Buyuni Kwetu
JF-Expert Member
- Sep 29, 2013
- 1,933
- 1,850
Umesema kweli mwananguMatamko yasiyofanyiwa utafiti wa aina yoyote yanazidi kuturudisha miaka mingi nyuma. Wanachojua wao ni kuwa wanatawala kwa kutumia Polisi, sasa sijui wanategemea watasafisha jiji kwa kutumia jeshi la Polisi? Usafi anaojua Polisi ni usafi wa zile Uniforms tu, nenda kakague usafi wa kuanzia pale anapoishi, ofisini na penginepo ndiyo utagundua Polisi wetu hawajui uchafu ni nini, sasa sijui watatumikaje kuhakikishaje Mkoa unakuwa msafi wakati hawajui tofauti ya hali hizo mbili!
Makonda ni Time buyer tu, na katika hilo ameweza sana kumkamata mkuu. Mpaka sasa sijui ameweza kufanikisha lipi kati ya yote.
Tusifanye masikhara na uongozi wa wa kijamii, hii tabia ya 'tuwape muda' ndiyo imesababisha miaka hamsini tuendelee kuchechemea tu, kila anayekuja tumpe muda, akipewa muda, mwaka umeisha tunaingia mwaka mwingine, tukikosoa tunaambiwa jamani mbona mwaka ndiyo umeanza hebu tumpe muda, mwaka wa pili unaisha, tunaingia mwaka wa tatu tukijaribu kukosoa au kuchangia tofauti tunaambiwa haraka ya nini wakati bado anaendelea kupambana, tusubiri akimaliza ndiyo tuone kama amweza au hajaweza. Akimaliza muda wake na akiwa amefeli na yeye ataungana na wakosoaji kulalamika eti mfumo umemkwamisha, tena atalalamika kwa sauti utadhani wakosoaji hawakuwahi kuonya hali hiyo ambayo wao waliikumbatia na kuitete kwa nguvu zote za kijeshi.
Miaka hamsini mingine itatukuta hapahapa...