Paul Makonda: Ahsante Mungu katikati ya machozi umenipa mapacha wawili!

Status
Not open for further replies.
Haya yote nadhani ni uwoga na kutumuliwa asikae jukwaa la viongozi, dah!

=======

Heshima na Mamlaka ni zako eee Mungu wa Mbingu na Nchi na kwako wewe tunalia Aba, nitaendelea kutaja ukuu wako siku zote za maisha yangu kwakua hujawahi kuniacha hata dakika moja.

Pamoja na mapito magumu na mazito lakini naiona nuru yako huku nikisikia sauti ya ROHO mtakatifu ikisema mwanangu Paul Christian Makonda nalikujua kabla sijakuumba na nikakutenga kwa kusudi langu usikubali TAA iwakayo ndani yako ikazimika.

Ona sasa unavyozidi kuniheshimisha katikati ya machozi umenipatia zawadi tena itokayo kwako.

Mimi nilieitwa tasa ulinipa mtoto KEAGAN ambaye alishangaza ulimwengu kwa ujio wake:Ukaona haitoshi LEO umenipa DOUBLE PORTION:Leo Mungu wangu umenipa MAPACHA tena wa KIUME na Wa KIKE hii yote ni kutangaza UKUU wako maishani mwangu.

Kwa wale ambao bado hawajakuamini na wanateseka juu ya uzazi,naomba kupitia watoto hawa wakauone ukuu wako Ewe YESU mwana wa Mungu ulie hai.

Hongera sana kipenzi changu Maria Mungu amejitwalia utukufu kupitia wewe.

Asanteni sana watumishi wa Mungu, wazazi wetu, dada na kaka zetu kwa kuwa nasi nyakati zote, kama ambavyo mmekuwa baraka kwetu.Naomba pia Mungu awainulie watu wema nyakati za uhitaji wenu.

EhhNafsiYanguMUHIMIDI-Bwana


MoyoWaShukrani
Ajifunze namna ya kuwa mzazi. Amshukuru mungu wake kimya tu. Hajui upepo anaowapulizia watoto wake.

Aliyoyafanya katika uongozi wake huenda malipo yake yakapitia kwa watoto hao, si vizuri kuwanenea maneno haya malaika hawa lakini uzoefu wa Karma, imani na philosophy huwa havina unafiki.

Atambue kwamba kuna wanaolia kwamba kuzaa si kupata na ni heri matumbo yao yangefungwa.

Aache ujinga, ni muda wa kusimama na kuwa mwanaume.
Kuna wenzake sasa hivi wanawapiga mnada mabint zao...
 
CHADEMA watasema ni njama ya CCM ili Makonda azungumziwe na CHADEMA idode kule uchochoroni Arusha, wanaogopa viwanja vikubwa sikuhizi.
 
Mkuu wa mkoa wa Dsm mstaafu Paul Makonda amemshukuru Mungu kwa mkewe kujifungua mapacha wa kike na kiume.

Makonda amesema katikati ya machozi aliyonayo sasa Mungu amemkumbuka na kumpa zawadi.

My take; Sijajua Paul Makonda analilia nini?!!

Maendeleo hayana vyama!
 
Wakati ukiendelea kumshukuru Mungu na kutupia mapicha uwakumbuke na wale wana wa wenzako waliodhulumiwa uhai wao kupitia wewe hata kufikia kupigwa ban ya kuingia marekani

Wale nao wana wazazi wanaowapenda kama unavyowapenda wakwako
Nao pia wana maumivu kama nawe utakapopata maumivu ukisikia Kegan ama wadogo zake wameumizwa bila hatia

Uzazi na kuwa mzazi ni zaidi ya kumshukuru Mungu na kwa maneno matamu na kutupia picha nzuri kwenye mitandao

Umeandika Mungu kakuheshimisha katikati ya matatizo...na wale walionusurika kifo kupitia udhalimu wako watasemaje!? Je kati yako wewe na wao ni nani yuko juu kwa sasa?

Ulijisahau sana...sasa hivi ndio unajua nini maana ya kuitwa mzazi...Badala ya kumshukuru Mungu mitandaoni nakushauri jitenge na hadhira ukajifungie mahali pa upweke usali na kumuomba Mungu sana aepushe uzao wako na karma mbaya...

Wote walioumia kupitia mikono na mdomo wao...damu yao bado inakutafuta ..imezaa kisasi...inasubiri kikue na kukomaa...JITENGE kabisa na media ukajinyenyekeshe chini ya miguu ya Mola ukiomba msamaha na kufanya kitubio
 
Ukibarikiwa hakuna haja ya wewe kupigana na matangazo. Acha hiyo baraka ifanye matangazo. Watu wanaotakiwa kufahamu umebarikiwa watafahamu tu. Wakufurahi na ww watafurahi, watakaoumia wataumia.
 
daaaah sijui kwanini binadamu hua tunakoswa aibu wakati tunajua tunamkufuru mwenyezi MUNGU
 
Mbona hajamshukuru Mheshimiwa Rais na Mwenyekiti wa chama chake?
 
Status
Not open for further replies.
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom