Paul Makonda azungumza miaka 18 bila Mwl Nyerere

bg_dg_dy

JF-Expert Member
Feb 27, 2009
604
489
Mheshima Paul Makonda kijana maarufu na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam anahojiwa na TBC kuhusu miaka kumi na minane bila uwepo wa mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwasisi wa taifa Letu na Baba wa Taifa.

Mwalimu hatuko nae kimwili ila kifikra tupo nae tunaishi misingi yake.

Mwalimu alianzisha vyama vingi vya kisiasa kwa nia njema ila vyama vya kisiasa vimekuwa vikiwana lengo la kujinufaisha.

Aelezea mfano serikali ya awamu ya tano inavyoishi misingi ya mwalimu nyerere, mfano suala la makinikia wasomi wetu kutokuwa wazalendo, Mwalimu awali alituasa tusubirie pale ambapo tutakuwa tupo tayari na kweli tumepata wasomi ila uzalendo umeshindikana.

Agusia swala la mfumo wa uwajibikaji kwa wafanyakazi ulivyowaathiri toka wakiwa vyuoni hadi kutokuishi uzalendo katika sekta ya umma. Mfano anapata fedha kutoka vyanzo tofauti kuanzia bodi ya mkopo na ndugu/jamaa kinachopelekea wanafunzi kupata fedha nyingi na maisha ya utajiri akiwa chuoni tofauti na kipato atakachopata akiwa kazini, hvyo ni chanzo hakika cha mfumo wa rushwa makazini kwa kutengeneza ugumu katika utoaji wa huduma ili kupata pesa zaidi.

Ashauri yafuatayo ili watanzania tuweze kuuishi uzalendo.

1. Takukuru iwezeshwe ifanye kazi yake vizuri.

2. Viongozi wa dini watusaidie kutukumbusha baada ya maisha ya hapa kuna maisha mwingine.

3. Mabadiliko kwenye sekta ya Elimu kuwezesha uzalendo zaidi kwa wanafunzi wetu.

Mfano tuwaangalie Nyerere, Kawawa na Warioba Hindi walivyo waadilifu hadi leo tujifunze kutoka kwao.

Pia somo la uzalendo hautoshi, bali viongozi na waalimu wauishi uzalendo wanaoutangaza na kusisitiza.

Mwisho, mwalimu nyerere alijiamini na aliamini katika umoja. Hvyo watanzania ninawasihi tuungane tushikamane tuweze kulifikisha taifa pale alipopataka mwalimu nyerere. Mungu atubariki na tumshirikishe Mungu katika yote.
 
Anajua nini kuhusu Mwl? ana nini ambacho kinafanana hata kwa theluthi na Mwl? Wakati mwalimu anafariki alikuwa secondary huko ambako alifail sasa Nyerere alimjua lini na kwa vipi? huu ndio ujinga hii nchi imefikia. kujikomba tuuuuuuuuuuuuu. Rioba naye sasa kweli kapoteza mwelekeo kabisa. Mtu wa kwenda kuzungumzia Mwl anakuwa Makonda? Hii ni dharau kubwa sana kwa familia ya Nyerere.
 
Paragraph ya tatu ni uongo!
1965 Mwalimu ndie alifuta Vyama vingi vya Siasa

1992 alieleta Vyama vingi ni Mzaramo wa Mkuranga anaitwa Ally Hassan Mwinyi ambae si Mpenda sifa, sambamba na kuleta Vyama vingi pia alifuta Azimio la Kishamba la Arusha ambalo sasa hivi kuna Mshamba yuko Bize kulirudisha kwa style tofauti
 
Mkataa kwao ni mtumwa
Usione vyaelea jomba, vina wenyewe, pumbaaavu! Unatema big g kwa karanga za kuonjeshwa?!

Hakuna budi zaidi ya kurejea ya wahenga kwamba: "Ng'ombe akivunjika mguu hukimbilia zizini!!!"
 
Bashite kumzungumzia Nyerere kwenye studio za Taifa ni dharau kubwa sana. Huyu Mkurugenzi wa TBC hajitambui kabisa. Wasiifanye TBC kuwa tundu la choo cha shimo ambako Bashite ndiko anakostahili kupanua domo lake lijae mainzi.
 
Hizi ni dharau. Daudi hafahamu chochote kuhusu Nyerere, Obulangata & IQ yake haina uwezo wa kushika na kutuza hisitoria halisi ya Nyerere.

Hizi ni dharau
Wameshindwaje kumualika Warioba ama Butiku wakatueleza uhalisia badala ya aliyesimuliwa kutusimulia uongo wa zero yake.
 
Anajua nini kuhusu Mwl? ana nini ambacho kinafanana hata kwa theluthi na Mwl? Wakati mwalimu anafariki alikuwa secondary huko ambako alifail sasa Nyerere alimjua lini na kwa vipi? huu ndio ujinga hii nchi imefikia. kujikomba tuuuuuuuuuuuuu. Rioba naye sasa kweli kapoteza mwelekeo kabisa. Mtu wa kwenda kuzungumzia Mwl anakuwa Makonda? Hii ni dharau kubwa sana kwa familia ya Nyerere.
Tuache wivu fitina makonda anajua kujieleza
 
Back
Top Bottom