Paul Makonda na Ufuatiliaji wa Sheria: Mfano wa kuigwa kwa viongozi vijana

Eric Cartman

JF-Expert Member
May 21, 2009
11,967
11,212


Katika viongozi vijana ninao anza kuwakubali huyu jamaa anastahili tuzo ya kiongozi bora kwa vijana katika muda mfupi aliowekwa kwenye public office.

Siku zote niliamini asilimia kubwa ya shida nyingi za watanzania ni zao la wafanyakazi wa serikari na si vyama vya siasa. Tumetengeneza sheria nyingi na nzuri tu kupitia copy and paste ya sheria za wengine mfano 'Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya Mwaka 2004'. Hii sheria inataka mahusiano mazuri kazini kwa njia ya mikataba, mazingira bora ya kazi na kuweza kubalance power za mtoa ajira na muajiriwa kupitia vikundi vyao.

Mantiki ya sheria yoyote ni kuleta mabadiliko yanayo tarajiwa na kunakuwa na regulator wake kuhakikisha sheria inafuatwa kama ilivyotarajiwa vinginevyo kuna adhabu za fine ya serikari au kulipa fidia kwa mfanyakazi kwa ukiukwaji wa sheria. Chini ya 'Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya Mwaka 2004' msimamizi wake ni idara ya kazi na malengo yake ya usimamizi wameyabainisha wazi kwenye website yao.

Sasa leo inakuwaje atoke mkuu wa wilaya kwenda kusikiliza vilio vya wafanyakazi vinavyo ambatana na ukiukwaji wa sheria. Inawezekana vipi mtu anafanyakazi kwa miaka nane kama kibarua bila ya mkataba, holiday pay, pengine na pension plan kutoka kazini? na idara ya kazi hipo na sheria wanaijua inasemaje kuhusu ukiukwaji huo. Sidhani kama Makonda ana mamlaka ya kutoa maagizo lakini the goodwill gesture is unquestionable.

Kuna wanaobisha lakini ukweli ni kwamba asilimia kubwa ya watu wanaopewa kuziongoza hizi taasisi za serikari awana uwezo ndio zao la hivi vitu vyenye malalamiko ndani ya jamii na si kitu kingine.
 
Last edited by a moderator:
Nashauri akaungane na Mzee warioba, manake wote ni timu makomeo!
 
Nashauri akaungane na Mzee warioba, manake wote ni timu makomeo!
Mkuu hili si swala la siasa za vyama; ni the extent ya watu wazembe walio serikarini katika kusimamia agenda za nchi. Ata ikitokea miujiza vyama vya siasa vikabadilika bado watatumia wafanyakazi hawa hawa kutimiza agenda zao za sera na usimamizi wa sheria.

Kitendo cha kiongozi kufuatailia haki za sheria despite uwepo wa kitengo chenye kazi hiyo maalum kwa sababu ya uzembe wao ni cha kukisifia bila ya ushabiki wa vyama kama kweli tunataka kuona mabadiliko.
 
Mkuu hili si swala la siasa za vyama; ni the extent ya watu wazembe walio serikarini katika kusimamia agenda za nchi. Ata ikitokea miujiza vyama vya siasa vikabadilika bado watatumia wafanyakazi hawa hawa kutimiza agenda zao za sera na usimamizi wa sheria.

Kitendo cha kiongozi kufuatailia haki za sheria despite uwepo wa kitengo chenye kazi hiyo maalum kwa sababu ya uzembe wao ni cha kukisifia bila ya ushabiki wa vyama kama kweli tunataka kuona mabadiliko.

Pole kwa kukukwaza ndugu. Ni kweli jamaa yuko vizuri. Ila tu alikosea kumlabua mzee wa watu pale ubungo plaza.
 
Hakuna wilaya Tanzania yenye matatizo na malalamiko kuhusu ardhi kama Konondoni kwasababu ya rushwa iliokithili kwenye halmashauri yake. Kama ni mchapakazi aanze kutatua keto hizo!
 


Katika viongozi vijana ninao anza kuwakubali huyu jamaa anastahili tuzo ya kiongozi bora kwa vijana katika muda mfupi aliowekwa kwenye public office.

Siku zote niliamini asilimia kubwa ya shida nyingi za watanzania ni zao la wafanyakazi wa serikari na si vyama vya siasa. Tumetengeneza sheria nyingi na nzuri tu kupitia copy and paste ya sheria za wengine mfano 'Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya Mwaka 2004'. Hii sheria inataka mahusiano mazuri kazini kwa njia ya mikataba, mazingira bora ya kazi na kuweza kubalance power za mtoa ajira na muajiriwa kupitia vikundi vyao.

Mantiki ya sheria yoyote ni kuleta mabadiliko yanayo tarajiwa na kunakuwa na regulator wake kuhakikisha sheria inafuatwa kama ilivyotarajiwa vinginevyo kuna adhabu za fine ya serikari au kulipa fidia kwa mfanyakazi kwa ukiukwaji wa sheria. Chini ya 'Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya Mwaka 2004' msimamizi wake ni idara ya kazi na malengo yake ya usimamizi wameyabainisha wazi kwenye website yao.

Sasa leo inakuwaje atoke mkuu wa wilaya kwenda kusikiliza vilio vya wafanyakazi vinavyo ambatana na ukiukwaji wa sheria. Inawezekana vipi mtu anafanyakazi kwa miaka nane kama kibarua bila ya mkataba, holiday pay, pengine na pension plan kutoka kazini? na idara ya kazi hipo na sheria wanaijua inasemaje kuhusu ukiukwaji huo. Sidhani kama Makonda ana mamlaka ya kutoa maagizo lakini the goodwill gesture is unquestionable.

Kuna wanaobisha lakini ukweli ni kwamba asilimia kubwa ya watu wanaopewa kuziongoza hizi taasisi za serikari awana uwezo ndio zao la hivi vitu vyenye malalamiko ndani ya jamii na si kitu kingine.


Hakuna la ajabu. Hiyo ni sehemu ya job description yake.
 
Last edited by a moderator:
Hakuna la ajabu. Hiyo ni sehemu ya job description yake.

Mamlaka husika ni hi hapa na majukumu yao yapo kama ifuatavyo

Idara ya Kazi

ambayo hapo awali ilijulikana kama Idara ya Kazi ina jukumu na wajibu wa kusimamia utekelezaji wa sheria za kazi na mahusiano bora sehemu za Kazi.Idara hii inaongozwa na Kamishna wa Kazi akisaidiwa na Makamishna wa Kazi Wasaidizi Watatu wanaoongoza Sehemu zifuatazo:-
Mahusiano Kazini (Labour Relations)·
Ukaguzi Sehemu za Kazi (Labour Inspections)
Hifadhi ya Jamii (Social Security)

Sehemu ya Mahusiano Kazini (Labour Relations Section)
  • Kuratibu na kusimamia mapambano dhidi ya maambukizi ya Ukimwi mahali pa kazi
  • Kuratibu na kusimamia uendeshaji wa shughuli za baadhi ya Taasisi zilizoundwa chini ya sheria ya Taasisi za Kazi, Na. 7 ya 2004 ambazo ni Bodi za Mishahara za Kisekta (Sector Wage Boards) na Baraza la Ushauri kuhusu masuala ya Kazi, Uchumi na Jamii (Labour Economic and Social Council-LESCO)
Sehemu ya Ukaguzi Sehemu za Kazi (Labour Inspections Section)
  • Kuzuia migomo na migogoro ya kazi ya migomo ya kikazi kwa kufanya kaguzi na uelimishaji katika maeneo mbalibali ya kazi kwa lengo la kuhakikisha Sheria za Kazi zinatekelezwa ipasavyo miongoni mwa waajiri na wafanyakzi, ikiwa ni pamoja na kuandaa mchakato wa kuwafikisha Mahakamani wale wote wanaokiuka au kushindwa kutekeleza Sheria za Kazi na Kanuni zake
  • Kupokea nakala za mikataba ya makubaliano ya pamoja kuhusu hali bora za kazi kwa mujibu wa kifungu cha 71(7) cha Sheria Na. 6 ya 2004, iliyofikiwa baina ya Waajiri na Wafanyakazi kupitia Vyama vyao.
  • Kukuza majadiliano ya pamoja (collective bargaining) miongoni mwa wadau katika maeneo ya kazi

Sehemu ya hifadhi ya jamii (social security)

  • Kuendelea kupokea taarifa za ajali kazini, kushughulikia na kusimamia malipo ya fidia za ajali kwa Watumishi wanaoumia au kufariki kwa ajali Kazini kama inavyoelekezwa katika Sheria ya Fidia, Sura 263, R. E.2002 hadi hapo Sheria ya Fidia (Workers Compensation Act), Na. 20 ya mwaka 2008 itakapoanza kutumika
  • kusimamia Sera, Sheria na utekelezaji wa Mpango wa hifadhi ya jamii.


source http://www.kazi.go.tz/pages/43

Unaweza kuona majukumu ya hii taasisi na uzembe uliopo nchini kwenye kusimamia kazi zao, sasa jiulize ni watu wangapi wanaathirika kutokana na uzembe huu uliokithiri nationally, hawa waajiri wangekuwa wanajua sheria inasemaje kuhusu ajira na inasimamiwa na idara ya kazi sidhani kama wangekuwa wanafanya mambo ya kipuuzi kama hayo.

Tukitaka kusonga mbele lazima tukomae kwanza na ueshimu wa sheria na katiba ndio njia pekee, maamuzi ya siasa ni sehemu ndogo sana ya lawama hila usimamizi wa serikari ndio kila kitu ambacho kinatuathiri mimi na wewe. Kwa hivyo kwenye kutoa pongezi toa tu bila ya kuangalia siasa za vyama.
 
Back
Top Bottom