Patrobas Katambi, Naomba uondoe nia yako ya kugombea ubunge Shinyanga Mjini

Mmechemka kumnyang'anya form sasa mapovu yanawatoka!Ha ha ha tulieni sindano za moto ziwaingie!
 
Mkabila mkubwa wee! Unataka kutambika?!


Wasalam Jamvini,

Kamanda Patrobas Katambi, nakuomba uondoe nia yako ya kugombea ubunge Shinyanga Mjini mara moja.

Kamanda, unafahamu kuwa wewe si mzawa wa hapa Shinyanga Mjini. Na kwamba turufu hii tuliitumia kama CHADEMA dhidi ya Masele na kusababisha ushindi kwetu.

Kamanda, unafahamu huna ndugu wala jamii yako hapa mjini unag'ag'ania. Kamanda Masele /Nkurunziza.

Kamanda, unafahamu jimbo la Kahama walikukatalia live, ambako kuna ndugu zako, umefika wilayani hapa na mbunga wamekukubalia kutia nia.

Kamanda, unafahamu ulivyoanzisha mtandao wa kimakundi CHADEMA wilayani hadi kata.

Kamanda, unafahamu wanashinyanga walivyo na misimamo. Juu ya uzawa wameonewa kwa miaka zaidi ya 10.

Kamanda, unafahamu kwana watia nia zaidi ya 10 wenye sifa ila umekomalia kisa ni kiongozi wa kitaifa utapata tu.

Kamanda, unajua ulikataliwa na walimu siku ya seminar yao. Ukimwakilisha Rechal Mashishanga ulizomewa kwa maneno yako kwao. (Ulimi hauna mfupa)

Kamanda unafahamu. Uongozi makao makuu unakubeba, hata mkutano wa hadhara juzi juzi NKMZ Salum Mwalimu alikubeba na kuwaacha watia nia wengine.

Kamanda ni hivi, kujenga CHADEMA si lazma uwe ni Mbunge, mbona una Cheo kizuri kukitumikia chama, BAVICHA TAIFA.

Jipime! usikibomoe chama kwa tamaa zako Kamanda.

Ukweli MCHUNGU wewe si MZAWA wa hapa.

Am always PERFECT.
 
uvccm wengi wanatoa maneno bila kujua hata hii thread ni ya lini? Angalieni kwanza uzi huuni wa lini
 
kama ni kweli mimi mwenyewe sikubaliani nae kabisa ifike wakati mtu kama yeye atulie ajenge chama bado kijana sana yasije kutokea ya heche na waitara tarime ...shinyanga ni jimbo ambalo wazawa wametumika sana kujenga chama sasa asitokee mtu mwingine kisa ana cheo akomalie kugombea....kuna makada wa chadema wanakubalika sana hapo shinyanga ....katambi anatakiwa atulie ajenge chama bado kijana sana ....tulilikosa jimbo la tarime kwa matatizo hayo hayo



Katambi kumbe ni tamaa mbele huyu kijana
 
Back
Top Bottom