Patrick Oita Nyapara: Askari Polisi aliyemtandika mpenzi wake Risasi 47

Patrick Oita Nyapara, ambaye ni police nchini Kenya alimuua mpenzi wake kwa kumtandika Risasi 7 baada ya binti huyo kumkataa, pindi alipomaliza masomo Chuo Kikuu.
Kwa maelezo ya Patrick ni kwamba alimchukua mdada huyo aliyejulikana kwa jina la Christine Maonga kutoka katika familia duni kijijini na kumpeleka mjini Nairobi kama mke wake ambapo aliamua kumsomesha mpaka chuo kikuu.

Alikuwa akimlipia karo na mahitaji mengine pamoja na kutuma pesa kwa mama mzazi wa binti huyo kama msaada kutokana na familia hiyo kutokuwa na uwezo wa kumudu gharama za maisha.

Baada ya kuhitimu masomo yake, Christine alimwambia Patrick kuwa amechoka kuwa naye kwani ni mtu asiyekuwa na hadhi yoyote na hafai kuwa mpenzi wake hivyo ni vyema kila mtu afanye mambo yake.

"Nimepata mpenzi mwingine ambaye ananifaa sana pia ni Mkurugenzi wa Kampuni moja kubwa sana jijini Nairobi hivyo siwezi kuwa na wewe Patrick mtu usiyekuwa na future na ni daraja D ambalo ni dhaifu kwangu", alisema Christine.

Patrick hakuielewa kauli ya mpenzi wake, akaamua kwenda kijijini kwa mama yake na Christine kuomba msaada wa suluhu ili aweze kumuoa binti yao kwani alikuwa ametumia gharama kubwa mno kumsomesha.

Mama yake binti alijibu kuwa hawezi kumpangia mtoto wake mume wa kumuoa hivyo anapaswa aachwe ajiamulie yeye mwenyewe. Patrick hakukubali, akamtafuta dada yake Christine na kumwelezea hali halisi lakini alijibiwa kuwa hana hadhi ya kumiliki mwanamke aliyehitimu Chuo Kikuu hivyo atafute mwanamke wa level ya mgambo kama yeye.

Aliondoka na kurudi nyumbani na kuchukua uamuzi mgumu wa kumuita Christine nyumbani kwa lengo la kuongea na kumaliza tofauti zao ili waachane kabisa, binti alienda nyumbani kwa Patrick mapema zaidi. Alifika na kumkuta Patrick amejihami kwa silaha, hawakuzungumza chochote zaidi ya kumkandamiza risasi 47 na zote zikapita mwilini mwa Christine hali iliyopelekea kifo chake papo hapo.
Nini maoni yako?
Uamuzi mzur hiyo ndio dawa ya usalit ile Mimi ningeongeza kidogo na mama mkwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"Nimepata mpenzi mwingine ambaye ananifaa sana pia ni Mkurugenzi wa Kampuni moja kubwa sana jijini Nairobi hivyo siwezi kuwa na wewe Patrick mtu usiyekuwa na future na ni daraja D ambalo ni dhaifu kwangu"

Hili neno "Dhaifu" kama vipi litolewe tu kwenye kamusi maana lazima lizue tafrani
 
wanaume tukutane kweny kikao chetu cha dharura tupongezane kwa ujasiri na wazoo la kishujaa na lakutuletea heshima alofanya mwanaume mwenzetu


Nikiwa kama msemaji wa chama cha wanaume nitoe pongezi kwa bwana kopro aka mgambo na chama kimeona juhudi za ndugu yetu


Mwisho kabisa ningependa kuwashauri wanachama kuuzuria vikao kwani kuna malengo mengi inabidi tufanikishe kama wanaume

Usiache mbachao kwa msala upitao... Sjui kama hii methali nimepatia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ALIMPIGA RISASI 47

Na Juma Sylvestre Max...

Patrick Oita Nyapara police jamii nchini Kenya alimuua mpenzi wake kwa kumtandika Risasi 47 baada ya binti huyo kujifanya mjanja.
Kwa maelezo ya Patrick ni kwamba alimchukua mdada Christine Maonga kutoka ktk familia duni iliyokuwa ikiishi kijijini na kumpeleka mjini Nairobi kama mke wake ambapo aliamua kumsomesha mpaka chuo kikuu.

Wakati akimlipia karo na mahitaji mengine Patrick alikuwa akituma pesa pia kwa mama mzazi wa binti huyo kama msaada kutokana na familia hiyo kutokuwa na uwezo wa kumudu gharama za maisha.

Baada ya kuhitimu masomo yake Christine alimwambia mpenzi wake kuwa amechoka kuwa naye kwani ni MTU asiyekuwa na hadhi yoyote na hafai kuwa mpenzi wake hivyo ni vyema kila MTU afanye mambo yake.

"Nimepata mpenzi mwingine ambaye ananifaa sana pia ni mkurugenzi wa kampuni moja kubwa sana jijini Nairobi hivyo siwezi kuwa na wewe Patrick MTU usiyekuwa na future na ni daraja D ambalo ni dhaifu kwangu" aliongeza Christine.

Patrick alichanganyikiwa sana akaamua kwenda kijijini kwa mama yake na Christine kuomba msaada wa suluhu ili aweze kumuoa binti yao kwani alikuwa ametumia gharama kubwa mno kumsomesha.

Mama yake binti alijibu kuwa hawezi kumpangia Mme wa kumuoa binti yake hivyo anapaswa aachwe ajiamlie yeye mwenyewe.
Patrick hakukubali akamtafuta Dada yake Christine na kumwelezea hali halisi lakini alijibiwa kuwa hana hadhi ya kumiliki mwanamke aliyehitimu chuo kikuu hivyo atafute wa level ya mgambo kama yeye.

Aliondoka na kurudi nyumbani kufanya uamzi mgumu wa kumuita Christine sehemu ya hotel au nyumbani, walikubaliana kukutana wayamalize na waachane kabisa na binti alienda nyumbani kwa Patrick mapema zaidi.
Alifika na kumkuta Patrick amejihami kama boko haram, hawakuzungumza chochote zaidi ya kumkandamiza risasi 47 na zote zikapita mwilini mwa Christine hali iliyopelekea kifo chake papo hapo.
 
Back
Top Bottom