Super Handsome
JF-Expert Member
- Jul 16, 2013
- 3,846
- 6,439
JIkiwa zimepita zaidi ya siku 5 tangu chama cha mapinduzi kipige kura za maoni, mapya yameibuka Busega!
Aliyewahi kua mbunge wa jimbo hilo kwa miaka 10 Raphael Chegeni kwa kishirikiana na Mkuu wa wilaya Paul Mzindakaya wameunda genge la uhuni kuhujumu matokeo ya halali ambapo matokeo hayo yanaonesha mbunge wa sasa Dr.Titus Kamani ameshinda kwa kishindo.
Aidha, kamati ya siasa ya wilaya kwa ushirikiano na watajwa, inadaiwa kukodi mabaunsa toka mwanza kufanya vurugu ili kuzuia matokeo yasitajwe kisa tu bw.Chegeni kuangukia pua.
Duru za siasa jimboni humu zinaonesha kukataliwa kwa chegeni ambaye ana lazimisha kurudi mamlakani licha ya wananchi kumpigia chapuo mbunge wa sasa Dr.Kamani.
Inaelezwa kua, Mkuu wa wilaya alikiuka taratibu mara baada ya kuanza kutoa matokeo ya uchaguzi kwa njia ya mtandao (whatsapp) ambapo matokeo hayo feki yalimpigia chapuo Chegeni lakini punde matokeo halali yalipotoka yalionesha Chegeni kaangukia neng`elu (pua) na mkuu wa wilaya huyo kuanza kulazimisha yatangazwe matokeo ambayo yeye aliyapost kwenye groups mbali mbali za whatsapp kinyume na matokeo halisi.
Inaelezwa kua mwekahazina wa wilaya amepigwa kiti cha kichwa na Mkiti wa Uvccm mara baada ya kutaka kutangaza matokeo hayo halali ambayo wagombea wengine wote wamekubali kushindwa huku Chegeni pekee akiyakataa na kuleta fujo kwa msaada wa Mzindakaya!
Nitaendelea kuwaletea updates mbali mbali toka jimboni Busega ambapo mkuu wa wilaya anaendeshwa na chegeni kama remote!
Wasalaam,
SH!
Aliyewahi kua mbunge wa jimbo hilo kwa miaka 10 Raphael Chegeni kwa kishirikiana na Mkuu wa wilaya Paul Mzindakaya wameunda genge la uhuni kuhujumu matokeo ya halali ambapo matokeo hayo yanaonesha mbunge wa sasa Dr.Titus Kamani ameshinda kwa kishindo.
Aidha, kamati ya siasa ya wilaya kwa ushirikiano na watajwa, inadaiwa kukodi mabaunsa toka mwanza kufanya vurugu ili kuzuia matokeo yasitajwe kisa tu bw.Chegeni kuangukia pua.
Duru za siasa jimboni humu zinaonesha kukataliwa kwa chegeni ambaye ana lazimisha kurudi mamlakani licha ya wananchi kumpigia chapuo mbunge wa sasa Dr.Kamani.
Inaelezwa kua, Mkuu wa wilaya alikiuka taratibu mara baada ya kuanza kutoa matokeo ya uchaguzi kwa njia ya mtandao (whatsapp) ambapo matokeo hayo feki yalimpigia chapuo Chegeni lakini punde matokeo halali yalipotoka yalionesha Chegeni kaangukia neng`elu (pua) na mkuu wa wilaya huyo kuanza kulazimisha yatangazwe matokeo ambayo yeye aliyapost kwenye groups mbali mbali za whatsapp kinyume na matokeo halisi.
Inaelezwa kua mwekahazina wa wilaya amepigwa kiti cha kichwa na Mkiti wa Uvccm mara baada ya kutaka kutangaza matokeo hayo halali ambayo wagombea wengine wote wamekubali kushindwa huku Chegeni pekee akiyakataa na kuleta fujo kwa msaada wa Mzindakaya!
Nitaendelea kuwaletea updates mbali mbali toka jimboni Busega ambapo mkuu wa wilaya anaendeshwa na chegeni kama remote!
Wasalaam,
SH!