Paul Makonda punguza siasa na drama badala yake fanya Kazi...

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,409
108,516
Mosi nianze tu kwa kusema kuwa nilikuwa miongoni na bado ni miongoni wa Watu ambao nimependa sana uteuzi wako kwa hiyo nafasi ya Ukuu wa Mkoa hasa kutokana na utendaji wako ulipokuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni kwani ulionyesha kuwa ni tumaini jipya kwa Vijana katika nyanja nzima ya Uongozi.

Mheshimiwa naomba tu utanivumilia kwa haya nitakayoenda kusema hapa kwani naamini ukiyachukulia kwa uzito wake mkubwa naweza nikawa nimekusaidia kama si kukuongezea kitu katika Uongozi wako ila ukiyachukulia kwa hisia hasi utaniona Mimi ni adui yako na bahati mbaya mno nimeumbwa kusema ukweli na kuwa muwazi bila uwoga.

Mheshimiwa Paul Makonda Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam itoshe tu kusema kuwa tokea upate hiyo nafasi ya Uongozi binafsi sijaona bado lolote ulilolibadilisha zaidi tu ya kuona kipaumbele haya yafuatayo:

  1. Kupenda publicity.
  2. Kufanya drama zisizo na mpango.
  3. Kutoa kauli bila ya kuzipima kwanza.
  4. Kupiga " mikwara " ya kitoto na isiyo na tija.
Mheshimiwa Paul Makonda nakumbuka huko nyuma uliwahi kutoa matamko kuwa hutaki kuona uchafu wowote jijini Dar je huo uchafu umeisha? Mheshimiwa Paul Makonda uliwahi kusema hutaki kuona Makahaba wakijiuza hapa jijini Dar je wameondoka? Mheshimiwa Paul Makonda uliwahi kusema hutaki Gereji bubu jijini Dar je zimeisha? Mheshimiwa Paul Makonda ni miezi michache tu ulisema kuwa Halmashauri zote za Dar zihakikishe barabara zote zipo katika hali nzuri je una uhakika hilo agizo lako limefanikiwa?,Mheshimiwa Paul Makonda ulisema kuwa hutaki kuona Kumbi za Starehe na Nyumba za Ibada zinapiga Mziki hadi usiku kucha na wa makelele je hilo umefanikiwa?

Labda nikusaidie tu Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa kwani yawezekana ukawa umesahau kuwa huu Mkoa wa " Changanyikeni Brains " nikimaanisha wa Dar es Salaam umeshawahi kuwa na Wakuu wa Mikoa ambao walikuwa wakali wewe cha mtoto lakini wameondoka na kuuacha Mkoa wa " Changanyikeni Brains " ukiwa vile vile.

Nadhani ungetumia muda wako mwingi kufanya utafiti wa jinsi gani unaweza kuuongoza vizuri huu Mkoa wa " Changanyikeni Brains " ungefanikiwa mno na sana ila bahati mbaya ninavyokuona na Wewe unataka kupita kule kule walikopita watangulizi wako na niseme sidhani kama utafanikiwa kama ambavyo umefanikiwa kuombewa sana hadharani na Viongozi wa dini kila uchao.

Kuna kauli ambazo umezitoa jana hasa za kuhusiana na Mashoga na Wavuta Sigara pamoja na Shisha. Binafsi nimeyapokea haya matamko yako kwa Wasiwasi fulani hivi hasa nikijua ugumu uliopo na ambao pengine utaupata juu yake.

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa hivi kama tu yale mambo niliyoyaorodhesha katika aya yangu ya nne ( 4 ) hapo juu ambayo ndiyo ya msingi bado mpaka sasa umeshindwa kuyatekeleza haya magumu kabisa ya Mashoga na Wavutaji " fegi " na hadi " sigara bwege " utayaweza kweli?

Nimalizie tu kwa kusema kuwa jitahidi sana uwe na Vipaumbele vyako vikuu kadhaa katika Uongozi wako na pia ukijipa time frame ya utekelezaji wake badala ya kutaka kufanya kila kitu kwa wakati mmoja kwani kwa Watu waliobobea katika Management na Administration wanaweza wakakushangaa. Kiongozi makini huwa na Vipaumbele vichache na ambavyo huwa na uhakika navyo kuwa ataviweza na siyo kama hivi ufanyavyo Wewe na ndiyo maana hapo juu nimekuambia kuwa punguza drama na acha siasa.

Nikutakie tu usomaji mwema wa huu UZI wangu Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa " Changanyikeni Brains " na yapokee tu haya katika dhana nzima kimtazamo na yafanyie kazi kwani kwa umri ulionao nina uhakika unaweza ukabadilika na hatimaye kuja kuwa Kiongozi mmoja wa mfano kwa sisi Vijana wenzio na labda nikutoe tu hofu kwa kusema kuwa so far unaenda vizuri kiasi ila nikuombe tu punguza " mashauzi ".

Uwe na Jumapili njema na naomba kuwasilisha.
 
Mimi rafiki yangu makonda namwita Mzee Wa kiki kabsaaa tatizo la mashoga nilikuwepo lakini baada ya wadau KUPIGA kelele kuhusiana na clouds TV kumuhoji shoga ndo Mkuu ukaja juu

Mimi kama kinaja mwenzio nakushauri hii Habari ya mashoga iweke pending kwanza mpaka haya yakamilike
1. Uchafu ulio kithiri ambao hisababisha mlipuko Wa magonjwa mbalimbali. Tumeona hili swala sio endelevu ingawa wana nchi walianza kulipokea vizuri sijui hii kampeni iliishia wapi
2, panya road pamoja na vibaka hili ni kundi sumbufu sana nazani unajua kuna maeneo dar ikifika SAA 12 jion yan mtaa mzima mnalala ya Wa ndani Wa ndani Wa Nje Wa nje. Kwa kadhia hii mashoga subiri kidogo
3. Mateja hili nalo ni kundi kubwa sana hebu dili nalo tuone Kwa kukamata wauza unga na hili kundi kulipeleka rehabilitation center hapo utakuwa umesaidia sana nguvu kazi ya Taifa hili.Kwa kweli mashoga wasubiri
4 .ufaulu ma shule ya serikali
5 walimu kusafili bureeeee sijui imeishia WAP
6. Machangu na ombaomba haya mashoga YAKO ngoja kwanza Mzee
 
Mimi rafiki yangu makonda namwita Mzee Wa kiki kabsaaa tatizo la mashoga nilikuwepo lakini baada ya wadau KUPIGA kelele kuhusiana na clouds TV kumuhoji shoga ndo Mkuu ukaja juu

Mimi kama kinaja mwenzio nakushauri hii Habari ya mashoga iweke pending kwanza mpaka haya yakamilike
1. Uchafu ulio kithiri ambao hisababisha mlipuko Wa magonjwa mbalimbali. Tumeona hili swala sio endelevu ingawa wana nchi walianza kulipokea vizuri sijui hii kampeni iliishia wapi
2, panya road pamoja na vibaka hili ni kundi sumbufu sana nazani unajua kuna maeneo dar ikifika SAA 12 jion yan mtaa mzima mnalala ya Wa ndani Wa ndani Wa Nje Wa nje. Kwa kadhia hii mashoga subiri kidogo
3. Mateja hili nalo ni kundi kubwa sana hebu dili nalo tuone Kwa kukamata wauza unga na hili kundi kulipeleka rehabilitation center hapo utakuwa umesaidia sana nguvu kazi ya Taifa hili.Kwa kweli mashoga wasubiri
4 .ufaulu ma shule ya serikali
5 walimu kusafili bureeeee sijui imeishia WAP
6. Machangu na ombaomba haya mashoga YAKO ngoja kwanza Mzee
Mashoga yake...? Haha
 
Niulize kidogo japo swali lenyewe lipo nje kidogo ya mada ila linahusiana na moja ya matamko kadhaa ya RC Makonda.

Hivi hawa walimu walio katika jiji la Dar es Salaam ambao walipata upendeleo wa kutolipa nauli kwenye daladala waendapo kazini na kurudi nyumbani wanaotumia njia zenye mabasi ya mwendo kasi nako hawalipi nauli kwenye hayo mabasi ya UDART?
 
Mosi nianze tu kwa kusema kuwa nilikuwa miongoni na bado ni miongoni wa Watu ambao nimependa sana uteuzi wako kwa hiyo nafasi ya Ukuu wa Mkoa hasa kutokana na utendaji wako ulipokuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni kwani ulionyesha kuwa ni tumaini jipya kwa Vijana katika nyanja nzima ya Uongozi.

Mheshimiwa naomba tu utanivumilia kwa haya nitakayoenda kusema hapa kwani naamini ukiyachukulia kwa uzito wake mkubwa naweza nikawa nimekusaidia kama si kukuongezea kitu katika Uongozi wako ila ukiyachukulia kwa hisia hasi utaniona Mimi ni adui yako na bahati mbaya mno nimeumbwa kusema ukweli na kuwa muwazi bila uwoga.

Mheshimiwa Paul Makonda Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam itoshe tu kusema kuwa tokea upate hiyo nafasi ya Uongozi binafsi sijaona bado lolote ulilolibadilisha zaidi tu ya kuona kipaumbele haya yafuatayo:

  1. Kupenda publicity.
  2. Kufanya drama zisizo na mpango.
  3. Kutoa kauli bila ya kuzipima kwanza.
  4. Kupiga " mikwara " ya kitoto na isiyo na tija.
Mheshimiwa Paul Makonda nakumbuka huko nyuma uliwahi kutoa matamko kuwa hutaki kuona uchafu wowote jijini Dar je huo uchafu umeisha? Mheshimiwa Paul Makonda uliwahi kusema hutaki kuona Makahaba wakijiuza hapa jijini Dar je wameondoka? Mheshimiwa Paul Makonda uliwahi kusema hutaki Gereji bubu jijini Dar je zimeisha? Mheshimiwa Paul Makonda ni miezi michache tu ulisema kuwa Halmashauri zote za Dar zihakikishe barabara zote zipo katika hali nzuri je una uhakika hilo agizo lako limefanikiwa?,Mheshimiwa Paul Makonda ulisema kuwa hutaki kuona Kumbi za Starehe na Nyumba za Ibada zinapiga Mziki hadi usiku kucha na wa makelele je hilo umefanikiwa?

Labda nikusaidie tu Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa kwani yawezekana ukawa umesahau kuwa huu Mkoa wa " Changanyikeni Brains " nikimaanisha wa Dar es Salaam umeshawahi kuwa na Wakuu wa Mikoa ambao walikuwa wakali wewe cha mtoto lakini wameondoka na kuuacha Mkoa wa " Changanyikeni Brains " ukiwa vile vile.

Nadhani ungetumia muda wako mwingi kufanya utafiti wa jinsi gani unaweza kuuongoza vizuri huu Mkoa wa " Changanyikeni Brains " ungefanikiwa mno na sana ila bahati mbaya ninavyokuona na Wewe unataka kupita kule kule walikopita watangulizi wako na niseme sidhani kama utafanikiwa kama ambavyo umefanikiwa kuombewa sana hadharani na Viongozi wa dini kila uchao.

Kuna kauli ambazo umezitoa jana hasa za kuhusiana na Mashoga na Wavuta Sigara pamoja na Shisha. Binafsi nimeyapokea haya matamko yako kwa Wasiwasi fulani hivi hasa nikijua ugumu uliopo na ambao pengine utaupata juu yake.

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa hivi kama tu yale mambo niliyoyaorodhesha katika aya yangu ya nne ( 4 ) hapo juu ambayo ndiyo ya msingi bado mpaka sasa umeshindwa kuyatekeleza haya magumu kabisa ya Mashoga na Wavutaji " fegi " na hadi " sigara bwege " utayaweza kweli?

Nimalizie tu kwa kusema kuwa jitahidi sana uwe na Vipaumbele vyako vikuu kadhaa katika Uongozi wako na pia ukijipa time frame ya utekelezaji wake badala ya kutaka kufanya kila kitu kwa wakati mmoja kwani kwa Watu waliobobea katika Management na Administration wanaweza wakakushangaa. Kiongozi makini huwa na Vipaumbele vichache na ambavyo huwa na uhakika navyo kuwa ataviweza na siyo kama hivi ufanyavyo Wewe na ndiyo maana hapo juu nimekuambia kuwa punguza drama na acha siasa.

Nikutakie tu usomaji mwema wa huu UZI wangu Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa " Changanyikeni Brains " na yapokee tu haya katika dhana nzima kimtazamo na yafanyie kazi kwani kwa umri ulionao nina uhakika unaweza ukabadilika na hatimaye kuja kuwa Kiongozi mmoja wa mfano kwa sisi Vijana wenzio na labda nikutoe tu hofu kwa kusema kuwa so far unaenda vizuri kiasi ila nikuombe tu punguza " mashauzi ".

Uwe na Jumapili njema na naomba kuwasilisha.
Asee umesema ya msingi sana...hawa mashoga ni ishu ngumu, coz ukiacha wanaojitangaza walio mtaani kimya kimya ni wengi lkn ushoga una vyanzo vingi sio wote wa kulaaniwa wataalamu wa hormon, psychology nk wana maelezo mazuri. Mimi nadhan vibaka na majambazi ndo tatizo kubwa maana hawa wanatoa roho kavukavu washughulikiwe hawa kuliko kutoa matamko ya kurukaruka km bisi...
 
Kuna kitu Makonda na hata Magufuli naona hawakielewi kabisa
Mtu pekee Tanzania ambae alikuwa akitoa tamko linakua sheria hapo hapo alikuwa Mwalim Nyerere
baada ya hapo katiba ikarekebishwa

kuanzia sasa tamko lolote la kiongozi yeyote linapaswa kuendana na sheria zilizopo
kama hakuna sheria ya ku support hilo tamko basi hilo tamko halina maana yoyote

Sasa unasema eti marufuku kumfollow gay kwenye Instagram....unabaki unajiuliza
je mkuu wa mkoa anazijua hata sheria?
je huyo mtu ukimkamata utamshitaki kwa sheria zipi?
na akisema mimi siishi Dar nimekuja tu?
 
HUU UZI NAOMBENI "MODERATOR'S" MUUUPIGE BAN TU; Una mwelekeo Wa kutetea Mashoga na uhalifu, Mkuu Wa mkoa Anajitahid kupambana Kwa hali na Mali lakini watu kama hawa wanaturudisha nyuma; huu Uzi naomba "mod's" muufute. Zoezi la kutokomeza ukahaba, ushoga na uchafu ni endelevu haliwezi kuisha Kwa siku mbili tu...mkiuacha huu Uzi uendelee kuwepo ni kuwa katisha tamaa viongozi! Ukuu Wa mkoa ni taasisi kubwa sana ina mambo mengi ya kufanya, mengine sisi kama wananchi husika tunatakiwa kumuunga mkono.
 
HUU UZI NAOMBENI "MODERATOR'S" MUUUPIGE BAN TU; Una mwelekeo Wa kutetea Mashoga na uhalifu, Mkuu Wa mkoa Anajitahid kupambana Kwa hali na Mali lakini watu kama hawa wanaturudisha nyuma; huu Uzi naomba "mod's" muufute. Zoezi la kutokomeza ukahaba, ushoga na uchafu ni endelevu haliwezi kuisha Kwa siku mbili tu...mkiuacha huu Uzi uendelee kuwepo ni kuwa katisha tamaa viongozi! Ukuu Wa mkoa ni taasisi kubwa sana ina mambo mengi ya kufanya, mengine sisi kama wananchi husika tunatakiwa kumuunga mkono.
Acha kutokwa Povu, jibu HOJA
 
HUU UZI NAOMBENI "MODERATOR'S" MUUUPIGE BAN TU; Una mwelekeo Wa kutetea Mashoga na uhalifu, Mkuu Wa mkoa Anajitahid kupambana Kwa hali na Mali lakini watu kama hawa wanaturudisha nyuma; huu Uzi naomba "mod's" muufute. Zoezi la kutokomeza ukahaba, ushoga na uchafu ni endelevu haliwezi kuisha Kwa siku mbili tu...mkiuacha huu Uzi uendelee kuwepo ni kuwa katisha tamaa viongozi! Ukuu Wa mkoa ni taasisi kubwa sana ina mambo mengi ya kufanya, mengine sisi kama wananchi husika tunatakiwa kumuunga mkono.
Kama kweli una nia njema na hao viongozi basi ilipaswa usifie uzi huu. Kuna tofauti kati ya upendo wa dhati na kuwa mamluki. Upendo wa dhati ni ule wa kuwa tayari kurekebisha yule umpendae kwa nia njema hata kama itamkera, umamluki ni ile hali ya kuwa tayari kumsupport umpendae hata kama unakereka ama anapotoka. Hapa unataka kuleta umamluki.
GENTAMYCINE hajasema lolote baya, alichofanya ni kumkosoa kwa kumjenga (Constructive criticism) sasa ndugu unapotaka ban na kufutwa kwa uzi kisa tu ukweli umesemwa tutafika kweli?
 
Back
Top Bottom