kwenye loan kabisa.
.
Si kweli mkuu, labda ulete kifungu gani kilikuwa kinatax gratuities kwa 100% na loan kama ilivyo sasa!

Lakini pia ukiangalia hizo brackets unazozizungumza utaona zimebaki kama zilivyo ispokuwa minimum exemption imeongezeka. na ukiongeza hiyo inamaana umepunguza kodi maana kuna pesa iko exempted.
Daah mkuu, watch out brackets ni mwaka wa fedha 2009/2010 tu hazijabadilika....miaka mingine yote from 2004 zinemekuwa zikibadilika mkuu...kwa mfano mpaka mwaka wa fedha 2007/2008 brackets zilikuwa na the highest amount of 540,000 but kuja 2008/2009 brackets zikachange kuwa na the highest brackect of 720,000 mkuu...so sikuelewi kabisa unaposema hazijabadilika tangia 1973!

Hoja ya msingi PAYE ni kubwa? Kulinganisha na wapi?
Soma post yangu hapo juu mkuu, nimejibu hili!

If we account for time series utaona imepungua

Time series gani hapa mkubwa? tunasema hivi benefits kama cafeteria na gratuities zilikuwa untaxed accord to ITA 1973 so kama mtu alikuwa akizipata kipindi hicho manake alikuwa halipii kodi sawa? lakini leo hii kama mtu anazipata hizo benefits analipia kodi....sasa unasemaje kodi haijaongezeka bali imepungua?
kama tutaongeza other benefits bado kuna loops ambazo zipo wazi na legal unaweza kukubaliana na mwajiri wako ingawa uwe tayari kufeel pain yake kwenye contributions
Zitaje hizo loops....kwa uelewa wangu hakuna loops zozote kwa mwajiriwa ambazo ni legal!
 
I agree with you 100%

Heading inasema employees wanalipa kodi kubwa (kulinganisha na makundi mengine)....so kama na hao wengine walipa kodi vizuri, then automatically employees wanaweza kuwa releived mkuu!



Naam mkuu!

Are you serious mkuu?

Umeshajiuliza hata siku moja landloards wa nchi hii wanalipa kodi kiasi gani? ulishajiuliza hawa wafanyabiashara kny informal sector (small &medium size) wanapata mapato kiasi gani na wanalipa kodi kivipi? umeshajiuliza hayo mahekalu ya hapo dar wealth billions of shilings ile capital imelipiwa kodi wapi? umeshajiuliza hawa watu kama MCs, tarumbetas, Bongoflavas,tax cabs, hotelians etc wanaoendesha mambo yao informally wanatengeneza pesa ngapi na wanalipa kodi kiasi gani?

Ukijiuliza hayo maswali na kupata majibu then will get to know kwamba employees wanalipa pesa mingi sana. Ukishindwa takuletea mifano na maelezo zaidi mkuu!

Si kweli, depreciation of currency and inflation inawakumba wote kwa pamoja si employees tu kaka!
Nimefurahia saana namna unavyojenga hoja. Ni wazi JF iko mbali saana. Yah hakuna haja ya kulalamika bila kuwa na hoja mbadala. Hoja wafanyakazi wanalipa kodi kuliko makundi mengine. Nadhani izibwe mianya kwenye makundi mengine. Hakuna jambo baya kama bajeti tegemezi kumbe tunaweza kujitegemea. Tujitegemee kwanza then tuanze kuona tunaelekea wapi. Mahitaji ya sasa kwa nchi nini? Tukipunguza kodi hiyo kubwa ya wafanyakazi, nini mustakabali wa wa bajeti yetu. Kwa mtiririko wa hoja zako ni wazi tunahitaji makundi mengine yalipe kodi na si tupunguze kodi labda tuextend kidogo bracket kutoka kwenye 100,000.
Hoja ya depreciation ya currency na inflation ni kweli inawakumba wote lakini kumbuka sasa hii inahit zaidi wale wanaotrade kwenye local currency ambapo wengi wa wafanyakazi wao wanapata mshahara kwenye local currency. Pia maumivu ya depreciation na inflation yanasikika vizuri kama kipato chako ni kidogo, na hii ni kwa wafanyakazi. Kwahiyo mshahara utakuwa unamaana tu kama pesa itakuwa na nguvu na inflation itadhibitiwa. Hata uongezeke mshahara na kodi zipungue bila kuzingatia uimara wa fedha bado ni kitendawili.
 
Tupo pamoja hapo mkuu!

. Si kweli mkuu, labda ulete kifungu gani kilikuwa kinatax gratuities kwa 100% na loan kama ilivyo sasa!

Daah mkuu, watch out brackets ni mwaka wa fedha 2009/2010 tu hazijabadilika....miaka mingine yote from 2004 zinemekuwa zikibadilika mkuu...kwa mfano mpaka mwaka wa fedha 2007/2008 brackets zilikuwa na the highest amount of 540,000 but kuja 2008/2009 brackets zikachange kuwa na the highest brackect of 720,000 mkuu...so sikuelewi kabisa unaposema hazijabadilika tangia 1973!

Soma post yangu hapo juu mkuu, nimejibu hili!



Time series gani hapa mkubwa? tunasema hivi benefits kama cafeteria na gratuities zilikuwa untaxed accord to ITA 1973 so kama mtu alikuwa akizipata kipindi hicho manake alikuwa halipii kodi sawa? lakini leo hii kama mtu anazipata hizo benefits analipia kodi....sasa unasemaje kodi haijaongezeka bali imepungua?
Zitaje hizo loops....kwa uelewa wangu hakuna loops zozote kwa mwajiriwa ambazo ni legal!
Inawezekana brackets mwezangu umezitazama kwa juu. Ukiacha bila kutax ila minimum amount hiyo tayari ni relief.
Hii ya kifungu nipe muda kidogo, maana nawafaham waajiri kwenye private sector ambao wanalipa mishahara kwa design na kukuta amont inayokuwa taxed ni kidogo na ndio inayo account kwenye pension na gratitute. Nitarudi kwenye hili.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom